TRC yatangaza kupokea vichwa vitatu vya treni ya Umeme na Mabehewa 27 ya abiria

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
e1cd5ec1-42d1-42e0-b7e6-41780b894c7b.jpeg
Shirika la Reli Tanzania limepokea vichwa vipya vitatu (3) vya treni za umeme vilivyoundwa na Kampuni ya Hyundai Rotem na mabehewa mapya 27 ya abiria yaliyoundwa na Kampuni ya 'Sung Shin Rolling Stock Technology (SSRST) kutoka nchini Korea Kusini.

Serikali kupitia Shirika la Reli Tanzania ilifanya manunuzi ya vichwa vipya 17 na mabehewa mapya 59 ya abiria kwa ajili ya uendeshaji wa reli ya kiwango cha kimataifa SGR. Mpaka sasa Shirika limepokea vichwa vya treni ya umeme vinne (4) kati ya 17 kutoka kampuni ya Hyundai Rotem na mabehewa 56 kati ya 59 kutoka kampuni ya 'Sung Shin Rolling Stock Technology' (SSRST) ya nchini Korea Kusini.

Mabehewa matatu (3) yaliyosalia yanatarajiwa kuwasili nchini Februari, 2024. Vichwa 13 vilivyobaki vinatarajiwa kuwasili kwa awamu kama ifuatavyo, vichwa sita (6) vitawasili mwezi Machi na vichwa saba (7) vitawasili Aprili, 2024.

TRC itaanza kupokea Seti ya kwanza (1) kati ya Seti 10 za treni za Kisasa (EMU) mwezi Machi 2024 Mei seti 2, Juni seti 2, Julai seti 2, Septemba seti 2 na seti ya mwisho mwezi Oktoba 2024.

Vichwa vilivyopokelewa, kiutendaji vina mwendokasi wa kilomita 160 kwa saa. Mabehewa 27 katika madaraja ya Uchumi na Biashara. Daraja la biashara (Business class) ni mabehewa 13, kila behewa lina uwezo wa kubeba abiria 45 na mabehewa ya daraja la Uchumi (Economy class) ni 14, kila behewa lina uwezo wa kubeba abiria 78 kwa kuzingatia viwango vya kimataifa kumuwezesha abiria kusafiri kwa amani na salama.

Shirika la Reli Tanzania linaendelea kupokea kwa awamu vitendea kazi kwa ajili ya uendeshaji wa reli ya kiwango cha kimataifa (SGR). Zoezi la majaribio ya vitendea kazi linaendelea kwa mujibu wa mkataba ili kuhakikisha vinaendana na mifumo ya miundombinu iliyojengwa nchini kabla ya kuanza uendeshaji wa kibiashara.
 
Mwenye miradi yake angekuwa hai saa hii tungemuona akitesti kukiendesha kichwa kimoja kwa kasi ya ajabu hawa wamebaki stori na machawa wengi tu!
 
Tupeane tarehe ya mwisho na issue is ipo kuwa yente tuliamushe vimemo kila siku vya nin
 
Nimejikuta nikiwaza sana kuhusu bandiko kuu, yaani the whole SGR "" thingmajing lakini nimejikuta mbali zaidi ya mada na nipo nje ya box; mbali sana na taarifa iliyo mbele yangu. Far from the truth.

Nimeandika na kufuta, nimejikuta nimebadilisha TRC, mabehewa 27, abiria n.k, kiufupi nimecheza na maneno na namba... anyways, I'll leave it to your own Imagination

Nikirudi kwenye mada, binafsi, naona hiyo ni heri ya mwaka mpya, kwamba TRC mpole mpole na tarativu tu siku tunaamka na bin vuu mtoto anatambaa kwa kuserereka...

....heri ya mwaka mpya
 
Vitendea kazi vyote Mpaka kufikia October 2024 ndo vitakua vimekamilika

Kwa maana hiyo huu mradi kuja kuanza labda 2025 baada ya uchaguzi
 
Back
Top Bottom