Inspirational Speakers wazidi kupungua

Inspirational Speakers wazidi kupungua

Mtu kama Bahresa, Dewji, Mengi....ndio walitakiwa kuwa Inspirational speaker maana wana ushahidi....wa kimapambano na kiutajiri.....sasa tz makabwela na akina pangu pakavu ...ndio kina Mr motivation speaker!!??haiingii akilini hata kidogo
 
Mtu kama Bahresa, Dewji, Mengi....ndio walitakiwa kuwa Inspirational speaker maana wana ushahidi....wa kimapambano na kiutajiri.....sasa tz makabwela akina pangu pakavu ...ndio kina Mr motivation speaker!!??haiingii akilini hata kidogo
Teh teh teh mwalimu wa ujasiriamali yeye mwenyewe ukisema awe mjasiriamali hawezi Ila anaweza kukusanya pesa za viingilio tu
 
Kuna Sister nilikutana naye kwenye basi kwa jinsi nilivyopauka kwa vumbi la mkaa akajua labda nina ngoma,akanipa kikaratasi akitangaza wanayo hospital inatoa tiba mdabala,inatibu magonjwa sugu na bla bla bla kibao,cha kushangaza huyo siter alikuwa anakohoa kinoma,nikajiuliza mbona na yeye hajitibu kwa hizo tiba mbadala?

Utakutana na hawa watu wanaouza mafuta sijui yanaondoa chunnusi na bla bla kibao,yeye anayeuza hayo mafuta uso wake una chunusi utafikiri fenesi au wanauza dawa za meno kwa kusema zinangarisha meno na bla bla kibao,ukiyacheck meno ya huyo muuzaji utafikiri ni Shabiki wa yanga.

Huwa sinaga upuuzi wa kusikiliza watu wa type hizo.
😂😂😂eti shabiki wa yanga
 
Inspirational speaker na motivational speaker tofauti yao ni ipi?
 
Nimecheka sana kwa kuwa na mimi ni mhusika wa muhimu sana katika fani hii ya inspirational speakers, hata hivyo tambua kwamba waliopungua hawakuwa na maandalizi bora, kujua kwamba majira ya kiangazi lazima utengeneze utomvu mwingi badala ya maji ili kuweza kustahimili ukame, na ndiyo maana mimea mingi ya jangwani ina utomvu na majani ya miiba, au mizizi mingi inayotambaa mbali sana kusaka maji. Sasa kama kuna kipindi kizuri cha inspirational speakers kulamba pesa bila jasho la kwapani basi kipindi hiki ndicho bango la salamu za mafanikio, nani atachomoka hapo! Tatizo la watu wa nchi hii walio wengi wanataka utajiri wa haraka haraka bila mikakati madhubuti. Kila fursa wanataka. Shida iko hapo. Mwenye nia ya kuendelea kui- inspire waungwana, ajisogeze karibu nimpe mbinu mbadala za kusimama kama inspirational speaker misimu yote ya majira ya mwaka bila kuteteleka.
 
Back
Top Bottom