Mimi nadhani hii ni nafasi pengine ya mwisho kwa JK kurudisha hadhi yake na ya CCM mbele ya umma. Anahitaji kufanya mabadiliko makubwa na kuondoa mawaziri legelege wote; pia mwanasheria mkuu wa sasa hatoshi, huyu hafai katika mchakato wa kupata katiba mpya. Pia ni muhimu kwa rais kubadili mfumo wa serikali, hasa sekta ya elimu na afya. Pia apunguze ukubwa wa baraza la mawaziri kwa kufuta wizara nyingine au kuziunganisha ili iwe ishara kwa umma ya kuanza kubana matumizi tunapoelekea bajeti mpya mwezi juni. Na katika hotuba yake kuunda baraza jipya, awe mkali na awe tofauti kabisa, na ashike uzi huo huo kwa kipindi chake kilichobakia. Akiachia nafasi hii imponyoke, atakuwa na shughuli nzito sana ya kukipa CCM uhalali mbele ya umma, na pia mawaziri wengi wataendelea kumchukulia kama mshijaki. Hili litakuwa janga kubwa kwake hasa kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani wa CCM, Novemba mwaka huu.