Mkuu yani hapa unanisema mimi kabisaa!Hii hali inanitesa sana kwakweli!Kujichanganya na watu napo naona shida na hata nikijichanganya najikuta nakaa kimya siwezi kuzungumza!Hivi dawa ya kupona tatizo ni ipi?
Mkuu ishi uwezavyo ishi ujisikiavyo si lazima sana kujichanganya kama huwezi.. maana kwenye kujichanganya pia kuna hasara zake na faida pia hivyo uwe tayari kukabiliana!.
Ukitaka kujichanganya angalia watu husika kama utaweza shea nao story au idea ambazo wewe unazipenda na wao watazipenda kuzisikiliza hapo ndio kutanoga..
Ipo hivi introvert wanapenda mambo mazito mazito,mada nzito nzito so ukikutana na watu wanaopenda kuongelea vitu vyepesi vyepesi kamwe hautapenda company yao!
Sometimes unajikuta unataka ujadili na mtu kitu lkn unakuta sio kwamba unatakiwa ujadili bali umfundishe!! Maana yeye hakijui au hana details za kutosha,yeye anajua diva kaachana na nani na ataenda kwa Nani!!!😂😂
So chagua pia company ya kukaanayo ili ujizoeshe taratibu pia kama kuna michezo unaipenda, penda kuzungumzia,utapata wadau tu taratibu haohao watakufanya uanze kuzoea social kiaina..
Ngoja nikurahisishie jitahidi upate rafiki ambae ni extrovert kundi la sanguine kupitia yeye utajuana na watu wengi so kampani itakuwa kubwa utajua kuwa muongeaji ila ukishaanza kuzoeana na jamii.. ila nakutahadharisha sanguine usiwaambie vitu vyako sana waambie vya kawaida maana hawana shipa la siri watakuliza😂
Jitengee kamuda kidogo ka kutoka na rafiki yako au kwenda hata kuangalia mpira au draft hata nusu saa tu, taratibu itainua hali ya kusocialize.
Ila mkuu usiache asili yako kuwa introvert kuna raha yake pia.. chakufanya weka vitu in a balance.
Unaposocialize angalia unasocialize na watu wa namna ipi utakuja kujiumiza bure kutaka uwiane nao.. unakuta hawakusikilizi hapo huwezi penda kuwa social.
So tafuta walau watu utakao share nao kitu watakaokuwa interest na wewe hi itakupa motisha ya kusocialize na itafungua mengine..
Yangu ni hayo angalia na wengine wanasemaje you'll get something.