Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 1,465
- 4,677
Kiukweli watu huko duniani Wana pesa aisee, imebidi nijitafakari upya nimekuja kufanya nini duniani kwa sababu kwa mambo niliyoyaona jana usiku nilirudi nyumbani kwa huzuni kubwa Sana, aibu na maumivu.
Nilikua zangu road nikasema Wacha niende rock city mall nikashangae maghorofa, nikajikuta nimeingia CASK bar maana nilisikia Fid q atakuepo kwa sababu Mimi ni mdau wa hip-hop nikaona acha nijisogeze nikasikie Ngoma kama bongo hiphop, I'm professional n.k.
Kufika nikakuta kwanza parking magari yamejaa yaani watoto ni wakali sijawahi ona, size zote zipo, class A, wachafu, wazuri yaani ni wewe tu, mluga luga nikasema Leo lazima niopoe nilikua na 50,000/= mfukoni nikasema Leo watanikoma sitakosa mtoto hata wa 20,000/=
Nikanyooka mpaka counter nipate hata wine chupa ndogo Ile ya imagi nizuge nayo huku nikiendelea kuangalia mrembo yupi atanifaa nichomoke nae, huku kitaa hiyo wine Wanauza 3500/= Sasa yule counter hakunisikia vizuri akaleta chupa ya maji akanambia 4000/= chupa ndogo nikamuuliza shingapi? huku nimepigwa na butwaa kusikia hiyo bei ya maji, Pembeni yangu walikua wamekaa mademu wamechafua meza vibaya wamejaza windohek, hennesy n.k yaani waliokua pale counter hakuna aliekua mnyonge, kipindi naleta mshangao nikamwambia yule anaehudumia counter anirudishie hela yangu maana siwezi nunua maji Mls 700 kwa 4000/= wakati hata bombani yapo, kipindi naondoka nikasikia vicheko kutoka kwa wadada na washikaji waliokua counter.
Nikaona huku nimekosea njia nimeingia kwenye Chaka la matajiri, hata sikumsubiri fid q aje nikatoka Moja kwa Moja mpaka nje huku niliona kama Kila mtu ananicheka kwa fedhea, nikaondoka kinyonge nikatembea kwa mguu mpaka coner ya bwiru kinyonge huyoo nikaingia gheto kulala huku moyoni nikiwa na masononeko.
Hila wadau tuambiane ukweli mnapata pesa wapi za kuspend kiroho mbaya hivyo? Hamna majukumu? Au mna pesa nyingi Sana mnatafuta sehemu ya kuzitumia?
Nilikua zangu road nikasema Wacha niende rock city mall nikashangae maghorofa, nikajikuta nimeingia CASK bar maana nilisikia Fid q atakuepo kwa sababu Mimi ni mdau wa hip-hop nikaona acha nijisogeze nikasikie Ngoma kama bongo hiphop, I'm professional n.k.
Kufika nikakuta kwanza parking magari yamejaa yaani watoto ni wakali sijawahi ona, size zote zipo, class A, wachafu, wazuri yaani ni wewe tu, mluga luga nikasema Leo lazima niopoe nilikua na 50,000/= mfukoni nikasema Leo watanikoma sitakosa mtoto hata wa 20,000/=
Nikanyooka mpaka counter nipate hata wine chupa ndogo Ile ya imagi nizuge nayo huku nikiendelea kuangalia mrembo yupi atanifaa nichomoke nae, huku kitaa hiyo wine Wanauza 3500/= Sasa yule counter hakunisikia vizuri akaleta chupa ya maji akanambia 4000/= chupa ndogo nikamuuliza shingapi? huku nimepigwa na butwaa kusikia hiyo bei ya maji, Pembeni yangu walikua wamekaa mademu wamechafua meza vibaya wamejaza windohek, hennesy n.k yaani waliokua pale counter hakuna aliekua mnyonge, kipindi naleta mshangao nikamwambia yule anaehudumia counter anirudishie hela yangu maana siwezi nunua maji Mls 700 kwa 4000/= wakati hata bombani yapo, kipindi naondoka nikasikia vicheko kutoka kwa wadada na washikaji waliokua counter.
Nikaona huku nimekosea njia nimeingia kwenye Chaka la matajiri, hata sikumsubiri fid q aje nikatoka Moja kwa Moja mpaka nje huku niliona kama Kila mtu ananicheka kwa fedhea, nikaondoka kinyonge nikatembea kwa mguu mpaka coner ya bwiru kinyonge huyoo nikaingia gheto kulala huku moyoni nikiwa na masononeko.
Hila wadau tuambiane ukweli mnapata pesa wapi za kuspend kiroho mbaya hivyo? Hamna majukumu? Au mna pesa nyingi Sana mnatafuta sehemu ya kuzitumia?