Inajulikana kuwa mwanzoni mwa miaka ya 1830 Amerika bado ilikuwa haijawa na Benki Kuu wakati majasusi hawa wa Ki-Italiano walihitaji benki nyingine Amerika ambayo wangetumia kuchota fedha kwa ajili ya kufanikisha mipango yao ya vita na ajenda nyingine za siri duniani kote.
Mnamo mwaka 1910 karibu na pwani ya Georgia katika kisiwa cha Jekyll wanaume saba walikutana kwa lengo la kuanzisha benki hiyo ambayo ingeitwa Benki ya Akiba. Hapa ninawazungumzia Nelson Aldrich na Frank Vanderlip ambao waliwakilisha taasisi ya fedha ya tajiri Rockefeller; Henry Davison, Charles Norton na Benjamin Strong waliowakilisha kampuni ya J.P, wengine ni Morgan na Paul Warburg waliowakilisha benki ya Uropa ijulikanayo kama Rothschilds ambayo ilikuwa ni wakala wa Kipapa ikifanya kazi moja tu, nayo ni kulinda utajiri wa kanisa la Katoliki.Ujenzi wa meli ya Titanic ulianza mnamo mwaka 1909 katika karakana ya kutengeneza meli ya Belfast, mji mkuu wa Ireland Kaskazini ukiwa na waumini wengi wa Kiprotestanti ambao walikuwa ni maadui wakubwa wa Jesuits katika harakati zao za kusimika Ukatoliki duniani.
Hii ilitokana na hofu kwa Jesuits kwamba watu hawa wangeweza kutumia umaarufu na utajiri wao kuzuia kuwepo kwa Benki ya Akiba. Na kwa kuwa hawa ni watu ambao walipenda starehe na kuponda raha, ni lazima wangependa kuishi ndani ya Titanic ambayo iliundwa maalumu kama kaburi lao bila kujua.