John Heche: Hakuna sheria inayozuia mtu kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine ndani ya Tanzania. Ni Udikteta.

John Heche: Hakuna sheria inayozuia mtu kutoka mkoa mmoja kwenda mkoa mwingine ndani ya Tanzania. Ni Udikteta.

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
24,143
Reaction score
56,407
Nchi hii hakuna sheria wala utaratibu wa polisi kupangia mtu aende wapi, au asiende wapi..

Polisi Tanzania hawana mamlaka kisheria wala kikatiba kuingilia uhuru wa watu kwenda wanapotaka wao wenyewe..

Polisi Nchi nzima wameweka barriers wanakamata viongozi na wanachama wa Bawacha waliokua wanaenda Musoma kusherekea Siku ya wanawake Duniani.

Magari yaliyobeba viongozi hawa yanakamatwa na wanashikikiwa maeneo mbalimbali ya Nchi bila sababu… Dakawa, Mlandizi, Geita na maeneo mengine.

Hili jaribio la kuzia watu kufanya movement ndani ya Nchi na kuzia watu kufanya shughuli zao halali, Wengine wanaweza kufikiri litaishia kwa Chadema..

Tukiruhusu madikteta wachache wao ndio waamue, wapi twende wakati gani, tule au tusile, tulale au tukeshe itakua hatari kubwa mno..

Uhuru uliopiganiwa na wazee wetu hauna maana tena katika mazingira haya.
 
Hii nchi inakoelekea ni sawa na Ayatollah alikoipeleka Iran, kuna siku mpaka tutalazimishwa tuvae nini, tuvae namna gani, tule namna gani, tujisaidie vipi, sawa na alipokuwa amewafikisha Wairan yule Ayatollah.
 
Haya matahila yanaipa CHADEMA AIRTIME NA pia kupata huruma ya wananchi bila wao kujua....
 
Tii amri za mahakama ambayo nyie wenyewe mlishitakiana huko
Walishitakiana ama walitumika na serekali kuwashitaki waliongia madarakani ili kuwakomoa? Kama ni kesi kweli na sio kutumia sheria kama dhana ya kukomoa, mbona kesi haiishi wakati ushahidi wote upo?
 
Kuna amri ya mahakama inazuia watu wasitoke eneo moja kwenda eneo lingine!!???
Unapokua uko nje kwa dhamana mahakama hutoa sharti la kutokutoka nje ya mkoa husika bila kuitaarifu Mahakama . Huwa iko hivyo miaka yote
 
Nchi hii hakuna sheria wala utaratibu wa polisi kupangia mtu aende wapi, au asiende wapi..

Polisi Tanzania hawana mamlaka kisheria wala kikatiba kuingilia uhuru wa watu kwenda wanapotaka wao wenyewe..

Polisi Nchi nzima wameweka barriers wanakamata viongozi na wanachama wa Bawacha waliokua wanaenda Musoma kusherekea Siku ya wanawake Duniani.

Magari yaliyobeba viongozi hawa yanakamatwa na wanashikikiwa maeneo mbalimbali ya Nchi bila sababu… Dakawa, Mlandizi, Geita na maeneo mengine.

Hili jaribio la kuzia watu kufanya movement ndani ya Nchi na kuzia watu kufanya shughuli zao halali, Wengine wanaweza kufikiri litaishia kwa Chadema..

Tukiruhusu madikteta wachache wao ndio waamue, wapi twende wakati gani, tule au tusile, tulale au tukeshe itakua hatari kubwa mno..

Uhuru uliopiganiwa na wazee wetu hauna maana tena katika mazingira haya.
Tukiruhusu madikteta wachache wao ndio waamue, wapi twende wakati gani, tule au tusile, tulale au tukeshe itakua hatari kubwa mno..
 
Viongozi wetu kusema ukweli huwa wanapenda kuzua taharuki tu wanahaingaika na vitu vya kipuuzi
Na wakipoteza kujadili mambo yasio na msingi Nchi inabaki pale pale siasa yetu imekua ya hovyo sana..
 
Back
Top Bottom