Wachina waliopo nchi za nje wajumuika na waislamu duniani kutoa michango katika mwezi wa Ramadhani

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111201494809 (2).jpg


Katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani imekuwa ni ada na desturi kwa Waislamu na wasiokuwa Waislamu kuendeleza moyo wa kuchangia na kuwasaidia watu wa makundi mbalimbali. Na hii ni pamoja na kufutarisha mayatima, watu wenye maisha duni, waumini wa misikitini ama hata watu kawaida kualikana majumbani na kufutarishana. Mbali na kufutarishana pia watu huwa wanatoa mchango wa fedha na kuwapa wale wenye uhitaji. Je makampuni ya China yanayoendesha shughuli zao katika nchi za nje yanashiriki vipi kusaidia watu katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani?

Tunafahamu kuwa Wachina wote wana moyo wa kujitolea hasa pale wanapoona wenzao wana tatizo ama wanahitaji msaada wowote ule. Hivyo katika mwezi huu wa Ramadhani makampuni mbalimbali yanakuwa mstari wa mbele kusaidia watu kadiri yawezavyo na kuhakikisha angalau muda wa kufutari unapofika, wale wenye uhitaji wanakuwa na futari mezani au popote pale walipo.

Kufanya matendo mema au kutoa zaka katika mwezi mutukufu wa Ramadhani, ni kitendo kinachochukuliwa kama kitakatifu zaidi, hasa katika kumi la mwisho wakati ambao Waislamu wanaamini Mungu alimshushia wahyi yaani aya za kuran mtume Muhammad (S.A.W). Hivyo Wachina waliopo nchi za nje ambao wengi wao sio Waislamu bali wanapenda kujumika na wenzao waislamu, wanatoa michango ya aina mbalimbali wakilenga kutoa msaada kwa watu wenye uhitaji, kueneza upendo na kujiamini na kuimarisha urafiki baina ya Watu wa China na wa nchi walizopo.

Mwaka jana yaani 2022, ubalozi mdogo wa China ukishirikiana na jamii ya Wachina waliopo nje na wanafunzi Wachina waliopo Dubai, walichangia futari yenye thamani ya zaidi ya Dh132,000 kwa Mamlaka ya Maendeleo ya Jamii (CDA) ambayo iko mbele zaidi kusaida watu katika miaka ya hivi karibuni. Halikadhalika, makampuni ya China yaliyopo Dubai yamechangia zaidi ya Dh63,000 ili kuongeza nguvu Mpango wa chakula wa Bilioni Moja (1 Billion Meals initiative) wa Amiri wa Dubai Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum.

Watu wengi wanajua kuwa Ramadhan ni wakati wa kutekeleza ibada ya kufunga, lakini wachache ndio wanafahamu kuwa huu ni mwezi ambao Waislamu wanachangia pesa zaidi kwenye mashirika ya hisani kuliko wakati wowote ule katika mwaka. Na hii ni kwasababu Uislamu una nguzo tano zikiwemo Kuamini Mungu Mmoja tu na Muhammad ni mtume wake, kusali sala tano kwa siku, kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, kwenda Maka kuhiji angalau mara moja maishani, na kutoa

mchango ambao ni lazima unaojulikana kama Zaka.

Kwa wachina waliopo nchi za nje, mara nyingi huwa wanafuatilia mila, desturi au utamaduni wa nchi walizopo, na hivyo kujumuika na wenyeji wao kwa chochote kile kizuri kinachofanyika katika nchi hizo. Mwezi Aprili mwaka jana, katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, makampuni zaidi ya 30 ya China yaliyopo Cairo, Misri, nayo pia yalitumia fursa hii adhimu ya kuchangia wakati wa Ramadhani na kutoa mchango wa pauni za Misri milioni moja (sawa na dola 54,245 za Kimarekani) ili kusaidia familia zenye uhitaji. Hafla hiyo ya mwaka jana ni ya nane tangu izinduliwe na Chama cha Wafanyabiashara wa China nchini Misri mwaka 2015.

Kwa miaka mingi, makampuni hayo yamekuwa yakitoa mchango wa maboksi ya zawadi za Ramadhani zaidi ya 10,000 na umenufaisha familia maskini zaidi ya 40,000. Hii ni dhahiri kwamba popote pale wanapokwenda, Watu wa China wanabeba maadili ya kitamaduni mioyoni mwao ya kuonesha na kurejesha wema, na kwa makampuni ya China kuweza kuchukua hatua kama hii ya kusaidiana bega kwa bega na wenyeji wao hasa katika kipindi hiki cha Ramadhani, inaonesha kuna urafiki mkubwa wa hali na mali kati ya Wachina na watu wa nchi walizopo.

Ni matumaini yangu kwamba watu wote wenye dhiki, shida na taabu katika kipindi hiki, watanufaika na michango na zaka zinazotolewa kwa ajili yao. Ni vyema pia kuwafariji mayatima katika vituo mbalimbali ili wajihisi amani moyoni wakati wanapotekeleza ibada ya funga. Ramadhani ni mwezi wa kurejesha fadhila unazobarikiwa na Mungu, hivyo mwenye uwezo ni vyema akachangia na kusaidia watu wenye matatizo mbalimbali.
 
View attachment 2579147

Katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani imekuwa ni ada na desturi kwa Waislamu na wasiokuwa Waislamu kuendeleza moyo wa kuchangia na kuwasaidia watu wa makundi mbalimbali. Na hii ni pamoja na kufutarisha mayatima, watu wenye maisha duni, waumini wa misikitini ama hata watu kawaida kualikana majumbani na kufutarishana. Mbali na kufutarishana pia watu huwa wanatoa mchango wa fedha na kuwapa wale wenye uhitaji. Je makampuni ya China yanayoendesha shughuli zao katika nchi za nje yanashiriki vipi kusaidia watu katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani?

Tunafahamu kuwa Wachina wote wana moyo wa kujitolea hasa pale wanapoona wenzao wana tatizo ama wanahitaji msaada wowote ule. Hivyo katika mwezi huu wa Ramadhani makampuni mbalimbali yanakuwa mstari wa mbele kusaidia watu kadiri yawezavyo na kuhakikisha angalau muda wa kufutari unapofika, wale wenye uhitaji wanakuwa na futari mezani au popote pale walipo.

Kufanya matendo mema au kutoa zaka katika mwezi mutukufu wa Ramadhani, ni kitendo kinachochukuliwa kama kitakatifu zaidi, hasa katika kumi la mwisho wakati ambao Waislamu wanaamini Mungu alimshushia wahyi yaani aya za kuran mtume Muhammad (S.A.W). Hivyo Wachina waliopo nchi za nje ambao wengi wao sio Waislamu bali wanapenda kujumika na wenzao waislamu, wanatoa michango ya aina mbalimbali wakilenga kutoa msaada kwa watu wenye uhitaji, kueneza upendo na kujiamini na kuimarisha urafiki baina ya Watu wa China na wa nchi walizopo.

Mwaka jana yaani 2022, ubalozi mdogo wa China ukishirikiana na jamii ya Wachina waliopo nje na wanafunzi Wachina waliopo Dubai, walichangia futari yenye thamani ya zaidi ya Dh132,000 kwa Mamlaka ya Maendeleo ya Jamii (CDA) ambayo iko mbele zaidi kusaida watu katika miaka ya hivi karibuni. Halikadhalika, makampuni ya China yaliyopo Dubai yamechangia zaidi ya Dh63,000 ili kuongeza nguvu Mpango wa chakula wa Bilioni Moja (1 Billion Meals initiative) wa Amiri wa Dubai Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum.

Watu wengi wanajua kuwa Ramadhan ni wakati wa kutekeleza ibada ya kufunga, lakini wachache ndio wanafahamu kuwa huu ni mwezi ambao Waislamu wanachangia pesa zaidi kwenye mashirika ya hisani kuliko wakati wowote ule katika mwaka. Na hii ni kwasababu Uislamu una nguzo tano zikiwemo Kuamini Mungu Mmoja tu na Muhammad ni mtume wake, kusali sala tano kwa siku, kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, kwenda Maka kuhiji angalau mara moja maishani, na kutoa

mchango ambao ni lazima unaojulikana kama Zaka.

Kwa wachina waliopo nchi za nje, mara nyingi huwa wanafuatilia mila, desturi au utamaduni wa nchi walizopo, na hivyo kujumuika na wenyeji wao kwa chochote kile kizuri kinachofanyika katika nchi hizo. Mwezi Aprili mwaka jana, katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, makampuni zaidi ya 30 ya China yaliyopo Cairo, Misri, nayo pia yalitumia fursa hii adhimu ya kuchangia wakati wa Ramadhani na kutoa mchango wa pauni za Misri milioni moja (sawa na dola 54,245 za Kimarekani) ili kusaidia familia zenye uhitaji. Hafla hiyo ya mwaka jana ni ya nane tangu izinduliwe na Chama cha Wafanyabiashara wa China nchini Misri mwaka 2015.

Kwa miaka mingi, makampuni hayo yamekuwa yakitoa mchango wa maboksi ya zawadi za Ramadhani zaidi ya 10,000 na umenufaisha familia maskini zaidi ya 40,000. Hii ni dhahiri kwamba popote pale wanapokwenda, Watu wa China wanabeba maadili ya kitamaduni mioyoni mwao ya kuonesha na kurejesha wema, na kwa makampuni ya China kuweza kuchukua hatua kama hii ya kusaidiana bega kwa bega na wenyeji wao hasa katika kipindi hiki cha Ramadhani, inaonesha kuna urafiki mkubwa wa hali na mali kati ya Wachina na watu wa nchi walizopo.

Ni matumaini yangu kwamba watu wote wenye dhiki, shida na taabu katika kipindi hiki, watanufaika na michango na zaka zinazotolewa kwa ajili yao. Ni vyema pia kuwafariji mayatima katika vituo mbalimbali ili wajihisi amani moyoni wakati wanapotekeleza ibada ya funga. Ramadhani ni mwezi wa kurejesha fadhila unazobarikiwa na Mungu, hivyo mwenye uwezo ni vyema akachangia na kusaidia watu wenye matatizo mbalimbali.
Vipi wale Wachina wakiislam wanaopewa mafunzo ya kuwa Wachina watiifu na kufungiwa kifungo kisichojulikana katika mazingira yasio utu, mnawapa nini?
 
 
Back
Top Bottom