Dar si Lamu,
Eeeeh mwenzetu wee ni mwanamama?... maanake majibu yako kidogo yameniacha nje kuwa wajua kwa nini wanafunzi wa vyuo vyetu wanajiuza.
Ama ndio Dar sii Lamu kweli?..
Sikiliza ndugu yangu kutembea na wanaume wengi kama starehe ni umalaya ambao unatokana na hulka ya mtu lakini mwanamke wa chuoni anapo UZA mwili wake kama biashara ya kusukuma maisha hili ni swala zito zaidi ya unavyofikiria wewe....Unless una hoja nyingineyo zaidi ya kuwashusha dada zetu kwa mtazamo wako.
Ni kweli Umalaya ulikuwepo toka zamani lakini umalaya huo haukuwa kwa wanafunzi kujiuza miili yao ila moja ya starehe zao...Walikuwa wakitoka majumbani mwao kwenda sehemu za starehe tena wengine watoto wa hawa vigogo lakini kutembea na mtu ilikuwa ni ktk starehe yao..Haikuwa na malipo zaidi ya chicken n Chips pale Mermaid!
Pili, sitegemei kabisa kwamba wewe mwanaume unaweza kunipa sababu zinahusu hisia za kike ktk swala hili. Na iweje leo iwe umalaya huu kwa wasichana wanaosoma vyuo vikuu wakati sikumbuki kuwepo kwa hulka kama hii miaka ya zamani.
Nitafurahi zaidi ikiwa kuna mwanamke humu ambaye anaweza kunambia kuhusu wimbi hili la wasichana kuuza miili yao kwa madai ya kutafuta Ada ya chuo anachosoma.
Pili, ndugu Dar hata huku nje UGENINI, wasichana wetu wengi wanajisomesha na kuna kila haja ya wao kupenda anasa zaidi ya huko nyumbani maanake vishawishi ni vingi zaidi, kila kitu kipo madukani kwa daraja tofauti.
Lakini hata hivyo wengi wao wameweza kutafuta njia nyingine nje ya kuuza miili yao, wakifanya kazi mbuzi kabisa ambazo wewe hapo Bongo huwezi kuzifanya wala kumshauri mtu kufanya. Na wameweza kulipa ada ya shule.. Wanaofanya umalaya kwa starehe wanafahamika na haihusiani kabisa na utafutaji wa karo ya shule...