JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

Wakuu naomba tusipuuze hizi taarifa alizoleta bwana Makoye2009 hata mimi hapo jana nikiwa nimekaa karibu na watu ambao si watu wa kuwabeza ni watu wazima na wabusara tena wako katika sekta za serikalini nilikua nawasikia wakiwa wanabadilishana mawazo kuusiana na hili sakata la waziri Pinda kua JK amekanusha hizi taarifa za posho kwa wabunge, lakini kuna kitu nikakisikia kutoka kwa hawa mabwana kua kutaweza kutokea maamuzi ya ghafla na yasiyotarajiwa kutoka kwa waziri Pinda au kutoka kwa mkuu wa nchi! Jamani lisemwalo lipo! Na kama halipo basi laja! Mungu ibariki Tanzania.
 
bora hata Pinda, maana mawazir wakuu wangapi walifanya madudu na wakapetaaa?

Wala Pinda hana ubora wowote,...sema nachojua ni kwamba akikalishwa kitimoto atalia,..ili watu wamuonee huruma.....kubwa jinga.
 
Walahi si kikwete anaweza kumfurusha pinda,labda mwingine.bt wy huyu bwana asiwajibike kwa kuudanganya umma na bunge,mana kwa kauli ya pinda LUSINDE NA RAGE walishachekelea
 
Maaskofu...................Mungu gani aliewaambia kua huyu jamaaa ndo chaguo lake?
 
Hamtambui siasa,, cdm mmejifunga goli wenyewe na kama hamuamini utafika wakati muone repray ya hii sakata mtaniambia, jk ni mtu makini sana na mjanja sana. Tusubiri muone
Spika: mmekubaliana mabadiliko yaliyofanywa na cdm?
Ccm: Ndiyoooooo
 
Watakaorudi kwenye baraza la mawaziri ni hawa:
Bernad membe,john magufuli,aggrey mwanri,prof tibaijuka,kagasheki,lukuvi,omari nundu,nyalandu.wapya wanaopaswa kuingia ni anne kilango,mwigulu nchemba,zakia meghji(fedha),said mtanda,livingstone lusinde,steven masele
Yeuuuwiiiii LUSINDE, MWIGULU nchi itaangamizwa kama sodoma na Gomora kwa uzinzi wa hizi mtu
 
Kwahiyo?? yupo na watendaji gani?
Pinda na Makinda hawa hawa aliowakana?
Watamwambia nini?
Au yupo na Ndugai......Bwana posho!!

Mkuu hapo kwenye red umenichekesha sana ila hilo jina ndio linamfaa!!
 
Lakini kama tunakumbuka, kuna taarifa zilivuja kwamba katika mkutano wake wa kwanza na Chadema, Rais aliwaeleza kwamba analifahamu fika suala wanalolizungumza Chadema lakini akifanya tofauti na maamuzi ya wabunge wa CCM, wabunge wa CCM pamoja na CCM kwa ujumla hawatamwelewa. Kwahiyo sio kweli kwamba Rais hakuwa makini kujua kilichojiri ndani ya muswada. Nadhani ni sahihi zaidi kusema kwamba, awali Rais alitawaliwa na uwoga juu ya kukubaliana na hoja za Chadema, jambo ambalo katika kikao chake na Chadema cha mara ya pili, ameamua liwalo liwe.

Mchambuzi itasaidia kama utaliangalia hili kialisia na kuacha kumtetea kiongozi wako wa kichama na nchi. Bill aitoki mbinguni kwenda bungeni kujadiliwa na mpaka hapa walipo kutaka kuipigia kura hiwe sheria ujue ni kwamba imepitia process ndefu sana. Sasa embu jiulize ni nani aliepeleka hii bill bungeni (ilianza kama a private motion au ilikuwa ni ya serikali). Kwakuwa imetoka upande wa serikali regardless nani kaianzisha na inahusiano na matumizi yetu wizara husika ilitakiwa itambue hili mapema sana.

Embu sasa jiulize hii kitu imepitia process gani mpaka kufikia hapo ilipo na raisi kakosa vipi information ya bill muhimu kama hiyo ambayo imeanzishwa na serikali yake au mwanachama wake mpaka imefikia hatua ya kutaka kupigiwa kura bungeni. We uoni kama Mr.President ni mzembe na hajui mengi sana yanayoendelea chini yake, surely mtu hawenzi jianzia expensive bills without his blessing mpaka hapa hilipo, kama alijua implications za hii bill in the first place ana madaraka ya kuizuia hata isifike bungeni, kumbuka yeye ndio Mr.President na kiongozi wa chama kinacho ongoza taifa ana mikono mirefu pande zote mbili.

My take ni kwamba ni muongo he knew all along isipokuwa ime-back-fire sasa anataka kuikana for the sake of his popularity. Kwanini nasema hivi waziri mkuu sidhani kama angeweza jiropokea kwenye umma na kumtaja raisi kama kweli hakujua, isipokuwa sasa tu ndio anatafuta mlango wa kucholopokea.

Worst off Spika wa Bunge anasema watu wameshaanza kupokea hizo posho since novemeber, kama muswaada ndio unataka kupigiwa kura sasa ni nani alieidhinsha wabunge kulipwa kama bunge lilikuwa bado hata alijapiga kura za kuridhia iwe sheria. Talk about political satire maana raisi pengine muongo (siamini kama alikua alijui hili) au labda aheshimiki na subordinates wake maana huko ni watu kujianzia tu ndio maana ana ukana leo huo muswada, Spika mlopokaji asiejua hata kauli zake zinakingana na simple roles of the house he runs. The PM is a joke kazi kutumiwa na kubadilikiwa mambo yanapoenda mrama. Thats Tanzania for you.
 
Baada ya kuona habari iliyoanzishwa na makoye2009 kwenye jamii forums kwamba kuna tetesi baraza la mawaziri linaweza kuvunjwa ili kuunda jipya, nimeona na mimi nionyeshe nia ya kumuomba Mh. Raisi wan chi tetesi hiyo iwe habari kwa haraka itakavyowezekana na itakapokupendeza.


Mh. Rais, kutokana na hali halisi ni maoni yangu kuwa watanzania wengi kwa sasa hawarizishwi na hali ya serikali inavyokwenda. Mh. Raisi Mimi kama mwananchi wa Tanzania napita kwenye mitaa mingi zaidi yako wewe kutokana na kazi yako ya urais na hiyo ndio hali halisi. Ndiyo maana kuna mwanamuziki wa bongo flavor katika beti ya wimbo wake anamwambia mwanao akueleze ya kuwa mtaaani hakufai hali ni mbaya.

Mh. Raisi, Hali hii mbaya haijatokea tu kwa sababu mungu hataki Tanzania yenye neema iwanufaishe wananchi wake bali ni zimwi la wasaidizi wako ambao hawataki kuwajibika ipasavyo kwa wananchi na hivyo kuzorotesha utendaji wa serikali kwa ujumla.

Mh. Raisi sasa imekuwa ni kawaida kuona maagizo yako hayatekelezwi, mawarizi wako wanapingana hadharani, wanabezana na kupoteza rasilimali za nchi kwa mikutano na vikao visivyokuwa na tija kwa taifa.


Mh. Raisi, Mwanafalsafa Niccolò Machiavelli (1469 - 1527) amewahi kusema “The first method for estimating the intelligence of a ruler is to look at the men he has around him.” Falsafa hii Mh. Rais inaelekea kufika katika ikulu yako, kiasi kwamba taasisi yako inaonekana ina ombwe kwasababu tu watendaji wako hawawajibiki kwa wananchi. Mh. Raisi mteule wako asipowajibika sahihisho pekee ni kumuwajibisha kabla hajafanya taasisi yako kudharauliwa.

Mh. Raisi kwa sas nchi sio kwamba inayumba bali nchi inakosa mwamuzi wa mwisho wa hatma ya watanzania ambayo ipo mikononi mwako. Tunajua mwaka huu umeanza vizuri kwa kukubali mapendekezo ya wadau wa katiba na kukataa ongezeko la posho za wabunge, sasa hivi wananchi wangependa kuona wanaoharibu serikali wanawajibishwa.

Mh. Raisi, waswahili wanasema ukiona kobe kainama ujue anatunga sheriaza. Nikiuliza swali kwenye taasisi unayoingoza Je bado unatunga sheria? Nadhani wakati wa kuona nguvu ya raisi ikichukua mkondo wake umefika kwasababu unayo dola ya kutumia kutekeleza matakwa ya watanzania.

Mh. Raisi wakati umefika wa kauli mbiu kama ile ya Tanzania bila ukimwi inawezekana sasa ya Tanzania bila baraza la mawaziri legelege inawezekana.

Wako Katika Ujenzi wa Taifa.

Mwananchi.
 
Angekua anasoma hoja za humu ndni JF nchi isingekua hapa ilipo sijui ni kiburi au dharau
mkuu umeelewekw sana sijui yeye kama atakuelewa
 
Mawaziri wamekosa nini? Acha kupindisha issues! Mkuu wao ndo aachie. Mbona waziri wa Italy aliachia kiutu uzima kunusuru watu wake. yeye vipi.
 
Kuna kikao cha waziri mkuu na mawaziri kinaendelea katika ofisi za TAMISEMI Dodoma, pengine tutapata suluhisho la mgomo wa madaktari na wabunge!
 
Back
Top Bottom