JK amteua Jaji Kiongozi mpya

JK amteua Jaji Kiongozi mpya

Nimesema uongo.

Usilete UTANI, hatuko katika utani hapa. Kwa kuwa ulianzisha Thread kwa kuleta mambo ya yasiyokweli, hutakiwi leta utani. Kama uko "serious" omba msamahani hapa JF, bila utani. Na mwerevu ama muungwana akikosea na kuomba msamaha, basi husamehewa. Lakini unapozidi kuleta utani, inaonesha tuna mtu wa namna gani.
 
Nimesema uongo kwamba:

Jaji Jundu alikuwa wakili wa kujitegemea kama mwaka mmoja uliopita kabla hajateuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.
 
Nimesema uongo.

MMK...Ili uonekane ni mwenye busara zaidi ni vema(kama kweli unaadmit umesema uongo) ukaongea kitu kinachoeleweka,hapa namaanisha kwamba ni vema ukatoa kauli yenye kuonesha kwamba unafuta kauli ile ya awali uliyoitoa wakati unatoa andiko hili(ambayo ndio msingi wa malumbano haya) na pia ukatutaka radhi sisi wana JF kwa kauli ile ambayo kwa namna moja ama nyingine illeta mtizamo tofauti kwa baadhi ya walioisoma mwanzo kabisa...Sasa unaposema 'nimesema uongo' then what next???...Kiustaarabu omba tu msamaha kwa wana JF(Hasa ukizingatia tayari umesema kwamba umetudanganya).....Otherwise kauli yako hii haioneshi kwamba umedhamiria(imekaa kihasirahasira na dharau zaidi)...be blessed
 
Mwanakijiji na wewe bana...yaani bado upo tu umeng'ang'ania kubishana na hawa jamaa...Lol....njoo kule kwetu na Cupcake....kule pouwa sana....hakuna hateoration...we're spreading the love
 
Mwanakijiji na wewe bana...yaani bado upo tu umeng'ang'ania kubishana na hawa jamaa...Lol....njoo kule kwetu na Cupcake....kule pouwa sana....hakuna hateoration...we're spreading the love

Nakuja huko maana nimewamiss tangu jana..
 
Nimesema uongo kwamba:

Jaji Jundu alikuwa wakili wa kujitegemea kama mwaka mmoja uliopita kabla hajateuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Pole Mkuu Mzee Mwanakijiji, kwangu mimi nimekusamehe kwa kutudanganya na kutufanya tujadili uongo. Mtu anapokubali kuwa alisema uongo, husamehewa, nimekusamehe.
 
Pole Mkuu Mzee Mwanakijiji, kwangu mimi nimekusamehe kwa kutudanganya na kutufanya tujadili uongo. Mtu anapokubali kuwa alisema uongo, husamehewa, nimekusamehe.
======

Kibarua chako kimepona kwa "kukiri" kwa Mwanakijiji, vinginevyo paycheck yako ya mwezi huu ilikuwa inapeta. Zidumu fikra!
 
Nimesema uongo kwamba:

Jaji Jundu alikuwa wakili wa kujitegemea kama mwaka mmoja uliopita kabla hajateuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Mzee Mwanakijiji,

You are great man!
Wewe ni mfano wa kupigiwa mstari kwa kitendo chako cha kukubali pale ulipoteleza na kuomba msamaha. Kitendo chako kinasaidia kuimarisha na kulinda JF standards.
 
Jaji Kiongozi Jundu amekuwa wakili kwa miaka zaidi ya kumi na tano namba yake ya uwakili ni 286 kwa mujibu wa Tanganyika Law Society.

Mfano mzuri ni wa jaji msumi ambaye amekuwa wakili 2004.cha muhimu JK jundu ana digri ya sheria ambayo ni sifa ya msingi lakini kusema kuwa ni muislam bila kuwa na ushahidi kwa vile jina lake ni Fakihi Jundu si sahihi kulikuwa na kiongozi wa karibu wa Hayati Saddam Hussein akiitwa Tariq Aziz alikuwa waziri wa mambo ya nje wa serikali ya Iraq lakini hakuwa muislam kama Saddam ni mkristu.

TRA kuna Salim Yusuf kati ya viongozi waandamizi kwa jina utasema ni muislam kumbe ni mkristu,Waziri wa utawala Bora Sophia Simba ni mfuasi wa kanisa la Mama Rwekatare ukiona jina lake unaweza kusema JK kampa uwaziri kwa vile muislam mwenzake.

Hoja ya udini haina mantiki kwani hatuna ushahidi kuwa Jundu ni muislam ndio maana Jk akamchukua kwa uislam wake.

Chuma kasema kuwa Jaji Hamis Msumi alipewa Ujaji Kiongozi na Rais Mkapa wakati Jaji Msumi alikuwa J11 hawa watu walikuwa dini mbili tofauti nina ushahidi kuwa jaji msumi ni muislam ni Alhaji na hivi karibuni alikuwa balozi wetu nchini Sauda Arabia, Nina ushahidi wa wazi kuwa Mkapa ni mkristu.

Rais Kikwete teuzi zake haziwabebi waislam hivi karibuni aliteua makatibu wakuu wa wizara mbali mbali na manaibu makatibu wakuu wengi wao ni wakristu, Kama alivyosema Chuma mtu kama Tido Mhando elimu yake ni kidato cha nne amepewa ukurugenzi mkuu wa TBC na Jk kama upendeleo basi anawafanyia wakristu kwa kumpa ukurugenzi mtu asiye na sifa na wala hakuwa kwenye taasisi husika.
Mtanzania la february 22 limetoa tangazo la kazi anatakiwa Mkurugenzi mkuu National Housing Corporation sifa awe na masters Degree in Estate Management,Business Administration,Engineering,Planning,Law and Human Resources Management.

hakuna nafasi ya Mkurugenzi mkuu mtu anaweza kupewa bila kuwa na masters na pia kuwa na uzoefu wa uongozi,nafasi hii Tido Dunstan Mhando kaipata jee Tido ni muislam?
 
======

Kibarua chako kimepona kwa "kukiri" kwa Mwanakijiji, vinginevyo paycheck yako ya mwezi huu ilikuwa inapeta. Zidumu fikra!

Haya tuambie na wewe unalipwa na nani(mambo ya paycheck)?...Acha hizo mazee,yaani mtu akiwa against na fulani ni kwamba katumwa na fulani(na analipwa kama unavyodai)..Kwa mtaji huu safari bado ni ndefu maana humu ndani ya JF kuna bendera nyingi mno tu,ni upepo tu wahitajika ziufuate...Lol
 
Amekiri!!! ok, assuming amekiri kuwa Jundu hakuteuliwa mwaka mmoja uliopita, je hii inaondoa ukweli kuwa Jundu hana uzoefu wa kutosha katika Mahakama ya Tanzania? Imetolewa orodha ya Majaji wa Mhakama Kuu, Jundu yuko chini sana....je huu ni uongo? Imetolewa CV yake inaonyesha hadi 2002 alikuwa wakili wa kujitegemea....huu ni uongo? Wapo majaji ambao wamekuwa Mahakama kuu kwa zaidi ya miaka 20...huu ni uongo? Jundu ameteuliwa kuwa Jaji Kiongozi akiwa amebakiza miezi mitano tu astaafu maana kazaliwa Julai....1949 ... huu ni uongo? Jundu ni kati ya Majaji kadhaa walioteuliwa kutoka katika uwakili wa kujitegemea ikiwa na maana kuwa hawakuwa katika utumishi wa mahakama kwa miaka mingi ya huduma yao ya kisheria.....huu ni uongo? kwamba katika hao majaji amabao walikuwa Mawakili wa kujitegemea most, if not all ni wa madhehebu ya Kiislamu. Wengine ni Salum Masatti, Nyangarika, Zainabu Mruke, Sheikh, Mujuluzi, nk. Ni Thomas Mihayo peke yake ambaye ni Mkristo aliyeteuliwa kuwa Jaji kutoka katika uwakili wa kujitegemea, na huyu aliwahi kufanya mahakamani kwa muda mrefu na katika mahakama za kazi na LART. Je ni kweli kusema kuwa Mawakili wa kujitegemea wa kikristo hawana sifa ya kuteuliwa kuwa Majaji? JK alimteua Wakili wa kujitegemea kuwa Balozi wa Tanzania huko Uingereza, Mwislamu asiye na uzoefu katika masuala ya mahusiano ya kimataifa. Wapo pia akina Adadi Rajabu, Hamisi Msumi nk. walioteuliwa kuwa Mabalozi! Huu nao ni uongo?

Hapa anayetakiwa kukiri si Mwanakijiji, ni wale wanaotetea uovu, upendeleo na ubaguzi katika teuzi za Rais.
 
Amekiri!!! ok, assuming amekiri kuwa Jundu hakuteuliwa mwaka mmoja uliopita, je hii inaondoa ukweli kuwa Jundu hana uzoefu wa kutosha katika Mahakama ya Tanzania? Imetolewa orodha ya Majaji wa Mhakama Kuu, Jundu yuko chini sana....je huu ni uongo? Imetolewa CV yake inaonyesha hadi 2002 alikuwa wakili wa kujitegemea....huu ni uongo? Wapo majaji ambao wamekuwa Mahakama kuu kwa zaidi ya miaka 20...huu ni uongo? Jundu ameteuliwa kuwa Jaji Kiongozi akiwa amebakiza miezi mitano tu astaafu maana kazaliwa Julai....1949 ... huu ni uongo? Jundu ni kati ya Majaji kadhaa walioteuliwa kutoka katika uwakili wa kujitegemea ikiwa na maana kuwa hawakuwa katika utumishi wa mahakama kwa miaka mingi ya huduma yao ya kisheria.....huu ni uongo? kwamba katika hao majaji amabao walikuwa Mawakili wa kujitegemea most, if not all ni wa madhehebu ya Kiislamu. Wengine ni Salum Masatti, Nyangarika, Zainabu Mruke, Sheikh, Mujuluzi, nk. Ni Thomas Mihayo peke yake ambaye ni Mkristo aliyeteuliwa kuwa Jaji kutoka katika uwakili wa kujitegemea, na huyu aliwahi kufanya mahakamani kwa muda mrefu na katika mahakama za kazi na LART. Je ni kweli kusema kuwa Mawakili wa kujitegemea wa kikristo hawana sifa ya kuteuliwa kuwa Majaji? JK alimteua Wakili wa kujitegemea kuwa Balozi wa Tanzania huko Uingereza, Mwislamu asiye na uzoefu katika masuala ya mahusiano ya kimataifa. Wapo pia akina Adadi Rajabu, Hamisi Msumi nk. walioteuliwa kuwa Mabalozi! Huu nao ni uongo?

Hapa anayetakiwa kukiri si Mwanakijiji, ni wale wanaotetea uovu, upendeleo na ubaguzi katika teuzi za Rais.

Nimeuliza zipi sifa muhim za kuchaguliwa/kuteuliwa umeshindwa kusema, pia Nimekuuliza uzoefu miaka mingapi unahitaji ili uteuliwe ktk nafasi kama hio?

Inavyoonesha kwako wewe mtu kuwa wakili wa kujitegemea sio uzoefu ....!!!sasa hujui kuwa mawakili ndio wanaopambana na majaji kila siku mahakamani kwa sheria hizohizo?au unapokuwa wakili unatumia sheria zingine na ukiwa Jaji au Hakim unatumia sheria zingine...? Kwa mtazamo wangu "sometimes", wakili anakuwa na uzoefu mkubwa kuliko hata baadhi ya majaji au mahakimu, kwani yeye anakuwa involved na kesi nyingi mahala pengi na ndio kwa mtaji huo teuzi zote za Rais kwa mawakili zipo sahihi.

Pia nimeuliza hivi wakristo ndio wanaHATI MILIKI ya kuongoza nchi hii pekee yao?.....hujajibu unatoa hoja zisizo na mashiko...

Katika hao majaji wote kwa number yao, waislam wangapi hadi wakuumize roho kiasi hicho? pengine hata kuswali hawaswali...?nafikiri wewe ni ktk wale wanaodhani waislam hakuna wasomi...!!!
 
Ni Thomas Mihayo peke yake ambaye ni Mkristo aliyeteuliwa kuwa Jaji kutoka katika uwakili wa kujitegemea ...katika hao majaji amabao walikuwa Mawakili wa kujitegemea most, if not all ni wa madhehebu ya Kiislamu...Huu nao ni uongo?

Huu ni uongo wa mchana mchana.

Rais Kikwete ameteua majaji 31 (kwanza aliteua ishirini mwaka 2006, halafu 11, mwaka jana, 2008).

Katika hao 31, kuna watano ndio walitoka kwenye uwakili binafsi:

Jaji Zainabu Muruke,
Jaji Upendo Msuya,
Jaji Kassim Nyangarika,
Jaji Crecencia William Makuru, na
Jaji Aloyisius Mujulizi.

Katika hao watano, wanne wana majina yanayoelekea kuwa ya kidini (Kiarabu na Kiingereza), mawili yakiwakilisha kila moja ya dini mbili, Kassim na Zainabu, pamoja na William na Aloyisius. Wa tano, Upendo, ana jina la Kiswahili, aweza kuwa kokote.

Umetoa wapi wewe habari kwamba jaji Thomas Mihayo ndio Mkristo pekee kutoka katika uwakili binafsi?

Sasa, kufuatana na viwango vya hii thread, ambayo ina mambo nyeti, shutuma kali, hatari, za udini, upendeleo, na teuzi zisizo zoefu dhidi ya Rais (hili lilidhihirika uongo), ukisema lisilo sahihi na likawa kichocheo cha kushambulia Rais kwa mambo nyeti, hatari, ni sawa na upotoshaji wa makusudi. Uongo.

Na pia kwa viwango vya thread hii, ukisema uongo unawajibika, bila kuumauma maneno, wala kubadilisha, kukaza au kulegeza sauti.

Sasa Jobo umeongopa. Wajibika.
 
Back
Top Bottom