NL,
Nafikiri hadi sasa yameandikwa mengi sana humu ndani na si hii issue ya Kikwete na Ze-utamu. Wamewekwa humu leo hadi akina Mange, Erick, Nsia Swai na wengine kibao. Kama tunajadili, hatuwezi kuwa wafungwa. Mwisho nilichosema ni kuwa "hawa viongozi wa dini matapeli, walitakiwa kuwa huko kwenye ze-utamu..." Maadamu issue moja wapo ni hiyo zautamu, tatuizo liko wapi? Yaani lazima tuongeee Kikwete vs zeutamu siku nzima? Kila kitu kinazaliwa, kukua na kufa. Hata hii issue hivyohivyo. Hivyo sioni ubaya wa kusema kuwa "badala ya kumuweka Kikwete, walitakiwa wawekwe vingozi wa dini Mafisadi...."
Kuja kwenye issue ya pili, sijui kama umesoma vizuri nilichoandika. Nimeandika wazi kabisa kuwa Watumishi wa Mungu Matapeli. Kama mtumishi wa Mungu si tapeli basi huyu alale salama wala sina shida naye. Hata mie nawafahamu watu wa dini wenye dini kweli. Hao na waendelee hivyohivyo ingawa hao maboss wao wanawaangusha sana.
Nakuelewa kama umesoma Missionary. Hata mie mwanzo nilikuwa mtu wa kuheshimu sana dini na watumishi wa Mungu. Siku moja nikiwa nchi za watu tulienda harusini, na baada ya misa tukaenda kujichana na mnuso mkali. Nilishangaa Padri mmoja akicheza na mama mmoja usiku mzima na watu wakiangalia kwa jicho nusunusu na wengine wakisifia tu kuwa Padri anaongoza vizuri katika kucheza (chezaji za wazungu).
Kwenye harusi nyingine ndiyo ikawa kali zaidi. Padri mmoja aliyekuwa ANAKULA SAHANI moja na mama fulani kwenye mnuso, kufika saa tani usiku ghafla akapotea na yule mama. Mzee mmoja akaana kuuliza "Huyu Padri yuko wapi? Si alikuwa hapa na huyu mama, wamepotelea wapi wote? Ngoja nimtafute huyu Padri nimtie adabu...." Watu walicheka. Hii mifano iko mingi.
Tanzania kuna akina Pengo, Mtikila, nk ambao kukicha wanamsafisha Lowasa, Mkapa na genge lao. Mie ndiyo nasema hao. Na nimeandika hapo juu kuwa unawatoa wakiwa kwa Lowasa wakipata visenti. Sasa ndiyo narudi kama mwanzo. Tusiwe watumwa kwenye uandishi. Huwezi kusema chochote kisa watu watasema una-generalise. Hebu acheni tupumue. Yaani hadi niandike kila kitu? Huwezi kusoma ujumbe wa mtu ukajua ujumbe wake analenga watu gani? Hebu angalia tena ujumbe wangu hapo juu uone kama nilimaanisha watumishi wote wa Mungu au wale Mafisadi/Matapeli tu? Sasa wee Mchungaji unasaidia watu watapeliwe kwenye DECI, tukweke wapi? Tukisema tuseme kwa uangalifu sana maana tutaonekana tuna-generalise? Wao wanapotapeli, mbona hawaogopi kuwachafua wenzao na kazi yao? Kama kuna wa kuona aibu ni wao na si sisi tunaokoma nyani...