Itakuwaje Lowassa akifukuzwa CCM, CHADEMA watampokea?

Itakuwaje Lowassa akifukuzwa CCM, CHADEMA watampokea?

Hivi ile List of Shame ya Mwembeyanga bado ipo au edited tayari??

Password ya ile Tovuti kapewa Lowassa ndio sababu siku ya Ufunguzi wa Kampeni walikusanya watu Jangwani ili awatajie Website aliyoweka Hotuba yake
 
Kwa wale mlikuwa hajui, huyu ndie mgombea wa Chadema 2015 na ndie rais 2015 Chadema itakapochukua nchi na pia litimie lile neno rais wa 2015 lazima atoke Kaskazini haswa kwa kuzingatia, ukimuondoa ZZK, Chadema haina any other candidates wanaoweza kuwapatia ushindi kwenye urais!.
Tena hata mimi nitaingia rasmi kwenye siasa kwa kujiunga rasmi Chadema na kuna jimbo nitalichukua kama nimeliokota!, mgombea wa CCM nitampiga chini kama kumsukuma mlevi!.
Pasco
Kakakuona in action..
 
Kwanza ni msahishe mleta mada,lowasa hakustaafu bali alilazimishwa kujiuzulu,Na kingine ni kwamba lowasa ni mtu Wa kulipiza visasi hivyo kikwete atashinikiza lowasa kutoswa na chama chake ili asije kunyanyaswa akimaliza muda Wake.
Kwa manti hiyo Ridhiwani alitia ujumbe huo kwa niaba ya baba yake.
Kikwete anapendekeza Mtoto Wa mwinyi au asha rose mmoja Wao awe rais na atakuwa tayari kuficha mapungufu yake.
Lowasa hakubaliki hâta kidogo chadema,asifikirie kabisa kuhamia chadema na kupewa fursa ya kugombea hâta ya uenyekiti Wa kitongoji.[SUB][/SUB]
Very painful kusalitiwa na uliowaamini...
 
CHADEMA kwa sasa hawapokei "viongozi" toka CCM, hivyo Lowassa hawezi kujaribu kuomba kujiunga CHADEMa.

Ila wanachama wa kawaida wa CCM wanaoguswa na elimu ya uraia pamoja na kuzinduliwa toka usingizi wa ujinga, maradhi, ufisadi na kulindana (hivyo kukosa uzalendo na haki zao za msingi) hao wataendelea kupokelewa kila iitwapo leo.
Njoo usome ulichoandika
 
Mosi, EL ni zaidi ya CDM sasa EL atahamiaje CDM? CDM ndio inaweza ikahamia kwa EL na sio EL kuhamia CDM.

Pili hakuna mtu mwenye akili timamu anayehama kutoka kwenye taasisi kubwa kwenda kwenye kigenge cha wahuni.
Ila anauwezo wa kununua kigenge cha wahuni na kukifanya chake..

Very good point!!
We have seen it happen..
 
Acha kupotosha umma, Lowasa sio waziri mkuu mstaafu, ni waziri aliyejihudhuru kwa matumizi mabaya ofisi ya umma, huyo ndiye mzee wa richmundi, kuhusu kwenda Chadema, unaota ndoto za alinacha, hiki ni chama cha watu makini.

Kuna watu saizi wanatamani kumwambia MOD aufute huu uzi
 
Nilishawahi kusikia kuwa jeuri ya EL ni kwamba anawatishia eti wakimtema, ataenda upinzani. Tusije tukawa mbulula tukampokea CCM wakapata credit. Huyu jamaa nadhani ndio katuletea matatizo ya umeme kwa maslahi yake binafsi. Umeme unapanda mara dufu tunahoji tukiwa bar afu tunatulia (tuingie barabara kidogo-tuonyeshe anger). Wenzetu Kenya walipandishiwa bei ya chakula, wakaingia barabarani na mabango, tumekuwa wabinafsi sana.
Lowassa leo anazunguka nchi nzima na gia yake kubwa ni ruswa kwa watanzania maskini na bodaboda. Na matatizo mengi tunayoyapata, kielimu(shule za kata), kiuchumu (ki-umeme) yalikuja akiwa PM, leo aje upinzani tumpokee. Tutakuwa waroho wa madaraka.
Yupo chadema sasa
 
Mbowe alishasema kuwa kama EL akiamua kuja CDM bac lazima arudishe mali zote za umma alizotuibia na kukiri kwa nini alifanya hivyo na kwa sababu zipi. Na hapo hata wananchi watampima na kumruhusu kuwa angalau mwanachama na si kupewa nafasi ya uongozi wala kugombea post yoyote.

:cool2:
Do u still trust maneno ya DJ Mwenyekiti??
 
Hebu fikiria baba yako amekufukuza harafu ukahamia kwetu, tutakufukuza pia au tutakupa hifadhi?? Ukombozi ni njia ngumu sana na falsafa yake ni wachache tu wanaoweza kuielewa, hatutupi kuni wakati bado tunapika hata kama ni kuni ya mnyaa ambayo ukipikia macho yanawasha, fikiria zaidi utajua itakuwaje.
Nakusifu aisee.. u said it very poetically and matured..
Kweli we kiona mbali..
 
Back
Top Bottom