Inaumiza sana mzazi kusomesha mtoto degree ya udaktari, ajira hapati anaishia kuwa muuza pafyumu kwa kucheza cheza mtandaoni wateja waone bidhaa

Inaumiza sana mzazi kusomesha mtoto degree ya udaktari, ajira hapati anaishia kuwa muuza pafyumu kwa kucheza cheza mtandaoni wateja waone bidhaa

Angalau hajaokota makopo kwenda kuuza Tsh 250 kwa kilo 1
 
Ajira sio lazima bongo,ajira ni world wide tafuteni ajira hadi nje ya nje kampuni nyingi tu zinaoffer visa na transport na cost zote ili ufike kule ukifika kule wanakata cost zao kupitia mshahara wako.
Tafuteni maarifa ndio dawa ya umasikini.

Raslimali kuu zama hizi ni kuwekeza kwenye fikra.
Pana sister alikuwa anafundisha shule hizi za st kapata ajira online Leo yupo Canada kaskazini ni mwalimu.

Watz mnatakiwa muwe na akili za wanigeria na wakenya wanaview global.
We ni kijana una nguvu badala ya kuangalia fursa nje unakomaa bongo tu
 
kuna mwalimu anatembeza mayai.
kuna mwalimu anashona viatu.
kusoma sio kupata ajira
 
Maisha mkuu hayanaga muongozo na dunia hii ya koneksheni ukikosa ndo basi tena. Inabidi tu utafute kitu cha kufanya.
 
Mbona mi nimekuwa dada kucha nasugua watu miguu tu saivi😂😂 kawaida sana!
 
Sio lazima aajiliwe, kusoma medicine kunakupa fursa nyingi za kufanya, mpereke china au muhimbili akapige alternative medicine kwa wiki kadhaa kisha ajiajiri awe anapiga combine

Utanishukuru baadae
 
Wasioajiriwa lazima wakiri kuwa kweli wanahitaji hizi nafas za kuajiriwa. Nje ya hapo hawawez kuhesabiwa kama hawana ajira
 
Hospitali zote hizi hta per time kakosa nafasi daktari kweli?
 
Haya mambo yanakatisha sana tamaa kusomesha watoto shule binafsi.

Wazazi wengi wamepeleka watoto shule za serikali nowdays

Maana unajibana kulipa ada kubwa halafu baadae anakuja kuzunguka na bahasha na ajira hapati

100% Fact.

Joannah endelea kuwafurahisha majirani wakuone una hela nyingi..
 
Kuna mtu aliwalazimisha kusoma. Kusoma usome wewe kisha ulaumu wengine
Kuna wenzio walioishia drs la 7 kidt 4 na wengine hawakupata bahati kabisa wala hawamlaumu mtu wanajipambania. Kwani uspesho wa nyie mliosoma ni nini mpaka serikali iweweseke na nyie.
 
Huyo st kayumba product. Angekua na English angeenda saka ajira nchi za wathunguuuuu
Ndo sasa utoe watoto wako EMS warudishe Kayumba fasta. Sio unasema inasikitisha sana halafu watoto wako bado wapo EMS😁😁😁
 
Back
Top Bottom