Inspirational Speakers wazidi kupungua

Inspirational Speakers wazidi kupungua

Wale jamaa wananishangaza sana anaweza kupa business plan ukifikiria unaona kabisa unatoboa

Ila ukiangalia yeye sasa kiatu chake kimelika sori upande 😀 😀 😀 😀 😀 😀 😀 😀 😀
Kumbuka kuna watendaji na wahimizaji. Ukipewa plan ifanyie kazi ukisha toboa mnunulie pair moja ya viatu umpe, kama asante.
 
Hivi kuna wale labda unaenda zako posta unashangaa anaaza kuaza kitabu sijui eti cha uchumi wakati yeye mwenye aliyekiandika anapigwa jua njia nzima
Point taken. Lakini ngoja nikuulize swali fikirishi na pengine chokonozi. Je hakukuwepo na matajiri enzi za kina Einstein?
 
Na huo ni ujasiriamali kuaminisha jamii na kutoa pesa yao kukusikiliza siyo kazi ndogo.
Sema UTAPELI wa kuaminisha watu mafanikio yanapatikana kiujanja-ujanja. Mafanikio yanakuja kwa kufanya kazi halisi si kubwabwaja jukwaani tu.
 
SIKU HIZI HATA WACHUNGAJI WAMEKUA MOTIVATIONAL SPEAKERS
HAWAHUBIRI HABARI YA DHAMBI NA MAUNGAMO WALA MOTO WA JEHANAMU
WAMEJIKITA KWENYEMAFUNDISHO YA MAFANIKIO YA KIMWILI TU
 
SIKU HIZI HATA WACHUNGAJI WAMEKUA MOTIVATIONAL SPEAKERS
HAWAHUBIRI HABARI YA DHAMBI NA MAUNGAMO WALA MOTO WA JEHANAMU
WAMEJIKITA KWENYEMAFUNDISHO YA MAFANIKIO YA KIMWILI TU
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji115]
U
 
Enyi wahamasishaji mnaosemwa kuwa mmeishiwa ni kweli mmeishiwa? Basi hamuoni mbali na mnapanga karibu. Jamii ina matatizo ambayo hayatokaa yaishe ndiyo fursa ya ninyi kula kwa kupiga mdomo tu mjini hapa.

Hii ya kudakia ufugaji wa sungura sijui mende, kware ni upepo tu.

Mfano mtu anaweza kujiengage katika kuhamasisha watu ulaji wa chakula bora/mpangilio mzuri wa kula ili kuepuka magonjwa yanayotokana na ulaji wa hovyo, uzito uliopitiliza na unene uliopitiliza. Ukifanya hivi kuna watu utawapata utawaunga kwenye magroup ya whatsApp na utawalipisha kiingilie kazi yako ni kuwaeleke wale nini asubuhi mchana na jioni. Muwe makini tu msijewalisha sumu watu walio desperate.

Kuna watu utawapata tu ila sio mimi maana Google napajua. Kila la heri 😀
 
Katika kuonyesha kuwa awamu hii hamna janja-janja wale ndugu zetu watia rangi kwenye maisha (Inspirational Speakers) wamezidi kupungua na kutafuta shughuli halisi na kuachana na mambo ya kupiga domo tupu. Asante sana Mheshimiwa. Tuendapo hata Ma-MC watatoweka kwenye ramani.
Walikuwa wauza madawa, akipata vihela hivyo vya madawa anakuja kuvitakatisha kwa kujifanya eti yeye katumia akili anawamotivate wadau. Wapo wengi mfano Mikono speakers etc
 
Back
Top Bottom