Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
Ukweli usiopingika kuwa walio wengi wanaamini hivyo ila ukweli ni kwamba CCM imetusaidia sana na kutufikisha hapa tulipo,ww fanya tathmini shule ya msingi umelipa Tsh 200/= kwa mwaka je fedha hii inatosha kumlipa mwalimu anayekufundisha kwa mwezi?jibu hapana basi serikali hii ya CCM tunayoichukia ndio inayojitoa muhanga kwa kuwalipa walimu,ila ni kwamba huwezi pendwa na wote na kuchukiwa na wote
Hizo sio pesa za CCM; ni kodi yangu na wewe. Walichofanikiwa CCM ni kuonesha kuwa kutoa huduma kama elimu na afya ni upendeleo (previledge) na sio haki! Kazi yangu mimi na wewe ni kuwaelimisha wananchi kuwa kazi ya kodi tunazolipa ni kwa ajili ya serikali kutoa elimu, afya na huduma zingine na wala sio kununua ndege ya kifahari, kumfanya Rais atalii dunia nzima, kufanya sherehe kubwa za sikukuu ya uhuru, kugharamia mazishi makubwa ya waziri, n.k.