Inspirational Speakers wazidi kupungua

Inspirational Speakers wazidi kupungua

Katika kuonyesha kuwa awamu hii hamna janja-janja wale ndugu zetu watia rangi kwenye maisha (Inspirational Speakers) wamezidi kupungua na kutafuta shughuli halisi na kuachana na mambo ya kupiga domo tupu. Asante sana Mheshimiwa. Tuendapo hata Ma-MC watatoweka kwenye ramani.
Wengine wanajitia midoko ya minduku hahaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi mtu akiniambia "madalali wanapungua, uchumi huu hautaki watu wanaoishi kwa ujanja ujanja wa kunyonya wenzao tu" naweza kumuelewa kuliko mtu akisemahivyo kuhusu "inspirational speakers".

Kwa nini?

Madalali wana ji impose wao kwenye maisha yetu katika shughuli na bidhaa za muhimu ambazo tunahitaji na ni za lazima.

Ukitaka kupanga chumba, kununua nyumba, kununua gari, utakutana nao.

Wanaongeza bei na kuchukua cha juu chao. Mara nyingine huwezikuwaepuka.

Hawa mtu akiwalalamikia na kufurahi wanapungu nitamuelewa sana.

Hao inspirational speakers ukiwasema, watu hawakulazimishi uende kwao wala semina zao si za lazima sana, wanajipigia hela kwa domo kivyao tu, ukisema unafurahi kuona wanapungua, watu wakasema unaona wivu wa kile Wajerumani wanachokiita "schadenfraude" (kufurahia mabaya yanayompata mwenzako bila wewe kufaidika lolote) naweza nikaona sababu ya watu kusema una wivu.

Hawa watu hawakulazimishi uende kwao,unaweza kuwapotezea tu.

Kama wanaishikwa ujanja ujanja wewe kinachokuuma ni kipi as long as wanafanya kazi zao legal na hawakulazimishi wewe uwalipe?

Madalali angalau naweza kuelewa wame tight sekta muhimu utawatumia utake usitake.

Hawa motoivational speakers hata kamawapigaji tu, wanatumia midomo kutengeneza pesa, kama kuna watu wanahitaji huduma yao na wanaipata kwa maelewano bila mtu kulazimishwa, tatizoliko wapi?

Amount of disposable incomein the economy is an indicator of the strength of the economy.

Unaweza kushangilia motoivational speakers wanapungua, kumbe hujui unashangilia uchumi kusinyaa na kesho utasikia effects zake hata wewe.
schadenfraude" (kufurahia mabaya yanayompata mwenzako bila wewe kufaidika lolote)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Me siwakubali tokea mwanzo,maana watatoa vimaneno maneno vingi mwisho wa siku wanakuomba ela,watafute shughuli za kufanya hata udalali


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom