Kesi inayopinga Watu kushtakiwa kwenye mahakama zisizo na mamlaka yakwama 'ombi lawasilishwa kutaka Jaji kukaa kando'

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
Kesi iliyofunguliwa na Mwanaharakati wa haki za Binadamu, Wakili Onesmo Olengurumwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Rufaa Na. 165 ya mwaka 2021 kuhusu kupinga vifungu vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai vinavyoruhusu washtakiwa kushtakiwa kwenye mahakama za chini ambazo hazina mamlaka ya kusikiliza kesi hizo (committal Proceedings) imeahirishwa mpaka itakapopangiwa siku nyingine ya kusikilizwa.

Kesi hiyo iliyopangwa kusikilizwa leo February 12, 2024 katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania,jijini Dar es Salaam mbele ya jopo la majaji watatu wa mahakama ya rufani Mhe. Jaji Sehel, Mhe. Jaji Kente, na Mhe. Jaji Masoud saa 3:00 asubuhi

Upande waleta rufaa baada ya kufika mahakamani wameomba ahirisho kutokana na Jaji mmoja kati ya jopo la majaji watatu wa mahakama ya Rufani (Mhe. Jaji Masoud) kuwa alikuwa katika sehemu ya majaji wa mahakama kuu walioshiriki katika kesi hiyo ambayo uamuzi wake umekatiwa rufaa kwenye mahakama ya rufani kabla hajateuliwa rasmi kuwa Jaji wa mahakama ya rufani.

Akifafanua kuhusu ombi hilo Wakili Paul Kisabo amesema kuwa taratibu za kimahakama zinamnyima nafasi Jaji huyo kushiriki tena kwenye uamuzi akiwa Jaji wa mahakama ya Rufani kama alikuwa sehemu ya majaji wa mahakama kuu waliosikiliza kesi hiyo.

Upande wa Jamhuri kupitia mawakili wake wamekubaliana na ombi hilo ambapo Mahakama itapanga siku nyingine kwa ajili ya kesi hiyo kwa kulingana na ombi husika.

Itakumbukwa Rufaa hiyo inatokana na uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania masijala ya Dar es Salaam uliotolewa mwaka 2020 ambapo Mahakama kuu ilitupilia mbali kesi hiyo.

Vifungu vinavyolalamikiwa ni kifungu namba 178, 243, 244, 245, 246, 247, 248, 249, 250, 256, 257,258 na 259 vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Katika Mahakama Kuu Wakili Olengurumwa aliitaka mahakama itoe amri ya Kubatilisha vifungu hivyo vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai akidai vinakiuka Katiba na haki za binadamu kwa mfano haki ya kusikilizwa kwa usawa, usawa mbele ya sheria pamoja na haki nyingine ambazo zipo katika Ibara ya 13 (1) (2) na (6) (a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977.
Screenshot_20240212-202002_1.jpg


Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 

12 February 2025​

KESI YA KUPINGA WATU KUSHTAKIWA KWENYE MAHAKAMA ZISIZO NA MAMLAKA YAAHIRISHWA MAHAKAMA YA RUFAA


View: https://m.youtube.com/watch?v=igFJxQi48PE

Wakili msomi Paul Kisabo kwa niaba ya Onesmo OleOlengurumwa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) imeahirishwa baada ya benchi la majaji 3 wa mahakama ya rufaa kuwemo jaji aliyesikiliza kesi ilipokuwa katika mahakama kuu ya Tanzania.

Mawakili wa pande mbili walikubali kuwa kupandishwa cheo jaji wa mahakama kuu mheshimiwa jaji Masoud aliyesikiliza kesi hiyo ngazi ya Mahakamu Kuu kutaathiri mwenendo wa kesi akiwemo tena kama jaji wa Mahakama ya Rufaa kusikiliza tena kesi hiyo ya kihistoria.

Kesi ya msingi inayokatiwa rufaa Mahakama ya Rufaa Tanzania :
Feb 13, 2020
February 13, 2020
Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa amefungua kesi namba 36 ya mwaka 2019 dhidi ya Mwanasheria mkuu wa serikali katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Masijala ya Dar es Salaam akipinga watuhumiwa wa mbalimbali nchini humo kufikishwa kwenye mahakama zisizokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi zao (committal proceedings).

Katika kesi hiyo, mwanaharakati huyo wa haki za binadamu nchini Tanzania, anapinga watuhumiwa wa makosa mbalimbali kukamatwa bila upelelezi kukamilika.

Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa leo Februari 13, 2020 kwa mara ya kwanza majira ya saa saba mchana mbele ya majaji watatu, Jaji Masoud, Jaji Mlyambina na Jaji Juliana Masabo.

Akizungumzia msingi wa kesi hiyo aliyoifungua tangu Desemba 16, 2019, Olengurumwa amesema kuwa analenga kuiomba Mahakama Kuu ya Tanzania kutoa tamko la kufuta vifungu vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 (Toleo la mwaka 2002), ambavyo amedai vinakiuka haki na uhuru wa watuhumiwa, kuminya utawala wa sheria, na kufifisha mchakato mzima wa uendeshaji wa kesi kwa usawa, sababu ambayo ameitaja kuwa inahamasisha matumizi mabaya ya mamlaka ikiwemo kufanya upelelezi kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Olengurumwa amesema kesi hiyo pia inalenga kuiomba mahakama hiyo kutoa tamko kwamba kifungu namba 178, 243, 244, 245, 246, 247, 248, 249, 250, 256, 257, 258 na 259 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 (Toleo la mwaka 2002) kuwa ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977 na kwamba vifungu hivyo vipaswa kufutwa na kuondolewa kabisa.

Olengurumwa ambaye ni msomi wa sheria na mchambuzi wa sera za umma nchini Tanzania ameeleza zaidi kuwa mtuhumiwa anapofunguliwa mashtaka kwenye mahakama ambayo haina mamlaka ya kuisikiliza kesi yake, mtuhumiwa huwa haruhusiwi kusema chochote, hivyo humfanya akose haki yake ya msingi ya kusikilizwa kwa wakati.

Akifafanua zaidi amesema kuwa sheria nayo pia bado haijaweka utaratibu wa namna ya kuhakikisha upelelezi unafanyika haraka na kwa wakati ili kuhakikisha kwamba mtuhumiwa anafikishwa mbele ya mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi yake.

Akinukuu kifungu namba 178 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 (Toleo la mwaka 2002), Olengurumwa amesema kifungu hicho kinasema kuwa, "pale ambapo kesi itaunguliwa kwenye mahakama ambayo haina mamlaka ya kuisikiliza, baada ya upelelezi kukamilika, mahakama hiyo inapaswa kutoa amri ya kesi hiyo kwenda kusikilizwa mahakama kuu."

Olengurumwa ameelezea changamoto ya kifungu hicho. ambapo amedai kuwa, kwakuwa upelelezi umekuwa ukichukua muda mrefu kwenye kesi nyingi ama pengine kutokamilika, kifungu hiko cha 178 kimekuwa hakina uhalisia, hivyo kinastahili kufutwa.

Olengurumwa ameeleza kuwa Ibara ya 64 (5) ya Katiba ya Tanzania ya Mwaka 1977 inaweka bayana kuwa, Bunge linawajibu wa kutunga sheria ambazo hazikinzani na Katiba.

Vilevile, Olengurumwa ameeleza zaidi kuwa, serikali inawajibu wa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977
 
Back
Top Bottom