Just in: UDSM wafukuzwa

Just in: UDSM wafukuzwa

Hebu tuliangalie hili kwa pande zote.
1. Hawa wanafunzi wanahitaji elimu ; wanahitaji ‘msaada’ wa serikali ya CCM ili waweze kupata hiyo elimu.
2.Katika suala la migomo, kati ya serikali na DARUSO, DARUSO ndio wako katika hasara (at a disadvantaged position). Serikali imashika mpini, wao wameshika Magali, wakivuta wao ndo wanaumia wakati serikali inapela.

3. Wakati wanagoma, hakuna aliyesimama kuwatetea. Wananchi, kuanzia hapa kwenye JF kuna waliowakandia, tukadidiriki thata kusema kuwa wanafunzi wenyewe wanaishia kwenye mabaa na madisko. Huko mitaani ndo kabisa hawakueleweka.
Ni baada ya wao kutimuliwa na dada zetu kuwa matatani ndo vyama vya upinzani wamesikika, na juzi tu ndo Dons wa Versity nao wakajitia kuwasupport. Hawa Dons ndo waliokuwaga wa kwanza kutoa tamko mara wanafunzi wanpaofukuzwa, leo wamesubiri kimbunga kimepita na vyama vya upinzani wameanza kujikusanya, ndo na wao tunawasikia.

4. Hawa wanafunzi, tupende tusiopende, ni mtaji kwa vyama vya siasa, be it CCM au wapinzani. Kila upande unawatumia kwa manufaa yao. Kumbuka ni majuzi tu CCM iliweka mkakati wa kufungua matawi katika vyuo vikuu. Wapinzani wakalivalia njuga, lakini nao katika hili nao wanaonekana kulifuatilia kwa namna Ambato itawasaidia wao, sio wanafunzi. Ikiwa walikuwa na nia ya kuwasaidia kikwelikweli walipaswa kujua kuwa hao wanafunzi walikuwa wanatakiwa kufanya mitihani mapema mwezi huu, na kwamba kufukuzwa kwao ni hasar asio tu kwao wao wanafunzi bali kwa Taifa mabalo linaishia kupata graduates fake, maana ili wasifeli watafanya biashara na mitihani hiyo ili tu wa-graduate. Wapinzani walijua sheria z anchi, wana wanasheria, walikuwa na uwezo wa kufungua kesi mahakamani mapema yalipotokea ili itolewe amri ya kuwarejesha wanafunzi madarasani. Lakini cha kushangaza waliendelea na vikao vyao ambavyo iliripotiwa kuwa vingime vilikuwa vikifanyika kwenye mabaa n ama-Don wa vyuo, sio viongozi wa DARUSO.
CCM nao hali wakijua kuwa sasa hili suala la wanfunzi limekuwa barata, wakaamua kuwazidi kete wapinzani kwa kutumia mbinu zao za medani, wakawaingia viongozi wa DARUSO kuwa hapa lazima muandike barua kuomba radhi, na sisi tutafanya yaliyobaki.
Sasa kwa barua hii wanafunzi wametumika kuwafunga wapinzani mdomo.
CCM ambao walikuwa mstari wa mbele kuwalaumu wapinzani kwa kutumia huo mgomo kama suala la kampeni wao ndo wameutumia kisawasawa. Nani anaumia?

5. Nini nafasi ya wazazi/wananchi katika hili.
Wale wanafunzi ni watoto/ndugu/rafiki zetu; wametoka katika jamii yetu; leo kwao kesho kwa wengine, ambao nao ni watoto/ndugu zetu. Hawa sio wakenye wala waganda, ni Watanzania wenzetu; uko wapi mshikamano wa wananchi katika hili. Imeonekana kama hawa wanafunzi ni wasaliti wakati wanatetea haki zao na kujaribu kuwapunguzia mzigo wazazi wetu.
Tumesoma mapato yaliyokusanywa na TRA, ni kodi zetu; yet inapokuja suala la kuzirudisha kwa jamii kama huduma muhimu serikali inajifanya hiyo ni favour. Bila aibu CCM na seriali yake inachota fedha hizo kama ruzuku;; ikifika wakati wa kampeni za uchaguzi wanachota kutoka kila idara, taasisi na ofisi ya umma; hiyo sio siri, ni situ kilo wazi; fedha halali za matumizi ya umma zinachotwa kwa ajili ya kampeni za CCM. Leo imekuwa vigumu kuzichota kuwapatia wanetu elimu amabayo hata sio kwa manufaa yao binafsi, bali ya Taifa.

6. Historia ya migomo vyuo vikuu inaonyesha wanaoumia ni viongozi wa DARUSO au wa migomo as the case may be. Hakuna mmoja wao ambaye hakuona joto ya jiwe haswa ile mogomo imara. Mbatia, Kaishozi na wenzao watakumbuka vizuri. Wakati wanafunzi wengine wanaruhusiwa kuendelea kusoma wao walifungiwa kusoma chuo chochote for some years, mpaka Mbatia akaamua kuingia zake upinzani jumala wakati Kaishozi alikuja rudia chuo na watoto wa nyuma yake sana baada ya kifungo chake baridi kuisha.
Ikifikia hapo linakuwa suala la ‘everybody for himself and God for us all’
Sitawalaumu uongozi wa DARUSO kwa kuomba radhi bila kufikiria yote haya , na hasa kujiuliza ni nini kiliendelea behind the scenes ambacho kimepelekea wao kuandika barua katika wakati ambao wapinzani na uongozi wa waalimu umeanza kuwasupport.
 
Hawa wanafunzi wa Udsm ni wababaishaji na huu mgomo umeandaliwa na Fikiraduni na Mwanasiasa.
walipoanza term kila kitu kilikuwa kinajieleza kuwa watapa kiasi gani? kama wagomaji genuine ilitakiwa wagome in the first place, leo wameona kuna mitihani na kichwani watupu kama FD na Mwanasiasa wakajua wanafeli ndio wakaleta balaa hili la kugoma.
Hivi nyinyi mnagoma wakati wenzenu wa Mzumbe wanakula buku kama wendawazimu.
Mlimani kuna precedence ya Mbatia na kundi lao. ikikaribia mitihani na mkijua mnafeli basi mnaanzisha migomo.
wewe mbatia shule huna unatoa kauli za kuchochea vurugu unataka wenzako nao wawe form six kama wewe?

Serikali.

Shekeni uzi huo huo hakuna kuwaachia hawa wajinga, wakati wao wanafanya ujinga wao Mzumbe University inazidi kufanya kweli juzi wametuwakilisha kwenye mashindano ya Celtel na wamewapiga bao Makelele (Oxford ya Africa).
 
Wewe Kichuguu ndio nani humu? kuna kipindi ulimkosoa Mjengwa na Blog yake. na Yakub nawe unamuelekeza wewe ni nani humu?

Mtindo alikuwa akitumia Mjengwa na sasa Yakub mie naupenda. Ndugu yetu Mwanakjj anautumia mbona husemi kitu?

wao wamefanya kazi na wanatuambia twende kwenye Blog zao. wewe unawapa kazi nyingine ya kuandika upya humu. nini maana ya Link?
au wewe ni nyapara humu JF?

Naona hukuwatendea haki Mjengwa na Yakub wewe si admin ni graduate wa Mlimani tu! full stop.

ifanyike kura humu sisi wa JF tuamue mtindo upi utumike sio dikteta mmoja kujifanya Nyapara ndani ya JF.

Wanafunzi wa Udsm waliogoma ni sababu ya kuogopa mitihani kufeli walikuwa wapi siku zote? wanaona term inaisha ndio wanakuja na gea ya kugoma.

fundisheni vizuri vijana wenu wasiwe waoga wa mitihani. ujinga huu wa kugoma aliuanzisha Mbatia na Haroun kimario hawa walikuwa watupu darasani na mitihani ilipokaribia wakamua kuanzisha migomo.

watu wa criminal Law (vitu vya mzee Lubengo pale Mzumbe) wana kitu kinaitwa cooling period. huwezi kutukanwa na mtu leo may na mkakaa na huyu mtu ikifika december ukampiga huyo aliyekutukana ukapelekwa mahakani ukijaribu kujitetea kuwa ulikuwa proved kwa yale matusi uliyotukanwa mei na sasa desemba hakimu hasikilizi ushahidi wako una kwenda jela tu.
contract law nayo itakuwa na kanuni zake. cheki upewe leo ukae miezi sita ukai depost? mlikuwa wapi Mlimani kugoma in the first place? mnagoma leo kwenye mitihani?
poleni sana.
JK hakuna kuweka huruma kwa wajinga hawa.
 
Nungwi,

Kuna link na link: Tatizo ni link zinazokwenda kwenye blogs za watu binafsi. Yaani mtu ana blogu yake ambayo vile vile ni forum inayohost majadiliano pale halafu anatumia forum hii kuvuta wachangiaji wa blogu yake. Katika mfumo huo, forum hii inakuwa inatumika kama bomba la kuvuta watu kwenye mada zilizo kwenye blogu nyingine. Swala hili liliwahi kuzungumzwa huko nyuma na ndipo admin akaamua kuazisha folder hii hapa kwa ajili ya kuhudumia mada zinazotakana na blogu za watu binafsi.

Kuhusu mchango wako kuhusiana na mgomo wa chuo kikuu nimekusikia na huwa najua tatizo lako na chuo kikuu cha Dar es Salaam. Kwako wewe, wanafunzi wote wa UDSM na SUA pamoja na vyuo vyake vishiriki vyote ni waoga wa mitihani. Kweli wewe unajua sana kuchambua mambo. Hujui kuwa Mwalimu Nyerere aliwahi kugomewa na wanafunzi wa chuo kikuu siku nyingi sana kabla ya Mbatia na Kimaro hawajingia pale chuoni; Jaji Waryoba mwenyewe aliwahi kuendesha mgomo wakati akiwa mwanafunzi wa pale UDSM. Angalia tena hiyo theory yako juu ya migomo ya wanafunzi.
 
Nungwi na Kichuguu;
naona humu ndani mnataka kuleta matabaka ya vyuo kitu ambacho hakitatupeleka wala kutusaidia chochote naona tujadili issue badala ya u UDSM, uMzumbe na USUAism humu ndani. Let us discuss issue for the benefit of our nation and our people. Wote ni wasomi tuu hoja zako zitasaidia bila kujali umesoma Mzumbe, UDSM, Oxford wala wapi hayo mambo ya uchuo hayana maana. That is my advice to you guyz.
 
Duh! hapa iko kazi. habari nilizosikia asubuhi radioni zinasema viongozi wa mgomo watafukuzwa au kusimamishwa. Kumbe bado DARUSO nao wako kidete kutetea mgomo. No wonder tishio la kufukuza viongozi limetolewa

Daruso disowns statement on students` crisis

2007-05-04 09:25:35
By Christina Mwangosi


In a dramatic turn, the Dar es Salaam University Students Organization (Daruso) yesterday disowned a statement made by the Tanzania Higher Learning Institutions Students` Organization (Tahliso) to the effect that the suspended students have apologized to the government.

Daruso also rejected the view given by Tahliso that the students’ strike was both wrong and illegal.

``The strike was legal…and the students have not apologized to the government.

We have not succumbed to the government`s stance,`` said Daruso President Daudi Deo in an interview with The Guardian yesterday.

He said university students organizations recently met under the umbrella of Tahliso, and agreed to write a letter of apology to President Jakaya Kikwete and other people who were insulted and damaged by the outcome of the legal strike through billboards, placards, and posters.

``We want to apologize to people whose reputation had been affected by the outcome of the strike…but that does not mean the strike was wrong and illegal,`` he said.

``Our grievances are still genuine. It was not our intention to insult anybody,`` he added.

The Daruso President said Tahliso had overlooked critical issues of the entire controversy and come up with different issues contrary to the recent universities students` organizations meeting.

In what appeared to be students bowing to government conditions, Tahliso said in its statement that the suspended students had apologized to the government and that the strike was a wrong and improper approach of resolving the problem.

``We appeal to the government to forgive all students who took part in the strike,`` read part of the statement.

The students` organizations` apex body had also warned political parties against using the strike in advancing their political interests.

But the Daruso president disagreed with the official Tahliso position saying: ``The idea when we sat as Tahliso was to write a letter of apology to President Kikwete. We agreed on this because Daruso was unable to control emotional and disturbed students who designed placards that carried insulting messages during the strike.``

Deo said they had planned to include genuine students` demands in the letter to the President rather than letting him receive students` complaints through the media.

``We had agreed to send a formal request to meet with the President and discuss problems in higher learning institutions,`` he added.

He said Daruso did not meet with Tahliso office bearers and agree to apologize to the government in relation to the strike as claimed by the students organizations` apex body.

``Daruso did not say the strike was wrong…the strike was legal,`` said Deo.

He blamed Tahliso for contradicting issues and calling a press conference that revealed different facts to the public.

In accordance with the country`s constitution, he said, Tahliso has no mandate to refrain anybody students, student organizations or political parties from pressing for other peoples` rights or voicing out against any misconduct.

``Daruso called on the public to help the students out of the problems. We did not single out specific political parties or politicians…it was a call for all Tanzanians,`` he said.

Daruso according to the student leader, was still readily available to defend students who would not manage to pay the 40 per cent contribution as required by the university management.

The organization wants the government to allow back all suspended students regardless of their financial position, taking into account the prevailing level of poverty facing majority of families.

SOURCE: Guardian
 
Kichuguu, nakuhurumia sana maana hayo mambo unayoyaeleza kwa nungwi ni mazito mno kwa yeye kuyabeba! Sisi humu wenzako tulisha-give up siku nyingi hadi pakawa na terminology ya unungwi!
 
Hawa wanafunzi wa Udsm ni wababaishaji na huu mgomo umeandaliwa na Fikiraduni na Mwanasiasa.

Really? Nungwi unaweza ukajitahidi zaidi ya hapa mwanangu! Nakutakia kazi njema hapo "Oxford of Africa"!
 
nungwi, you are really a pain in the neck.haya bwana may ur mzumbe intelect take u far.
 
Nungwi na Kichuguu;
naona humu ndani mnataka kuleta matabaka ya vyuo kitu ambacho hakitatupeleka wala kutusaidia chochote naona tujadili issue badala ya u UDSM, uMzumbe na USUAism humu ndani. Let us discuss issue for the benefit of our nation and our people. Wote ni wasomi tuu hoja zako zitasaidia bila kujali umesoma Mzumbe, UDSM, Oxford wala wapi hayo mambo ya uchuo hayana maana. That is my advice to you guyz.

Mtoto wa Mkulima,

Nadhani hii ulikuwa umemwelekezea Nungwi, ila jina langu limeingia pale kwa makosa kwa vile sijazungumzia ubora wa chuo chochote katika mada hii. Hebu pitia posts zangu tena.
 
what on earth is Tahliso.... na jinsi gani walihusika na mgomo? kuna uhusiano gani kati ya Daruso na hiyo tahliso?
 
Cellphone?
Ya Nyumbani?
Ofisini!

Na kuna mtu ana namba ya Mama Katunzi?

Cell
Nyumbani..

Mwenye hizo namba nipenyezeeni kwenye PM jamani!! why is this guy so "unreachable"!!!?


Hawa watu wawili itabidi wawajibu Watanzania kwanini wamekuwa so incompetent, indifference to the plight of our children in HLIs, and why they shouldn't render their resignation immediately for their gross negligence, arrogance, and total mediocrity in their management of the current crisis in our universities and colleges. Mr. President please do us a favor, fire them or just give Msolla that ambassadorial post that has just opened in Ethiopia!! We'll forgive you for recycling him there.... !! grrrrrrr!!
 
Tanzania, resignation is a foreign terminology!!!! What you can do, just cut the chess with Muungwana and dont waste your time with Msolla or mama Katunzi...
 
Mikuki.. JK.. nilizungumza naye mwishoni mwa mwaka jana. Nikaomba kufanya naye mazungumzo kuhusu mambo mbalimbali yanayoendelea nchini (ilikuwa wakati suala la Richmond limeiva). Kwa maneno yake mwenyewe alinikubalia na akaniambia nizungumze na watu wa ofisi yake. Nikamwandikia mmoja wa waandishi wake waandamizi (ambaye tuna mawasiliano) lakini hakunijibu. Na yeye mwenyewe Rais aliniambia kuwa atawaambia hao ili wapange itakuwa vipi. Sasa ni miezi sita baadaye hakuna aliyetayari kufanya mazungumzo hayo yawe kweli....

In that case, I still need to talk to Msolla, nimwache Rais aendelee na shughuli zake, hili la Elimu ya Juu ni la Msolla na tutaendelea kukabana naye hadi ajiuzulu, aondolewe, au aumbuliwe kwa uzembe, kukosa uwezo wa kuongoza na kusimamia wizara muhimu kama hiyo.. !!
 
Ndugu zangu wahusika wa baraza hili, ningeliomba thread hii pamoja na ile ya Msola zipelekwe katika ile thread ya chuo kikuu kufungwa ili tuweze kuchangia utaratibu mzuri na rahisi.

Samahani kwa kuwasumbua isipokuwa wengine tusingependa kuripuka tuu na kutoa maumivu yetu moyoni bali tungependa kutoa mawazo ambayo yatakuwa na matunda.
 
Hivi ni kweli ama ninaota.

Nimetoa ombi chini ya masaa mawili na tayari kuna mabadiliko. Kweli hii inatia moyo. Hivyo tutakavyoweza kujenga jamii yetu badala ya kujisimika katika kutowa machungu yetu tuuuuu.

Hongera administrators.


Tanzanianjema
 
wanafunzi warejeshwa chuo.

41.2 watimiza masharti. Wengine watakiwa kulipa kabla ya mwaka wa masomo kuanza.

vinara 56 watajwa na kutakiwa kutoa maelezo ya ziada juu ya mgomo
 
Back
Top Bottom