JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

JK na wabunge wa CCM Dodoma kimenuka

Amuoaye mama yako ni baba yako. JK afanye maamuzi magumu na asiogope. mimi niko nyuma yake. Pinda hafai kuwa PM kwa kuwa hajiamini.
 
bora hata Pinda, maana mawazir wakuu wangapi walifanya madudu na wakapetaaa?
 
mafaili mengi ya yako kwa kikwete toka TISS lakini hayafanyii kazi....ni mbishi sana huyo rais....anaivuruga nchi sana...hana maana
 
Natamani kuona watachangia nini bungeni
 
Safi sana wameamua kuufyata, masrahi ya Taifa mbele sio masrahi ya matumbo yao wabunge wa CCM.
 
Kuna tetesi kuwa huenda yale yaliyotokea mwaka 2008 yakajirudia tena. Safari hii mtoto wa Mkulima Mizengo Kayanza Peter Pinda Waziri Mkuu anaachia ngazi ya Uwaziri Mkuu baada ya tuhuma nzito tatu(3)zinazomkabili katika ofisi hiyo nyeti.
  1. Mizengo Pinda anatuhumiwa kuwa kwa kushirikiana na spika wa Bunge Anne Makinda AMELIDANGANYA BUNGE KUHUSU POSHO ZA VIKAO ZA WABUNGE KUWA RAIS KIWETE ALIKUWA AMERIDHIA NYONGEZA HIYO YA POSHO KUTOKA SHS.70,000/= MPAKA SHS.200,000/=kitu ambacho siyo kweli.
  2. Mizengo Pinda akishirikiana na Waziri wa Afya na NAIBU wake anatuhumiwa kushindwa kusimamia ipasavyo ili kuepusha au kuzuia MGOMO WA MADAKTARI MUHIMBILI MGOMO AMBAO HATIMAYE ULIPELEKEA MGOMO WA MADAKTARI NCHI NZIMA.
  3. Mizengo Pinda kama Mkuu wa shughuli za Serikali Bungeni ameonyesha UDHAIFU mkubwa kwa kushindwa kuwasimamia Wabunge wa CCM ambao wametishia kupiga KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NA RAIS WAO Kiwete na pia kutishia KUPINGA MSWADA WA KATIBA MPYA YA JMT.
Kwa mwenye habari za undani zaidi kuhusu hizi tetesi naomba aendelee kutupasha zaidi.

Nawasilisha
Hizi tetesi hizi...!

Hili la posho labda amfukuze kwa kushindwa kutumia busara....maana maagizo yake illikuwa busara itumike bila kusema hiyo busara katika suala husika ni nini! Hilo la madaktari asipoangalia hata yeye linaweza kumshinda....na kwa mbaaaali yale yaliyotokea tunisia, masr na kwengineko yanaanza kupata kasi hapa kwetu. Wanaweza kupata suluhu ya haraka kama wataanza kwa kuisambaratisha wizara ya afya na kutengeneza upya.
 
Mm sijaelewa mantiki ya kchwa cha habari na habari yenyewe.

Na hautaelewa kamwe make tangia uko shuleni maswali rahisi sana yalikuwa yakisumbua.Sasa kwa hili suala wewe utakuwa umedandia kitu ambacho akiri yako haina uwezo wa kukijadili.Wewe kwako ni taarabu tuuuu!!!.
 
he he he politics is a dirty game...nothing is going to change
 
hivi hili la wabunge wa ccm kutaka kupiga kura ya kutokua na Imani na raisi umelipata wapi jombaa.
 
Panda ataendelea ili kukwepa mzigo wa kulea wastaafu
 
Ukinipiga umenionea!!! Ukiniacha
umeniogopa!!!! Wabunge wa ccm njia panda
 
hawa jk atawadanganya kuwa atasaign posho kisha wataupitisha na itakuwa imekula kwao vilaza hawa

umenifurahisha sana inaelekea huyu bwana unamfahamu vizuri,natamani awapige mchanga wa macho muswadaukishapita awachenchie mbaya.
hawana msaada kwake,hata akiwateua mawaziri wanamwangusha.
 
wewe hizo habari ulizoleta si za ndani?........


Na kama hizo habari ulizoleta si za ndani wewe umezipata wapi? Unaziita ni tetesi, kwa nini umezileta hapa jukwaa la siasa..... peleka jukwa la tetesi bana!
 
dhambi ya kuiba kura wakishirikiana na jaji lewis makame ile 2010 sasa inawatafuna, ujue ni ngumu sana ku-mobilize hili baraza la mawaziri coz wengi wa mawaziri hao hawatambui hata nini umuhimu wao kwa taifa hili, ona kina ngeleja, kombani, wassira, maghembe, maige, na kina magufuli....! wote hawa ni janga la kitaifa ndo maana wanatoa matamko bila hata kusoma nyakati. their days are numbered, tunawasubiri majimboni 2015, died or alive watatumbua vijana wao, salam kwa prof. kapuya kule urambo magharibi...
 
Back
Top Bottom