..
..
..
rais jakaya kikwete ameweka rekodi mpya katika utumishi wa idara ya mahakama nchini kwa kuwateua majaji wapya 20 wa mahakama kuu ya tanzania kwa mpigo.
Katika uteuzi huo umekwenda sambamba na mkakati wa kutoa nafasi kwa wanawake ambao umekuwa ukionekana zaidi katika nafasi za kisiasa kwa kutenga nafasi maalumu kwa wanawake, asilimia 30 ya walioteuliwa kuwa majaji ni wanawake.
Wanawake walioteuliwa ni alice chingwile ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa mkurugenzi msaidizi mambo ya katiba na sheria katika ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.
Wanawake wengine ni imani aboud aliyekuwa mkurugenzi msaidizi, utawala katika ofisi ya rais menejimeni ya utumishi wa umma; stella mugasha aliyekuwa mwanasheria mkuu tume ya uchaguzi (nec) na aisha nyerere, aliyekuwa hakimu mkazi mfawidhi mkoa wa kilimanjaro.
Pia wamo aishiel sumari ambaye alikuwa mkurugenzi msaidizi idara ya mashitaka katika ofisi ya mwanasheria mkuu; na mwanaisha kwariko aliyekuwa msajili wa wilaya, mahakama kuu ya tanzania kanda ya iringa.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na idara hiyo jana na kusainiwa na naibu msajili mwandamizi wa mahakama ya rufani, sophia wambura, imetaja wengine walioteuliwa kuwa ni wakili wa kujitegemea, aloyse mujulizi na mkurugenzi wa mashtaka nchini (dpp), geoffrey shaidi.
Wengine walioteuliwa ni msajili wa mahakama ya rufani, augustine mwarija, kaimu naibu msajili wa mahakama hiyo, zaiduni chocha na msajili wa mahakama kuu ya tanzania, augustino shayo.
Pia katika uteuzi huo wa kihistoria yumo jaji wa mahakama kuu ya zanzibar, sekieti kihiyo. Wengine ni msajili wa wilaya mahakama kuu ya tanzania, kanda ya arusha, shabani lilla na mkurugenzi mahakama za wilaya-rufani, lawrence uzia.
Taarifa hiyo iliwataja wengine kuwa ni mkurugenzi wa katiba na haki za binadamu, frederick werema, naibu mwenyekiti mahakama ya kazi, kakusulo sambo na mkurugenzi wa mahakama za mwanzo, mahakama ya rufani, agathon nchimbi.
Wengine ni msajili wa baraza la ushindani, amiri mruma na kamishna tume ya haki za binadamu, robert makaramba.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, uteuzi wa majaji hao wapya unaanza mara moja na taarifa kuhusu tarehe ya kuapishwa kwao na rais itatolewa baadaye.
Uteuzi huo wa kihistoria kutokana na wingi wao kwa mpigo, ni utekelezaji wa ahadi ya rais aliyoitoa wakati akihutubia bunge desemba 30, mwaka huu alipoahidi kwamba angeteua majaji wengi ili kukidhi upungufu wa majaji pia kuongeza uwezo wa idara ya mahakama kutekeleza majukumu yake.
Kumekuwako na kilio cha muda mrefu juu ya ucheleweshaji wa kesi mahakamani hususani mahakama kuu kutokana na upungufu wa majaji. Kasoro hiyo imekuwa ikielezwa kwamba ni kikwazo katika kutoa haki kwa raia.