Je, ilikuwa bora kununua ndege badala ya mabehewa na vichwa ili kufanya safari za treni kwenda Mwanza, Kigoma na Moshi?

Synthesizer

Platinum Member
Feb 15, 2010
11,185
18,930
Kulikuwa na ubishi humu ndege za Dreamliner na Airbus ziliponunuliwa, kwamba hilo lilikuwa jambo la manufaa kwa wananchi wa Tanzania. Hilo nimelipinga siku zote, kwa sababu unaposema manufaa kwa Watanzania, Watanzania wepi wanaopanda hizo ndege? Na hata ukisema wengine wanafaidika indirectly, kuna siku ATCL imepata faida ili hata Watanzania wasiopanda ndege wafaidike na mapato yanayoingizwa na hizo ndege?

Siku zote nimefikiria kwamba tuna reli ambayo ndio inafaidisha watanzania wote - wale wanaopanda first class, second class na hata third class. Lakini huduma za reli nchini ziko taabani. Treni ya abiria kwenda Kigoma ni mara mbili kwa wiki - kwa kuwa hatuna mabehewa na vichwa vya kutosha.

Sasa hawa viongozi, huyu Magufuli, alihitaji degree ngapi kutambua kwamba ilikuwa afadhali kununua mabehewa hata 200 na vichwa vya treni vya kutosha ili kurudisha hali ya zamani kwamba treni zinafanya safari za mikoani kila siku? Kweli hilo lisingekuwa bora sana kuliko hizi ndege ambazo kila siku zinapaki bila kufanya kazi au zinakamatwa kwa sababu za mambo ya kilevi tu yanayofanywa na viongozi?

Kwa kuwa tulinunua hizi ndege kwa cash, mie ninapendekeza ziuzwe zote ili tukanunue mabehewa na vichwa vya treni vya kutosha kuanza safari za treni za kila siku na kuwanufaisha Watanzania wa aina zote na kuchangia mapato ya serikali. Hili sio suala la Chadema au CCM, ni suala ambalo viongozi wenye busara wataliona liko wazi kabisa.
 
"Tunachokijua" Kama mnajua mnahangaika na nini hapa sasa?

Kwanza Watu huwa tunaishi kwa kwenda mbele sawa na wewe uliona wapi Mtu anatembea kinyume nyume?

Yaliyopita si ndwele......................
 
1671093667252.png


Tunapoongelewa kunufaisha Watanzania wote, ni kufanya vitu kama hivi, sio kununua Dreamliner. Hawa abiria wananufaikaje na hizo Dreamliner zilizopaki?
 
"Tunachokijua" Kama mnajua mnahangaika na nini hapa sasa?

Kwanza Watu huwa tunaishi kwa kwenda mbele sawa na wewe uliona wapi Mtu anatembea kinyume nyume...
Hayajapita, hizo ndege zipo, ziuzwe tufunge hii chapta. Nimeongea tatizo na suluhisho lake. Watu wenye busara wanaongea hivyo, hawaongei kukosoa tu kama unavyofanya wewe
 
Kulikuwa na ubishi humu ndege za Dreamliner na Airbus ziliponunuliwa, kwamba hilo lilikuwa jambo la manufaa kwa wananchi wa Tanzania. Hilo nimelipinga siku zote, kwa sababu unaposema manufaa kwa Watanzania, Watanzania wepi ewa na vichwa vya treni vya kutosha kuanza safari za treni za kila siku na kuwanufaisha Watanzania wa aina zote na kuchangia mapato ya serikali. Hili sio suala la Chadema au CCM, ni suala ambalo viongozi wenye busara wataliona liko wazi kabisa.
Ulishawahi kufika hata airport kweli wewe kilaza? Hao abiria wanaojaa pale utawasafirisha na nini.

Kutwa kuponda ATCL yetu alafu kutwa kusifia Kenya na Rwanda airways
 
Ulishawahi kufika hata airport kweli wewe kilaza? Hao abiria wanaojaa pale utawasafirisha na nini.

Kutwa kuponda ATCL yetu alafu kutwa kusifia Kenya na Rwanda airways
Wewe ndio kilaza hujapita airport. Hao abiria waliojaa airport wamejaa pale kwa ajili kupanda ndege za ATCL?

Funga ATCL yako ya kiyeboyebo uone kama hakutakuwa na abiria wamejaa airport

Uliza Watanzania wangapi wako tayari kwenda China kutumia ATCL badala ya Emirates au Ethiopian Airlines, mbumbumbu mkubwa.
 
Naunga hoja uza zote zibaki ndege 3 moja ya kimataifa moja route za ndani nyingine ya mizigo. Ccm ni vilaza Sana hawaelewi wapo kwaajili ya nn maboga kabisa inauma kweli yani
 
Wewe ndio kilaza hujapita airport. Hao abiria waliojaa airport wamejaa pale kwa ajili kupanda ndege za ATCL?

Funga ATCL yako ya kiyeboyebo uone kama hakutakuwa na abiria wamejaa airport

Uliza Watanzania wangapi wako tayari kwenda China kutumia ATCL badala ya Emirates au Ethiopian Airlines, mbumbumbu mkubwa.
Kwa maelezo yako haya wewe ni kilaza haujawahi kukanyaga airport hata siku moja.
 
Hii mada kuijadili lazima uwe umekatwa kichwa umebaki kiwiliwili.


Mleta uzi,, kagua tena kama kichwa chako na kiwiliwili viko pamoja.
 
Kulikuwa na ubishi humu ndege za Dreamliner na Airbus ziliponunuliwa, kwamba hilo lilikuwa jambo la manufaa kwa wananchi wa Tanzania. Hilo nimelipinga siku zote, kwa sababu unaposema manufaa kwa Watanzania, Watanzania wepi wanaopanda hizo ndege? Na hata ukisema wengine wanafaidika indirectly, kuna siku ATCL imepata faida ili hata Watanzania wasiopanda ndege wafaidike na mapato yanayoingizwa na hizo ndege?

Siku zote nimefikiria kwamba tuna reli ambayo ndio inafaidisha watanzania wote - wale wanaopanda first class, second class na hata third class. Lakini huduma za reli nchini ziko taabani. Treni ya abiria kwenda Kigoma ni mara mbili kwa wiki - kwa kuwa hatuna mabehewa na vichwa vya kutosha.

Sasa hawa viongozi, huyu Magufuli, alihitaji degree ngapi kutambua kwamba ilikuwa afadhali kununua mabehewa hata 200 na vichwa vya treni vya kutosha ili kurudisha hali ya zamani kwamba treni zinafanya safari za mikoani kila siku? Kweli hilo lisingekuwa bora sana kuliko hizi ndege ambazo kila siku zinapaki bila kufanya kazi au zinakamatwa kwa sababu za mambo ya kilevi tu yanayofanywa na viongozi?

Kwa kuwa tulinunua hizi ndege kwa cash, mie ninapendekeza ziuzwe zote ili tukanunue mabehewa na vichwa vya treni vya kutosha kuanza safari za treni za kila siku na kuwanufaisha Watanzania wa aina zote na kuchangia mapato ya serikali. Hili sio suala la Chadema au CCM, ni suala ambalo viongozi wenye busara wataliona liko wazi kabisa.
Hata hivo mabehewa yamebadilishwa gia angani kutoka SGR automatic kwenda MGR manually dunia inakwenda kwakasi sana
 
Ulishawahi kufika hata airport kweli wewe kilaza? Hao abiria wanaojaa pale utawasafirisha na nini.

Kutwa kuponda ATCL yetu alafu kutwa kusifia Kenya na Rwanda airways
Kinachopondwa ni gharama za ununuzi wa mabehea mitumba kwa gharama za juu,na si usafirishaji wa treni
 
Ulishawahi kufika hata airport kweli wewe kilaza? Hao abiria wanaojaa pale utawasafirisha na nini.

Kutwa kuponda ATCL yetu alafu kutwa kusifia Kenya na Rwanda airways
kuna watanzania wangapi wenye uwezo wa kusafiri kwa ndege kutoka Dar kwenda Kigoma? unawaita watu vilaza wakati wewe na huyo aliyenunua ndege ni vilaza wa kutupwa?
unadakia kila jambo mengine hata huyaelewi we una jilamba midomo tu
hovyooo
 
Kulikuwa na ubishi humu ndege za Dreamliner na Airbus ziliponunuliwa, kwamba hilo lilikuwa jambo la manufaa kwa wananchi wa Tanzania. Hilo nimelipinga siku zote, kwa sababu unaposema manufaa kwa Watanzania, Watanzania wepi wanaopanda hizo ndege? Na hata ukisema wengine wanafaidika indirectly, kuna siku ATCL imepata faida ili hata Watanzania wasiopanda ndege wafaidike na mapato yanayoingizwa na hizo ndege?

Siku zote nimefikiria kwamba tuna reli ambayo ndio inafaidisha watanzania wote - wale wanaopanda first class, second class na hata third class. Lakini huduma za reli nchini ziko taabani. Treni ya abiria kwenda Kigoma ni mara mbili kwa wiki - kwa kuwa hatuna mabehewa na vichwa vya kutosha.

Sasa hawa viongozi, huyu Magufuli, alihitaji degree ngapi kutambua kwamba ilikuwa afadhali kununua mabehewa hata 200 na vichwa vya treni vya kutosha ili kurudisha hali ya zamani kwamba treni zinafanya safari za mikoani kila siku? Kweli hilo lisingekuwa bora sana kuliko hizi ndege ambazo kila siku zinapaki bila kufanya kazi au zinakamatwa kwa sababu za mambo ya kilevi tu yanayofanywa na viongozi?

Kwa kuwa tulinunua hizi ndege kwa cash, mie ninapendekeza ziuzwe zote ili tukanunue mabehewa na vichwa vya treni vya kutosha kuanza safari za treni za kila siku na kuwanufaisha Watanzania wa aina zote na kuchangia mapato ya serikali. Hili sio suala la Chadema au CCM, ni suala ambalo viongozi wenye busara wataliona liko wazi kabisa.
Lengo ilikuwa ni kupiga pesa wala hakuwa na nia njema yoyote
 
Wanasiasa wana mikopo bank, wamekopa pesa nyingi kununua mabus. Ukiweka train za uhakika utawafanya wafe na ugonjwa wa moyo
Nadhani katika kuendeleza reli tunahujumiwa kindani. Ona nauli za SGR walizoweka, kama vile kuwaambia watu wasithubutu kwenda SGR waendelee kupanda mabasi!
 
  • Thanks
Reactions: Cpp
Behewa moja billion ngapi?
Kichwa cha treni ya umeme ni kama USD 3M
Behewa la abiria ni kama USD 1,300,000
Behewa la abiria la ghorofa ni kama USD 1,600,000
Behewa la kulala USD 1,600,000
Buffet car ni USD 2,000,000

Uhai wake ni kama miaka 25, na gharama za kuendesha (maintanance cost) ni ndogo sana kulinganisha na ndege

Bei ya Dreamliner moja ni kama USD 250m

Kwa hiyo Dreamliner moja inanunua mabehwa 190 ya kukaa, au 155 ya kulala, au vichwa 80 vya treni za umeme
 
Kichwa cha treni ya umeme ni kama USD 3M
Behewa la abiria ni kama USD 1,300,000
Behewa la abiria la ghorofa ni kama USD 1,600,000
Behewa la kulala USD 1,600,000
Buffet car ni USD 2,000,000

Uhai wake ni kama miaka 25, na gharama za kuendesha (maintanance cost) ni ndogo sana kulinganisha na ndege

Bei ya Dreamliner moja ni kama USD 250m

Kwa hiyo Dreamliner moja inanunua mabehwa 190 ya kukaa, au 155 ya kulala, au vichwa 80 vya treni za umeme
Nadhani kwa takwimu hizi utaona mambo yalifanyika kinyume kabisa cha maumbile
 
Back
Top Bottom