Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
Masikini jk,wahanga waliokwisha wekwa na watakaowekwa zaidi!..Ni vijimambo tu
Inaonyesha jinsi gani watu wana confidence kuexpress wanavyotaka na hii ni mojawapo ya gharama za teknolojia. We have to face it!..
 
Gembe ile picha bado ipo.

Hivi haiwezekani kuwatoa hawa WALA VYA BURE yaani viongozi wa dini? Ingelikuwa poa sana kuwaweka pale Pengo na rafiki zake wakiwania visenti vya Lowasa. Ila ambao sielewi ni WATUMISHI WA MUNGU. Sijui kwa nini wanajiita hivyo ilihali ni watumishi wa wanasiasa. Mie naona heri viongozi wa dini wawe wanapita kugombea uongozi huo ili na wao watudanganye from day one wakiwa wanaomba kazi. Watoe hongo kupata kazi hiyo, watuahidi maneno matamu na kuchinya ng'ombe siku ya mkutano. Tupewe na T-shirt mpya maana hatimaye tutavaa vazi jipya baada ya miaka kadhaa tukiwa tunavaa vya kununua umeinama.

Bahati mbaya muda sina na picha zao sina. Vinginevyo hawa PENGUIN wala vya bure ningelilala nao sambamba kwa huyo Zeutamu hadi washike adabu zao na waanze kuwa watumishi wa Mungu kwelikweli na si utapelitapeli.

Mkuu sikonge,

Issue yangu ya kwanza ni kwamba maneno yanayohusu wachungaji na kashfa zao, hayana uhusiano na thread hii, so nikasema labda ungeipeleka kny thread husika!

La pili, kwa maoni yangu si sahihi kuweka comments za ujumla .like, mapadre...bla blaaaabla, wachungaji....blablabla....maaskofu.....! mashekhe etc ..kama unakuwa na uhakika na unalo sema , just point out kwamba kwa mfano, Askofu Pengo kafanya hili na lile au Kakobe kafanya ......! Ukijumlisha unakwaza waumini wao, updre ni taasisi nyeti ambayo waumini wao wanaiheshimu sana...so better kuheshimu hilo na sisi!

Mimi binafsi ni ex seminarian, so najua maisha ya kiroho ya mapadre wetu hasa, wanajua kuna exceptions pia, najua pia kuna case by case ambazo naweza kuzitaja kabisa zilizotokea na kuleta mkanganyiko kanisani......!

Lakini siwezi sema eti Mapdre ni wahuni, matapeli...though kuna padre mmoja (sasa ni marehemu, RIP) alishanitapeli mkwanja wangu! siwezi generalise kusema...wachungaji ni wezi....kuna baadhi walikuwa fantastic acha kabisa!


NL,

Nafikiri hadi sasa yameandikwa mengi sana humu ndani na si hii issue ya Kikwete na Ze-utamu. Wamewekwa humu leo hadi akina Mange, Erick, Nsia Swai na wengine kibao. Kama tunajadili, hatuwezi kuwa wafungwa. Mwisho nilichosema ni kuwa "hawa viongozi wa dini matapeli, walitakiwa kuwa huko kwenye ze-utamu..." Maadamu issue moja wapo ni hiyo zautamu, tatuizo liko wapi? Yaani lazima tuongeee Kikwete vs zeutamu siku nzima? Kila kitu kinazaliwa, kukua na kufa. Hata hii issue hivyohivyo. Hivyo sioni ubaya wa kusema kuwa "badala ya kumuweka Kikwete, walitakiwa wawekwe vingozi wa dini Mafisadi...."

Kuja kwenye issue ya pili, sijui kama umesoma vizuri nilichoandika. Nimeandika wazi kabisa kuwa Watumishi wa Mungu Matapeli. Kama mtumishi wa Mungu si tapeli basi huyu alale salama wala sina shida naye. Hata mie nawafahamu watu wa dini wenye dini kweli. Hao na waendelee hivyohivyo ingawa hao maboss wao wanawaangusha sana.

Nakuelewa kama umesoma Missionary. Hata mie mwanzo nilikuwa mtu wa kuheshimu sana dini na watumishi wa Mungu. Siku moja nikiwa nchi za watu tulienda harusini, na baada ya misa tukaenda kujichana na mnuso mkali. Nilishangaa Padri mmoja akicheza na mama mmoja usiku mzima na watu wakiangalia kwa jicho nusunusu na wengine wakisifia tu kuwa Padri anaongoza vizuri katika kucheza (chezaji za wazungu).
Kwenye harusi nyingine ndiyo ikawa kali zaidi. Padri mmoja aliyekuwa ANAKULA SAHANI moja na mama fulani kwenye mnuso, kufika saa tani usiku ghafla akapotea na yule mama. Mzee mmoja akaana kuuliza "Huyu Padri yuko wapi? Si alikuwa hapa na huyu mama, wamepotelea wapi wote? Ngoja nimtafute huyu Padri nimtie adabu...." Watu walicheka. Hii mifano iko mingi.

Tanzania kuna akina Pengo, Mtikila, nk ambao kukicha wanamsafisha Lowasa, Mkapa na genge lao. Mie ndiyo nasema hao. Na nimeandika hapo juu kuwa unawatoa wakiwa kwa Lowasa wakipata visenti. Sasa ndiyo narudi kama mwanzo. Tusiwe watumwa kwenye uandishi. Huwezi kusema chochote kisa watu watasema una-generalise. Hebu acheni tupumue. Yaani hadi niandike kila kitu? Huwezi kusoma ujumbe wa mtu ukajua ujumbe wake analenga watu gani? Hebu angalia tena ujumbe wangu hapo juu uone kama nilimaanisha watumishi wote wa Mungu au wale Mafisadi/Matapeli tu? Sasa wee Mchungaji unasaidia watu watapeliwe kwenye DECI, tukweke wapi? Tukisema tuseme kwa uangalifu sana maana tutaonekana tuna-generalise? Wao wanapotapeli, mbona hawaogopi kuwachafua wenzao na kazi yao? Kama kuna wa kuona aibu ni wao na si sisi tunaokoma nyani...
 
Significant hits !!
Currently Active Users Viewing This Thread: 135 (56 members and 79 guests)
911, B52, BabaDesi, Bint, BINTI SAYUNI, bob, Bonnie1974, borntown, Burn, Congo, Damky, Dawson, Degauche2008, Gozigumu, Iteitei Lya Kitee, jethro, Kaka Mdogo, Kang, Kidatu, Lifer, Magehema, mahesabu, matejoo, Mbogela, Mbweem, mchizi, mimi, Mkora, Morani75, mshiiri, mwalimu, mwanahawa, MyTanzania, Nassoroc, newmzalendo, Ngorunde, obhusegwe, Opaque, rolemodel, sambah, samvande2002, Sem, semilong, Shaycas, Shemzigwa, shishye, Sikonge, Single D, SMU, Son of Alaska, ygjunior, Zak Malang, Zanaki, Zungu Pule
 
Mkuki kwa Nguruwe kwa binadamu mchngu, watu kibao wamechafuliwa kule. Ila siku itakapokuwa zamu yako ama ya ndugu wako wa karibu ndio utajua kuwa ile web haifai.

Mimi binafsi nimepatwa na simanzi hasa ukizingatia huyo bwana sijui bibi ametuweka hata sisi kwenye kikaango...maana wasivyo na dogo watawasaka wote wanahusika na teknolojia hizi. Nasema potelea mbali.

Kwa muda mrefu serikali imekalia kimya suala la kuwasaka wamiliki wa mtandao huo pamoja na kulalamikiwa sana wananchi...waswahili husema ukicheza sana na mbwa utaingia nae msikitini...kwahiyo mi sioni sababu ya kushangazwa na ushenzi huo ila nafikiri wanausalama watakuwa makini zaidi na teknolojia hizi..

Kwa upande mwingine naungana na wanajamii kulaani kitendo hiki kwani si tu kimemdhalilisha Mhe. Rais bali wanaume wote nchini Tanzania kwa kuwa amejaribu kuionyesha dunia kinachoendelea hapa kwetu....hiki kitendo kwa kweli hakivumiliki na akipatikana huyo mwanaharamu (atakuwa hivyo tu...sidhani kama anawazazi halali) naomba na mimi nipatiwa kipande cha mwili wake hata ikiwa sikio sawa tu.

Tujo pamoja nawe Mkuru na tutahakikisha Mnyama huyu anapatikana kwa gharama zozote zile na hii si tu kwa ajili yako bali kunusuru maadili ya vizazi vijavyo na yetu kama watanzania.
 
masikini jk,wahanga waliokwisha wekwa na watakaowekwa zaidi!..ni vijimambo tu
inaonyesha jinsi gani watu wana confidence kuexpress wanavyotaka na hii ni mojawapo ya gharama za teknolojia. We have to face it!..

dada belinda sasa tovuti hiyo imeshafungwa toka saa 10 mchana wa leo saa za afrika ya mashariki
 
dada belinda sasa tovuti hiyo imeshafungwa toka saa 10 mchana wa leo saa za afrika ya mashariki

Ipo hewani wewe! labda Tanzania nimeangalia sasa hivi...habari ndo hiyo
 
Mi nakwambia jamiiforum ingeruhusu kutoa mitusi basi mi nafikiri ningeandika kijitabu...kwa kweli inaniuma ile mbaya bora uwe hujaiona ile picha jamani unaweza kutoa hata chozi hasa ukijua wazi si ukweli na amefanyiwa mtu muhimu sana katika usalama wa nchi. Mi najua uwezekana wa kuifuta kabisa ni ngumu labda kampuni ya google ilegeze masharti yake. Uzuri ni kwamba wanaweza kupatikana kirahisi kwasababu ile si blog kama ile ilivyokuwa mwanzo bali ni tovuti ambayo huwezi kuipata bila kulipia.

Sasa kama walilipa kwa credit card au bank...then wanakamatika kabisa. Muhimu ni kuwashiwishi host wa ule mtandao ambao watakuwa google kutoa information zao basi hao hadi kesho tushawatia mikononi. Mgogoro ndo wenzetu huko majuu wako serious na kufuata sheria....yaaani umaskini huuuu jamani we unafikiri angekuwa Obama wangekubali???
 
alafu utamu ameweka signature yake kwenye picha
kweli amejiandaa na litakalokuwa na liwe
hela zetu wanagawana wenyewe kwani sisi hatusikii uchungu
akienda fbi/cia kuishtaki ze utamu watamwambia toa upuuzi hapa hata sisi rais wetu yuko na hizo picha kibao rudi kwenu TZ ukakamate mafisadi na uwache kuzurura ovyo
 
naomba na mimi nipatiwa kipande cha mwili wake hata ikiwa sikio sawa tu.

Mie nakupa kipande chake cha nyama kiitwacho ........... Mhhh sasa utakifanyia nini? Sijui kama kweli ni hasira au na mie niandike........
 
dada belinda sasa tovuti hiyo imeshafungwa toka saa 10 mchana wa leo saa za afrika ya mashariki

Shy mkuu
Labda siyo Utamu unayoijua wewe ila kama ile ya sijui kujing'ata kwa ulimi ipo sana tu na inang'ata huku inapuliza kama panya!..

Hivi wewe si mtu wa ICT, hiyo tunaitaje? ICT penetration au?! Maana kazi kweli kweli sasa ni kama nyanya chungu.
 
Haya malalamiko pelekeni tume ya Mawasiliano na kwa ISP wote ndani ya Tanzania waiblock ili isiwe accessible nchini.
Na kama umechafuliwa au ndugu yako amechafuliwa wasiliana na Host wao ukiambatanisha na ushahidi
 
Haya kwa wale mnasema MAADILI YA KIAFRICA,je haya ya Mkapa ndiyo mnayomaanisha?


Na Saed Kubenea

MwanaHALISI~Maslahi ya Taifa Mbele

RAIS mstaafu Benjamin Mkapa amelalamika kuwa anasakamwa na wanasiasa na anachafuliwa, MwanaHALISI limeambiwa.

Kwa miaka miwili mfululizo sasa, Mkapa amekuwa akitajwa na kuhusishwa na baadhi ya tuhuma za ufisadi na utovu wa "utawala bora" wakati wa kipindi chote cha utawala wake – 1995 hadi 2005.

Kufuatia malalamiko hayo, wachunguzi wa siasa za Tanzania wanasema inawezekana ukaidi wa Mkapa umeyeyuka na sasa yeye ameona kuwa "ni maji shingoni."

Taarifa zinasema Mkapa alitoa malalamiko yake kwa mwanasiasa mmoja nchini (jina tunalo) nyumbani kwake, Sea View, Dar es Salaam hivi karibuni.

Alimkomalia mwanasiasa huyo kuwa na yeye anashiriki kumchafua huku akionyesha kuwa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ya "kuwaacha viongozi wastaafu kupumzika" kuwa imeshindikana kutekelezwa.

Rais Kikwete aliwaambia waandishi wa habari mwaka 2007, alipoulizwa iwapo atachukua hatua dhidi ya Mkapa kufuatia tuhuma alizokuwa akibebeshwa, kuwa viongozi waliostaafu waachwe wapumzike.

Kilio cha Mkapa kimekuja kufuatia mlolongo wa tuhuma za kale na sasa kurudiwa mara kwa mara na kumnyima, yeye na familia yake, kuishi kwa raha hata katika jiji la Dar es Salaam ambako aliwahi kukutana na vijana mitaani wakiimba "Fisadi! Fisadi! Fisadi!"

Chanzo cha taarifa kinasema, hata hivyo, mwanasiasa huyo hakumsaidia Mkapa, kwani alikana kumkashifu na kusema angekuwa anataka kumkashifu, angefanya hivyo kwa vile alikuwa na ushahidi wa mambo yake mengi.

Huyo ni mwanasiasa wa pili katika kipindi cha miezi miwili kukutana na Mkapa. Mwingine ambaye ni waziri mwandamizi anadaiwa kumwambia Mkapa kuwa hakuna anayemwandama bali "mambo ni mazito."

Taarifa zinasema waziri huyo alimweleza kuwa ahadi ya rais Kikwete ipo palepale lakini kwa hapo alipofika, ingekuwa vema naye (Mkapa) akajitahidi kujenga upya sura yake kwa "kurejesha baadhi ya mali unazodaiwa kumiliki kutoka serikalini."

"Ni kweli nimekutana na Mkapa. Tumezungumza mengi. Nimemwambia tutakulinda, lakini na wewe jaribu kujisafisha kwa kurudisha mali serikalini, hasa ule mgodi wa Kiwira," chanzo cha habari kimemnukuu waziri wa Kikwete akisema.

Mkapa anahusishwa na umiliki wa mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira mkoani Mbeya kupitia kampuni yake ya ANBEN anayomiliki na mkewe, Anna ikiwa miongoni mwa makampuni matano yaliyoingia ubia na kampuni ya TanPower Resources Company Limited.

Kupatikana kwa taarifa kuhusu waziri kubadilishana mawazo na Mkapa kunathibitisha kuwepo ufuatiliaji wa karibu wa Rais Kikwete kuhusu tuhuma zinazomkabili Mkapa.

Wakati Mkapa anatajwa kukutana na waziri na mwanasiasa machachari akitaka hatua zichukuliwe kumlinda, tuhuma mpya zimeibuka dhidi yake.

Mkapa, kupitia TanPower Resources Limited, anahusishwa na dhamana ya serikali ya kupata mkopo wa Sh. 17.7 bilioni kutoka CRDB Bank kwa ajili ya kuendeleza mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira.

Kwanza, inadaiwa kuwa Mkapa alimiliki kampuni akiwa bado rais (ANBEN 1998) wa nchi na hivyo atakuwa alitumia nafasi yake kujinufaisha binafsi na kampuni yake.

Pili, kwa kuwa alikuwa bado madarakani na kwa kuwa uamuzi wa kuuza Kiwira ulifanyika ndani ya Baraza la Mawaziri aliloliongoza, basi uamuzi huo ulikuwa wa upendeleo kwa kampuni yake.

Tatu, hata waziri aliyejenga hoja mbele ya baraza la mawaziri, Daniel Yona ametokea kuwa mshirika katika umilikaji wa mgodi huo, jambo ambalo haliendani na utawala bora.

Nne, mkataba wa kampuni ya Mkapa kuuza umeme kwa Tanesco ulifungwa Mkapa akiwa madarakani (Septemba 2005), jambo linaloonyesha upendeleo kwa kampuni yake na utovu wa utawala bora.

Kwa mujibu wa mkataba huo, kampuni ya Mkapa ingelipwa (dola 3.65 milioni – sawa na zaidi ya Sh. 4 bilioni kila mwezi.

Tano, Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini imegundua mwanzoni mwa mwaka huu, kuwa fedha za mkopo zilizodhaminiwa na serikali (Sh. 17.7 bilioni) hazikutumika kama ilivyokusudiwa.
Kutokana na kutotumia fedha palipohitajika, jenereta moja ya kuzalisha umeme imechakaa kiasi cha kutoweza kufanya kazi; na nyingine ina uwezo wa kuzalisha megawati moja tu ya umeme kutoka megawati sita wakati mgodi unabinafsishwa.

Nyaraka zinaonyesha kuwa TanPower Resources Limited kimkataba ilitakiwa kuzalisha megawati 200 za umeme kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza ni kuzalisha megawati 50 kufikia Julai 2007 na megawati 150 ifikapo Machi, mwaka huu. Yote hii sasa ni ndoto.

Uchakavu wa miundombinu umeathiri pia uzalishaji wa mkaa wa mawe na mwekezaji "ameuza baadhi ya vifaa vya mitambo kama vyuma chakavu," wameeleza wafanyakazi mgodini.

Sita, TanPower Resources Limited imeshindwa kulipa wafanyakazi wake 1,632 kwa karibu mwaka sasa licha ya kuonyesha kwenye mchanganuo wake kwamba ilitenga Sh. 3.0 bilioni kwa ajili hiyo.

Katika mazingira haya, serikali ambayo bado ina hisa katika mgodi huo (asilimia 15) italazimika kuwalipa wafanyakazi kwa mtindo wa Tanzania Railways Limited (TRL) ambako serikali imekuwa ikikingia kifua wawekezaji.

Mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira ulioanzishwa kwa msaada wa serikali ya China, Novemba 1988, ulitarajiwa kuzalisha tani 150,000 za mkaa ghafi kwa mwaka na kwamba uzalishaji ungekua hadi kufikia tani milioni moja kwa mwaka.

Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, tayari imependekeza mgodi wa Kiwira urejeshwe serikalini, jambo ambalo waziri aliyekutana na Mkapa anapendekeza.

Tathmini ya mgodi mwaka 1988 wakati ukibinafsishwa, na Mkapa akiwa madarakani, ilionyesha ulikuwa na thamani ya Sh. 4.2 bilioni. Lakini tathmini iliyofanywa na Taasisi ya Ardhi mwaka 1991 ilionyesha thamani ya Sh. 7 bilioni.

Kamati ya Bunge inasema imeshindwa kuelewa vigezo vilivyotumika kutupilia mbali tathmini iliyofanywa miaka mitano baadaye na serikali kuamua kuuza hisa zake kwenye mgodi huo kwa gharama ya Sh. 700 milioni tu.

Hata hivyo, kampuni ya Mkapa ililipa Sh. 70 milioni tu.

TanPower Resources Limited ina wanahisa watano – kila mmoja akiwa anamiliki hisa 200,000 ikiwamo ANBEM Limited inayomilikiwa na Mkapa na mkewe.

Makampuni mengine ni Devconsult International Limited ya S.L.P. 65440 Dar es Salaam inayomilikiwa na Daniel Yona na Dan Yona.

Mengine ni Universal Technologies Limited inayomilikiwa na Wilfred Malekia na Evans Mapundi; Choice Industries Limited inayomilikiwa na Joe Mbuna na Goodyear Francis; na Fosnik Enterprises Limited inayomilikiwa na Nick Mkapa, Foster Mkapa na B. Mahembe.

Makampuni matatu ya mwisho yanatumia anwani moja ya posta ambayo ni S.L.P 8764 Dar es Salaam.

Mkapa anakabiliwa pia na tuhuma za kuuza benki ya NBC kwa "bei poa," na kupokea Sh. 500 milioni kutoka benki ya Afrika Kusini (ABSA) iliyonunua NBC ambazo hazikutolewa maelezo.

Vilevile Mkapa anatuhumiwa kuuza makampuni ya umma kwa kasi kana kwamba ameshikiwa bakora; kuuza nyumba za serikali kwa njia ya upendeleo na kwa bei ya bure na kuingilia zabuni ya Hotel 77 ya Arusha ambako serikali imelazimika kulipa fidia ya Sh. 3.3 bilioni na gharama nyingine.

Hivi karibuni, wakili wa mahakama kuu amekaririwa akidai kuwa Rostam Aziz, mbunge wa Igunga, alimwambia asaini hati za mikataba ya kampuni ya Kagoda Agriculture Limited ili wachote zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka Benki Kuu (BoT).

Alisema, na bado haijakanushwa, kwamba aliyetoa amri ya kuchukua fedha hizo kutoka BoT, mbele ya Katibu wa CCM wakati huo Philip Mangula na marehemu Daudi Ballali, ni Benjamin Mkapa.

Asasi mbalimbali za kiraia na wananchi wa kawaida wamekuwa wakitaka serikali kumchukulia hatua Mkapa.
 
Utamu akili zake zimekwenda mrama.Kitualichokifanya kimemvunjia heshima Rais na does not add any value in our society.Maadili yetu yameporomoka sana, na ukiangalia mambo mengi yanayomiminika zeutamu yanathibitisha hili. Tujitazame zaidi na zaidi ili tujue wapi tunakosea. Kikulacho ki nguoni waswahili wanasema.
 
Tangu jana ilipotoka hii picha nimepokea binafsi maswali ya watu wengi hasa kutoka TZ. Na wengine walinitafuta kwa simu na ninawashukuru. Binafsi nina majibu machache sana kwenye suala hili:

a. Kwanza, naendeleza kanuni ile ile ya kukataa kuwaandika watu kuhusu mambo yao binafsi ambayo hayahusiani na fedha za walipa kodi au kutumia muda wa kazi. Kanuni hii niliitumia wakati mwingine huko nyuma.

b. Kuna watu ambao wanakumbukumbu ndogo kuhusu kwanini nilitoa taarifa ya uwezpo wa picha ambayo inamuonesha JK katika compromising position na dada fulani. I never gave out the detail of the nature of the picture licha ya watu wengi kutaka kujua ilikuwa ni ya vipi, wapi, na nani? Wanaosahau ni kuwa mjadala ule ulisababishwa na issue fulani. Anayekumbuka atakumbuka na wanajua ni nini kilisemwa Bungeni as a compromise ya tishio langu.

Na niliahidi wakati ule as I do now, kuwa ukicheza kwa uchafu utachafuliwa na katika hili hakuna immunity.

c. Kuanzia wakati ule baada ya suala lile kuzima nikaamua kwa makusudi kabisa kupinga udhalilishaji wa mtu yeyote na nikajenga hoja na hoja na watu wakafikiri ninawatania. Ilipokuja suala la Mengi na mambo yake ya binafsi nikapinga watu wakasema ninamtetea Mengi!

Hofu yangu ilikuwa ndiyo hii ambapo wiki iliyopita niliandika kwenye ile makala ya "Ngono, kusagana na serikali ya CCM" ambayo nimeiendeleza kwenye makala yangu iliyotoka jana kwenye Tanzania Daima kuhusu suala hili. Hofu yangu ambayo sasa imetimia japo sivyo nilivyofikiria ni kuwa kwa vile tumekubali uozo huu kwenye vyombo vyetu vya habari na kukaa kimya wakati mabinti na watu na familia zao wanadhalilishwa basi siku moja hiki kitakuja kugeuka.


d. Kuna watu ambao wanapinga picha hii kwa SABABU ni Rais ndiyo victim. Ingawa ninashare hasira, uchungu na fedheha kwani fedheha ya Rais ni fedheha ya nchi (kumbuka ya Clinton na Monica) kwangu ninaona jambo kubwa zaidi. Tusije kujenga mitazamo ya nani ana heshima zaidi au anastahili hadhi zaidi kuliko mmachinga au mama James na kina Juma na Rosa ambao hawana utetezi huo.

Kwa muda mrefu magezeti ya Udaku, na hata hapa JF kuna watu wameandikwa mara kadhaa na wengine tumepinga mambo hayo. Kuna dada mmoja aliandikwa kiuchafu sana hapa na wengine wakifikiria ni sehemu ya Uhuru wa maoni. Hao tuliowaandika hapa na kuwaita kwa kila aina ya majina na wenyewe wana familia zao, wana ndugu na watoto vile vile na wapo waliaondikwa kule kwenye zeutamu na ambao na wenyewe wana vionjo vinavyoumizwa. Hawa nao wanahitaji utetezi wetu.

e. Mapema mwaka huu au mwishoni mwa mwaka niliwaandikia zeutamu na kutoa maoni yangu juu ya jukumu lao kama whistleblow linapokuja suala la mambo ya kingono. Niliandika na kuwasihi kutowaandika watu ambao hawalipwi na fedha za kodi, hawako katika nafasi za umma na mambo wanayoyafanya yanawahusu wao na familia zao. Ilikuwa ni sehemu yangu ya utetezi wa wale mabinti kina Nsia Swai.

Niliamini na bado naamini hivyo, kiiongozi wa umma anayetumia madaraka yake vibaya au pesa za umma kuendeleza vitendo vya ngono au kunyanyasa watu kijinsia mtu huyo ni fair game kuumbuliwa. Mtu ambaye ni mtumishi na anaendeleza vitendo hivyo asishangae kujikuta kwenye mazingira ya aina hiyo.

Hata hivyo ninaamini pia kuwa kuna masuala ambayo mtu mzima au mtu na familia yake wanatakiwa kuyakabili. Kama kuna mtu ana matatizo na kiongozi yeyote wa umma kwenye masuala hayo ya ngono ni bora amconfront au kumueleza juu ya suala hilo ili ajirekebishe. Endapo juhudi hizo zinashindikana au mtu huyo anaonesha kutokujali basi mambo kama haya yakitokea asishangae kwani mtu huvuna anachopanda.

g. Mwisho, utamu walichokifanya siyo tu kumdhalilisha Rais (kitu ambacho kinaonekana kuwakwaza wengi) lakini kwangu binafsi ni kumuandika raia mwingine katika mwanga wa mambo ya uchafu na kumzulia mambo ambayo ni ya aibu na kumpaka matope. Hili mimi linanikera na kuniudhi kwa sababu kutengeneza picha ya namna hiyo ni sawa na kile waswahili tunakiita "kumpakazia". Lengo lake siyo kueneza habari za ukweli (kama alivyofanya Larry Flynt kwa wanasiasa mbalimbali) baali kuudanganya umma kwa kiwango kisichoelezeka.

Kitendo hicho ni cha kulaaniwa, kupingwa na kukataliwa na hayo yafanyike si kwa sababu ni Rais bali ni kwa sababu Mtanzania mwenzetu amekutwa na jambo hilo na ushirikiano wote utolewe ili watu hao wachukuliwe hatua zinazostahili na kuwaomba Watanzania msamaha na familia nzima ya Rais. Na tunapodai mambo hayo ni lazima pia tukubaliane kuwa jambo hilo lisivumuliwe kwa mtu mwingine yoyote hata kama ni adui yetu.

Isije kuwa tunaumizwa kwa sababu tunampenda JK kibinafsi lakini kama huyo angekuwa ni Mrema, Mbowe au Mengi au Lipumba na Seif watu wasingepiga kelele hivyo! Ni lazima tutafute kanuni tuisimamie na hapo ndipo tutakuwa kweli tunaitetea haki na kuipinga dhulma.

Vinginevyo, isije kuwa katika utetezi wetu huu wa kumtetea tunathibitisha tu unafiki wetu na jinsi gani tulivyo na doubel standards.

Isije kuwa kama nilivyoandika jana kule kwangu kuwa isije kuwa watu wanaumizwa kwa sababu wanatambua wanaishi kwenye "shambal a wanyama" ambapo wanyama wote wan ahaki, nlakini wapo wanyama wengine wenye haki zaidi kuliko wengine. Katika ulimwengu wa namna hiyo, wapo wanaochekelea wakiona nguruwe kapigwa mkuki na kugeuzwa mlo, lakini wanataharuki wakati nguruwe huyo huyo anageuka na kuwatafuta wao!

zeutamu imelelewa kwa kuvumiliwa kwa sababu muda wote imekuwa ikiwagusa kina hohe hahe na watu wakafurahia. Ninafahamu watu ambao wameandikwa mle ambao wengine ndoa zao zimeingia matatani na wengine hata wakafikiria kujiua; ninafahamu kuna watu ambao mahusiano yao yamevunjika baada ya habari fulani fulani au picha za aina fulani kuandikwa mle na watu mabingwa wa maoni kwenda kuwachamba kama kwa usongo! Wakati huo wote, wanachama wenye kadi wa zeutamu wamekuwa wakiripoti mle kila kukicha na kufurahia maigizo ya udhalilishaji wa kijinsia.

Utamu haina sababu ya kufungwa kwani watakuwa na utetezi mkubwa wa uhuru wa maoni; lakini ni sisi wenyewe wanachama na wanaotembea humo kujifunga kutokuvumilia mambo fulani. Vinginevyo, kama mtu mmoja alivyosema kuwa mambo haya ya ngono ni mambo ambayo tayari yanafanyika, na mambo ya kishoga tayari yapo kwenye jamii yetu muda mrefu tu hakuna cha kushangaza. Sasa kama hili ni kweli (na magazeti yetu yanaandika hivyo kila siku) iweje leo tutaharuki?
 
Mimi nataka kujua hivi wamarekani wali-react vipi kutokana na kile kikatuni cha Bush akiwa anamtia Osaba Bin Laden?.Maana kwa issue hii ya Jk siyo katuni ya kwanza kwa raisi kufanyiwa hivi imeshawahi kutokea kwa maraisi wengine.Au Bush na Condo Rice walikuwa nao wako katika tendo la ndoa?

Mwanakijiji naona umeto amfano wa Bill clinton na monica tuu lakini kuna mtano bora ni wa Bush na Osama.
 
Mimi nataka kujua hivi wamarekani wali-react vipi kutokana na kile kikatuni cha Bush akiwa anamtia Osaba Bin Laden?.Maana kwa issue hii ya Jk siyo katuni ya kwanza kwa raisi kufanyiwa hivi imeshawahi kutokea kwa maraisi wengine.Au Bush na Condo Rice walikuwa nao wako katika tendo la ndoa?

Mwanakijiji naona umeto amfano wa Bill clinton na monica tuu lakini kuna mtano bora ni wa Bush na Osama.

Hey Sasha..bado nasubiri ile quote...🙂
But you have a point....kuna moja ya John Kerry akilana denda na John Edwards.....au Nailin Palin....

Sisemi kwamba ni sawa lakini natambua hali halisi na mazingira tunayoishi sasa kuwa kuzuia mambo kama hayo HAIWEZEKANI!!
 
Hey Sasha..bado nasubiri ile quote...🙂
But you have a point....kuna moja ya John Kerry akilana denda na John Edwards.....au Nailin Palin....

Sisemi kwamba ni sawa lakini natambua hali halisi na mazingira tunayoishi sasa kuwa kuzuia mambo kama hayo HAIWEZEKANI!!


Oh Nyani sorry nilikuwa carried away na baby sitting my niece.

I haven't seen hiyo ya Palin with who? with her maverick partner McCain?.tsk tsk tsk.Oh well mim nadhani we should at least respect viongozi wetu.Like wakati wa uchaguzi pia si walitoaga ile katuni ya obama na mke wake kama manyani? tena kwenye gazeti la maana kabisa kama new york times na watu walisema wameenda far sijui hata kama new york times waliapologize for that.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom