Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
Nyangumi, hicho ndicho CCM imejaribu kufanya.. nacho ni kushika hatamu na utamu wa nchi!! Wao wanajenga, wao wananunua, wanalima na kuvuna!! Mwananchi wa kawaida hahitaji kufanyiwa kila kitu. Tunachohitaji ni kujengewa mazingira mazuri ambapo soko linatuamulia nani afanye nini. Nimeshaeleza toka huko nyuma ni nini wapinzani wafanye. La kwanza, wawe majasiri kusema:
a. Upinzani ukichukua madaraka itaundwa tume huru itakayochunguza mali zote ambazo viongozi waliopita walichuma wakiwa madarakani na kuoanisha na mapato yao. Wale itaoonekana mapato yao hayawiani na mali zao basi mali zao zitafilisiwa! Wasema watalifanya hilo ndani ya miezi sita ya mwanzo ya utawala wao.
b. Wapinzani wawaambie wananchi kuwa kila kijana wa Kitanzania aliyefaulu kwenda chuo Kikuu Serikali itagharimia nusu ya ada zao na matumizi. Anayepata daraja la kwanza kila mhula analipiwa 75% Wanaoenda shahada ya uzamili watalipiwa 75% na wa shahada ya Udaktari 100% Hii ni kuonesha kuwa upinzani unatilia maanani elimu. Na kwenye hilo la Elimu Wapinzani waseme chini ya uongozi wao, Elimu ya Msingi hadi ya Sekondari (O'Level) itakuwa ni ya bure!
Pia waamue kusema kuwa yeyote anayetaka kusomea Udaktari (Utibabu) analipiwa gharama zote! (nafikiri CCM inafanya kitu kama hiki).
c. Wapinzani waweke wazi kuwa pindi wakichaguliwa, watasitisha mara moja mikataba yote ya Nishati na Madini na kurenegotiate na kampuni yoyote ambayo inataka kuendelea kufanya kazi Tanzania. Katika kufanya hivi wawaambie wananchi kuwa Serikali hiyo mpya itawachunguza viongozi wote waliohusika na mikataba hii na wale ambao walinufaika kwa namna yoyote ile watafikishwa mahakamani kwa ufujaji wa mali ya umma.
d. Wapinzani wawahakikishie wananchi kuwa Watadumisha Muungano wetu na umoja wetu wa kitaifa! Hakuna mabadiliko yoyote ya mfumo au utendaji kazi wa Muungano yatakayofanywa pasipo ridhaa ya wananchi.
Hayo ni machache ya kuanzia!
Huyu ndiyo Mzee Mwanakijiji ninayemjua mimi. Mwingine anakuwaga photocopy. Good points. Of course you need to be careful in the presentation, lest they easily backfire!