In Edward Lowassa, I trust...

In Edward Lowassa, I trust...

Rev ; Sio kweli na si haki. Chagua kula Keki au kuiweka, na wala hakuna mrengo wa kati juu ya hili. Tupe msimamo wako tushike yepi uliotamka Awali au Leo?

Jujuman,

Msimamo wangu utakusaidiaje wewe kutumia haki yako ya kumchagua yule unayemdhani ni bora?

Je Mchungaji kusema Lowassa atatufaa, basi nawe bila kujipima na kufikiria unaunga tela na kuafikiana nami? Je kufanya kwako hilo la kuunga tela si ndilo tunalolipigia kelele kuwa wale 80% walitekwa kwa tabasamu na kuunga tela?

NImesema, na narudia tena bila kujing'ata ulimi kuwa nilichokisema awali kuhusu Lowassa kitabakia kama nilivyokitamka na nilichokisema leo nacho nakisimamia vile vile.

Sasa sababu zangu za kumnadi Lowassa, nimezitaja. Uamuzi ni wako kukubaliana nami au kutokubaliana nami.
 
Tatizo lake mkuu watafuasi wanakufuata mkuu wangu.. sii swala lako wewe kama kiongozi wa dini fahamu kuna waumini..

Ndivyo Tulivyo ni pamoja na kushindwa kuelewa haramu..Nitakuuliza wewe, Hitler na Stalin nani mbora!

Hitler na Stalin walikuwa ni wadhalimu na walifanya unyama machoni petu.

Ingawa wote walikuwa na ambo ambayo hayapendezi, lakini kuna mambo yaliyofanywa nao kama viongozi ambayo si ya kupuuzia au kuyaacha kisa eti ni Hitler na Stalin.

Hitler na Stalin walikuwa na waliyoyafanya ambayo leo hii tumejifunza kutoka kwao ambayo ni kuhusiana na uongozi, na uhamasishaji.

Hata Karl Peters na Ayatollah Khomeini nayo wana yao ambayo tumejifunza na tunayatumia katika maisha yetu, ingawa kila mmoja wetu anaweza kutoa wasifu wenye taswira moja na chafu.
 
Hitler na Stalin walikuwa ni wadhalimu na walifanya unyama machoni petu.

Ingawa wote walikuwa na ambo ambayo hayapendezi, lakini kuna mambo yaliyofanywa nao kama viongozi ambayo si ya kupuuzia au kuyaacha kisa eti ni Hitler na Stalin.

Hitler na Stalin walikuwa na waliyoyafanya ambayo leo hii tumejifunza kutoka kwao ambayo ni kuhusiana na uongozi, na uhamasishaji.

Hata Karl Peters na Ayatollah Khomeini nayo wana yao ambayo tumejifunza na tunayatumia katika maisha yetu, ingawa kila mmoja wetu anaweza kutoa wasifu wenye taswira moja na chafu.
Mkuu sikuomba maelezo nimeuliza Hitler na Stalin nani mbora..
 
Knowing Rev. Kishoka very well I make the following observation::

Rev. Is trying to invoke debate so we can discuss who is capable of leading TZ.

He picked EL knowing very well this will make the most bang and will force people to really question the crisis in leadership we are facing in Dar and what needs to be done in 2010 and 2015.

Binafsi, nasema EL is a no no lakini swala je huyu Jk naye vipi?? Nani mwingine ambaye anaweza kutuongoza watanzania tukatoka kwenye hili giza nene la umaskini, magonjwa na matatizo lukuki???
 
Moelex23,
Mkuu wangu nilimuuliza swali Rev kwa makusudi kabisa na nadhani kaingia kizani kwa sababu anajua kuna mtego..

Mimi hoja yangu ni kwamba unapowapa Ndivyo Tulivyo swali kama hili mara nyingi kama sii zote watachagua kweli kati ya Hitler na Stalin lakini ukweli ni kwamba Ukisema hakuna mbora kati yao hutakuwa umekosea na ndilo jibu watu wenye akili zao timamu watategemea..
Edward kwa mazuri alofanya hakuyafanya kwa sababu ni kiongozi mzuri ila kayafanya kwa sababu yamo ktk mikakati yake ya Ubwana, Ushenzi na Udikteta kama hao kina Hitler na Stalin.
Sasa kuweka mazungumzo ambayo yana suggest hata kwa uchache kuwa Lowassa anatufaa sasa hivi wakati mimi binafsi naweza taja majina 10 kama sii 20 toka hata hapa JF wanaoweza kuwa mbele ya Lowassa ni kulitukana Taifa na wafuasi wake wote..
Hapana mkuu wangu kila tunapomzungumzia Lowassa na kumpa sifa fulani ni sawa na kuwakumbusha Wayahudi Genocide!
 
JKN alisema huyu jamaa ni KIBAKA.

Acha tusahau UKIBAKA wake na tusonge mbele.

Alikuwa na PUPA na ushamba fulani hivi. Wee mtu na akili zako utawafokeaje wakuu wa mikoa mbele ya RAIA? Kesho wakiacha kumuheshimu? Mtu wa busara unaangalia tu mambo na kusifia ila mkifika ndani, panakuwa hapatoshi.

Halafu mipupa yake. Nina wasiwasi akisikia Wazungu wamejenga Space Station, na yeye atakurupuka basi na sisi tujenge. Kasikia Mvua za Asia basi na sisi anataka kutuletea. HAna subira ya kuwauliza washauri wake.

Kwa ujasiri alionao, na kama angeliacha UKIBAKA na KUKURUPUKA, basi nakubaliana na wewe kuwa NI KIONGOZI IMARA SANA. Ila ni mtu anayeweza kutupeleka hatua mbele mbele na mbili nyuma. Hapo tunakuwa tuko palepale kama tulivyo kwa Kikwete.

Chagua langu ni Dr. Slaa na/au Davis Mwamunyange. Mwamunyange akiwa PM na washauri kadhaa na Slaa akiwa Rais. Mjeshi atatunyoosha sisi.
 
Ogah,

Kwa nini uuchome waraka wa mchungaji? kwani waraka una kosa gani na ni kosa gani ninalolifanya hapa kumnadi Lowassa?

Si hata Kikwete baada ya kumtukana na s c rew Muungwana nilimpa props zake na Thanks God for giving us Kikwete?

Sasa mwashangaa nini? kama nimeona kito ndani ya Lowassa, kwa nini nisikiseme pamoja na maneno yangu ya awali bado nayasimamia kama yalivyokuwa?

Kumkataa EL si kwa sababu hana uwezo kiutendaji.........la hasha.....certainly you know this........hicho ulichokiona ndani ya EL most of JF members wanafahamu........

Mkuu Rev. hebu tutoke nje ya box angalau.................
 
Na mvua yake ya kubumba(kuumba) iliishia wapi kweli?.Inaonekana huku kukosekana kwa umeme kunamuuma sana EL kwani angekuwa ameshavumbua hata mfereji wa kuchota maji kutoka Bahari ya hindi mpaka kidatu.
 
wee unayejiita mchungaji unajua kama unatia kichefuchefu......
sijaona jitu lisilokuwa na maarifa ya kufikiri duniani kama wewe.
Yale yale ya wanawaisrael jangwani....ni bora Misri utumwani kulko hapa jangwani.
 
wee unayejiita mchungaji unajua kama unatia kichefuchefu......
sijaona jitu lisilokuwa na maarifa ya kufikiri duniani kama wewe.
Yale yale ya wanawaisrael jangwani....ni bora Misri utumwani kulko hapa jangwani.

Tapika basi, tutapiga deki kwa kuwa wewe ni Pharaoh!
 
Yes, I have said it. Ili tuendelee, tunamhitaji Edward Ngoyayi Lowassa!

Ni mchapakazi, mfuatiliaji na mkali asiye na masikhara na walioko chini yake si kuwa wanamheshimu tuu, wanaogopa kushukiwa na zali kutokana na ukali na ufuatiliaji wake.

Kila kazi aliyopewa, kaifanya kwa bidii na kwa ufanisi. Kuna tofauti kubwa sana za kiutendaji kati yake na wenzake walioshika nafasi za uongozi ambazo alizishikilia.

Naamini kwa dhati kuwa ili Tanzania iweze kuamka na kurudi katika mstari ulionyooka wa kujituma, kufanya kazi kwa bidii na maarifa bora na la zaidi kwa nidhamu ili tuendelee vyema na safari yetu ya kujijenga kiuchumi na kijamii ili kuleta maendeleo ya kweli, basi hakuna mwingine zaidi ya Lowassa!

Kama unaye wa kwako, tupe jina na umnadi, wangu miye ni Lowassa!

Mkuu Rev Kishoka. naona kama kuna ujumbe fulani muhimu sana ndani ya hii post yako ya "kichekesho". Nakubaliana na wewe kuwa kuna nyakati fulani tunahitaji Mrema style na Lowassa style of leadership. Lakini Tunahitaji Lowassa asiyefisadi na mjanjamjanja, au visionary and less emotional Mrema. Kama ukilinganisha na Muungwana kuna hali fulani inayoonesha kukosa waktu kama hao wawili kumweka vacuum fulani.
 
Companero,
Hata kama uchumi wetu utastawi under Edward nakuhakikishia 50% itakuwa mali yake. Ataigeuza Tanzania kuwa Lowassa Inc. Mark my words. Lakini it is very sad kwamba Tanzania tumesink this low hata kumfikiria mwizi aliyekubuhu kutuongoza just because ana uwezo wa kuhakikisha anachotaka kifanyike kinatekelezwa. Don Corleone was also a good Catholic.

Hey something is better than nothing. Heri yeye achukue 50% sisi atuachie 50%. Hiyo ni afadhali mara 100 kuliko mrahaba wa madini wa 3% na mgao wa umeme wa 58%!
 
Haya ni maneno ya Rev.Kishoka bout a year ago.I loved the LAST paragraph!

"....A task at hand is to neutralize his supportes by unseating them from our Parliament and even within CCM ranks. We should expose all his backers and supportes and treat them as traitors to our country and our constitution.
My fellow Tanzanians, we should be aware of Lowassa intentions to become our leader.
We should treat him and isolate him like a leper, a man who is infectious and never to be trusted."
 
Hata kwa ufisadi na kujilimbikizia mali IN EDWARD I TRUST
 
Back
Top Bottom