Je, wapinzani ni wakombozi?

kama sheria inasema siku 7 basi itakuwa ni ujinga kunyamazia kitu hiki badala ya kupinga mahakamani mara moja.
 
NEC imenishangaza,eti imewaongeza wapiga kura 56 tuu huku ikikataa kuwaandikisha wapiga kura wengine wenye vigezo
 
NEC is just like a revised CCM. Kwa hiyo lazima itekeleze matakwa ya boss wake CCM.
 
Tume imetoa ufafanuzi na kukanusha kuwa hivyo vituo 55 unavyovisema havipo na kama kuna ushahidi wa kuvitambua vitue hivyo si muutoe ili hatua zichukuliwe!
 
Tunahitaji
ukombozi
wa kweli
yatupasa kupiga kelele. Tusikae kimya siku si nyingi tutakuwa tumepata ukombozi. Kuendelea kubaki kuwa mwana ccm ni kwamba wewe ni maiti.
 
Kwa kuelewa hulka za binadamu bila kujali itikadi zao na mitazamo yao kutegemea wapinzani kuwa wakombozi wa Tanzania kwa vile tu ni Watanzania wanaotoka Chadema, TLP, CUF, NCCR, au vyama vingine ni mategemeo ambayo yatapeperuka kama unyasi upeperushwavyo na upepo, ni kama umande unavyopukutika kwenye majani asubuhi inapofika! Manabii wa upinzani wako wapi watutabirie?

Mzee MM, mimi nijikite kwenye para ya mwisho. Ninakubaliana na wewe 100% kwa assessment yako. Ila mimi binafsi bado ninaona wapinzani ni wakombozi kwa sababu zifuatazo
  1. Kitendo cha CCM kushindwa uchaguzi na chama mbadala kuchukua uongozi itakuwa ni one big step towards having a government which is accountable to the people not party tycoons.
  2. Unapokuwa madarakani kwa kuahidi kufanya kitu fulani, ni dhahiri utajitahidi ukijua kuwa kutofanya hivyo ni kuwafanya waajiri kukuweka kando uchaguzi mwingine
  3. Kitendo cha CCM kushindwa kitawafanya watu wanaoona siasa ni ajira kukaa pembeni na kuacha watu wanaoona siasa ni wito na uzalendo wa kufanyia nchi mazuri
  4. Kutokuwa na chama monopoly wa serikali maana yake ni kuwa vyama vitashindana katika kuonesha nani ameweza kuipeleka nchi katika prosperity. Hivyo basi kupisha vichwa makini vyenye uwezo wa kijasiliamali wa kuendeleza nchi kuwa kidedea kila wakati.
  5. Kwa CCM kushindwa itakuwa ni reset button kwa nchi kujiangalia upya katika kipindi kingine baada ya kupoteza miaka karibu 50 baada ya uhuru bila kuwa na mikakati practical, ukiacha slogans za kuombea kura.
  6. Ule mtindo wa kupeana vyeo kwa urafiki na kujuana bila kujali uwezo utaisha, maana kumuweka mbumbumbu katika nafasi ya utendaji ni kujichimbia kaburi uchaguzi ujao.
  7. Pia ni matumaini yangu kuwa CCM ikiwa nje ya madaraka Tanzania itapata mageuzi ya kweli ya kiuchumi na kisiasa. Kutakuwa na utendaji mzuri wa serikali na uwajibikaji tofauti na kulindana kunakofanywa na CCM
  8. Ni matumaini yangu kuwa vyombo vya dola vitakuwa huru bila kuwa affiliated na chama chochote na hivyo kutokumuogopa mtu yeyote kwa amri ya yeyote, hii ni baada ya kupata katiba ya watanzania (Siyo hii ya CCM inayopigiwa chapuo sasa)

Kwa maana hiyo bado ninaamini kuwa Tanzania yenye uongozi bora na imara itakuwa ni Tanzania yenye kujali watu zaidi kuliko makundi ya kirafiki yanayofanywa na CCM. Ni matumaini yangu kuwa CCM nje ya power itakuwa ni chachu nzuri ya kuwapukutisha kupe wote walioji-attach kwenye chama na kutoka povu kwa kujifanya makada wazuri wakivizia nafasi za uongozi ili waliibie Taifa na Watanzania.

Ni ukweli usiopingika kuwa Matatizo haya ambayo yamejengwa polepole kwa kipindi cha miaka hamsini hayawezi kumalizwa na chama chochote cha siasa kwa usiku mmoja au muhula mmoja au miwili, ila nina hakika kuwa watanzania watakuwa better-off when CCM is out of power. Pia ninaamini kiusalama wa Taifa na ustawi wa amani itakuwa ni national security interest when CCM agrees to let Tanzanians choose freely their leaders without intimidations and chakachua. Ule usemi wa mtoto akililia wembe mpe una maana kubwa sana hapa katika kunyamazisha kilio cha watanzania, kwani wengi wana kiu ya mabadiliko, kama watayapata pasi watatulia, ila kama watanyimwa basi wanaweza shawishika kufanya kitu kibaya na kusababisha maafa yasiyo ya lazima.
 
Hoja hujibiwa kwa hoja!

Lunyungu:

Wapinzani wanataka tuwaamini, wanataka tuwape madaraka! Ina maana hadi hivi sasa wamejiamini kiasi cha kutosha na wameamini wameimarika kiasi cha kutosha hadi wamefikia kumsimamisha mgombea Urais. Walishindwa. Kwa wao, kufikia mahali kusimamisha wagombea Urais, Wabunge na wawakilishi kibao ina maana wako tayari kuongoza na kutawala, ama sivyo?

Je kama wapinzani wangeshinda uchaguzi 2005 na kuchukua Ikulu, na Bunge je ni mabadiliko gani yangetokea Tanzania hadi hivi sasa (mwaka mmoja baadaye)? Mimi nawakilisha mawazo ya Watanzania ambao hawajaridhika na CCM na hawajavutiwa na upinzani! Lakini wakipewa uchaguzi wa pande hizo mbili wanaipa kura ya ndio (licha kusita sita) CCM! Ni jukumu lenu wapinzani kuwashawashi Watanzania ni kwa nini wawape madaraka ya kuongoza nchi yetu!!

Msituambie tuwape madaraka ati kwa sababu CCM mbovu na inanuka, tunajua hilo, tuambieni kwanini tuwape nyinyi madaraka na tofauti ya viongozi mtakaowaweka nyinyi na wale waliopo CCM ni nini? Ninawapa somo la bure hapa, mkiweza kujenga hoja inayojibu swali hilo basi mnajitengenezea njia nyeupe kwenda Ikulu!!

Jasusi:

Kwa karibu miaka zaidi ya kumi Democrats walikuwa upinzani na Republicans wakishikilia vyombo vyote vya Ikulu na Bunge. Je, jukumu la kujiimarisha Democrats lilikuwa ni la Republicans kutengeneza mazingira mazuri ili Democrats washinde? Kwanini, unafikiri Democrats walishinda? Unafikiri ni kwa sababu watu wanadhani Democrats ni tofauti sana na Republicans? la hasha! Democrats walijenga hoja kuwa nchi inahitaji kufuata mwelekeo tofauti na wa Republicans na pia viongozi wa Democrats walishajulikana, hakukuwa na suprise!

Ndo maana ninawapa somo la bure wapinzani wa Tanzania:

a. Endapo wanasubiri na kuombea kuwa CCM itaweka mazingira mazuri ili wao wachukue nchi "kwa upole, kama kumsukuma mlevi" wafikiri tena. CCM haina nia wala wazo la kuona upinzani unaimarika Tanzania! It is not in their best interest!

b. Jukumu la kuviimarisha vyama vya upinzani ni kwa wale waliomo ndani ya vyama hivyo! Tarehe 8/10/2005 Freeman Mbowe akizungumza wakati wa kampeni kule Mbeya alisema kuwa kukosekana umoja katika kambi ya upinzani kumedhoofisha upinzani kiasi kwamba wameshindwa kupigia kelele kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi! Alifanya nini kuunganisha nguvu zake na wapinzani wenzake? Je, anafanya nini leo ili kuunganisha kambi ya upinzani kabla ya 2010?

Sheria ya kuruhusu vyama kuungana itajadiliwa baadaye mwaka huu na bila ya shaka itapita. Unafikiri itafanya vyama hivyo vikubwa kuungana na kuunda chama kimoja au yatakuwa yale yale ya NARC Rainbow ya Kenya?

Kuhusu njia za kuimarisha upinzani Tanzania, mbona zipo nyingi na tumezitaja sana. Je wapinzani wa Tanzania wanasikiliza? Haya, ngoja nizirudie hapa.

a. Badala ya kunuia kupewa Urais kwenye uchaguzi wa 2010, wapinzani wadhamirie kuchukua Bunge, kwa kunyakua angala theluthi mbili ya Bunge zima. Kwa jinsi walivyo sasa hiyo itakuwa ni ndoto.

b. Kama wapinzani kweli wanataka kuongoza nchi, njia rahisi ni kujiandalia viongozi watakaochukua nchi. Kwa idadi ya wabunge walionao sasa, hata baraza la mawaziri wasingetosha! Ushauri wangu ni huu. Mara tu sheria ya kuunganisha vyama itakapopitishwa baadaye mwaka huu viongozi wa vyama vya upinzani vikubwa (Lipumba, Mbowe, Mrema, na Mbatia) wakae chini kwa pamoja, waandike Memorandum of Understanding ya kukubali kuviua vyama vyao na kuunda chama kipya kimoja kikubwa cha upinzani, kushirikishana mali za vyama hivyo n.k. Halafu ceremonically, watangaze kuvunjika kwa CHADEMA, TLP, CUF, NA NCCR na kuundwa kwa chama kipya. Wapo viongozi watakaopoteza nafasi zao na kwa maoni yangu, wenyeviti wote wa sasa wa vyama hivyo wasipewe uenyekiti wa chama hicho kipya!!! guess why?

c. Pindi wakishaunda chama hicho kipya, waandike ilani yao ya kuelekea 2010, wainadi kwa wananchi, na wana miaka karibu mitatu ya kuonesha ukomavu wa kisiasa na ya kuwa wanaweza kufanya kazi pamoja licha ya migongano ya huko nyuma na tofauti ya kimitazamo.

d. Jambo la nne, waanze kampeni ya kupata wanachama wapya, na kuwashawishi hata wana CCM mashuhuri kuungana nao ili kuipatia Tanzania mwelekeo mpya, kwani ule wa CCM umeshindwa!!

Quarz:

Sijasema mahali hata pamoja kuwa turudi kwenye Chama kimoja isipokuwa kama kuwepo kwa vyama vingi dhaifu na visivyo na mwelekeo ni sawa na kuwa na chama kimoja! Jukumu la vyama upinzani siyo kukosoa chama kilichoko madarakani (of course, ni sehemu ndogo ya majukumu yake). Jukumu kubwa la chama chochote cha upinzani ni hatimaye kuchukua hatamu za uongozi wa nchi na kutengeneza sera za kuongoza Taifa. Ndiyo sababu nimeuliza wapinzani wa Tanzania kweli wanaweza kuwa ni wakombozi wa Taifa letu? Sijauliza kama wanaweza kuwa wakosoaji wa Taifa letu!

Mimi hapa nawasaidia kimawazo ya jinsi gani vyama vya upinzani vinatakiwa kujijenga na kujiimarisha. Baadhi ya hoja ninazojenga, siyo kusudio langu kuipigia debe CCM bali kuwapa nafasi wapinzani wanaopitia humu wajue jinsi baadhi ya Watanzania wanavyowafikiria na hivyo kuchukua mikakati ya kuwashawishi kuwaamini. Hadi hivi sasa hakuna aliyenijibu angalau kwa kiduchu kuniambia ni kwa nini tuwaamini wapinzani badala ya CCM. Kung'ang'ania kusema CCM imeoza na haifai haitoshi! Tuambieni kwanini nyinyi mnafaa na hamjaoza?!!

mkuu, mi nafikiri kwanza katika bold uwe umejiridhisha vya kutosha kuwa wananchi huwa wanipa ccm pindi wanapopiga kura, una uhakika huwa wanaipa au ccm wanajipa wenyewe kwa kuiba ama kujiwekea kura ili kuzidisha wingi wa kura unaopelekea ushindi. ushahidi tunao sehemu n yingi ccm wamekuwa wakiiba kura hata tabata katika uchaguzi uliopita mgombea wa ccm alitaka kuuwawa na wananchi baada ya kukimbia na box la kura akisaidia na askari.
haya bado huwezi kusema vyama vya upinzani hawajafanya lolote wameshafanya baadhi ya mambo na kushinikiza mengi hapo ndio wapo wachache! kumbuka mkuu kuwa ikipigwa kura ya ndio au siyo lazima ccm washinde bungeni sasa mabadiliko ni magumu kuonekana ama kuja kirahisi. wangekuwa wengi hapo tungesema jambo la lawama. nafikiri wakipewa nchi wanaweza kubadilisha maisha ya mtanzania ikiwa kwa sasa kwa udogo wao wameshafanya vitu vingi ikiwa pamoja na kufanya uwazi wa mambo mengi yanayosaidika kudai mabadiliko.
udhaifu wa wapinzani ni kweli kuna migongano na mikwaruzo lakini hii haimaanishi hawawezi kufanya vizuri wakishika madaraka. kumbuka kuwa waliopo katika vyama vya upinzani ni binadamu wenye interest tofauti na tabia tofauti hata ndani ya ccm kuna migongano na mizozano.
wakipewa nafasi wataweza.
 
Back
Top Bottom