Just in: UDSM wafukuzwa

Just in: UDSM wafukuzwa

Mwakjj

Wala usipate taabu kutafuta namba, hakuna mwanafunzi wa kufanya hayo uliyoshauri. Huna haja ya kwenda mbali kujua ni kwanini. Wakati waliposimamishwa na kupewa masharti magumu, over 40% walitimiza masharti yote na waliobaki walishindwa kwa sababu tu ya uwezo na sio msimamo.

Hoja yangu hapa ni kuwa, ikiwa wameshindwa kuonyesha msimamo wakati wa shida (kifungoni) unadhani watafanya hivyo sasa hivi wakati wa raha? Naambiwa kuna wengine wamepelekwa benki kulipiwa na baba zao huku wamesimamiwa na kupewa maneno makali makali.

Mwanasiasa.

Im 100% sure no one will show any sort of solidarity towards banned Daruso leaders. U keep wait and u will see....
 
hii inasikitisha... halafu kesho tushangae viongozi wetu wakisukumwa kwa vitisho vya wakubwa!!
 
Mwakjj

Wala usipate taabu kutafuta namba, hakuna mwanafunzi wa kufanya hayo uliyoshauri. Huna haja ya kwenda mbali kujua ni kwanini. Wakati waliposimamishwa na kupewa masharti magumu, over 40% walitimiza masharti yote na waliobaki walishindwa kwa sababu tu ya uwezo na sio msimamo.

Hoja yangu hapa ni kuwa, ikiwa wameshindwa kuonyesha msimamo wakati wa shida (kifungoni) unadhani watafanya hivyo sasa hivi wakati wa raha? Naambiwa kuna wengine wamepelekwa benki kulipiwa na baba zao huku wamesimamiwa na kupewa maneno makali makali.

Mwanasiasa.

Im 100% sure no one will show any sort of solidarity towards banned Daruso leaders. U keep wait and u will see....
Tuwasaidie vipi DARUSO?
 
hapo hakuna msaada,historia inajirudia na hao wote wanaweza kwenda na maji ya mto topetope.mfano kimaro,mbatia na wenzake .
 
ndio maana nasema pasipo kuwa na viongozi madhubuti hilo haliwezekani. Viongozi wenyewe waoneshe mfano hata ikibi mmoja tu aende kuketi pale au kusimama nje ya Wizara ya elimu ya juu!. Hakuna haja ya kusubiri hadi wanafunzi wote wawe pale, wale viongozi wa Daruso na wenzao 56 waanze sit ins very organized, kila siku hadi kilio chao kisikike..
 
yaani kama wanafunzi wetu wa vyuo vikuu ni waoga na wasio na msimamo isipokuwa kufuata mkumbo basi inaelezea ni kwanini tuna viongozi tulio nao!! Suala la intellectual honest halipo tena.

Mzee Es said it! Viongozi wetu ni reflection ya sisi wenyewe......
Kuna ukweli usiopingika katika maneno ya Mzee Es
 
ndio maana nasema pasipo kuwa na viongozi madhubuti hilo haliwezekani. Viongozi wenyewe waoneshe mfano hata ikibi mmoja tu aende kuketi pale au kusimama nje ya Wizara ya elimu ya juu!. Hakuna haja ya kusubiri hadi wanafunzi wote wawe pale, wale viongozi wa Daruso na wenzao 56 waanze sit ins very organized, kila siku hadi kilio chao kisikike..

Easier said than done in Tanzania.....
 
Serikali inayotumia mabavu inaweza ikawakalia wanafunzi shingoni na wasiweze kabisa kufanya chochote. Chini ya serikali ya Mao Tse Tung, kwenye miaka ya 70, mitihani na digrii viliondoloewa kwenye vyuo vikuu, na wanafunzi hawakuweza kupinga.

Serikali ya sasa ya CCM inatumia nguvu za jeshi la polisi kukandamiza wanafunzi. Inatumia vile vile wasomi wakandamizaji kama VC wa UDSM, kudhalimu wanafunzi, na kuzorotesha uhuru wa Watanzania kwa ujumla.

Kwa upande mwingine, wanafunzi wanavuna walichopanda. Wamekuwa hawamwangalii JK kwa akili. Amewadanganya mengi, nao wakawa wanamshangilia tu kama vile mtu anavyoshangilia mpira.

Wanafunzi wamepata somo la nguvu. Kuanzia hapa, watakuwa na mtizamo wa kukaa na kufikiria ni nini kinasemwa na watawala. Hawatashangilia tena bila kufikiri. Hata VC wao watakuwa wamemwona kwa ukweli kwamba anaweza kulishauri Baraza la Chuo liwatimue na kuwapa muda kidogo tu wa kuondoka, bila huruma. Na wanawaona sasa wasivyojali kabisa umasikini wao. It is a very hard lesson. The guys in their Admin Building are not "in loco parentis". They are their persecutors.

Wananchi wanapashwa kushirikiana na kuibana serikali iwarudishe wanafunzi wote, na iwape mikopo kwa asilimia 100. Fedha zipo. Makusanyo ya TRA ya mwezi 1 (260bn/-) ni zaidi ya mara tatu ya fedha ambazo serikali inatakiwa iongeze ili wanafunzi wote wapate mikopo ya kwa silimia 100.
 
MWANAKJJ mawazo yako mengine hayatekelezeki!!!!!!!! ni kama ahadi za Chama....Kwa aliyesoma Mlimani au kwa ufadhili wa serikali atakwambia kwamba mawazo yako ni mazuri mno lakini yameelekezwa kwa walengwa wasio sahihi!! Ingekuwa hivyo si hata wale wanaosoma huko Ukraine, Russia nk wangeigomea serikali..mpaka wapewe pesa? Unagoma au kufanya hayo unayoyasema ukiwa na ALTERNATIVE KAKA!!!!!! MKKJ unless hukukulia TZ! jaribu kuangalia hali halisi on the ground kabla ya kutoa mawazo ya "sit in". Tuliosoma kwa kutegema boom..tutakwambia kwamba mawazo yako hayatekelezeki!!

Nilivyofukuzwa shule those days wakati nimegoma kwa ajili ya kudai haki..niliambiwa nirudi kijijini hata nauli sikuwa nayo (Dar Es Salaam ilikuwa chungu ghafla)....wengine walitafutiwa shule ulaya..je ungetegemea nilivyorudishwa baada ya miezi sita..nigome tena? ningefukuzwa kimoja..si ningekuwa concided kwenye dustbin ya umaskini huko kijijini? nyi acheni bwana........Mtoto wa mkulima mwache aiogope serikali..kwa sababu mfumo uliopo..haumpi nafasi ya kuhoji mambo yanayomhusu..otherwise atafukuzwa shule na atakuwa inconsequential..hata MKJJ hutamtetea kwa sababu anakoishi hakufikiki either kwa mtandao au kwa usafiri...your advise is best suited kwa wanafunzi au watoto wa akina Kingunge na mhehimiwa Raisi wetu..na wala sio kwa mtoto wa fungamtama au Kalumanzira!!!
 
Mikuki, kwa haraka haraka maneno yako yana ukweli wa ndani na ni hoja madhubuti. Hata hivyo yamejaa hali ya kukata tamaa na kuweka manyanga chini. Mimi nimekulia Tanzania na nimesoma humo humo. Ninachokisema siyo kitu ambacho kiko nje ya vile vinavyowezekana. Katika Tanzania ya zamani wao kama hili nililotoa halina nafasi. Hata hivyo hii ni Tanzania mpya na mbingu na taratibu mpya za kuisukuma serikali ni lazima zianze kutumika.

Wakati Mahtama Gandhi alipoanza sit ins hakuna aliyefikiria kuwa zingechangia katika kusambaratisha himaya ya Muingereza. Watu waliaibishwa na kudharauliwa n.k lakini ilipopamba moto Waingereza walifunga virago!!

Wakati mpigania haki za raia wa Marekani Bi. Rosa Parks alipoamua kukaa kwenye sehemu ya basi ambayo ilikuwa ni kwa watu weupe tu, hakuna aliyejua kuwa ile ilikuwa ni cheche ambayo iliwasha na kukoleza harakati za kupigani haki za watu weusi! Hatimaye sheria ya Haki za Raia ya mwaka 1964 ikapitishwa!!

Wakati wanafunzi weusi walipolazimisha kuingizwa katika vyuo vikuu vilivyotengwa kule Alabama, Gavana wa Jimbo Bw. George Wallace aliapa kuwa wanafunzi hao hawataingia kwenye vyuo hivyo na alisimama mlangoni kuonesha kupinga kwake kuchanganywa wanafunzi. Wanafunzi Vivian Malone na James Hood wakisindikizwa na Polisi wa Wizara ya Sheria waliingizwa chuoni hapo. Gavana Wallace alikufa mwaka 1998 akiona Alabama ikiwa ni jimbo lenye mchanganyiko wa watu katika kila kona!

Je hili haliwezekani Tanzania? Kutowezekana kwa jambo hili na njia hii siyo kwa sababu watanzania hawatajitokeza bali bado hatujafikia mahali pa kusema "sasa inatosha" (enough is enough). Tumeendelea kusukumizwa tunachekelea, tunasukumwa tunapiga makofi, tunadharauliwa tunasema hewala!! Tumefikia mahali pa kuiogopa serikali yetu tuliyoiweka wenyewe madarakani!! NI hofu hii serikali inajua ndio maana wanaweza kusema "mtalipa asilimia 40 mtake msitake" tunabakia kunung'unika!!

Wazazi wetu wanaiogopa serikali kwani wengi wao bado wana mawazo ya "chama kimoja" na wanaona serikali ni "kitu cha kuogopwa"! Ni hawa wanafunzi ndio wanaoweza kuanza kuonesha mabadiliko!! Wao wakisukumwa wakakubali, wale wasioenda shule, wamachinga, na watu wa makundi mengine itakuwaje?

Halitekelezi siyo kwa sababu haliwezekani bali ni kwa sababu hatujapata watu wenye ujasiri wa kujaribu! Sisi ni wastaarabu mno na kugangamala mbele ya serikali tunaona ni kuvunja heshima!! Hawa viongozi wa Daruso wataendelea kuvaa tai na kutokea kwenye TV na hakuna watakachofanikiwa!! Hadi wafanye kile ambacho serikali haitarajii! Hili la kukaa chini ni mojawapo na litaiumbua serikali mbele ya wananchi na mbele ya ulimwengu! Hadi wapatikane viongozi kama kina Martin Luther ambao hawataogopwa kubebwa mzoba mzoba na kurushwa kwenye makarandinga au kufunguliwa mbwa!! Hadi wawepo viongozi walio tayari kusomea "riot act" lakini wasibabaike, watakaokubali kupigwa mabomu ya machozi!! NI kwa sababu hiyo ndiyo maana tunaona mambo haya hayawezekani!

Mimi siko nyumbani na siko shule! kama hawa wanafunzi wanafikiri kwa kuendelea kucheza ngoma inayopigwa na serikali basi watailazimisha serikali kubadili msimamo basi watachoka!! Kuna mambo mengine serikali haiwezi kufanya hadi pale inapolazimishwa, haya ya kusubiri serikali ifanye mambo kwa kupenda au kama hisani na huruma ndio yaliyotufikisha hapa tulipo!! Ninyi wana na mabinti wa Tanzania umefika wakati wekeni miguu chini na muwe na msimamo!!
 
ili kujenga mfumo imara wa elimu ya inabidi kila mmoja wetu ashiriki 'kuikandamiza' serikali ili isikilize kilio cha wanafunzi wa elimu ya juu.

Nakumbuka vyama vya siasa, vilitoa tamko kuwa kama wanafunzi wasiporejeshwa vyuoni bila masharti wataitisha mgomo nchi nzima, kuishinikiza serikali kuwatendea haki hawa wadogo zetu.

Natoa changamoto kwa wanasheria ambao nao ni wahanga wa huu mgogoro wa wanafunzi na serikali, kwani wengi wao wamepita vyuoni, kama kuna sheria imekiukwa ni vema wakajipanga ili kuiburuza serikali mahakamani.

jumuiya zisizo za kiserikali huu ni wakati muafaka kupiga kelele, Haki elimu mko wapi?

Kwa pamoja tutaweza, tukiwaachia wanafunzi peke yao wataonekana wahuni na wakorofi na watendelea kuonewa
 
Mkjj Umenena niliyowashauri baadhi ya wanafunzi wenzetu wa huko UDSM.
Pia hao waliorejea wanatakiwa kuwa na msimamo hasa viongozi waungane na hao 56 wahakikishe kwanza wanarejeshwa chuoni.Ikiwezekana waitekeleze hii mbinu kulazimisha wenzao warudi then wawe kitu kimoja sasa kuiwashia serikali moto.
Sasa hivi wafanye juhudi za kuufanya umma ujionee wenyewe huu ukandamizaji.Nilifurahi kuona TUCTA wanaingilia kati.Sasa inabidi taasisi mbalimbali ziige huu mfano.
Tatizo wanafunzi wengi ni waoga.Mimi ni kiongozi wa wanafunzi hapa na tatizo kubwa ni uoga wa wanafunzi.Serikali kama kawaida yake ni watu wa kutumia vitisho hata mabalozi wao.Pia bado wanafunzi wengi hawajui haki zao.
 
wakati mwingine inachosha hata kutoa mawazo/maoni kuhusu jambo lolote hapa TZ. Tumesema mengi sana kuhusu Vyuo vikuu na haki za wanafunzi; leo serikali inaonyesha mabavu yake kwa kufanya divide and rule, hakuna anayesema hapana akasikika. Hapa JF tuna mawazo mazuri; tunayafanyia nini? hawa viongozi wa DARUSO wanahitaji msaada wa haraka, ikiwa tuko sincere na msaada wetu basi tuweke mkakati ambao unatekelezeka; tukiambiana sisi wenyewe haitawasaidia. Hawa vijana hawaji huku JF, ni namna gani tuwasaidie na wasaidike kweli hili ndio suala la msingi. wanahitaji kurudi madarasani kama wenzao, ni kitu gani kifanyike?
Hapa ndipo hao wapinzani na taasisi za haki za binadamu wanahitajika sana. Nguvu ya pamoja. Inahitajika amri ya mahakama ya kuutaka uongozi wa chuo kuwarejesha madarasani bila masharti. Nani afungue kesi; kwa gharama ya nani; hapa ndio tunahitaji nguvu za pamoja za taasisi za kisheria na haki za binadamu. Pale UD kuna legal aid(kama bado ipo am not sure), waangalie maslahi ya hawa vijana.
Na hao Dons wa chuo niliwasoma wakisema kuwa vijana walikuwa na haki, leo wamekaa kimya.
wapinzani nao walisema yao, leo wako kimya; vijana hawaruhusiwi kuingia madarasani; and we keep on talking and talking; this talk is not going to get them back to class.
Lets get the message across to them by some means; lets urge the public to rise up against the gov..and the million dollar question still is; how on earth are going to get the popular mass rise against the govt; how are we going to get those who matter act?

Mi naona giza mbele...nani amfunge pake kengele shingoni...lets come up with a solution which can be implemented practically, not theoretically, so far we have given them the theory and it didnt get them anywhere, can we come up with something tangible?...God knows
 
yaani kama wanafunzi wetu wa vyuo vikuu ni waoga na wasio na msimamo isipokuwa kufuata mkumbo basi inaelezea ni kwanini tuna viongozi tulio nao!! Suala la intellectual honest halipo tena.


Mwanakijiji

Uongozi, ujasiri na kutokuwa mwoga hakuanzii ukiwa chuo kikuu; hayo ni malezi ambayo tunakuwa nayo...jamaii inabidi ibadilike from top to bottom.

Watawala wetu ni reflection ya wananchi; na ili mabadiliko yaje ni lazima iwe process kama hii ya kuelimisha jamii. Wengine watabadilika haraka wengine itawachukua karne....Kizazi Kijacho; watoto watakao lelewa na wakina mwanasiasa na mkjj hao ndio wataleta mabadiliko katika jamii. Hawa ambao tayari wapo chuo kikuu it's very too late. Maana hao pengine ni kama mimi niliyewahi kuambiwa na Mama yangu "usiende shule na kiatu cha gharama kuliko anachovaa mwalimu wako". 18 years later ndio naelewa alikuwa anamaanisha nini.
 
Back
Top Bottom