seedfarm
JF-Expert Member
- Feb 9, 2020
- 260
- 2,654
Dunia kuna vituko sana, Moja ya vituko vinapatikana Bungeni vikiongozwa na Job Ndugai. Huyu Ndugai anajulikana kama mheshimiwa Spika.
Leo Ndugai ametumia dakika nyingi Bungeni akitaka kutetea legacy yake na kujifananisha na Spika Marehamu Samwel Sitta, Ndugai anaumia na kukwazika sana kwanini watu walimuheshimu Samwel Sitta na kuheshimu Bunge la tisa la Samwel Sitta.
Ndugai amejitahidi kulia na kubembeleza kwa wabunge kuwa naye atajitahidi kuandika mambo aliyoyafanya ili watu wamuelewe, Je mbona Samwel Sitta hajaandika popote legacy yake lakini anakumbukwa.
Ndugai ni moja ya Spika atakaye Kumbukwa kwa maovu na ukatili wa hali ya juu kinyume na mwanadamu wa kawaida.
Ndugai asipojirekebisha ataunganishwa na mwendazake kama watu walioharibu Uchumi wa nchi mpaka kufika ukuaji wa asilimia 4% ambao watu wengi wamepoteza ajira.
Ndugai atakumbukwa kama mtu asiyekuwa na busara na Hekima kwa maamuzi yake yaliyoharibu Taifa.
Maamuzi ya kupitisha sheria uchwara kama za uhujumu Uchumi ili kumfurahisha mwendazake, Bila aibu Ndugai anashawishi sheria hizi sasa ziletwe Bungeni tena baada ya kuona upepo umekaa hovyo.
Ndugai ameshiriki kupitisha sheria za mifuko ya jamii kandamizi ili kuwaumiza wastaafu, Mifuko ya jamii iliunganishwa na pesa kufilisiwa kwa kisingizio zinajenga miradi, Leo Mama Samia anapata wakati mgumu sana.
Ndugai atakumbukwa kama mtu aliyegeuza Bunge genge la watu wasiojielewa ambao kazi yake imekuwa kuzurula na mwendazake kila kona wakati wa kuzindua miradi, Ndugai alipokea maagizo hata ya kuwanyima stahiki zake wabunge kama Tundu Lissu.
Ndugai Leo amepoteza muda kujibu hoja za Nape kwa aibu kubwa, Ndugai bado haamini kama Mwendazake hayupo alishatangulia, Nina uhakika kauli ya Nape kuwa wabunge wale 19 na chadema wapo pale sio kihalali angetamka wakati ule Ndugai angemfukuza Nape Bungeni ili kumfurahisha Mwendazake.
Hawa ni viongozi wa kitaifa lakini mwisho wa siku wataandikwa kwenye historia kama moja ya watu pekee kutokea Tanzania walioendesha nchi kama gari bovu isiyokuwa na sheria, kanuni na taratibu.
Hakika Ndugai atatumia muda mwingi kutetea legacy yake huku akisahau legacy inajitetea yenyewe.
Pole Sana Mheshimiwa Ndugai, Tafuta mwalimu wa Saikolojia aliyekufunza ukatili hayupo tena.