Jedwali la RA: Nani hayumo?

Dau ni mwizi...kibaka..fisadi....na watu wote wanaomtetea ukiwemo wewe (unajijua ni nani) ni mafisadi. Mfe kifo cha mateso wote nyie na mwende motoni mkaungue kwa milele. I hate you all.
 
dau ni mwizi...kibaka..fisadi....na watu wote wanaomtetea ukiwemo wewe (unajijua ni nani) ni mafisadi. Mfe kifo cha mateso wote nyie na mwende motoni mkaungue kwa milele. I hate you all.

inna illah wainalilah rajoon
 
Bila kusahau Msatafa Mkullo alikuwa ndio Director wa NSSF hapo before , Kwahiyo alipoondoka aliacha watu wake wengi sana pale jikoni, kwahiyo madili yote ya kina RA yalikuwa yanapikwa na kupakuliwa na Vibaraka wa Mstaffa Mkullo.

Zawadi yake toka kwa RA ilikuwa ni Uwaziri wa Fedha

Kwa hio mkuu tunaweza kusema kwamba RA huwa anashiriki kupanga cabinet ya serikali!
 
Na mimi nachangia jedwali langu kama lifuatavyo:

3. Dr Idris Rashidi=BOT+NBC= ACB(Akiba Commercial Bank)
Kwa hio, ACB+TANESCO=TMF(Tanzania Mtaji Fund)

NB:
Dr Rashid alikuwa mjumbe wa bodi ya REPOA mwaka 2006, akitokea TMF.
 
Kuna wimbo mmoja uliimbwa na kwaya ya Bulyankulu Barabara ya 13 uitwao "Samson". Sehemu ya wimbo huo nikikumbuka inasema:

"Tafadhali niambie asili ya nguvu zako, tafadhali niambie waweza kufungwa na nini?" alilalamika mwanamke wa Kifilistina. Sasa, simlinganishi RA na Samson Mnadhiri wa Mungu ila kwenye hili suala la nguvu ambazo inaonekana hazidhibitiki!

Nikiwa nafikiria hilo nikakumbuka mambo ya kuchora majedwali ambamo unaweka makundi ya vitu mbalimbali na ndipo wazo limenijia. Yawezekana ili kuweza kuelewa nguvu za RA ni lazima tuchore jedwali moja hivi na kujaribu kuweka ndani yake watu ambao wanahusiana au wamehusiana moja kwa moja na RA na sasa watu hao wako madarakani au kwenye nafasi fulani za maamuzi.

a. Wale aliowafadhili na kuwasaidia kushika au kudumisha nafasi za kisiasa.

Kundi hili litakuwa na wale wote ambao aliwasaidia wakati wa kampeni au kuwafadhili na kuwasaidia kushika nafasi za kisiasa. Wabunge, Wagombea wa Urais n.k Yaani hapa ni jumla ya wanasiasa ambao wamepata ufadhili kwa RA.

MATOKEO:
1. Jakaya M. Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2.Benno Malisa - (a) - Makamu Mwenyekiti- TAIFA, UVCCM
3.Sofia Simba - (a) - Mwenyekiti Taifa- UWT(CCM)
4. Prof. Juma Kapuya - Waziri wa Kazi & Maendeleo ya Vijana (Mbunge Urambo Magharibi)
5. Adam Malima - (a) - Naibu Waziri, NISHATI NA MADINI (Mbunge, Mkuranga)

b. Wale ambao wamewahi kuwa watumishi wake kwenye Vodacom.
Akiwa ni mmoja wa wenye hisa kubwa pale Vodacom (ingawa nasikia alikuwa na mpango wa kuuza hisa hizo) kuna watu ambao wamewahi kufanya kazi Vodacom au kupewa mkataba wa kazi Vodacom. Watu hao wengine wameenda na kuwa na nafasi za kisiasa (yawezewa kuwa kwenye "a" hapo juu). Kama mtu anatokea kwenye "a" na anatokea kwenye "b" basi wawekwe vile vile.

MATOKEO:
1.Pius Msekwa - Vodacom B. - Makamu wa Mwenyekiti CCM (Bara)
2. William Ngeleja - Vodacom - Waziri wa Nishati na Madini
3. Dr. Idris Rashid (Vodacom) - Mkurugenzi Mtendaji Tanesco

c. Wale ambao wametumika kwenye vyombo vyake vya habari
Hawa ni wale ambao kwa namna moja au nyingine wamewahi kuwa na ubia pamoja au utumishi wa vyombo hivyo vya habari na sasa hivi wako kwenye nafasi fulani fulani za kisiasa au za kiserikali. Hapa ninawaondoa watumishi ambao wanafanya kazi tu kwenye vyombo vyake vya habari. Msisitizo ni wale waliovuka toka kwenye vyombo vya habari kwenda kwenye serikali au siasa.

d. Wale wenye ushirikiano wa kibiashara.
Kundi jingine ni la wale ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa na mahusiano ya kibiashara na RA au makampuni yake mengine na hawa nao wametoka huko na sasa wana nafasi serikalini (idara, wizara au wakala mbalimbali). Na nafasi zao kwenye idara hizo.


Jinsi ya kufanya:
Bila kuweka maelezo mengi, linatajwa
Jina (Salva Rweyemamu);
kundi lake (c)
na nafasi yake ya sasa (Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais).

Nitaendelea kuupdate tunayoyapata labda tunaweza kuona pattern ya aina fulani hivi ikijitokeza. Ukiweza kuweka na some kind of the story behind ya chaguo lako that will help too to make sense.

Baada ya hapo tutachora majedwali ya watu wengine wawili halafu tutaona hiyo picha inayotokea inatuonesha nini. Yawezekana kuna kitu ambacho tumekimiss kwa muda mrefu juu ya RA na nadharia niliyonayo yaweza kuthibitika kisayansi juu ya "asili ya nguvu yake".

Kama huna lolote unalojua; sit down and enjoy!

Kuna mapungufu kwenye habari hii Benno Malisa hakusaidiwa na Rostam kwenye nafasi ya umakamu wa mwenyekiti wa Uvccm,fuatilia au uliza utapata habari kwa waliofuatilia uchaguzi wa Uvccm.inajulikana kila kona kuwa Hussein Bashe ndio alikuwa kijana wa Rostam anatoka Tabora na ndiye alikuwa akipambana na Benno Malisa kwenye uchaguzi wa Uvccm desemba na kuleta upinzani wa hali ya juu.kwa maelezo yako hapa kuwa Benno alikuwa mtu wa Rostam sikubaliani nawe huna source ya uhakika kwenye hili.
Adam Malima sio kweli kuwa alisaidiwa na Rostam wala hakuwa mtu wa Rostam.

Kakalenda kasema kuwa 1994 Rostam alikuwa kapuku,1994 hiyo hiyo prof Kapuya alikuwa kwenye harakati za kampeni za ubunge na mwaka uliofuatia akawa mbunge/waziri.hakuna conection hapa.au kusema kuwa Kapuya alipata ubunge kupitia kwa Manji nalo halina msingi 1994 Manji hakuwepo kwenye ramani ya wafanyabiashara wenye kujulikana ilikuwa baba yake na si yeye.

DR.Idrissa alikuwa gavana wa BOT na mkurugenzi mkuu wa NBC kabla ya Mkapa kuwa rais au kuwa Vodacom na Akiba bank Ltd,hilo nalo uzingatie.
Lowassa ni mtu wa karibu na Rostam kwa miaka mingi anaingia wapi kwenye jedwali hili?

Emmanuel Nchimbi ndio waliokula fadhila za uchaguzi toka kwa Rostam 2005 DR.Gama anaweza kukupa ushahidi vizuri juu ya hili na ugawaji wa simu za mkononi kwenye uchaguzi songea mjini.

William Ngereja ni mwanachama wa Victoria Club kama unaijua ambayo moja ya majukumu yake kutafuta vijana wa kanda ya ziwa wenye uwezo wa kuongoza mwaka 2005 club hii ilikuwa na zaidi ya milioni 200 kufanikisha azma hiyo jee Rostam yumo humo? swali hili sote tutafute jibu,
A
 
Watanzania tusiwe wajinga kiasi hicho kufikiri matatizo ya Tanzania ni ya mtu mmoja badala ya system nzima ambayo ni mbovu na imeshindwa kutimiza majukumu yao. Hii ni tabia ya watu ambao wanashindwa kukubali part yao katika failures hizi mbalimbali na badala yake wanakimbilia kutafuta scapegoat.

Hata leo akifa RA ufisadi hautaisha Tanzania. Ni siasa za mufilisi kuamini kwamba nchi inayumba shauri ya mtu mmoja. Huyo RA hajaenda kuiba bank kwa mtutu au hajawafunga kamba viongozi wetu, amefanya anayofanya kwa kutumia watu ambao sisi wenyewe wengi wetu tukiwepo hapa JF tumewaweka serikalini pamoja na makosa yao mengi ya huko nyuma.

Miaka 20 iliyopita hakukuwa na ufisadi na bado nchi ilikuwa maskini pamoja na jitihada kubwa za watu kama Nyerere. Sasa badala ya kuelemisha jamii juu ya tufanye nini ili kuwasaidia wananchi wengi hasa wa vijijini ambao wanaishi kwa dhiki kubwa, kushuka kwa elimu, huduma mbovu za afya, mifuko iliyotoboka, sisi tunatumia zaidi ya 90% ya muda wetu kumjadili mtu mmoja tena with zero result.

Watu hao hao ambao kwa wakati mbalimbali walikuwa wakishirikiana na RA huku wakijua madudu yake, leo wanajifanya ni vinara wa kutuambia matatizo ya TZ ni RA.

Ili Tanzanzania iende mbele ni muhimu sisi sote nikiwemo mimi mtanzania, tujiangalie tena kwa kioo na kuona vipi tunaweza kubadilika na kutenda haki kwa watu wetu, kabla ya kummulika mtu mwingine kwa kioo hicho, tujimulike sisi kwanza. Tuna uwezo wa kubadili matendo yetu kabla ya kubadili matendo ya mtu mwingine.

Ni sawa ni vizuri kuweka pressure kupambana na madhambi mbalimbali katika jamii lakini sio kwa kiwango cha sasa cha upotoshaji kuonyesha kwamba kama sio RA nchi ingekuwa na mabomba yanayotoa maziwa. Nenda kwenye kampuni zozote za Tanzania au institutions za serikali au hata kwenye majumba ya wasomi, utagundua madudu lundo tu kwa muda mfupi. Je na huko nako RA ndiye anatutuma?

RA tumemtengeneza wenyewe shauri ya tamaa zetu za haraka haraka na kufikiri maisha bora yanakuja kwa ujambazi. Kuamua kusaliti mamilioni ya wananchi waliotupa nafasi ili tujilundikie mapema na kuishi kama tuko ahera. Leo sisi Watanzania wote tukiamua kutimiza wajibu wetu, hao akina RA hawatakuwepo.

Ni nani mbunge wa CCM ambaye anaweza kuapa kwa mungu kwamba hakufaidika na mapesa yaliyooza ya Rostam na genge lake? Mtu akisema hivyo atakuwa anadanganya tu kama wanavyodanganya kwenye mambo mengi.

Ndio maana watu wengine tumepunguza kuchangia JF kwasababu mwelekeo sasa umeanza kuwa mtu badala ya system au fikra. Tumeanza kugeuza fikra zetu na kuanza kuwa mimi na yule au sisi na wale. Tunajaribu kwa nguvu zote bila mafanikio kuingiza pumba kwenye vichwa vya Watanzania ili waweze kuamini kwamba tatizo letu ni mtu mmoja.

Binafsi naamini mawazo kama haya hayamsaidii mtu yeyote na badala yake yanazidi tu kuligawa taifa. Lazima tutengeneze principles ambazo tuko tayari kuzisimamia na kuzilinda bila kujali aliyekiukwa na RA au Mengi. Vinginevyo na sisi wengine tunageuka kuwa vikaragosi vya hawa wababe ambao wameitumia system kufika pale walipofika na sasa wameamua kugeukana.

Umemaliza kila kitu Mtanzania kwani hata timing ya mjadala huu umekuja wakati mbaya.

inawezekana mleta mada akawa hana uhusiano na Tajiri Mengi lakini ni vigumu kuamini kuwa mawazo yake haya hayajaathiriwa na kauli ya Mengi dhidi ya mafisadi papa.

vyema Mwanakijiji ungeweza soma makala ya Jackson Manyerere Gazeti la Mtanzania Jumapili hii 26.04.09 amehoji mambo mengi juu ya kauli ya bwana Mengi mfano jee Gavana wa BOT ambaye alikuwa Mtanzania mzalendo vipi asilaumiwe kwa uzembe wake kazini na uzembe wake wabebeshwe mafisadi papa?
Katibu mkuu wa Hazina alishindwa kufanya kazi yake jee Manji au Rostam wanahusika vipi na uzembe wa Mgonja? Ununuzi wa rada na ndege ya serikali huko Rostam anahusika vipi?

tusitafute mchawi au wachawi tujitizame sisi wenyewe kwanza.ubaya zaidi mjadala kama huu umeingiliwa na mapenzi ya vyama kama inavyosemwa kuwa MENGI ni mfadhili wa helkopta chadema na Rostam ni mfadhili wa wana ccm,kabla ya Kagoda kwa Rostam kama inavyosemwa pia MENGI alichukua pesa NBC na hajalipa hadi sasa toka 1990s.Ukweli wetu nje ya Rostam uko wapi?

kutokana na nukta hapo juu inakuwa vigumu kwetu sisi wafuasi kuwa neutral kwenye michango yetu humu jf kwani tumejikita kwenye ushabiki wa vyama au timing ya mjadala sio nzuri.
 
Wa Tanzania wote: D Biashara.

Labda uwe hujawahi kutumia Voda kupiga au kupigiwa au hujawahi kunywa chai, kwani kote yumo.

Mwanakijiji unakumbushwa kwaya mimi hii thread yak inanikumbusha rusha ro '' kama unaweza, panda juu nenda ukazibe''
 
Kwa hio mkuu tunaweza kusema kwamba RA huwa anashiriki kupanga cabinet ya serikali![/QUOTE
sio kweli ahusike kama nani? kwahiyo Mizengo Pinda amewekwa na Rostam Aziz? naona mnampa nguvu asizo nazo.kama ana uwezo huo kwanini hakuzuia swahiba wake Lowassa asivuliwe Uwaziri mkuu?
 
hayupo kwenye jedwali la RA

Mkuu, kama alikuwa mgombea Mwenza 2005, halafu tumejadili hapa kwamba CCM ilifadhiliwa na RA pamoja na mafisadi wa aina yake,ni ktk mfumo huo huo naye alifaidika ama direct au indirect katika ushindi wa Kishindo walioupata! Au unataka kusema hajui kwamba walihisaniwa na nani kwenye hili?
 
Dr Dau ni Fisadi mkubwa na nitamuanika hivi karibuni,Nini alikifanya Bandari na kwanini yeye na Mkullo hawaelewani?

Walikwaruzana wapi?na kwanini nasema DAU siyo Mtu safi..Wote wezi tu na Mungu atakuja kulipa.Mie nauliza hivi hakuna waganga wa kufanya mafisadi wawe vichaa?

Ukifanya hivi unaweza kutoa majibu ya maswal mengi ambayo yananitatiza..
 
- Mzee Ndejembi - Rostam alimpa Shillingi Millioni 10 mwaka 2000 zilizomuwezesha kushinda Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma - kundi A.

FMES!
 
1. Abdulaziz - RC.
2. Lukuvi - RC.
3. J Mongella - DC.
4. Membe - Ubunge.
5. Mzindakaya - Ubunge.
6. Nyami - Ubunge.
7. Sita - Ubunge & U-spika.
8. Mahanga - Ubunge.
9. Guninita - CCM Mkoa.
10. Kamala - Ubunge.
11. Marmo - Ubunge.

- Hawa wote hapo juu wamepewa hela za Kagoda na Rostam, ili kushinda nafazi zao za ubunge na uongozi wa CCM. Tunaendelea kukumbuka pole pole!

FMES!
 
- Mzee Ndejembi - Rostam alimpa Shillingi Millioni 10 mwaka 2000 zilizomuwezesha kushinda Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma - kundi A.

FMES!

Nilifikiri Wagogo ni watu wa Dini sana. Kumbe kwa Wagogo pia kuna "vyura wanaomeza..."
Asanteni kwa data. Mwaka huu watajifunza kunawa kabla ya kula.
 
Dr Dau ni Fisadi mkubwa na nitamuanika hivi karibuni,Nini alikifanya Bandari na kwanini yeye na Mkullo hawaelewani?

Walikwaruzana wapi?na kwanini nasema DAU siyo Mtu safi..Wote wezi tu na Mungu atakuja kulipa.Mie nauliza hivi hakuna waganga wa kufanya mafisadi wawe vichaa?

Fanya fasta maana sikuzote huwa anasahaulika huyu.
 
Back
Top Bottom