Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
Gembe ile picha bado ipo.

Hivi haiwezekani kuwatoa hawa WALA VYA BURE yaani viongozi wa dini? Ingelikuwa poa sana kuwaweka pale Pengo na rafiki zake wakiwania visenti vya Lowasa.

Wanasiasa ni watu wasio na haya. Ndiyo maana huenda mbele ya watu mailioni kwa mamilioni na kusema " ... I naver had sex with this woman....." Nashindwa kuelewa mtu kama Marehemu Dito, swala kama hili lingelimpa pressure. Wanasiasa kuanzia anaanza kuomba kazi, huomba kwa kudanganya. Wanadanganya hadi unapata raha. Hii ilimpelekea hadi Lucky Dube kuimba wimbo wake wa "We wanna thank you father" kuwa anaishukuru Bangi kwa kuwapa ujasiri wanasiasa ili wadanganye watu wao huku wanawaangalia machoni na muda huo taifa linateketea (Angalia zile picha za akina mama wanaojifungua/wamejifungua hospital Temeke kwenye blog ya Chem CheMponda). Ila hiyo ndiyo kazi ya wanasiasa. Hawakuja hapo kutangaza dini. Wapo pale kwa ajili yao, familia zao, ndugu zao marafiki na jamaa na mwisho Watanzania/watu wao. Hawa mie sijali sana kwani kazi yao iko vile.

Ila ambao sielewi ni WATUMISHI WA MUNGU. Sijui kwa nini wanajiita hivyo ilihali ni watumishi wa wanasiasa. Mie naona heri viongozi wa dini wawe wanapita kugombea uongozi huo ili na wao watudanganye from day one wakiwa wanaomba kazi. Watoe hongo kupata kazi hiyo, watuahidi maneno matamu na kuchinya ng'ombe siku ya mkutano. Tupewe na T-shirt mpya maana hatimaye tutavaa vazi jipya baada ya miaka kadhaa tukiwa tunavaa vya kununua umeinama.

Bahati mbaya muda sina na picha zao sina. Vinginevyo hawa PENGUIN wala vya bure ningelilala nao sambamba kwa huyo Zeutamu hadi washike adabu zao na waanze kuwa watumishi wa Mungu kwelikweli na si utapelitapeli.

Picha ile SI KIKWETE. Nashangaa mnacholalamika ni nini. Mtu kaunganishaunganisha na tena unaona kabisa kaunga na wewe bado unalalamika kuwa "Wamemtoa Kikwete?" Najua si vizuri ila ndivyo hivyo tena. Badala ya kutengeneza vitambulisho, kuiba hela za EPA nk nafikiri kuna haja UWT waanze kuajiri vijana wapya wanaoijua kazi na kujua kuwa vita vya sasa duniani si VIFARU na Ndege ila ni kwenye mtandao. Yes, usalama wa taifa kengele inalia, anzeni kazi maana vinginevyo ........tutakuja aibika kikwelikweli na si hizi za kulazimisha na kupindisha.
 
tehe tehe shem unajua kiswahili kimekua sana siku hizi......unajua maana ya hilo neno siku hizi?

Kugawana rasilimali tulizonazo ama mzee ina maana gani? Ni PM please usije ambiwa hapa unatukana !
 
Mkuu, hebu niulize. Mimi nina personal computers 2 na ninazitumia kutokana na mahitaji. Kama wife anatumia moja mimi natumia nyingine. Halafu ofisini (20km away from home) natumia almost computer 3 kwa siku kutokana na computer ipi iko free na wakati mwingine naenda internet cafes kama hakuna umeme sehemu nilipo.

Swali, je kwa hizo computer zote zitakuwa na IP address moja? IP postcode moja? IP address latitude moja? IP address longtude moja?

Ninasema hivi nikimaanisha kuwa huyo jamaa anaweza asiwe anatumia computer yake na inawezekana pia akawa anaenda sehemu anayofanyia hiyo kazi yake. Ila kitu kimoja kinaweza kuwa sahihi ni kwamba computer aliyotumia siku hiyo inaweza kuwa na 'details' kama ulivyoorodhesha hapo juu. Unasemaje?

Kuna moja kati ya hizo computer utakuwa unatumia mara nyingi kuliko nyingine. Na isitoshe ninaweza kujua uko mji gani na sehemu gani ingawa unaweza kuwa na IP address tatu ama zaidi.

Mkuu, hakuna kinachoshindikana dunia ya leo. Ukitumia mitambo ya mawasiliano dunia ya leo utajulikana ulipo kama watu wanataka kujua ulipo.

Unajua kwamba Osama Bin Laden hatumii kabisa simu katika kuwasiliana?, anatumia punda na watu katika kupata na kupokea mawasiliano yake. Video zake anazotoa ni recording na katika background ya kutengenezwa kwa muda na kubomolewa mara tu baada ya kurecord.
 
Si mahali anapopatikana mwenye ze utamu ila ni sehemu zilipo servers ambazo ndani yake kuna documents za ze utamu. Ieleweka mapema. Hapa Texas ni hosting provider alipo. Inawezekana ze utamu yuko hapo hapo Tanzania ama magomeni ama kariakoo ama michokeni ama kokote. Kimsingi si mshenzi kwa vile kamtoa mkuu wa nchi ila ni tangu mwanzo; it is like bad fortune, ikimpata masikini, tajiri anaona ni kawaida, ikimpata tajiri anasema kwa gharama yoyote n.k. We need to be fair and realistic kwamba kama mkuu wamemtoa personality yake should be protected and not spoiled as should have been anybody that appeared in ZEUTAMU. At least it is my opinion.


Ninaweza kukupa jina lake kamili, alisoma wapi na college ID yake ilikuwa nini, ana benki na bank gani, ana kiasi cha pesa kwa leo, simu yake na aliwasiliana na nani kwa mara ya mwisho iwe kupigiwa na kupiga. Si vyema kufanya hivi alivyofanya ni bora aache mapema.
 
Kugawana rasilimali tulizonazo ama mzee ina maana gani? Ni PM please usije ambiwa hapa unatukana !
siku hizi kiswahili kimekua shem.....maana yake sio hio pamoja na kwamba inasomeka hivyo......naogopa kuanzishiwa thread maana siku jf mtu anamka asubuhi na thread yake "sizitaki post za masanilo" teh etehe
 
Ninaweza kukupa jina lake kamili, alisoma wapi na college ID yake ilikuwa nini, ana benki na bank gani, ana kiasi cha pesa kwa leo, simu yake na aliwasiliana na nani kwa mara ya mwisho iwe kupigiwa na kupiga. Si vyema kufanya hivi alivyofanya ni bora aache mapema.
tehe tehe nimemkumbuka Lodi lofa
 
siku hizi kiswahili kimekua shem.....maana yake sio hio pamoja na kwamba inasomeka hivyo......naogopa kuanzishiwa thread maana siku jf mtu anamka asubuhi na thread yake "sizitaki post za masanilo" teh etehe

NiPM bwana sijui kabisa zaidi ya maana hiyo ...
 
Hivi haiwezekani kuwatoa hawa WALA VYA BURE yaani viongozi wa dini? Ingelikuwa poa sana kuwaweka pale Pengo na rafiki zake wakiwania visenti vya Lowasa.

Dah mkuu naona unaingia choo cha jinsia nyingine hapa! Huyu Pengo anakujaje hapa tena? Kama una hoja, nenda kule kwenye thread husika sio kuchanganya madesa hapa!


Bahati mbaya muda sina na picha zao sina. Vinginevyo hawa PENGUIN wala vya bure ningelilala nao sambamba kwa huyo Zeutamu hadi washike adabu zao na waanze kuwa watumishi wa Mungu kwelikweli na si utapelitapeli.

Wamekutapeli nini mkuu?

Picha ile SI KIKWETE. Nashangaa mnacholalamika ni nini. Mtu kaunganishaunganisha na tena unaona kabisa kaunga na wewe bado unalalamika kuwa "Wamemtoa Kikwete?" Najua si vizuri ila ndivyo hivyo tena. Badala ya kutengeneza vitambulisho, kuiba hela za EPA nk nafikiri kuna haja UWT waanze kuajiri vijana wapya wanaoijua kazi na kujua kuwa vita vya sasa duniani si VIFARU na Ndege ila ni kwenye mtandao. Yes, usalama wa taifa kengele inalia, anzeni kazi maana vinginevyo ........tutakuja aibika kikwelikweli na si hizi za kulazimisha na kupindisha

Hapa umenena mkubwa na haya maneno ndo mahala pake hapa....sio umbea wa hapo juu!
 
Kidatu acha kutia chumvi.

Ndiyo utaweza kumkamata mtu mwenye ujuvi kama wangu hapa ila GURU wa computer kama hawa wanaofanya kazi kwenye masite ya sex, itakuwa ni shida sana. Kumbuka pia mtu anaweza kuwa anatumia antena na kwenda sehemu kulipo na hotspot. Anaweza kuwa ndani ya gari na umbali hata wa km 1 na akawa anafanya vitu vyake.

Kumkamata inawezekana ila labda uombe msaada ya FBI au Wajep. Maana wenzetu kwenye FBI wamemwaga mapesa hasa na wale huwa hawashindwi. Watakutafuta hadi mwisho watakudaka. Kuna watu wengi sana waliwasumbua FBI na wengine hadi kwa kipindi kirefu. Ila wenzetu sijui kwa kuwa Wazungu? Wakidhamiria jambo wanalifanya hadi mwisho. Sasa hivi hapa Kidatu anahangaika peke yake. UWT wako wapi walau kuwasiliana naye kusema "Kijana njoo ufanye kazi kwetu utusaidie?" Kama mambo yataendelea kuwa hivi, basi kazi tunayo.

Tujikumbushe maneno ya Spika 6, kuwa RAIS UWE MKALI KIDOGO.

NB: Osama hutumia simu ila sema mara moja tu na kuitupa.
 
Nakumbuka wakati Utamu imefungiwa mara ya kwanza Gembe alikuja hapa na kupinga kitendo hicho kwa kusema "Imechangia kupunguza maambukizi ya ukimwi na n.k." Hiyo picha ya mkuu bado ipo huko?
 
sasa mkuu nikikuambia unionyeshe wapi nimeitangaza web hio ni wapi utanionyesha?

Gembe,
title ya thread inatosha kujibu swali lako ! its as if tuliihitaji hiyo zeutamu before ! Je tunahitaji TENA zeutamu ? ndio swali lako, ina maana tuliihitaji zeutamu hapo awali, (am guessing kulikuwa na maadili mema hapo tulipoihitaji)!

Eti gembe, naskia ulipiga kelele kwa nini zeutamu ilifungwa kwa sababu kwa upande wako uliona ilipunguza maambuzi ya ukimwi, hii ni kweli mzazi ? LoL
 
Zeutamu is an online tabloid.Na when it comes to tabloids, everyone is fair game, hata Mkuu wa nchi.
 
Dah mkuu naona unaingia choo cha jinsia nyingine hapa! Huyu Pengo anakujaje hapa tena? Kama una hoja, nenda kule kwenye thread husika sio kuchanganya madesa hapa!

Wamekutapeli nini mkuu?


NL,

Nimewahi kuishi nchi ya Kikatoliki hasa hasa ila taa zikizimwa ndiyo utajua hawa Kunguru wanafanya nini. Nilikaa na mmoja wao hadi akawa ananipa Jokes za kanisani. Akikupa jinsi wanavyokula GOOD TIME wala huwezi amini. Boss wao mmoja alinunua JAGUAR na mwingine akanunua MAYBACH na kumbuka hawa wamefunga HARUSI kuishi katika umasikini na wao ni kumhubiri tu Mungu. Kuna hadi ile story kuwa Papa Pius alikuwa akishirikiana na Hitler/Musolini. Pia kwa Italy, huwa wanakula sahani moja na Mafia.

Haya naona yamefika hadi Tanzania. Dini imekuwa ni utapeli tu. Unaweza kukuta Pengo ana kimama ki-secretary ambacho kila akihama, anahama nacho. Mwingine alishawahi niambia Padri..... ambaye sasa nasikia ni Askofu .... ambaye ni mjomba wake, huko kwao Dodoma ana mtoto. Sisemi sana maana ni rahisi kumfahamu na hii habari sijaithibisha.

NB: JOKE ya Mapadri.
Yesu akaonekana akitembea juu ya maji. Petro akamwambia kuwa na yeye aje kumlaki? Yesu akasema njoo. Jamaa kuanza kutembea akaanza kuzama na kupiga kelele. Yesu akamwambia " Wee idiot, fata hizo PILES foundation.."
 
NL,

Nimewahi kuishi nchi ya Kikatoliki hasa hasa ila taa zikizimwa ndiyo utajua hawa Kunguru wanafanya nini. Nilikaa na mmoja wao hadi akawa ananipa Jokes za kanisani. Akikupa jinsi wanavyokula GOOD TIME wala huwezi amini. Boss wao mmoja alinunua JAGUAR na mwingine akanunua MAYBACH na kumbuka hawa wamefunga HARUSI kuishi katika umasikini na wao ni kumhubiri tu Mungu. Kuna hadi ile story kuwa Papa Pius alikuwa akishirikiana na Hitler/Musolini. Pia kwa Italy, huwa wanakula sahani moja na Mafia.

Haya naona yamefika hadi Tanzania. Dini imekuwa ni utapeli tu. Unaweza kukuta Pengo ana kimama ki-secretary ambacho kila akihama, anahama nacho. Mwingine alishawahi niambia Padri..... ambaye sasa nasikia ni Askofu .... ambaye ni mjomba wake, huko kwao Dodoma ana mtoto. Sisemi sana maana ni rahisi kumfahamu na hii habari sijaithibisha.

Mkuu sikonge,

Issue yangu ya kwanza ni kwamba maneno yanayohusu wachungaji na kashfa zao, hayana uhusiano na thread hii, so nikasema labda ungeipeleka kny thread husika!

La pili, kwa maoni yangu si sahihi kuweka comments za ujumla .like, mapadre...bla blaaaabla, wachungaji....blablabla....maaskofu.....! mashekhe etc ..kama unakuwa na uhakika na unalo sema , just point out kwamba kwa mfano, Askofu Pengo kafanya hili na lile au Kakobe kafanya ......! Ukijumlisha unakwaza waumini wao, updre ni taasisi nyeti ambayo waumini wao wanaiheshimu sana...so better kuheshimu hilo na sisi!

Mimi binafsi ni ex seminarian, so najua maisha ya kiroho ya mapadre wetu hasa, wanajua kuna exceptions pia, najua pia kuna case by case ambazo naweza kuzitaja kabisa zilizotokea na kuleta mkanganyiko kanisani......!

Lakini siwezi sema eti Mapdre ni wahuni, matapeli...though kuna padre mmoja (sasa ni marehemu, RIP) alishanitapeli mkwanja wangu! siwezi generalise kusema...wachungaji ni wezi....kuna baadhi walikuwa fantastic acha kabisa!
 
Haya mambo kufika hapa kwet yanaashiria kitu kimoja tu -- nchi inakwenda pabaya sana, na kusiko, na wakulaumiwa wanajulikana. kuna wachache wanatupeleka puta, maana valangata likitokea wao haoooooooooo, wanalikwaa pipa na kwenda majuu walikopeleka hela zetu.

Watanzania tutakuja kujuta -- kule Sri Lanka serikali ilikuja kujuta kupuuzia mambo yakiwa bado madogo madogo, leo hii wanajitahidi kumaliza vita ya miaka 27 kwa gharama kubwa sana!

Hii nchi inahitaji maombi kwa Mwenyezi Mungu. Mkuu wa kaya ajitutumue kidogo na kuonyesha ukali kwa wale wanaomharibia, maana yeye ndiyo wa kwanza kujuta.
 
mbona ze utamu yenyewe haifunguki kwa sasa? au iko bize sana? Anyway, nalaani vitendo vyote vya udhalilishaji vinavyoendeshwa na site hiyo
 
Ninaweza kukupa jina lake kamili, alisoma wapi na college ID yake ilikuwa nini, ana benki na bank gani, ana kiasi cha pesa kwa leo, simu yake na aliwasiliana na nani kwa mara ya mwisho iwe kupigiwa na kupiga. Si vyema kufanya hivi alivyofanya ni bora aache mapema.

Naona hajaacha mkuu! Toa basi hizo data zako! tehe tehe tehe
 
.........duh ebwanee hao UWT wapo hivi kweli na hao wanao jiita intelejinsia vp hawajaamuka bado........nimechungulia mmmh hakufai hali ya hewa imechafuka.

Acha fujo Fidel80, mbona kupo swari tu. Kwani we hujawahi ona mambo hayo?, Bushi walishamtoa sana, viongozi wengine vilevile. Guys tushakubali utandawazi tunashangaa nini
 
Sijamwona kimwana kwenye ile picha jamani mbona mnataka kumharibia Villager wetu?
Wiki kadhaa zilizopita tulitahadharishwa juu ya taskforce flani hivi inayokuja...Huenda tuliunderestimate kile watakachokifanya na namna watakavyokifanya.Mimi nilitegemea kuwa watakuja sooo negative ktk issue za mafisadi/ufisadi.But what if they use other way round.Nimeona hivi karibuni a U-turn katika mitazamo ya some memberz.Sasa nadhani ni wakati wa kutulia na kuanza kufanya conspirancy...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom