In Edward Lowassa, I trust...

In Edward Lowassa, I trust...

Zakumi,

Pepo la uwajibikaji na kuchapa kazi limenipanda leo.

Nilikuwa nyumbani kwa wiki tatu, nikatalii nchi kwa kiasi fulani ili nijionee kile nilichokuwa nabezwa kila siku eti kubeba kwangu maboksi najua nini zaidi ya kutumia funguobao(keyboard).

What I saw in Tanzania ni Chaos, Disorder and Disorganization!

Hakuna efficiency, hakuna mwenye ku-demand accountability au kumhold mtu responsible, kila mtu anajifanyia anachotaka.

It is not about BOT statistics au zile za CIA factbook, bali ni reality on ground.

Watu wengi wana afya nzuri na uwezo wa kufanya kazi. Nilipoandika kuhusu Idlelism, watu walinijia juu, sasa kama ile ilikuwa ni kitu nilichokiona Dar, sasa nilipokwenda vijijini ndio zaidi. Wewe mtu akiamka asubuhi anaoga na saa moja na nusu anapuyanga kwenda kuunga Azimio la Kimpumu!

What we lack is decisive and strong leadership and Lowassa stands tall above all!

He can do it, I trust that he can deliver! It may not be the way we want it, and its impact will never be short term but long term!

Mkuu:

Get your acts together maana unachanganya vitu vingi hapa. Je wakati Lowassa alipokuwa waziri mkuu watu walikuwa wanafanya kazi au walikuwa wanaenda kupiga chimpumu???

Je wakati Sumaye alipokuwa waziri mkuu watu walikuwa wanafanya kazi au walikuwa wanaenda kupiga chimpumu???

Matokeo uliyoyaona yana sababu nyingi na Lowassa sio mtu wa kutatua hayo. Kwani kufokafoka au kupanda mori hakubadilishi order ya maendeleo ya kiuchumi duniani.

Watu watafanya kazi, watu watakuwa wanafanya mambo kwa utaratibu iwapo wataona INCENTIVES ya kufanya hivyo.

Lowassa likely anafanya biashara ambazo alizilipiwi kodi, biashara ambazo ni corrupt. Hivyo mwenyewe atakuwa ni chanzo cha hayo mambo. Hivyo hakuna atakayemsikiliza. Na watakaomsikiliza watafanya hivyo kwa woga wa kupoteza kazi.

N.B: Sababu ya watanzania kutokuwa wazalishaji, inawezekana ni kukumbatia sera za Macro-economy.
 
Let us make use of the best we have - The lesser evil!
 
Sasa kwa kipmo hicho na wala si mambo ya Uhujumu au Ufisadi, utagundua kuwa Tatizo la Tanzania ni mfumo mbovu wa uongozi na jamii ambao unahitaji mtu fyatu na mkali ili tunyooke.

Give Lowassa 10 years and trust me we will see a big difference na ndipo sasa tuanze kutafuta watu softisofti kama Membe au sijui ni majina gani!

Let Lowassa take the reigns and you will se the change that we can all believe in!

Kweli Lowassa ni mkali, lakini ukali wake ni wa kutetea ufisadi na maslahi yake binafsi. Lowassa was a PM, na alikuwa amem-overshadow hata Rais, hakuna kitu ambacho Lowassa alitaka then JK akasema NO. Kama angekuwa kiongozi mzuri na mkali angeonyesha kipindi akiwa PM.

Mama Kilango alituambia kwamba several times alionywa asije akagusa baadhi ya hoja kuzipeleka Bungeni kwa kuwa zinagusa wakubwa. Uliona siku anatoa hotuba ya kufunga kikao cha Bunge kilichomfungia Zitto kuhudhuria vikao kwa kuwasilisha hoja binafsi ya Mkataba wa Buzwagi? Kwa maneno yake alisema wametoa onyo kwa wabunge watakaokuja na hoja kama ya Zitto. Je, tunamhitaji kiongozi kama huyo? Kiongozi anaye zima hoja kwa kutumia ubabe na vitisho. Labda kama Mchungaji unataka kusema hoja ya Zitto haikuwa na maslahi kwa wananchi.

Aonyeshe ukali kwa maslahi ya Taifa na wananchi na sio aonyeshe ukali kwa kulinda maslahi yake ama pale ambapo hajapewa mgao ama hajahusishwa kwenye deals za kifisadi.

Deals zote ambazo Lowassa alihusika kwa njia ama nyingine yuko mstari wa mbele kuzitetea, na kama kwenye deal hakupewa mgao ama hakuhusishwa, yuko mstari wa mbele kuwa mkali kwa kisingizio cha kulinda maslahi ya Taifa.

Sioni kama Lowassa ana ukali tunaouhitaji, ukali wake ni wa kuficha madhambi yake na kutisha watu. Angekuwa na ukali wa Sokoine, ningekubaliana na wewe lakini siyo huu ukali alio nao na ujasiri wa kifisadi.
 
Edward ni mwizi na muongo who belongs to places like keko/ukonga/segerea, pia si fisadi tu bali ni fisadi mnafiki...alijidai anachapa kazi ili msimshtukie

mimi namsubiri Asha Rose MIgiro
 
Kweli Lowassa ni mkali, lakini ukali wake ni wa kutetea ufisadi na maslahi yake binafsi. Lowassa was a PM, na alikuwa amem-overshadow hata Rais, hakuna kitu ambacho Lowassa alitaka then JK akasema NO. Kama angekuwa kiongozi mzuri na mkali angeonyesha kipindi akiwa PM.

Mama Kilango alituambia kwamba several times alionywa asije akagusa baadhi ya hoja kuzipeleka Bungeni kwa kuwa zinagusa wakubwa. Uliona siku anatoa hotuba ya kufunga kikao cha Bunge kilichomfungia Zitto kuhudhuria vikao kwa kuwasilisha hoja binafsi ya Mkataba wa Buzwagi? Kwa maneno yake alisema wametoa onyo kwa wabunge watakaokuja na hoja kama ya Zitto. Je, tunamhitaji kiongozi kama huyo? Kiongozi anaye zima hoja kwa kutumia ubabe na vitisho. Labda kama Mchungaji unataka kusema hoja ya Zitto haikuwa na maslahi kwa wananchi.

Aonyeshe ukali kwa maslahi ya Taifa na wananchi na sio aonyeshe ukali kwa kulinda maslahi yake ama pale ambapo hajapewa mgao ama hajahusishwa kwenye deals za kifisadi.

Deals zote ambazo Lowassa alihusika kwa njia ama nyingine yuko mstari wa mbele kuzitetea, na kama kwenye deal hakupewa mgao ama hakuhusishwa, yuko mstari wa mbele kuwa mkali kwa kisingizio cha kulinda maslahi ya Taifa.

Sioni kama Lowassa ana ukali tunaouhitaji, ukali wake ni wa kuficha madhambi yake na kutisha watu. Angekuwa na ukali wa Sokoine, ningekubaliana na wewe lakini siyo huu ukali alio nao na ujasiri wa kifisadi.

Strong points mkuu,bottom line ni nia halisi ya utendaji wake na matokeo ya utendaji huo...Matokeo ya utendaji huwa yanareveal nia halisi ya mtendaji. Uchapakazi wa wananchi haujabadilika kama alivyoainisha Zakumi kuhusiana na chimpumu before Lowassa kuwa waziri mkuu na hata baada ya kuwa waziri mkuu...Based on mjadala unavyokwenda,inaonyesha kuwa ukali wake kwa subordinates ni katika jitihada za kufanikisha malengo binafsi. Points hizo hapo juu ni nzito so lets see wenye mawazo ya tofauti watakavyo jibu hoja hizo.
 
kwanini watu huwa hawapendi kujibu hoja aliyotoa mtu?
sasa mtu katoa maoni yake ya kwanini anaona lowasa anafaa,kataja na sifa za kuisimiamia hoja yake,badala kujibu hoja mtu unaishia tu kusema kweli bongolala,
ndio maana mimi nimesema watu wanaompinga lowasa[waliochangia mpaka sasa]wanaonesha hawana hoja,ila tu ni chuki waliyonayo kwa mtu,bia sababu wa la hoja ya msingi,watu wameamua tu kupinga,hawaoneshi mbadala,zaidi wanabaki tu kusema watu wanaomtetea lowasa ni mafisadi/wametumwa na mafisadi,as if lowasa ndiye baba wa mafisadi au ndiye fisadi pekee,na wapinzani wake kisiasa ni wasafi kama sufi,
mnyonge mnyongeni,haki yake mpeni.

Angalia vizuri. BONGOLALA ni jina lake!
 
Yaani katika watu milioni 40 umekosa wengine na kuamua ku recycle from the archives? Rev. pleeeease!!!

Julius una busara kama za wa jina lako...

alafu invisible mbona mmeanza kugawa mali zangu wakati bado nipo hai na sina matatizo ya shingo?

thanks zangu mmezitoa zote siyo?
 
Naomba pia proof kuwa hajaiba au kuhujumu uchumi pale Tanzania. Inabidi atuonyeshe utajiri wake na kwa familia yake umetokea wapi na kwa kipato gani? Atuonyeshe vyanzo vyake vyote vya mapato vilivyomfanya awe tajiri na kuweza kuwekeza hisa katika makampuni mbalimbali huku akimiliki biashara na majumba mbalimbali kutoka Dar mpaka Arusha.
mbona viongozi wengine hamuwaulizi? David Hosea mwenyewe amepata wapi pesa ya kujenga Lodge karatu? mbona amuulizi, Mkapa mbona amuulizi? Sumaye mbona amuulizi.
huyu jamaa ni mchapa kazi asiye muangalia nyania usoni, we need him period. All the rest ni speculation zenu.
 
Naona mapepo yamewaingilia watu hapa. Lowasa si alikuwa waziri mkuu. Na katika kipindi cha miaka miwili alichofanya ni kitu gani zaidi ambacho sasa hivi watanzania wanaki-miss???
Uongozi bora na mwelekeo wa maendeleo.
 
Tunajua ulikuwa likizo bongo hivi karibuni. I hope haya uliyoyaandika hayatokani na kukatiwa vituz au kuhaidiwa ndururu za ufisadi ili uachane na mabox!

...Ama kweli........... %%$#@%
 
Mkuu Kishoka nakuvulia hekima kwa kofia zako ops nakuvulia kofia kwa hekika zako.

Jamaa ingawa alikuwa ni bazazi ila alijitahidi kujituma ktk utendaji (hata wa hovyo hovyo) ili aonekane anafanya kitu.

Mie naomba tumjadili Baba HOSEA ambaye hayupo ktk likizo ya kustaafu. Sina wasifu wake ila naamini kuna mdau atatumwagia data zake hasa zilizo positive ili tumpunguzie hasira na laana zetu tulizompania....
 
Mie naomba tumjadili Baba HOSEA ambaye hayupo ktk likizo ya kustaafu. Sina wasifu wake ila naamini kuna mdau atatumwagia data zake hasa zilizo positive ili tumpunguzie hasira na laana zetu tulizompania....

Mjadala wa Hosseah hauko mbali, maana serikali naona inajikanyaga na imeshindwa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kwenye Kamati ya Nishati na Madini. Mpaka sasa JK hajapata jibu la namna ya kum-handle Hosseah kwa kuwa wenzake karibu wote wameondoka kwa kisingizio cha kustaafu.

Ninashangaa wamejitahidi kuwaondoa akina Mwanyika na Mwakapugi, lakini kelele za wabunge wengi zilikuwa kwa Hosseah sasa sijui kama JK ana pipi za kuwagawia wabunge wa CCM ili wakae kimya na wapokee ripoti ya serikali na kuiunga mkono bila kuhoji.
 
Sipo will lead this country to reach where majority of Tanzanians always expect to be.
 
Je ni mchapa kazi au mbangaizaji?

Kama ni tamaa za mali, au ufisadi, ni Mtanzania gani ambey si mwenye tamaa ya mali au fisadi?
hapo kwenye blue hayo maneno hayawezi kwenda pamoja kabisa hasa neno MBANGAIZAJI unapozungumzia na level ya maisha ya Mhe. Lowassa haliendi na yeye kabisa
Hapo pa red hat mimi naona kama vile Watanzania wengi,sio wote nasisitiza wameanza kuwa na roho ya kifisadi, jaribu kuwafanyia research wanafunzi wanaomaliza vyuo vikuu na mawazo yao kwenye kazi wanazozitzfuta au wanazozifanya then mtanijibu na sio hao wanafunzi tu bali na wengineo. Ni mawazo ya kifisadi tu
 
rev.nakuunga mkono,
na ukitaka kujua bongo hakuna kichwa kama lowasa linapokuja suala la utendaji,angalia majibu kwenye posts zote hizi watu hawatoi mbadala wa lowasa,yaani hawamtaki tu kwasababu hawamtaki,ila hawana mbadala,kama wangekuwa nambadala wangeitikia mwito wako wa kusema mtu aseme anaemwona anafaa,
lowasa ni kifaa angalau kwa nchi yetu hii ilipofikia,tunahitaji mtu atakaetoa amri na watendaji wake wakajua anamaanisha anachosema,nani kama lowasa kwa sifa kama hiyo kwa sasa,watu hapa wamebaki kujadili sijui kaiba,nani hajaiba?hata tufanye nini hatuwezi kupata rais malaika,lazima atatoka miongoni mwa sisi binadamu tu,ndivyo Mungu alivyoamua,alitupa nchi tuzitawale wenyewe,
wengine hapa wanaojifanya kuujua uchafu wa lowasa ndio walewale walikuwa mstari wa mbele kutuamninisha jk alikuwa ndio chaguo la Mungu[labda kwakuwa sijui ni mungu yupi walimaanisha]
Kuna mchangiaji moja anaitwa Ndahani, amesema waofaa wengi wao wamefunikwa na huu mfumo wa mal-administration, lakini wapo, sasa ukiongelea kwa misingi ya kutaja tu watu, kuna mtu atakuja na Magufuli, mwingine Mwandosya, lakini tunachelea kufanya hivyo tukiangalia suala la uadilifu, wapo watu waadilifu au wenye nia ya kuwa viongozi na wawe waadilifu, tusubiri hiyo 2010 watajitokeza , na tutawapima. suala la uongozi kuongezea si ukali tu, hata kuulizia, kikwete hahitaji kuwa mkali, bali kuwa mfuatiliaji, sasa hii weakness ni ya kwake mwenye, na ile hali ya kuweka marafiki katika uongozi, na kuwapa tenda watu walio mfadhili.
 
Back
Top Bottom