Je umemuona kijana huyu

Status
Not open for further replies.

MNDEE

JF-Expert Member
Jul 10, 2009
491
68
Kijana wa umri wa miaka 17, mweusi na mrefu amepotea toka saa kumi jioni jana Jumanne June 4. Mara ya mwisho alikuwa amevaa kaptura nyeusi na flani yenye mistari. Jina lake ni Junior, ana matatizo na haongei (autistic), lakini anaelewa ukimuita jina na pia anaweza kufuata maelekezo rahisi.

Alitoweka toka nyumbani kwao maeneo ya Science Kijitonyama jana. Mara ya mwisho alionekana Tandale uwanja wa mpiria.

Polisi wamekataa kutoa msaada wowote wanadai mpaka yapite masaa 24, tatizo mtoto ni mgonjwa sio mtu mwenye uwezo wa kufanya maamuzi mwenyewe au kurudi nyumbani. Kama kuna kiongozi wa Polisi hapa, au kama unaweza kutusaidia tutashukuru.

Kama utamuona kijana huyu maeneo ya Tandale, Kijitonyama, Sinza, Mwenge au popote pale tafadhali toa taarifa kituo chochote cha polisi pia unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hii xxx-xxxx-xxx unaweza au niPM.

Tunahitaji maombi na tunatanguliza shukrani zetu. RB ya hii issue ni XXXXX

UPDate

 
Ahsante mkuu, niko kwenye harakati ya kupata picha toka Dar.
 
kama maeneo ya karibu kilikua na harusi au sherehe yeyote, jaribuni maeneo kama hayo... hawezi kua amelala nje, marafiki zake wa karibu wanaweza kua msaada mkubwa sana pia,
 
Maeneo ya karibu na kwao hayupo, ufuatiliaji wa nyendo zake baada ya kutoka kwao uliishia Tandale mitaa ya saa sita usiku. Kwa vile hatuna msaada wa polisi tunategemea jamii kutusaidia na tunakwenda nyumba kwa nyumba.
 
Kama mnajimudu kiuchumi jaribu pia kuweka matangazo kwenye vituo vya redio. Poleni sana!
 
Maeneo ya karibu na kwao hayupo, ufuatiliaji wa nyendo zake baada ya kutoka kwao uliishia Tandale mitaa ya saa sita usiku. Kwa vile hatuna msaada wa polisi tunategemea jamii kutusaidia na tunakwenda nyumba kwa nyumba.

poleni.
Naelewa hapo mlipo mna hofu sana.
Hata mimi nasikia hofu ila nina amini kabisa Mungu atamrudisha ndugu yetu salama nyumbani.
Tuko pamoja katika maombi.
Naomba atakapopatikana mtujulishe.
 
maliberali cjui kama wamembakiza

Hapa ndo naamini kuwa kila mtu mungu kamuumba kivyake, yaani kuna watu wa ajabu sana huku DUNIANI. Mimi nashauri maeneo husika waone viongozi wa Misikiti mara nyingine huwa wanatoa matangazo kuitaarifu jamii juu ya watu kama hawa. Ploeni na mUNGU atawasaidia apatikane akiwa mzima wa Afya
 
poleni.
Naelewa hapo mlipo mna hofu sana.
Hata mimi nasikia hofu ila nina amini kabisa Mungu atamrudisha ndugu yetu salama nyumbani.
Tuko pamoja katika maombi.
Naomba atakapopatikana mtujulishe.

Ahsante tunashukuru kwa maombi, ni kipindi kigumu, kutofahamu mtoto wako yuko wapi na hujui amelala wapi wala amekula nini na nini kinaendelea. Tuko kwenye maombi na tunaamini Mungu atamlinda na kumrudisha.

Tunawaomba wanajamii mtusaidie kushare hii taarifa kwa majirani, makazini na kwa kila mtakae weza. Nitawaupdate kinachoendelea.
 

Mkuu kuna mtu ameshauri kuwa mjaribu kwenye kutangaza redioni.
Nadhani inaweza kusaidia kuharakisha kupatikana kwa ndugu yetu.
Sidhani kama gharama zitakua kubwa sana.
Pia nina imani wanaweza kusaidia kutangaza hata bure maana nao ni binadamu sio kila kitu watataka pesa.
 

Hapo nilipo weka red Yaani Polisi wanataka hadi ameng'olewa meno na kupelekwa Mabwepande ndani ya saa 24 ndipo waibuke kutoa msaada. Je angekuwa Mtoto wa Kamanda Kova wangesubiri saa 24 zipite kwanza ndipo waanze kumtafuta??? Kweli sheria za Kikoloni tulizorithi zimetuharibu sana!!!
 
Bado hajapatikana, watu wako mitaani na kwenye vyombo vya habari. Mimi niko mbali najaribu pia kufuatilia kwa karibu.
 
Atapatikana tu inshallah. taarifa hii umeweka facebook pia?
maana kuna vijana wengi wapo facebook hawapo humu JF
 

Misikiti imeombwa na wameshatangaz. Hawa watu wengine ni kuwaombea Mungu, watu tuko kwenye tatizo mtu mwingine analeta maneno yanayokatisha tamaa. Hatukuomba hili litukute na tunaamini litapita.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…