Innaa lillahi wainnaa ilayhi raaji uun waislamu tumefikia hatua hii ?!!!

Status
Not open for further replies.

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,408
33,285



KIWANDA CHA POMBE CHATOA MSAADA PEMBA KWA AJILI YA RAMADHANI..

PICHANI: Mkurugenzi wa Kampuni ya (KUTENGENEZA POMBE YA KONYAGI) Tanzania Distilleries Limited (TDL) David Mgwassa (kushoto),

akiwakabidhi msaada wa vyakula na mafuta ya kupikia vyote vikiwa na thamani ya sh.milioni 9, wabunge wa Zanzibar, Ahmed Ngwali (kulia), wa

Jimbo la Ziwani na Khalifa Suleiman wa Jimbo la Kagando kwa ajili ya kuwasaidia wajane na yatima waliofiwa na wategemezi wao katika ajali ya meli

ya Mv Spice na Skagit zilizotekea visiwani humo. Makabidhiano hayo yalifanyika Dar es Salaam juzi.

Mgwasa, alisema,"Kampuni yetu inatoa msaada hasa kwa ajili ya Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani ili watoto hawa yatima wakapate futari.

Alisema msaada uliotolewa umelenga kuwasaidia yatima walioko Pemba kwanza. Mbunge wa Gando, Khalifa alisema "...Na pia wananchi wasitizame

nani ametoa msaada ila ini amesaidia ili tu kuwasaidia hawa wenye uhitaji," alisema Khalifa. (via HabariLeo)

chanzo. Habarileo


Kama ningelikuwa ndio mimi mpokezi wa huo Msaada ;Wallah nisingelipokea kamwe Msaada wa haramu huo.

SURAT AL MAIDA Sura 5:90-91-92

90. Enyi mlio amini! Bila ya shaka ulevi, na kamari, na kuabudu masanamu, na kupiga ramli, ni uchafu
katika kazi ya Shet'ani. Basi jiepusheni navyo, ili mpate kufanikiwa.



91. Hakika Shet'ani anataka kutia kati yenu uadui na chuki kwa ulevi na kamari, na akuzuieni kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kusali. Basi je, mmeacha

92. Na mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume, na tahadharini. Na ikiwa mtageuka basi jueni ya kuwa juu ya Mtume wetu ni kufikisha ujumbe tu ulio wazi.

Pesa inayotokana na Pombe na Kamari ni Pesa ya Haramu haifai kwa Muislam kuitumia kwa kulia futari ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
 
mzizi mbona katoa chakula na mafuta wala hajatoa chupa ya nyagi au kiroba!! hizo aya hapo zinaongelea pombe siyo vyakula.
Hebu lete inayosema chanzo cha mapato gani sisi tukatae!!
SP
 
Poleni sana Mzizi!

nyie kuleni bhana mungu ndiye nayefahamu kuwa huyu amekose na yule ampatia na kamwe si binadamu tuacheni kutishiana.

Ni msaada wa chakula si pombe, hivyo hamna kosa hapo, kuleni tu.
Mkuu mayenga Mkuu NAHINGA Mkuu Mkereketwa_Huyu
WA-DANGANYIKA kwakupenda misaada hamuwezekani kamwe. Rias Obama kaja kuwapa misaada ya Umeme na anataka kwenu muruhusu Mashoga wawe na haki kama binadamu wengine Je mtakubali misaada ya Masharti? Unajuwa Rais Obama kazungumza kitu gani na Mzee J.K. kwa njia ya siri? ninaombeni majibu toka kwenu.

WADANGANYIKA MUKIPENDA MISAADA SIKU MOJA MTAOMBWA NA NYINYI MULIPE HIYO MISAADA MSIJE KURUSHA NGUMI TU.
 
Huu ni msiba. Ipo siku tutawapa hawa makafiri mimbari watoe hut'ba ili tupate pesa.

Juzi tumemuita Lowasa na kumvisha kilemba, leo tunapokea misaada.

Huu ni msiba.
Mkuu Mzee Siasa na mambo ya Dini ni vitu 2 Tofauti kabisa Serikali ya Tanzania haina dini.

Kumvisha Lowasa kilemba ni sawsawa kumvisha kilemba mbuzi atabadilika mbuzi ukimvisha kilemba? Si atakuwa huyo huyo Mbuzi Sio hatabadilika mbuzi kuwa ni Binadamu?
 
Hawatakua radhi mayahudi na manaswala,mpaka mfate mila zao.
Ikiwa mtafanya hivyo mtakua mmeshaingia katika mtihani!
 
Kama mkisusia iteni watu,kuna watu hawana chakula.
Bora wapewe Watu wasiokuwa Waislam kuliko

kupewa waislam tena kwa ajili ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani wanapewa misaada ya haramu kutoka kwa wafadhali wa haramu

ahhhhhh Allah Akbaru Mwenyeezi Mungu Mkubwa
ray05 wangeli wasaidia hao Mayatima kwa kusema tunatoa msaada wetu kwa

hawa waliopata ajali sio kwa ajili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wanangojea mpaka Mwezi Mtukufu wa Ramadhani uingie

wanajitia kutoa huo msaada wao wa haramu ahhhh ili wapate kuonekana kuwa nao wametoa Misaada inayotoka kwenye

kiwanda cha Bia?
 
Acha unafiki. Ni aheri ya hao wauza pombe wanaojali yatima kuliko wewe unayejifanya mcha mungu unawaacha wakitaabika. Tuambie ni msaada gani uliowapa yatima??
 
Sheikh Qatada na familia yake na yeye naskia alikua anategemea nyonyo kutoka kwa serikali ya Uingereza inayosapoti uhuru wa mashoga na vurugu zote zilizokatazwa na allah/
 
Mkuu mayenga Mkuu NAHINGA Mkuu Mkereketwa_Huyu
WA-DANGANYIKA kwakupenda misaada hamuwezekani kamwe. Rias Obama kaja kuwapa misaada ya Umeme na anataka kwenu muruhusu Mashoga wawe na haki kama binadamu wengine Je mtakubali misaada ya Masharti? Unajuwa Rais Obama kazungumza kitu gani na Mzee J.K. kwa njia ya siri? ninaombeni majibu toka kwenu.

WADANGANYIKA MUKIPENDA MISAADA SIKU MOJA MTAOMBWA NA NYINYI MULIPE HIYO MISAADA MSIJE KURUSHA NGUMI TU.


Hayo yaliyozungumzwa kwa siri kama ushoga ni kati yake basi laana italala kwao sie si mashoga, ukuta unapandwa tu kama unakimbia ugoni ila haushikwi kwa kulazimishwa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom