Nimejaribu kufuatilia mwenendo wa mashindano haya ya CHAN hasa ushiriki wa mashabiki uwanjani, ukweli ni kuwa Tanzania bado sana. Sio tu mashabiki, hata viongozi wenyewe ni kama vile wanajilazimisha tu kujihusisha na CHAN ila wako serious sana na siasa. Inawezekana vipi timu ya Taifa inacheza alafu uwanja ni mtupu? Katika mechi zote tatu za Stars hakuna mechi hata moja tumejaza uwanja. Tutatia aibu sana mashindano ya 2027. Kuna wakati naona bora mashindano ya 2027 yahamishwe tu. Ladha ya soka ni mashabiki, sasa watu wamefanyiwa 2000 kiingilio na hawaendi uwanjani, seriously? Picha hapo chini ni mechi ya Stars ya Jana vs Madagascar