Mkandara,
Ni heri wewe umenisaida kumjibu FMES, maana inaelekea yeye U-Political strategist wake umeanza kuchokachoka na wala haoni na kuelewa ninachozungumza ambacho ni kwa faida yake yeye FMES na wale Wapiganaji wake!
Siasa ni mchezo mchafu, kila mtu anajua. Muulize Malecela, Salim, Msuya hata Lowassa mwenyewe na Kikwete, watakuambia siasa ni mchezo mchafu.
Leo hii kila mtu kakata tamaa ya kuongozwa na Kikwete, lakini hakuna mwenye kuamka na kusema huyu bwana hafai tena! Lakini tunampigia debe na kusema apewe miaka mingine mitano, ili afanye nini?
Kama katika miaka hii mitano ya kwanza kashindwa kuonyesha kuwa ana uwezo wa kuwa Rais, je hiyo mitano iliyobakia atatuthibitishia nini kuwa yeye ana uwezo wa kuongoza nchi?
Hao wanaosema jamani mwacheni Kikwete aendelee kutawala na tatizo si Kikwete bali ni Mafisadi, ni sawa na punguani. Leo tunadiriki kusema eti Mafisadi wana nguvu kuliko dola? Kama ni hivyo basi dola ina maana gani kuendelea kuwepo?
Ikiwa JK na unyenyekevu wake na uadilifu wake anashindwa kuwa na sauti ya kiutawala, yenye nguvu za kirais, si heri basi tumpe huyu Lowassa ambaye anatuhujumu, lakini ana nguvu za kiutendaji na akinena anasikilizwa?
Hatuwezi kuendelea kulaumu Mafisadi kwa kila kitu kinachotokea Tanzania ikiwa Serikali iliyoko madarakani inafanya kazi kama imetekwa nyara! Basi wapeni hao mafisadi hatamu waongoze nchi maana kama wameshikilia nchi nzima kiasi cha Mkuu wa Polisi kudai Polisi haina nguvu kukabiliana na Mafisadi, then pave the way for Mafisadi to rule and govern tujue moja.
Mafisadi hawana tofauti na Mabeberu, lao moja, lakini leo tunakaribisha Ubeberu kwa kupitia mfumo wa kibepari ambao unatuacha tunanyanyasika kwa jina la Uwekezaji.
Then tuwaachie Mabeberu wa ndani watuongoze na wajenge majumba na miji ndani ya nchi yetu na si kupeleka pesa na hazina Toronto exchance kama Barrick wanavyofanya.
Ikiwa Serikali ya CCM inashindwa kutoa hamasa za kuzalisha mali na kuimarisha shughuli za maendeleo, kisa mikono ya mafisadi, ikiwa Serikali ya CCM inashindwa kuleta utiifu na unyoofu wa sheria na kuanuni kisa Mafisadi wana nguvu sana, ikiwa Serikaili ya CCM inakataa hata kuangalia upande wa pili na kubadili mfumo wa katiba ili kuwepo na nguvu mpya ya Uwakilishi na Upinzani ndani ya mfumo wa kisiasa kisa eti Mafisadi hawapendi hilo na si maslahi ya Chama, then kama Chama cha Mapinduzi kimeshikiliwa na Mafisadi, then kila inachokifanya si kwa ajili ya maslahi ya Watanzania au wanaCCM (Chama) bali ni kwa maslahi ya Mafisadi wanaokihodhi chama na kukidhibiti.
Hivyo ama kulikuwa na upeo finyu sana kunielewa au ni hasira za kitoto kukimbilia kudai Mchungaji karukwa akili au kamegewa.
Its all about politics and if they dare to play the dirty game, why should JF and Mchungaji also play dirty game?
But I still stand on my argument, give the job to Lowassa and you will see the turn around, regardless of his filthyness.
As far as I am concerned, there is no one within CCM who is not tainted or will never bow down to preasure from Ufisadi and Mafisadi! They are all the same and to save the party's image they will never dare to reform the party or get rid of Mafisadi led by Lowassa, Rostam, Chenge and others!