Introverts Vs Relationship

Introverts Vs Relationship

Mimi ni extremely introvert, hivyo nitajielezea mimi ili mtu ajue jinsi ya kuishi na sisi:

1. Ninapenda sana sehemu tulivu, isiokuwa na makelele na fujo

2. Nina aibu sana mbele za watu hivyo naweza kukaa kimya muda wote hata kama najua swali au chochote mpaka niulizwe direct

3. Ninapenda sana kukaa ndani peke yangu kwa muda mrefu, naweza hata kumaliza siku tatu sijatoka nje

4. Ninapanga vitu vya baadae sana hata kama ni baada ya mwaka au miaka mingi kuja utekelezaji wake

5. Ni mtu wa mawazo sana asa kufikiria vitu tofauti vinavyo nizunguka na kutaka kuvitolea majibu

6. Nina maumivu ya ndani na uwa ni kazi kumwambia mtu kama ameniudhi au vipi na uwa simuoneshi mtu kukasirika kwangu hvyo ni ngumu mtu uyo kujua kma nimekasirika

7. Sipendi usumbufu wa vitu kuingilia ratiba yangu ambayo nimeipanga

8. Maisha yangu yanaenda kwa ratiba, kwani kila ninachofanya ni tayari nilikipanga kabla.

9. Sipendi mwanamke anayeongea sana kwani nachoka kumsikiliza mapema pia naona ananisumbua pale napo taka utulivu

10. Kuna kipindi uwa sitamani kuongea na mtu yeyote kwa simu wala ana kwa ana bali nataka nikae peke yangu niwaze tu

11. Sipendi kurudia rudia kitu kile kile kwa mtu

12. Uwa sio mpenzi wa sherehe ndo maana hata graduation yangu sikwenda

13. Ni msiri sana, kutoa siri ni mpaka pale nipende mwenyewe na uwa kitu kishapita ndo natolea maelezo

14. Sijawahi kuwa na mapenzi ya dhati kwa mwanamke, hivyo sijadumu kwa mahusiano yoyote, hadi sasa nimebreak mara tatu naona ni usumbufu kuwa kwenye mahusiano.

15. Ni mkimya sana uwa wengi wananiona mpole mno

16. Sipendi kuchat muda mrefu

17. Nimepanga kwenda kujenga polini, sehemu yenye utulivu na vegetation kwani ndo nahisi napata raha uko

18. Sipendi outings kabisa

19. Nina roho ya ukarimu ya kutoa hata kama najua najiumiza

20. Nina huruma uliopitiliza

21. Ninapenda sana kusoma

22. Ni mtu wa kupanga vitu kabla ya kutekeleza, na ninapenda vitu vyangu viwe systematically and not randomly

23. Uwa niko defensive sana kwenye hisia zangu, hvyo kma naona kuna kitu hichi kitanipa au kinaelekea kunipa maumivu uwa napotezea na kuepuka hicho kitu

24. Nikashaamua jambo fulani uwa ni ngumu kubadilisha au kubadilika maana na kuwa nimeshafikiria sana peke yngu na kuamini kuwa niko sahihi.

25. Overthinking ndo ugonjwa wangu kwani kuna muda uwa hadi nakonda kwa kuimagine tu mpaka wengine wanahisi nastress

26. Uwa ni mtu wa kukaa nawaza muda wote, naweza nkawa na watu hapa kumbe mimi mawazo yangu yapo mbali sana.

27. Sina rafiki hapa maeneo ya nyumbani, ni mtu wa ndani au ni moja kwa moja kazini na kurudi ndani

28. Ninaumia sana kama kitu nilichopanga kikafeli au kushindikana kwani ninakuwa nilitumia nguvu nyingi na muda mwingi kukitengenezea plan.

Vipo vingi sana hadi naona sitomaliza, itoshe tu kusema hali hii nilizaliwa nayo na wala sio malezi.




Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wakitaka kuanza mahusiano inawawia vigumu sana kuchukua hatua ya kwanza hasa kwenye kutongoza ni midomo zege!,Ni watu wenye hofu kuichukua hatua yoyote ile bila kuona usahihi wa yeye kuichukua hatua husika! Ni logics people so kufikia maamuzi kitu kimepangwa kikapangika!.

Wanakuwa disappointed ama wao wenyewe au watu waliomzunguka kutokana na ugumu walionaokuichukua hatua hiyo wengine huwaona kama si binadamu aliekamilika so husemwa vibaya sometime na yakimfikia hujisikia hovyo na huenda akaacha jambo husika.

Tabia pia za mhusika huenda zikamkwaza asichukue hatua ya kuamua kuingia kwenye mahusiano!

Let's say yeye ni mpole ila anatokea kumpenda mtu mwenye gubu,kukurukakara aisee hawapendi hivi.. wao wanapenda utulivu na maelewano.

Kutokuwa karibu na watu huwaleteleza kuwa na aibu,kutokujiamini mbele ya watu hasa jinsia iliyotofauti nae so hayo yanaweza mpatia ugumu ktk kutongoza n.k

Mkuu moja ya usuruhishi wa tatizo ni kulitambua tatizo introvert husubiri mahusiano ila pindi yafikapo huruka mbali😅

Akiweza tambua kuwa ili kupata ushirikiano na watu na kujiongezea kujiamini ni lazima ashiriki na watu hili litamfanya awazoee watu,maana kwanza introvert wana akili nyepesi ya kutambua na pia inaweza mrahisishia kupata mwenza humohumo kutokana na mazoea n.k

Nadedaga Lolo😂😅
Mkuu yani hapa unanisema mimi kabisaa!Hii hali inanitesa sana kwakweli!Kujichanganya na watu napo naona shida na hata nikijichanganya najikuta nakaa kimya siwezi kuzungumza!Hivi dawa ya kupona tatizo ni ipi?
 
Wewe ndio hujui,ku socialize kwa live ndo huwa tabu,mitandao ya kijamii ni mizuri sana kwa intros,hujasikia hapo kwenye kuandika watu wako vizuri lakini kwenye public ndio tatizo?
Mi nadhani huyo jamaa hapo juu Ndio haelewi, sisi introverts kwenye mitandao ya kijamii Ndio Hassa mahala petu kwa sababu hatuna muda wa kujitokeza kwenye vijiwe ama bars kupiga stories, mi binafsi hata kama nikiamua kutoka tena kwa kujilazimisha sana nikifika bar ama club sitaki kushirikiana na mtu yoyote, ni kutulia tu sehemu na mwisho wa siku nitatoka pale kwa majuto ya kwa nini nilienda mahala pale, masikio wiki nzima yanalia kengele kwa zogo la muziki. Huwaga ninajuta sana
 
Mkuu yani hapa unanisema mimi kabisaa!Hii hali inanitesa sana kwakweli!Kujichanganya na watu napo naona shida na hata nikijichanganya najikuta nakaa kimya siwezi kuzungumza!Hivi dawa ya kupona tatizo ni ipi?
Mkuu ishi uwezavyo ishi ujisikiavyo si lazima sana kujichanganya kama huwezi.. maana kwenye kujichanganya pia kuna hasara zake na faida pia hivyo uwe tayari kukabiliana!.
Ukitaka kujichanganya angalia watu husika kama utaweza shea nao story au idea ambazo wewe unazipenda na wao watazipenda kuzisikiliza hapo ndio kutanoga..
Ipo hivi introvert wanapenda mambo mazito mazito,mada nzito nzito so ukikutana na watu wanaopenda kuongelea vitu vyepesi vyepesi kamwe hautapenda company yao!
Sometimes unajikuta unataka ujadili na mtu kitu lkn unakuta sio kwamba unatakiwa ujadili bali umfundishe!! Maana yeye hakijui au hana details za kutosha,yeye anajua diva kaachana na nani na ataenda kwa Nani!!!😂😂

So chagua pia company ya kukaanayo ili ujizoeshe taratibu pia kama kuna michezo unaipenda, penda kuzungumzia,utapata wadau tu taratibu haohao watakufanya uanze kuzoea social kiaina..

Ngoja nikurahisishie jitahidi upate rafiki ambae ni extrovert kundi la sanguine kupitia yeye utajuana na watu wengi so kampani itakuwa kubwa utajua kuwa muongeaji ila ukishaanza kuzoeana na jamii.. ila nakutahadharisha sanguine usiwaambie vitu vyako sana waambie vya kawaida maana hawana shipa la siri watakuliza😂

Jitengee kamuda kidogo ka kutoka na rafiki yako au kwenda hata kuangalia mpira au draft hata nusu saa tu, taratibu itainua hali ya kusocialize.
Ila mkuu usiache asili yako kuwa introvert kuna raha yake pia.. chakufanya weka vitu in a balance.

Unaposocialize angalia unasocialize na watu wa namna ipi utakuja kujiumiza bure kutaka uwiane nao.. unakuta hawakusikilizi hapo huwezi penda kuwa social.
So tafuta walau watu utakao share nao kitu watakaokuwa interest na wewe hi itakupa motisha ya kusocialize na itafungua mengine..

Yangu ni hayo angalia na wengine wanasemaje you'll get something.
 
Siku ya kufunga ndoa ndio huwa patashika sana kiufupi introvert maisha ya kama ya USA yanatufaa zaidi uswailini kunakuwa kugum kweli kweli hasa kwa waliopanga nyumba za jumuiya
 
Back
Top Bottom