JK amteua Jaji Kiongozi mpya

JK amteua Jaji Kiongozi mpya

Mwanakijiji umesema tuandikie wino na si mate.
hapa kuna thread uliyoanzisha kuiponda Nssf nathitisha ukinyonga wako, kwa faida ya wasomaji naweka link ya thread yote wasomaji wajue nani muongo na nani kinyonga au Tambwe Hizza.

wasomaji someni mjadala uliyoanzishwa na Mwanakijiji against Nssf na haikuwa issue ya Tabora bali DR.Masau.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...erikali-na-hatima-ya-taasisi-ya-moyo-thi.html
 
Najaribu kuweka link inakataa ila msomaji asome thread ya SAKATA LA DR.MASAU:MSIMAMO WA SERIKALI NA HATIMA YA TAASISI YA MOYO(THI) kama ilivyoanzishwa na Mwanakijiji humu kawaponda sana Nssf au jaribuni ku google muone vinyonga tuliona nao humu.

salamu za mwaka mpya za Mwanakijiji ziko kwenye KLH News aliyoyasema humu na aliyoandika kwenye cheche ni vitu viwili tofauti.simuelewi!
 
Zungu Pule said:
Bro, huyu Upendo Msuya ni yupi? Kuna wakati fulani nikiwa bongo, Mzee mmoja wa "system" akawa ananipa stori kuhusu Kiongozi wa nchi anavyofanya mambo kienyeji. Akanipa mfano wa dada/mama mmoja ambaye (to the best of my memory) alikuwa anamiliki Antelope Safaris - kampuni ambayo ofisi zake ziko Millenium Tower, Kijitonyama. Huyu mama ilikuwa ateuliwe "within few days" kushika wadhifa fulani nyeti (based on the principle of camaraderie or personal affairs). I suspect ni huyu Upendo Msuya. Someone should know what I am trying communicate.

Zungu Pule,

..nimepata wasifu mfupi wa Jaji Upendo Msuya ambao nimeuweka hapa chini.

..Jaji Msuya alisajiliwa kuwa Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania mwaka 1996. alikuwa kundi moja na watu kama Samuel Sitta, Adadi Rajabu, na Jaji Sauda Mjasiri wa Mahakama ya Rufaa.


tanzania daima said:
tume ya haki za binadamu yapata katibu mtendaji

tume ya haki za binadamu na utawala bora imepata katibu mtendaji mpya ambaye ni wakili wa kujitegemea, upendo msuya (50), aliyeapishwa na rais jakaya kikwete, jana ikulu.

msuya, mwenye uzoefu wa masuala ya sheria kwa zaidi ya miaka 25, aliteuliwa na rais kikwete kushika wadhifa huo, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na gad mjemmas, aliyeteuliwa kuwa jaji wa mahakama kuu ya tanzania mwishoni mwa mwaka jana.

Waliohudhuria sherehe fupi ya kuapishwa kwa msuya ni pamoja na makamu wa rais, dk. Ali mohamed shein, waziri mkuu, edward lowassa, waziri wa nchi ofisi ya rais (siasa na uhusiano wa jamii), kingunge ngombale-mwiru, waziri wa katiba na sheria, dk. Mary nagu, mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na utawala bora, jaji robert kisanga.

Viongozi wengine waliohudhuria katibu mkuu kiongozi (ikulu), philemon luhanjo, katibu mkuu wizara ya katiba na sheria, sazi salula, na mkurugenzi mkuu wa takukuru, edward hoseah, makamishna wa tume ya haki za binadamu na baadhi ya maofisa waandamizi wa tume hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuapishwa kwake, katibu mtendaji huyo mpya alisema moja ya masuala muhimu atakayoanza nayo ni kuhakikisha majukumu ya tume yanatangazwa vya kutosha kwa wananchi, ili wajue namna ya kuitumia katika matatizo ya ukiukaji wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora.

uzoefu wa kisheria na masuala ya utawala alionao msuya unatokana na kuwa hakimu mkazi katika mahakama za kivukoni na kisutu (1983-1991), mkurugenzi wa idara ya mahakama za mwanzo (1992- 1996), wakili wa kujitegemea (1996 hadi sasa), wakili wa serikali na msajili wa makampuni na masuala ya hatimiliki katika serikali ya botswana (1998 – 2004).
 
Swala la Jaji jundu tuliache sasa tujadili Jaji mpya kachaguliwa na Rais Kikwete anaitwa Catherine Opiyo amechaguliwa leo kwenda mahakama ya Rufaa.tupeni wasifu wake,dini yake, ameolewa au bado,kwanini kamchagua Mwanamke ameacha wanaume

Kanda2 na Jokakuu, na wengine wanaojaribu kutafuta facts,

Huyu Catherine Opiyo huyu aliyetualiwa kwenda Mahakama ya Rufaa, kwa mujibu wako Kanda2, katoka wapi huyu nae? Mbona nae yuko fishy fishy kwa sababu kwa mujibu wa Tanganyika Law Society hakuwa hata jaji. Sasa kumpeleka mtu Mahakamu ya Rufaa, ya juu kupita zote, bila hata kumpitisha kwenye ujaji wa kawaida that may be a serious problem there.

Unless info za TLS sio current, maana website za Kibongo zinachukua mwaka kuwa updated. Inawezekana walim fast track kwenye ujaji within the last year or so? Or maybe ni yule Katherine Urio, that rings a bell, lakini sio Catherine Opiyo. Mnasemaje wakubwa hapo?

By the way mtu wangu Kanda2, I know we strive to dare and talk openly here lakini data za kuoa na kuolewa, dini na kabila la jaji mteule sijui kwa kweli zitatusaidia nini hapa. Siku Mama Opiyo akigombea Urais hapo kweli hata mimi ningependa kujua idadi na majina ya wanaume wote aliopita pita nao maishani mwake including whether Liyumba the playboy nae yumo! Lakini kwa ujaji sidhani ni lazima sana kujua. Na pia unapouliza ni kwa nini hakuchaguliwa mwanamme, unajua hata wanawake nao wangeweza kuuliza kwa nini asichakuchaguliwe mwanamke. Hilo swali, sikufichi wala sikuonei aibu, linaonyesha wewe ni chauvinist, bigoted!

Okay, turudi kwenye mada ya professional qualifications za hawa wana wateule.
 
Kuhani,

..hata mimi sijamuona Jaji anayeitwa Opiyo.

..nadhani umepatia, Jaji aliyeteuliwa ni Katherine Oriyo.


NB:

..nimekutana na "ze dataz" kwamba the 1st Tanzanian woman to attain a PhD in law ni Hawa Sinare. sasa hivi ni wakili wa kujitegemea DSM.
 
Jokakuu,

Speaking of women in the field, hivi enzi zile, awamu ya kwanza na ya pili, kulikuwa na jaji mwana Mama kweli?

Majina ya wale heavy hitters wa wakati ule wote mi-ndume watupu, jaji Kissanga, Nassor Mzavas, Nyallali, Damian Lubuva, Augustino Ramadhani, jaji Samata, Kissanga, Makame, the late great Lugakingira etc. etc.

I mean I'm sure kuna wanawake wawili watatu walikuwa wamechimba sheria na wangeweza kuwa considered for judgeship, lakini kina Mwinyi na Nyerere mmmh! I am not so sure about Mwinyi but I think ma man Julius didn't give a hoot, or did he have a female judge? Noma!
 
Joka Kuu.
Vipi kuhusu Asha Rose Migiro kuna mtu aliwahi kuniambia ndio wa kwanza kuwa na PhD na alikuwa best student Udsm sina uhakika na hilo nalileta kwako kama changamoto.

Kuhani.

Habari kama kaolewa au laa haina uhusiano hapa ila nimeweka kutokana na watu kuwa na tabia ya kuhoji vitu vya ajabu ajabu au kuzua.Kwani wakisikia kuwa JK kateua jaji mwanamke kwao haitoshi watataka kujua kwanini mwanamke? au dini gani au amezaa au ameolewa n.k.nimeona mtu humu anahoji balozi Mwanaidi Maajar kachaguliwa kuwa balozi UK kwa kigezo gani?ameshindwa kujua kuwa huyu mama Mwanaidi ni msomi na toka 1970s alikuwa wakili wa kuaminika.
wazungu wana msemo wao IT TAKES ALL THE SORTS TO MAKE THIS WORLD!!
 
Kuhani,

..kuna mama anaitwa Julie Manning alikuwa AG wakati wa Juliasi. nadhani wakati huo AG alikuwa pia ndiye waziri wa sheria.

..sijui ni katika mazingira gani Mama Manning aliondoka ktk wadhifa wa AG. baada ya hapo hakusikika tena, mpaka majuzi Mkapa alimpokuja kumpa kazi.

NB:

..inawezekana Julie Manning ndiyo mwanamke wa kwanza Mtanzania kuhitimu LL.B pale UDSM.

..Damian Lubuva alitokea wapi kabla hajawa AG? sakata ya OIC ndiyo ilimuondoa wizara ya sheria na kupelekwa mahakama ya Rufaa.
 
Joka Kuu.
Vipi kuhusu Asha Rose Migiro kuna mtu aliwahi kuniambia ndio wa kwanza kuwa na PhD na alikuwa best student Udsm sina uhakika na hilo nalileta kwako kama changamoto.

Huyu Asha Rose ni wa juzi juzi tu hapa na wala sio zamani. Sasa ina maana TZ kulikuwa hakuna mwanamke mwenye hiyo "PhD" ya sheria kabla yake yeye?
 
kanda2,Nyani Ngabu,

..Asha Rose Migiro alipata LL.B 1st class. nilichosikia mimi ni kwamba alikuwa ni mwanamke wa kwanza kufaulu kwa kiwango hicho pale Faculty of Law. nadhani pia ilikuwa baada ya kupita miaka mingi ya "ukame" wa 1st class za LL.B

..Ph.D ya kwanza ya sheria kwa kina mama wa Kitanzania aliipata Hawa Sinare, ambaye ni dada yake Mwanaida Sinare Maajar.

NB:

..hata mimi naona uteuzi wa Mwanaidi Maajar kuwa Balozi una walakini kidogo. najua Raisi hakuvunja sheria alipomteua. lakini sijui ni vigezo gani vilitumika kumpa wadhifa huo.

..kama ni suala la kuwa msomi, na wakili wa muda mrefu, mbona hata Fakihi Jundu ana sifa hizo? sasa kwanini Raisi hakumteua Fakihi Jundu kuwa balozi London badala yake akamteua Mwanaidi Maajar?

..nadhani katika kuteua mabalozi Raisi atoe kipaumbele kwa watumishi wa wizara ya mambo ya nje.
 
Kuhani,

..kuna mama anaitwa Julie Manning alikuwa AG wakati wa Juliasi. nadhani wakati huo AG alikuwa pia ndiye waziri wa sheria.

..sijui ni katika mazingira gani Mama Manning aliondoka ktk wadhifa wa AG. baada ya hapo hakusikika tena, mpaka majuzi Mkapa alimpokuja kumpa kazi.

NB:

..inawezekana Julie Manning ndiyo mwanamke wa kwanza Mtanzania kuhitimu LL.B pale UDSM.

..Damian Lubuva alitokea wapi kabla hajawa AG? sakata ya OIC ndiyo ilimuondoa wizara ya sheria

Jokakuu,

Umenikumbusha kitu, you are absolutely right Mama Manning alikuwa Waziri wa Sheria wa Nyerere, mwaka 1975 mpaka 1979. Na aliwahi kuwa jaji pia, duu, afadhali nimeuliza. Namshtukia yule Mama vizuri tu, kapandisha madaftari yule maza you're right. Mkapa ndio alimuibua zaidi, lakini originally alieanza kumrudisha rudisha kwenye scene ni Mwinyi, alimpa u-member tume ya uchaguzi ya kwanza kabisa, 1993.

Na Lubuva kumbe ni OIC ndio the cause of his undoing pale Wizara ya Sheria, ha hahahaaaa aa duuu. Kwa nini walim-maindi sasa, hebu lete mchongo. Lakini ishu ya OIC kwani ilifika Wizara ya Sheria au iliishia Zanzibar halafu Bara wakaipiga buti, Lubuva alikuwa implicated vipi maskini ya Mungu.

By the way Lubuva aliwahi kuwa AG Zanzibar pia. Na kabla ya kuwa AG wa bara na waziri wa sheria alikuwa jaji Mahakama Kuu mwaka mmoja, around 1984. Kabla ya hapo sijui alikuwa wapi. Kwa hiyo the picture building up pale Justice ni kwamba Lubuva alimfuata Warioba, Warioba alimfuata Manning, Manning ndio atakuwa aliwafuata kina Fundikira and them, you know?

Sakata la OIC na Lubuva ilikuwaje?
 
Jobo is back!
Wana JF Kuhani, Kanda2 na Pundamilia, naheshimu michango yenu lakini siyo lazima nikubaliane nayo. Naomba niseme kuwa sitaomba radhi kwani sijadanganya chochote. Nitaeleza kidogo kuhusu huo "ukweli" mnaosma kuwa umebainika, na kwamba nilichosema mimi ni uongo.

Kwanza kabisa naomba Kuhani uwe unafanya utafiti kabla ya kuandika au kuelezea mambo kadha wa kadha. Umeeleza kuwa kati ya Mawakili 20 walioteuliwa na Rais mwaka 2006 watano walikuwa Mawakili wa Kujitegemea na kwamba siyo kweli kuwa Wakili wa Kujitegemea Mkristo aliyeteuliwa ni Mihayo peke yake. Orodha yako inaonyesha kuwa wengine ni Zainabu Mruke, Upendo Msuya, Kassim Nyangarika, Cresensia Makulu na Mujulizi. Kwa taarifa yako ni kuwa Makulu alikuwa Wakili wa Serikali kwa muda mrefu kule Mbeya kabla ya kuteuliwa kuwa Mwanasheria wa Jiji la DSM wakati wa Keenja. Baada ya hapo aliteuliwa kuwa Katibu wa Tume ya Kurekebisha Sheria na ndiko alikoteuliwa kuwa Jaji. Kama aliwahi kuapishwa kuwa Wakili, basi hakuwahi kupractice kama Wakili wa Kujitegea. Upendo Msuya, kama wengine walivyoeleza hapo juu alikuwa Hakimu kwa muda mrefu haddi kufikia cheo cha Msajili, kuteuliwa kwake si ajabu. Mujulizi ni mwislamu wa swala tano pamoja na ukweli kuwa ana jina la kikristo nadhani alibadili dini. Nyangarika na Mruke ni waislamu, walikuwa Mawakili wa Legal cooperation kabla ya kuwa mawakili binafsi.

Hoja yangu kubwa ilikuwa siyo kupinga uteuzi wao kuwa majaji kwa sababu ya dini yao, bali kuuliza kama hakuna Mawakili Wakristo wenye sifa za kuteuliwa kama wao. Kanda2 unasema kuwa Jundu ana uzoefu kwani amekuwa "wakili wa serikali" tangu 1977, hiyo si kweli. Amekuwa Wakili wa Serikali kwa mwaka mmoja tu. Kama argument ni muda ambao mtu amekuwa Wakili au mwanasheria kabla hajawa jaji basi tungewateua Jaji Shaidi, Jaji Lyimo au Jaji Mushi kuwa Jaji kiongozi maana hao wamefanya kazi za sheria serikalini tangu mwaka 1973. Jundu anaweza kuwa amefanya kazi ya sheria kwa muda mrefu lakini si katika Mahakama au serikalini kama wenzake.. ndo maana tulijiuliza ni kwanini yeye?? Jibu likaja kuwa ni kwa sababu ya dini yake ya kiislamu maana cheo hicho ukimmwacha Jaji Samatta, hakijawahi kushikiriwa na Jaji Mkristo? Je hii ni kwa sababu ya uwezo wa hao majaji wa kiislamu au ni unwritten law/condition kuwa nafasi hiyo ni lazima ishikwe na Mwislamu kwani Jaji Mkuu ni Mkristo (by the way, hatujawahi kuwa na Jaji Mku Mwislamu)!
 
...Kwanza kabisa naomba Kuhani uwe unafanya utafiti kabla ya kuandika au kuelezea mambo kadha wa kadha...Kama aliwahi kuapishwa kuwa Wakili, basi hakuwahi... pamoja na ukweli kuwa ana jina la kikristo nadhani alibadili dini.

Aaaah, kumbe na wewe hujui jui, huna hakika. Umeharibu pati bana! Brother sister, kuna watu wanasubiri hiyo sherehe kwa udi na uvumba ya mimi kuleta mchongo feki feki hapa, kutokana na tabia yangu chafu ya kuswalisha data ambazo nimeona kama hazi make sense. Come on man, umearrrrib! Umearrrrib!

"Nadhani alibadili dini," Unadhani? Nani ana keep track ya fulani kabadili dini lini, kabla na, au baada ya kuteuliwa? Na kama ndio hivyo, unajuaje jaji Jundu nae kama hajabadili dini Jumapili iliyopita? Unadhani?

"Kama aliwahi kuapishwa kuwa Wakili..." Nani katika field ya sheria hajawahi kuapishwa kuwa Wakili? Unaongea nini hapo? Kama aliwahi? Unatania kweli wewe.Au una maana kama aliwahi kuapishwa kuwa wakili wa kujitegemea? Well, there is no such thing! "Kama aliwahi..."?

Tell you what. Let me give you a hint here, because I would also benefit from being corrected. Next time around this is how you do it : "Kuhani umekosea / umeongopa uliposema Fulani bin Fulani ni kabila fulani. Ukweli ni kwamba mtu huyu ni wa kabila fulani. Hii ni kwa vile....( unatoa sababu/uthibitisho wako), kwishne. Kwishne. Usianza "oooh...nadhani...atakuwa alibadili kabila...kama aliwahi kuwa hilo kabila ulilosema basi itakuwa....). No no no, unaaarib! Kama unataka kusema kwamba inawezekana nimekosea, basi usianze na lugha ya uhakika, kwamba sijafanya utafiti, halafu humo ndani ukisomwa na wewe unaonekana hujui hujui, au hujui kitu kabisa "kama aliwahi kuapishwa kuwa wakili." Jaji ataacha kula kiapo cha Uwakili? Unaaaarib!

Unadhani?
 
Kuhani said:
Na Lubuva kumbe ni OIC ndio the cause of his undoing pale Wizara ya Sheria, ha hahahaaaa aa duuu. Kwa nini walim-maindi sasa, hebu lete mchongo. Lakini ishu ya OIC kwani ilifika Wizara ya Sheria au iliishia Zanzibar halafu Bara wakaipiga buti, Lubuva alikuwa implicated vipi maskini ya Mungu.

By the way Lubuva aliwahi kuwa AG Zanzibar pia. Na kabla ya kuwa AG wa bara na waziri wa sheria alikuwa jaji Mahakama Kuu mwaka mmoja, around 1984. Kabla ya hapo sijui alikuwa wapi. Kwa hiyo the picture building up pale Justice ni kwamba Lubuva alimfuata Warioba, Warioba alimfuata Manning, Manning ndio atakuwa aliwafuata kina Fundikira and them, you know?

Sakata la OIC na Lubuva ilikuwaje?

Kuhani,

..hivi Jaji Lubuva ni Mzenji? ilikuwaje akawa AG wa Zanzibar? au aliazimwa toka Bara kinamna fulani?

..Zanzibar pia wana historia ya kuajiri watu toka nje hata kwa nafasi nyeti kama hizi. nadhani kuna jamaa akiitwa Kwa-Swanzy alitokea Ghana na akawa AG[sina uhakika] wa Zanzibar. nadhani Swanzy ndiyo alimtia Aboud Jumbe kwenye matatizo.

..kuhusu OIC my understanding ni kwamba Ofisi ya AG ilikuwa against na hili suala. nadhani walieleza vizuri tu kwamba ni Tanzania na siyo Zanzibar wenye uwezo wa kufanya hivyo. baada ya wahusika kuona wanaletewa "longolongo" wakaona wahamishie mambo yao Zanzibar.

..to be on the safe side, na ukizingatia kwamba we have set the bar so high in this thread, naomba nisomeke kwamba, Lubuva aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa baada ya kashfa ya OIC na hoja ya serikali ya Tanganyika.
 
Jokakuu,

Lubuva ni m-Bara wa Kondoa. Japo alikuwa Attorney General wa Zanzibar. Hivi unajua hata Jaji Mkuu Ramadhani alikuwa Jaji Mkuu Zanzibar? Na kabla ya kuwa Jaji Mkuu Zanzibar, Ramadhani alikuwa deputy Attorney General wa Lubuva. Kwa hiyo wa-Bara wawili walikuwa wana run the show at Justice in Zanzibar! Duuuh noma! Ila wenyewe wanapenda manake huwa wanaleta hata Wanaigeria wawe majaji! Sijui hakuna wataalam Zanzibar? Hivi Zanzibar ina watu wangapi anyway?

Wakina Mwiba wasije wakanirukia, lakini wenyewe Wanzanzibar wanapenda kupangiwa pangiwa sheria na ma aliens, kama ulivyo intimate, we utamletaje m-Nigeria awe jaji? Yani unawa dis wazawa wote kuwa hakuna anaefaa mpaka ulete wakuja?

By the way, according to "ze dataz" ni kwamba jaji mwanamke wa kwanza ni Mama Eusebia Munuo: "...Eusebia anasema April 1987, aliteuliwa kuwa jaji wa kwanza mwakamke katika Mahakama Kuu mkoni Arusha...Eusebia ambaye ni hakimu wa kwanza mwanamke Tanzania..." Unless wanamaanisha alikuwa jaji wa kwanza Arusha, simuelewi hapo mwandishi Happiness Katabazi wa Tanzania Daima (hiyo mi-typo yenyewe inakutia mtu mashaka na kile anachokisema.) Na kama Mama Mnuo ndio alikuwa jaji wa kwanza wa kike, je jaji mstaafu Mama Manning ambae pia AG in the 70's, alikuwa jaji lini?
 
Kuhani,

..kwani Julie Manning alipotoka kuwa AG moja kwa moja aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu?

..binafsi sifahamu Mama Manning alikuwa akifanya shughuli gani baada ya kuondoka wizara ya sheria, mpaka Raisi Mwinyi alipomteua kuwa mjumbe wa Tume ya Uchaguzi.

..vilevile sifahamu ni sababu zipi zilizopelekea Mama Manning akaondolewa toka kuwa Waziri wa Sheria na Mwanansheria Mkuu wa Serikali, na nafasi yake kuchukuliwa na Joseph Sinde Warioba.

..hivi kutoka kuwa AG na kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu siyo DEMOTION? vipi kuhusu AG[lubuva] kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa? au DPP[shaidi] kuwa Jaji wa Mahakama Kuu?

NB:

..kama madai ya Jaji Munuo ni kweli, kwamba yeye ndiye mwanamke wa kwanza kuteuliwa Jaji wa Mahakama Kuu, basi inawezekana Mama Julie Manning alikuwa mtaani kwa kipindi fulani kabla naye hajateuliwa kuwa Jaji.
 
Jobo.

COLIN POWELL wakati anafanya endorsement kwa Baraka Obama alisema "KWANI KUNA TATIZO KWA MUISLAM KUWA RAIS WA MAREKANI"?

Nilitegemea kauli ya POWELL ingekusaidia kuondoa sumu na chuki kwa waislam,kama ni uzoefu Obama kwa mara ya kwanza kaongea kwenye mkutano wa chama chake DEMOCTRATIC 2004 hakuwa kiongozi wa chama wala hakuwa na madaraka makubwa kwenye serikali wala uzoefu.

mmarekani John Mccain wa Republican ana uzoefu toka miaka ya 1960s lakini wamarekani wakampa urais Obama wakamuacha mzungu mwenzao walitizama MERITS sio dini wala rangi ya mtu kama anavyofanya JK. hivyo Jaji Jundu asikunyime usingizi kwa kuwa muislam.

Joka kuu.

Alimpa Balozi Mwanaidi kwa vile ana masters ya sheria ya mwaka 1977 na ana uzoefu mkubwa kuanzia alipokuwa serikalini BOT ndio maana hukusikia EPA alipokuwa wakili wa benki kuu.

Angempa JUNDU angekuja Jobo na kusema JUNDU hana masters digri.

Mwanakijiji.

Naona kimya unaweza kupitia maneno yako uliyosema kwenye podomatic yako desemba 30 2008.kuwa utahakikisha wasioguswa kama kina DR.DAU unapambamba nao www.mwanakjji.podomatic.com.

ile thread ya dr.Masau nimekuwekea hapo juu ipitie taratibu najua una mambo mengi na unaandika mengi lazima mengine unayoandika au kusema utasahau kwani wewe ni binadamu, udhaifu ni sehemu ya maumbile yetu, huwezi kubishana na uhalisia.
 
Last edited:
Kanda2.. ni wewe umesema kuwa mimi nilisema x,y ni jukumu lako kuonesha hicho nilichokisema. Kwa maneno mengine the burden of proof is on you. Sasa iweje mimi nipoteze muda kuanza kukutafutia kile nilichosema wakati nimekuambia sikukisema. Labda uliowaomba kutafuta watafanya hivyo, mimi huo muda sina.
 
Jokakuu,

Lubuva ni m-Bara wa Kondoa. Japo alikuwa Attorney General wa Zanzibar. Hivi unajua hata Jaji Mkuu Ramadhani alikuwa Jaji Mkuu Zanzibar? Na kabla ya kuwa Jaji Mkuu Zanzibar, Ramadhani alikuwa deputy Attorney General wa Lubuva. Kwa hiyo wa-Bara wawili walikuwa wana run the show at Justice in Zanzibar! Duuuh noma! Ila wenyewe wanapenda manake huwa wanaleta hata Wanaigeria wawe majaji! Sijui hakuna wataalam Zanzibar? Hivi Zanzibar ina watu wangapi anyway?

Wakina Mwiba wasije wakanirukia, lakini wenyewe Wanzanzibar wanapenda kupangiwa pangiwa sheria na ma aliens, kama ulivyo intimate, we utamletaje m-Nigeria awe jaji? Yani unawa dis wazawa wote kuwa hakuna anaefaa mpaka ulete wakuja?

By the way, according to "ze dataz" ni kwamba jaji mwanamke wa kwanza ni Mama Eusebia Munuo: "...Eusebia anasema April 1987, aliteuliwa kuwa jaji wa kwanza mwakamke katika Mahakama Kuu mkoni Arusha...Eusebia ambaye ni hakimu wa kwanza mwanamke Tanzania..." Unless wanamaanisha alikuwa jaji wa kwanza Arusha, simuelewi hapo mwandishi Happiness Katabazi wa Tanzania Daima (hiyo mi-typo yenyewe inakutia mtu mashaka na kile anachokisema.) Na kama Mama Mnuo ndio alikuwa jaji wa kwanza wa kike, je jaji mstaafu Mama Manning ambae pia AG in the 70's, alikuwa jaji lini?

Ukweli wa mambo, na kama watu tunasoma na kufuatilia historia ni kwamba Julie Manning ndiye mwanamke wa kwanza kuwa jaji wa mahakama kuu nchini Tanzania, na kimsing alikuwa mwanamke wa kwanza kuwa jaji wa mahakama kuu katika Afrika Mashariki na kati.Hii imerekodiwa kwenye kitabu kinaitwa "Chronology of Womens History" kilichoandikwa na Kirstin Olsen. Na hii ilikuwa mwaka 1973. Na kisha mwaka 1975 Julie Manning alikuwa waziri wa sheria hadi mwaka 1979. Baadaye amekuwa kamishna kwa muda mrefu kwenye Law Reform Commission, na pia kamishna kwenye tume ya uchaguzi ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom