RICHMOND report does not implicate him directly!this is my understanding na kama anahusika why serikali haimfikishi mahakamani?the problem is not him ni weekness ya serikali yenu ya kuungaunga hii
Kama alipora kiwanja cha kanisa Mbezi ,mbona mkapa na sumaye kapora mahekta ya ardhi kibaigwa hamsemi.
Utajiri wake wewe ndo huuelewi na huuelewi kwa kuwa wewe ni masikini so utaendelea kutoelewa kwa kuwa wewe si miongoni mwa matajiri
Suala la jengo la vijana CCM akongelee huko CCM sio hapa ndo maana wenyewe waliona hana kosa na mpaka leo ujenzi unaendelea..na aliyeleta kidomodomo juu ya jengo hilo Nnape kilichompata umekiona.
mengine ni chuki binafsi na umasikini ndo unawasumbua walio wengi...
Maana nyingine ya "Kigogo" ni a body mass lisilo na uwezo mkubwa au haupo kabisa wa kufikiri.
Hujajibu tuhuma zilnazomkabili fisadi wa mafisadi na harakati zake za kujisafisha.
Richmond hapelekwi mtu mahakamani maana mkakati ule unaonekana kuwa ulikuwa katika hatua za awali za utekelezaji.Hebu niambie basi kwa nini EL alijiuzulu?
Ili amfurahishe nani?
au ilikuwa kujifurahisha roho yake?
Ukiwa mtendaji mkuu wa serikali kampuni hewa inashindikana kuiona kama sio mkakati wa makusudi wa kuhujumu Taifa na kujipatia mabilioni?
Mbwana Kigogo-the dead mass-kumbuka mvua ya brief case .Wazo la mvua hii lilikufa na kujiuzulu kwa Lowassa.Unalielezaje hili mkuu.
EL hakuanzia mabomu akiwa Waziri Mkuu, hata Baba wa Taifa alishtukia.
It is on record kuwa kijana mdogo huyu amepata wapi utajiri wa kutisha.
Kumbuka vizuri harakati za EL akiwa Waziri katika Ofisi ya Rais,akishughulikia Maafa na Misaada na ndo utapata kufunguka akili.
Suala la uporaji wa kiwanja cha Mbezi ndo unaniacha hoi.
Unasema kwa vile Mkapa na Sumaye wamepora viwanja basi it is fair game kwa EL.
Very poor thinking indeed.Mtu akibaka basi na wewe waweza vilevile kubaka.
Hii ni Ruksa ya ajabu sana.
EL went further, kapora kiwanja cha Kanisa.Laana anayoipta wewe unaijua, hapo la kusema kwake sina ila kumwaombea.Mtu mwenye uwezo wa kuiba cha Mungu hana moral sense.Kuliibia Kanisa mtu haoni ubaya, kuiibia serikali ndio uchochoro kabisa.
Kuhusu jengo la UVCCM kuwa hili ni la CCM na halikuhusu, nitakuambia kuwa Mwizi ni Mwizi tu aibe cha CCM au aibe cha serikali.
Inasikitisha kuwa pamoja na uwezo wako finyu wa kichambua mambo, unaendeleza ushabiki usio na tija.
Kuhusu suala la umasikini wangu hilo lisikupe shida , tupo masikini wengi tu hapa Tanzania .
Utajiri wetu ni uwezo mzuri wa kufikiri na kuchambua mambo.
Mimi simchukii EL kama mtu, ila utendaji wake unajieleza.Ni kama wale utingo au wapiga debe wanao fanya kazi kubwa sana uingie kwenye basi, lakini basi haliondoki mpaka wapewe chochote!
Kigogo-body mass , kwaheri mkuu.