Saint Anne
JF-Expert Member
- Aug 19, 2018
- 77,819
- 233,246
Hembu acha kujilinganisha na vitu vya ajabu chizi weweHivi wewe Shwaini ulishaniona mimi ni Joti sio?









Sent using Jamii Forums mobile app
Hembu acha kujilinganisha na vitu vya ajabu chizi weweHivi wewe Shwaini ulishaniona mimi ni Joti sio?









Na sisi tusio wazuri kwenye text wala calls jeMkuu introverts kwenye kuandika hawajawahi kufeli so hata kuchangia hapo wako very comfortable ila usiombe ukutanee nae yaani mpolee na maneno yanakataa![]()
Unanichanganya nimefanyaje..??
They think too much kabla ya kuongea au kufanya chochote, like je nitaonekanaje, atanifikiriaje, itakuwa okay au la, mpaka aamue anakuwa out of timeSio hawawezi ila wanakua hawako comfortable sana na mara nyingi inachukua muda mrefu kwa wao kuzoeana na wengine au kuinteract kirahisi ila wakishafanikiwa kukufahamu vizuri watakuwa comfortable sana na wewe. In short introverts are good at one to one communication hasa kwa watu wao wa karibu sana na kwenye mass ya watu wengi kiukweli wengi hawana confidence.
Kwelibahati mbaya sikuona hii quote mapema. Nadhani wengi humu wanachanganya shyness au lack of confidence na kua introvert. Ninavyofahamu mimi introverts hawapendi kusocialize iwe kwa maneno au kwa maandishi. Kama huwezi kuongea mbele ya watu ila unapenda kuchat, wewe sio introvert bali ni mtu mwenye aibu!
🚶🚶....
Hatuna tofauti sana japo mimi huwa starehe yangu kubwa ni football hivyo Kama natoka basi naenda kuangalia mpira ukumbini au uwanjani hapa mtaani,sina closely friend ambaye mda wote nitakuwa naye japo siyo kila mtu anaweza kuwa rafiki yangu,napenda kusaidia,nina huruma,nikikosa hela siwezi kukaa kwa amani, graduation niliyowahi kufanya ni ya form four tu,form six sijafanya.Kuna wakati nilikua na bahati sana kupendwa na wanawake wazuri lakini mwisho wa relationship huwa sio mzuri,ktk relationship zangu sijawahi mwambia mwanamke tuachane huwa sitaki aumie ila huwa naanza kumpotezea taratibu,kutongoza mwanamke huwa mtihani sana na nikitaka kumtongoza demu huwa naandaa plan nyingi sana kwamba iwapo akikataa nitakuwa ktk hali gani na akikubali nitajipangaje kuhusu mahitaji yake madogo madogo,nina vitu vingi sana kichwani ktk sector za siasa,uchumi,michezo, entertainment,elimu lakini huwa sipendi kubishana na mtu au kuvijadili kwa sababu sipendi kelele,watu huwa wananichukulia mimi kauzu sana hivyo ni ngumu kujenga mazoea,ni ngumu sana kumuomba mtu vitu vidogo vidogo yani bora nikae tu ila mimi ni mtoaji.Mimi ni extremely introvert, hivyo nitajielezea mimi ili mtu ajue jinsi ya kuishi na sisi:
1. Ninapenda sana sehemu tulivu, isiokuwa na makelele na fujo
2. Nina aibu sana mbele za watu hivyo naweza kukaa kimya muda wote hata kama najua swali au chochote mpaka niulizwe direct
3. Ninapenda sana kukaa ndani peke yangu kwa muda mrefu, naweza hata kumaliza siku tatu sijatoka nje
4. Ninapanga vitu vya baadae sana hata kama ni baada ya mwaka au miaka mingi kuja utekelezaji wake
5. Ni mtu wa mawazo sana asa kufikiria vitu tofauti vinavyo nizunguka na kutaka kuvitolea majibu
6. Nina maumivu ya ndani na uwa ni kazi kumwambia mtu kama ameniudhi au vipi na uwa simuoneshi mtu kukasirika kwangu hvyo ni ngumu mtu uyo kujua kma nimekasirika
7. Sipendi usumbufu wa vitu kuingilia ratiba yangu ambayo nimeipanga
8. Maisha yangu yanaenda kwa ratiba, kwani kila ninachofanya ni tayari nilikipanga kabla.
9. Sipendi mwanamke anayeongea sana kwani nachoka kumsikiliza mapema pia naona ananisumbua pale napo taka utulivu
10. Kuna kipindi uwa sitamani kuongea na mtu yeyote kwa simu wala ana kwa ana bali nataka nikae peke yangu niwaze tu
11. Sipendi kurudia rudia kitu kile kile kwa mtu
12. Uwa sio mpenzi wa sherehe ndo maana hata graduation yangu sikwenda
13. Ni msiri sana, kutoa siri ni mpaka pale nipende mwenyewe na uwa kitu kishapita ndo natolea maelezo
14. Sijawahi kuwa na mapenzi ya dhati kwa mwanamke, hivyo sijadumu kwa mahusiano yoyote, hadi sasa nimebreak mara tatu naona ni usumbufu kuwa kwenye mahusiano.
15. Ni mkimya sana uwa wengi wananiona mpole mno
16. Sipendi kuchat muda mrefu
17. Nimepanga kwenda kujenga polini, sehemu yenye utulivu na vegetation kwani ndo nahisi napata raha uko
18. Sipendi outings kabisa
19. Nina roho ya ukarimu ya kutoa hata kama najua najiumiza
20. Nina huruma uliopitiliza
21. Ninapenda sana kusoma
22. Ni mtu wa kupanga vitu kabla ya kutekeleza, na ninapenda vitu vyangu viwe systematically and not randomly
23. Uwa niko defensive sana kwenye hisia zangu, hvyo kma naona kuna kitu hichi kitanipa au kinaelekea kunipa maumivu uwa napotezea na kuepuka hicho kitu
24. Nikashaamua jambo fulani uwa ni ngumu kubadilisha au kubadilika maana na kuwa nimeshafikiria sana peke yngu na kuamini kuwa niko sahihi.
25. Overthinking ndo ugonjwa wangu kwani kuna muda uwa hadi nakonda kwa kuimagine tu mpaka wengine wanahisi nastress
26. Uwa ni mtu wa kukaa nawaza muda wote, naweza nkawa na watu hapa kumbe mimi mawazo yangu yapo mbali sana.
27. Sina rafiki hapa maeneo ya nyumbani, ni mtu wa ndani au ni moja kwa moja kazini na kurudi ndani
28. Ninaumia sana kama kitu nilichopanga kikafeli au kushindikana kwani ninakuwa nilitumia nguvu nyingi na muda mwingi kukitengenezea plan.
Vipo vingi sana hadi naona sitomaliza, itoshe tu kusema hali hii nilizaliwa nayo na wala sio malezi.
Sent from my iPhone using JamiiForums
Tumezaliwa hivyo mkuu wewe ni introvert ila ukijaribu uwe extrovert utakuwa kichekesho kwa watu huo sio ugonjwa jikubali.Labda kama upo ktk groups na huwez kuzungumza angalia kipaumbele chako yani unapendelea nini labda siasa,michezo nk anzisha mada ukiwa una uhakika nayo hapo wote watakusikiliza weweMkuu yani hapa unanisema mimi kabisaa!Hii hali inanitesa sana kwakweli!Kujichanganya na watu napo naona shida na hata nikijichanganya najikuta nakaa kimya siwezi kuzungumza!Hivi dawa ya kupona tatizo ni ipi?
Shukran mkuu ngoja niufanyie kazi ushauri wakoMkuu ishi uwezavyo ishi ujisikiavyo si lazima sana kujichanganya kama huwezi.. maana kwenye kujichanganya pia kuna hasara zake na faida pia hivyo uwe tayari kukabiliana!.
Ukitaka kujichanganya angalia watu husika kama utaweza shea nao story au idea ambazo wewe unazipenda na wao watazipenda kuzisikiliza hapo ndio kutanoga..
Ipo hivi introvert wanapenda mambo mazito mazito,mada nzito nzito so ukikutana na watu wanaopenda kuongelea vitu vyepesi vyepesi kamwe hautapenda company yao!
Sometimes unajikuta unataka ujadili na mtu kitu lkn unakuta sio kwamba unatakiwa ujadili bali umfundishe!! Maana yeye hakijui au hana details za kutosha,yeye anajua diva kaachana na nani na ataenda kwa Nani!!!😂😂
So chagua pia company ya kukaanayo ili ujizoeshe taratibu pia kama kuna michezo unaipenda, penda kuzungumzia,utapata wadau tu taratibu haohao watakufanya uanze kuzoea social kiaina..
Ngoja nikurahisishie jitahidi upate rafiki ambae ni extrovert kundi la sanguine kupitia yeye utajuana na watu wengi so kampani itakuwa kubwa utajua kuwa muongeaji ila ukishaanza kuzoeana na jamii.. ila nakutahadharisha sanguine usiwaambie vitu vyako sana waambie vya kawaida maana hawana shipa la siri watakuliza😂
Jitengee kamuda kidogo ka kutoka na rafiki yako au kwenda hata kuangalia mpira au draft hata nusu saa tu, taratibu itainua hali ya kusocialize.
Ila mkuu usiache asili yako kuwa introvert kuna raha yake pia.. chakufanya weka vitu in a balance.
Unaposocialize angalia unasocialize na watu wa namna ipi utakuja kujiumiza bure kutaka uwiane nao.. unakuta hawakusikilizi hapo huwezi penda kuwa social.
So tafuta walau watu utakao share nao kitu watakaokuwa interest na wewe hi itakupa motisha ya kusocialize na itafungua mengine..
Yangu ni hayo angalia na wengine wanasemaje you'll get something.
App imerekebishwa? Niliona sehem unalia
Ndo ninaye mimi naishi naeIntrovert wanatakiwa wawapate introverts wenzao vinginevyo wataishia kuwaumiza wale ambao sio introverts.
Hii ni Kama Mimi kabisaaa.Mimi kuongozana na mtu wa kusimama simama njiani walahi atanikutia nyumbani.
Ndio maana huwa sipendi kutembea tembea,na nikiwa na shida sehemu basi niende mwenyewe chap nirudi.
Ni juzi tu hapa nyumbani wamenilazimisha niende nao sokoni maana tangu nije hata sokoni sikujui..niliwaacha njiani maana walikuwa na vituo vingivingi
Hata shule nilikuwa nikitoka lecture, Mimi ni mwendo,maswala ya kusubiriana sijui kufwatana nilishayashindwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ukimpata mwanamke anaekuelewa wewe ni mtu wa namna gani basi shida inakuwa hakuna.
Uko sahihi na ikitokea mwanamke akaxungusha basi ndio anapotezewa kihivyo. Pili huwa tunakuwa straight forward, hatutumii janja janja kuomba kHata mm nimemkatalia ishu ya kutongoza haina uhusiano sana,personally kila siku natokea mwanamkeila muendelezo wake ndo huwa mgumu kwa maana focus yetu kubwa inakuwa kusoma tabia za mtu
Mimi nipo kundi ganj sasa?
Ni muongeaji mzuri tu nikiamua kuomgea tena nina story hasa na mtu akinianza kuniongelesha atahisi rafiki kapata ila nikitoka hapo simtilii maanani tena yaani hata anaweza nitxt nisijibu kwa wakati akapiga cm nisipokee nakua sijisikii kuongea nae au kuchat nae!
Napenda kukaa ndani tena peke yangu naweza kukaa ndani hata siku tatu nisionekane nje! Nimesoma shule zote day school ila ht majirani walikua wanadhani niko boarding na sijawah kuchoka kukaa ndani.
Sina marafiki na i hate friends nawachekea juu juu tu ila sijawahi kuwaamini na wala sijawahi tendewa nao ubaya! Sipendi kuongozana na mtu km ushost yaan ht nilivyokua chuo ni nitoke room kwangu niingie class nitoe hi niweke earphone niingie netflix niamgslie movie km lecture hajaingia kimyaaa ila ukiniongelesha narespond kwa bashasha mok unaweza shangaa
Napenda kutoka out peke yangu nijinunulie kinywaji changu nisikilize mziki ila asije mtu kunipa company ananiharibia tu starehe ht km ananijua anisalimie tu apite aniache alone.
Am a girl ila nikimpenda mtu namwambia straight forward kua i like u sinaga aibu yaani na nikiwa na mahusiano my boyfrnd anakuaga anatake over almost ratiba yote ya maisha yng yaani ni mimi na yy sijui inakuagaje ht awe vp utashangaa tumestick together and life is all abt us inshort na yy automatic anapoteza marafiki anakua na mimi tu na sijawahi command hilo kwa mwanaume nilienae.
Am very confident hasa kwenye kujieleza pale itapotakiwa nifanye hivyo siogopi mtu wala watu eg. kwenye presentation ilikua lzm nipate extra points
Naweza nikacheka na ww nisijue ht jina lako nimesoma na baadhi ya watu miaka3 mitatu kozi moja darasa moja ila siwajui majina na wengine siwajui hata sura zao!
Nikipenda napenda haswaa na nakuaga km nina ka convicing power fulani hv..sifokeagi mwanaume wala kumuamrisha ila automatic anakua vile ninavyotaka awe and ina turn out kua healthy relationship ever.
Nina huruma mnoo..ni mwepesi kutoa msaada ila mgumu kukopesha hela yaani bora nikupe kidogo sababu siwezi kudai...naonekana km kauzu ila hakuna mtu ninaeumia emotionalyy km mimi.
Nina wivu wa mapenzi sijawahi ona yaani i want my man to be only mine nikinusa harufu ya usaliti nahisi km moyo unachemka kwa hasira I can even kill wallah personally nikipenda nimependa
Nina visasi yaani ukiniudhi kitu kikaniingia sawasawa lazima nitakulipizia tuuu hata baada ya miaka.
Naambiwaga ninaringa na nina dharau while najiona sina tabia hiyo sababu kutoka moyoni naheshimu kila mtu kwa class yake na sipendangi kumjudge mtu inshort niseme hua na mind my own business na mwanaume ambae niko nae tu.
Hata uniseme au unisengenye nakuona hv usitegemee nikareact na nikiamuaga kitu nimeamua sitaki mtu anibadilishe mawazo yangu nahisigi nilichoamua kiko sahihi maana natumiaga mda mref sana kufikia maamuzi.
Nipo kundi gani? Extrovert? Introvert? None of the above au wapi exactly?