sonofobia
JF-Expert Member
- Jun 21, 2015
- 1,249
- 4,537
Nimesikitishwa na taarifa hii ya Chama ,pamoja na kutolewa kwa kuchelewa sana ,masikitio yangu yanatokana na mambo yafuatayo;
1. Chama hakikuona haja ya kulaani tukio la kiongozi wa wanawake taifa kupigwa na kuumizwa ,kipigo kilichotolewa na Mwanaume,bali kinasema ni taarifa zinazosambazwa mtandaoni .
2. Chama hakikutoa pole kwa mgonjwa ,mbona kinatoa pole hata kwa viongozi wa CCM wanapopatwa na majanga ? Huu uadui wa kushindwa kumpa pole kiongozi umeanza lini?
3.;Chama kinamtishia mgonjwa na kumpangia nani wakumpa faraja na nani hatakiwi kwenda kumpa faraja .Nani amchangie ,wakati huohuo hakijaonyesha kuwa kipo tayari kuwezesha matibabu yake .
4. Chama kinasema kinaendelea na uchunguzi ,sasa kama kinachunguza kwanini kinatoa vitisho kwa mgonjwa? Hivi mgonjwa anayetishiwa atatoa ushirikiano kwenye huo uchunguzi ? Kinachunguza jambo ambalo kinasema ni 'tuhuma za mtandaoni'
5.;Kauli za kikatili kama hizi nilizoea kuzisikia wakati wa Mwendazake ,walupopotea watu tuliambiwa tujikite kwenye maendeleo kwani wapo wanaokwamisha .....kumbuka kauli dhidi ya Ben Saanane,Azwory,Kanguye na wengineo wengi .
Nalaani kitendo cha kiongozi wa Wanawake kupigwa na wanaume ,huu ni ukatili wa kijinsia na unapaswa kupingwa na kila mtu mstaarabu bila kujali nani katendewa ukatili huo .
Ukatili huu hauna tofauti na ukatili unaofanywa kwa wanawake wengine nchini ,tuungane kuupinga ,kuukemea na kutokimeza matendo ya kikatili katika vyama vya siasa na nje ya vyama vya siasa .
Eid Mubarak .
Source: Ukurasa wa X
1. Chama hakikuona haja ya kulaani tukio la kiongozi wa wanawake taifa kupigwa na kuumizwa ,kipigo kilichotolewa na Mwanaume,bali kinasema ni taarifa zinazosambazwa mtandaoni .
2. Chama hakikutoa pole kwa mgonjwa ,mbona kinatoa pole hata kwa viongozi wa CCM wanapopatwa na majanga ? Huu uadui wa kushindwa kumpa pole kiongozi umeanza lini?
3.;Chama kinamtishia mgonjwa na kumpangia nani wakumpa faraja na nani hatakiwi kwenda kumpa faraja .Nani amchangie ,wakati huohuo hakijaonyesha kuwa kipo tayari kuwezesha matibabu yake .
4. Chama kinasema kinaendelea na uchunguzi ,sasa kama kinachunguza kwanini kinatoa vitisho kwa mgonjwa? Hivi mgonjwa anayetishiwa atatoa ushirikiano kwenye huo uchunguzi ? Kinachunguza jambo ambalo kinasema ni 'tuhuma za mtandaoni'
5.;Kauli za kikatili kama hizi nilizoea kuzisikia wakati wa Mwendazake ,walupopotea watu tuliambiwa tujikite kwenye maendeleo kwani wapo wanaokwamisha .....kumbuka kauli dhidi ya Ben Saanane,Azwory,Kanguye na wengineo wengi .
Nalaani kitendo cha kiongozi wa Wanawake kupigwa na wanaume ,huu ni ukatili wa kijinsia na unapaswa kupingwa na kila mtu mstaarabu bila kujali nani katendewa ukatili huo .
Ukatili huu hauna tofauti na ukatili unaofanywa kwa wanawake wengine nchini ,tuungane kuupinga ,kuukemea na kutokimeza matendo ya kikatili katika vyama vya siasa na nje ya vyama vya siasa .
Eid Mubarak .
Source: Ukurasa wa X