Insane coincidence: Futility and Titanic

Insane coincidence: Futility and Titanic

Kwahiyo mkuu na jambo hili linaweza kuwa ni kama haya matukio ya ndoto unayoyasema?

Ni kwanini Morgan Roberson hakuwa na maono mengine zaidi ya haya?
Nijuavyo mimi (kwa mujibu wa Biblia), Mungu humuonesha mtu amtakaye jambo fulani kwa muda fulani na akiwa na kusudi fulani (ingawa hata shetani huwaonesha watu wake wamwabuduo), na mwingine huoneshwa jambo lingine kwa kusudi fulani. Hata manabii hawakufunulia mambo yote bali kila mmoja alipewa vipande vipande na vipande vilivyobaki akapewa mwingine ili kukamilisha maandiko.

Kwa mfano Yeremia alikuwa akifunulia sana kuhusu majanga/ maafa kiasi kwamba walimpachika jina la nabii wa majanga, lakini Isaya akapewa zaidi mafuno kuhusu Masia, Daniel ndiye aliyepewa mafunuo kuhusu kitabu (Dan. 12:4) alichoambiwa akifunge na kukitia muhuri, lakini kikaja kuonekana kwenye maono na Yohana (kwenye Ufunuo)...
 
Kwahiyo mkuu na jambo hili linaweza kuwa ni kama haya matukio ya ndoto unayoyasema?

Ni kwanini Morgan Roberson hakuwa na maono mengine zaidi ya haya?
Sijawahi kusoma zaidi kuhusu historia ya huyu mtu kujua ni wapi alipopata hayo aliyoyaandika, lakini nadhani kuna connection fulani kati ya 'mtu wa ndani' aliyemwakilisja Morgan na ulimwengu wa roho. Pia sijui kama hajawahi kuandika kitu kingine kilichokuja kutokea kuwa kweli, hivyo nashindwa kumuelezea zaidi...
 
Nijuavyo mimi (kwa mujibu wa Biblia), Mungu humuonesha mtu amtakaye jambo fulani kwa muda fulani na akiwa na kusudi fulani (ingawa hata shetani huwaonesha watu wake wamwabuduo), na mwingine huoneshwa jambo lingine kwa kusudi fulani. Hata manabii hawakufunulia mambo yote bali kila mmoja alipewa vipande vipande na vipande vilivyobaki akapewa mwingine ili kukamilisha maandiko.

Kwa mfano Yeremia alikuwa akifunulia sana kuhusu majanga/ maafa kiasi kwamba walimpachika jina la nabii wa majanga, lakini Isaya akapewa zaidi mafuno kuhusu Masia, Daniel ndiye aliyepewa mafunuo kuhusu kitabu (Dan. 12:4) alichoambiwa akifunge na kukitia muhuri, lakini kikaja kuonekana kwenye maono na Yohana (kwenye Ufunuo)...
Sawa....

Pamoja na yote haya ninajiuliza sana mambo mengi kuhusu hili tukio ambalo kimsingi naliona kama la kushangaza miongoni mwa matukio mengi sana yaliyopo humu duniani....

Ngoja tuendelee kufanya utafiti ili tuone ni kipi kipo kwaajili ya nini....

Shukran sana kwa maelezo yako haya mkuu....
 
Nimekusoma mkuu...

Ninavyojua masuala haya anayekuwa na "maono" haya hawi na maono mara moja tu bali hata zaidi,nashangaa huyu ni tukio hili hili tu.....
Nadhani naiona pointi yako, labda wewe kwa mtazamo wako unadhani kwanini ilikuwa hivyo?...
 
Sijawahi kusoma zaidi kuhusu historia ya huyu mtu kujua ni wapi alipopata hayo aliyoyaandika, lakini nadhani kuna connection fulani kati ya 'mtu wa ndani' aliyemwakilisja Morgan na ulimwengu wa roho. Pia sijui kama hajawahi kuandika kitu kingine kilichokuja kutokea kuwa kweli, hivyo nashindwa kumuelezea zaidi...
Historia ya jamaa inaonesha alikuwa "wa kawaida sana" na wengine walikuwa wakidhani alikuwa na matatizo ya akili....

Kifo chake nacho ni cha kustaajabisha sana maana alikutwa akiwa amekufa kwenye chumba cha hoteli.Wakati Morgan robertson anaishi hakukuwa na wazo la meli hiyo kutengenezwa hadi miaka mingi kidigo baadaye....

Hapo ndipo ugumu wa jambo hili unapokuja....
 
Mbona kunasehemu nilisoma kwamba huyo jamaaa aliyesimamia hiyo meli Mpaka ikakamilika alipo hojiwa uimara wake ulitoa kufuru akasema kwa kwa jinsi ilivyo imara hata mungu hawezi kuizamisha matokeo yake ndo hayo alileta kufuru huyo majinga
Imeandikwa hapo "Meli isiyozama"
 
Historia ya jamaa inaonesha alikuwa "wa kawaida sana" na wengine walikuwa wakidhani alikuwa na matatizo ya akili....

Kifo chake nacho ni cha kustaajabisha sana maana alikutwa akiwa amekufa kwenye chumba cha hoteli.Wakati Morgan robertson anaishi hakukuwa na wazo la meli hiyo kutengenezwa hadi miaka mingi kidigo baadaye....

Hapo ndipo ugumu wa jambo hili unapokuja....
Nilitegemea kusikia kuhusu huu mwisho wake. Sasa naamini kabisa kuwa jambo hilo lilikuwa na uhusiano na ulimwengu wa roho, maana wengi wao huwa na sifa kama za huyo mtu: wanaonekana kuwa ni watu wa kawaida sana, wanaonekana kama wana matatizo ya akili (kwa kuwa wanaishi katika dunia inayoitwa 'beyond imagination'), na hata vifo vyao huwa ni vya kutatanisha, au huambatana na mauzauza fulani...

Nikipata nafasi nitaeleza zaidi kuhusu dunia ya 'beyond imagination' (kwani kwa sasa kuna kazi muhimu naifanya kwanza), kwani wengi waliofanikiwa sana (kama marais, wafanyabiashara wakubwa, watu mashuhuri) walianzia kwenye hii dunia kabla ya kufika hapo walipo...
 
Mwaka huu niliota ndoto nipo katikati ya Kundi la Polisi wenye vyeo vya juu (CP, DCP SACP, ACP) katika Jeshi la Polisi wakiniskiliza tukiwa tunapiga stori (mimi sio Polisi) tukiwa maeneo ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, nilipoamka asubuhi nikajiuliza sana juu ya ndoto hii na sikupata majibu. Nikaamua kupuuzia, lakini wiki iliyofuata nikawa katika mazingira yaleyale Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (katika ulimwengu wa mwili na sio ndoto tena) nikiwa nimezungukwa na Polisi walewale niliowaona ndotoni tukipiga stori, hii ilikuwa wakati tukisubiri kuuaga mwili wa mpwa wangu Peter Kubezya (yule OCCID aliyeuawa Kibiti ambaye mwili wake uliagwa Muhimbili kabla hajasafirishwa kwenda kuzikwa Ushirombo). Wakati nikiongea na askari hao ikanijia picha ileile niliyoiona kwenye ndoto...
Hii hali hunitokea
 
Mkuu Eiyer kuna habari titanic ilizamishwa kwa sababu ya matajiri watatu waliokwemo ndani ya titanic,ambao ni Benjamin Guggeenhein, Isador Strauss pamoja na John Jacob Astor aliyeaminiwa kuwa tajiri namba moja duniani kwa wakati huo.
Pia ni vyema tukawajua hawa kina Ismay na mrs astor walikuwa ni kina nani na kwa nini waliatract public interests,vifo vyao vilikuwaje latter on?pia walikuwa wanajihusisha na taasisi gani?
 
Nimekusoma mkuu...

Ninavyojua masuala haya anayekuwa na "maono" haya hawi na maono mara moja tu bali hata zaidi,nashangaa huyu ni tukio hili hili tu.....
Huenda mengine hayakuwa ya kusisimua kama hilo kiasi yasingelipa kama angeandikia vitabu.
 
Historia ya jamaa inaonesha alikuwa "wa kawaida sana" na wengine walikuwa wakidhani alikuwa na matatizo ya akili....

Kifo chake nacho ni cha kustaajabisha sana maana alikutwa akiwa amekufa kwenye chumba cha hoteli.Wakati Morgan robertson anaishi hakukuwa na wazo la meli hiyo kutengenezwa hadi miaka mingi kidigo baadaye....

Hapo ndipo ugumu wa jambo hili unapokuja....
Note hii pointi"alikuwa na matatizo ya akili"
 
Back
Top Bottom