In Edward Lowassa, I trust...

In Edward Lowassa, I trust...

Hapa tunazungumzia nadharia tu au mgombea halisia 2010? Kama ni halisia basi ni JK na hana mpinzani. Kama ni nadharia tu basi tungoje 2011 baada tu ya JK kuingia 2nd term. Hapo na mimi nitakuja na jina langu, most likely from the opposition. Nadhani mnajua ni nani...Sitaki kumtaja sasa wasije waka Mkolimba mapema.

Watamkolimba kama wanajuwa tk ni nani.
 
TK,

How do we build opposition? By exploring and exploiting the current environment.

!

- Jamani sometimes hizi theory ni incredible, yaani ku-build up political opposition Tanzania ni lazima kumtumia kiongozi ambaye rather than facing Wananchi bungeni on his charges za wizi yeye akaamua kukimbia mwenyewe bila kufukuzwa, wala kukubali responsibility ya wizi wake, sasa leo eti the right political thinking ni kumtumia kiongozi huyo huyo mwizi as a tool of exploring and exploiting the current political environment as the opposing figure kwa a legitimate sitting government, and no other way arround kwamba afikishwe kwenye mkondo wa sheria kujibu mashitaka yake as away of cleaning our political system na uozo?

- I mean this kind of thinking inakatisha tamaa sana, ni wa-Tanzania wangapi wanaoweza ku-figure out kwamba the intention ya hii thread ni just an-exploitation of the current political environment na sio exactly meaning what it says? Wakuu huu uwanja JF ni mkubwa sana think before you write anything hapa, we are JF the best in the political analysis business ya our nation na hasa on what direction tunahitaji kwenda kiuongozi, sasa tunahitaji kuwa makini sana na ushauri wetu kwa taifa.

- Sasa kushauri kwamba Lowassa ni the best ever yaani kama Mwalimu, sijui kama ni the right thinking, hasa kwa vijana wetu, na kudai eti ushahidi wa ufisadi wake uko wapi ni an insult kwetu wananchi wa Tanzania hasa the JFs, ambao tumewahi kulala macho kusaidia ripoti ya tume ya Mwakyembe, on Richimonduli ambayo ndiyo iliyoishia kumfanya Lowassa akimbie uongozi bila kufukuzwa.

Respect.

Field Marshall Es!
 
- Jamani sometimes hizi theory ni incredible, yaani ku-build up political opposition Tanzania ni lazima kumtumia kiongozi ambaye rather than facing Wananchi bungeni on his charges za wizi yeye akaamua kukimbia mwenyewe bila kufukuzwa, wala kukubali responsibility ya wizi wake, sasa leo eti the right political thinking ni kumtumia kiongozi huyo huyo mwizi as a tool of exploring and exploiting the current political environment as the opposing figure kwa a legitimate sitting government, and no other way arround kwamba afikishwe kwenye mkondo wa sheria kujibu mashitaka yake as away of cleaning our political system na uozo?

- I mean this kind of thinking inakatisha tamaa sana, ni wa-Tanzania wangapi wanaoweza ku-figure out kwamba the intention ya hii thread ni just an-exploitation of the current political environment na sio exactly meaning what it says? Wakuu huu uwanja JF ni mkubwa sana think before you write anything hapa, we are JF the best in the political analysis business ya our nation na hasa on what direction tunahitaji kwenda kiuongozi, sasa tunahitaji kuwa makini sana na ushauri wetu kwa taifa.

- Sasa kushauri kwamba Lowassa ni the best ever yaani kama Mwalimu, sijui kama ni the right thinking, hasa kwa vijana wetu, na kudai eti ushahidi wa ufisadi wake uko wapi ni an insult kwetu wananchi wa Tanzania hasa the JFs, ambao tumewahi kulala macho kusaidia ripoti ya tume ya Mwakyembe, on Richimonduli ambayo ndiyo iliyoishia kumfanya Lowassa akimbie uongozi bila kufukuzwa.

Respect.

Field Marshall Es!

Sawa sawa kabisa Mkuu FMES! tungeongeza vilevile kuwa ni vyema sasa EDDO akapelekwa kwa Pilato juu ya Richmond, ili tujue aliijuaje, aliijua muda gani na alichukua hatua ipi kabla ya kuumbuliwa na Tume ya Bunge.
 
Mkuu FMES,
karibu sana mkuu wangu sijakusikia muda..
Mkuu mbona umekuja na wazimu mpya! Huyo Lowassa si wenu mkuu wangu iweje leo iwe mkosa ni yeye wakati makosa yote alofanya ni ktk mikakati na sera za chama..Hana makosa kwa sababu alofanya ni within sera za chama chenu na ndio maana hata rais na wabunge wengine wanamtetea kutokuwa na makosa.

Ikiwa wewe unaona wazi kuwa Lowassa ni mkosa, basi hilo ni wewe, sii mawazo ya wanaCCM wote kwani siku zote mkosa hufikishwa mahakamani na kuhukumiwa. Haikufanyika hivyo yupo huru ni mtu asokuwa na makosa.

je nani wa kumlaumu ikiwa hata huyo kiongozi wa Takukuru anachaguliwa na kiongozi wa chama chako bila uchaguzi huo kupitishwa na Bunge... Hivi kweli unafikiria Lowassa alijiuzuru tu hivhivi yaani kjaamka asubuhi akafikiria kujiuzuru pasipo ushauri wa viongozi wenzake.. Na mbona alisema anafanya hivyo kukinusuru CHAMA! haya maneno yalikuwa na maana gani?

Mkuu wangu taifa stars wameshindwa kuingia world cup finals, tumetolewa round ya pili ni aibu kwa nchi yetu ni aibu kwetu sote na tukubali matokeo. Tanzania inakuwa ranked kutokana na hao watu 11 tu waliocheza sasa kama wewe unabisha kuhusiana na ranking hizo ati kwa sababu ni watu 11 tu walicheza.....kazi kwako!
 
Kaka unaweza kuwa huko sahihi na mawazo ya kweli japo umeyaweka kwenye jamvi la watoto wa Mwakyembe na Mengi...........leo nawashangaa watu wanaoshindwa kuwaza na wala kujiuliza kwa nini mpaka sasa mitambo ya umeme haijaletwa nchini na bado watu hawajui ni kwa nini tuko gizani mpaka sasa.
Rais ameamua tuwashe mitambo ya IPTL kwa gharama ya shilingi billioni 23 kwa mwezi kwa kuwa tuna roho mbaya na chuki dhidi ya mitambio ya dowans na ukijumlisha hofu ya kikwete kwa mwkymb,tunaacha kusave hela zetu kwa kuwasha mitambo ya dowans yenye sifa zifuatazo to compare with iptl
1.tungelipa bilioni 3 kwa mwezi kwa dowans na tutalipa bil 23 kwa mwezi kwa iptl.
2.tunatumia fedha za kigeni kununua mafuta lita elfu 5 kwa siku kwa iptl na tunatumia gas ya asili kwa mitambo ya dowans
3.dowans ni rafiki wa mazingira wakati iptl inachafua mazingira.
4.mitambo yote miwili ina kashfa ya ufisadi na ina kesi mahakamani na inazalisha megawati 100
 
Yes, I have said it. Ili tuendelee, tunamhitaji Edward Ngoyayi Lowassa!

Ni mchapakazi, mfuatiliaji na mkali asiye na masikhara na walioko chini yake si kuwa wanamheshimu tuu, wanaogopa kushukiwa na zali kutokana na ukali na ufuatiliaji wake.

Kila kazi aliyopewa, kaifanya kwa bidii na kwa ufanisi. Kuna tofauti kubwa sana za kiutendaji kati yake na wenzake walioshika nafasi za uongozi ambazo alizishikilia.

Naamini kwa dhati kuwa ili Tanzania iweze kuamka na kurudi katika mstari ulionyooka wa kujituma, kufanya kazi kwa bidii na maarifa bora na la zaidi kwa nidhamu ili tuendelee vyema na safari yetu ya kujijenga kiuchumi na kijamii ili kuleta maendeleo ya kweli, basi hakuna mwingine zaidi ya Lowassa!

Kama unaye wa kwako, tupe jina na umnadi, wangu miye ni Lowassa!


Niko kwenye basi lako, I miss the guy big time, In fact I realized that the moto "Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya" was actually belong to him.
 
Fisadi mtoto,
Waswahili wanasema Ukikosa ziwa la mama hata la Punda linafaa.. sasa wewe unapokuja pima sababu kwa nini isiwe la nguruwe au mbwa ambaye anapatikana na rahisi kumfuga kuliko Punda unaleta habari nyingine..
Dowans ni Noo! Noo! hili sakata lake linahusiana na Kiongozi wa juu huyu Lowassa anayesifika ambaye tunataka afikishwe yeye mahakamani achana na habari ya Dowans kuwa mahakamani pia.. Hawa wameweka hivyo tu buy time tu na sababu..
IPTL nayo ina matatizo yake lakini ndo tambara la kiraka kuziba pachu la takoni..Binafsi naelewa kwa nini IPTL inasisitizwa kuingia mkataba hatuna sababu nyingine fedha zimeshaliwa kwa mtindo wa EPA..Ni vurugu tupu hatuna la maana zaidi ya kukubali matokeo..
Kwa maneno ya Jk mwenyewe anasema, hii ni mitihani ya Mungu yaani mnajaribishwa imani zenu!
 
Kaka unaweza kuwa huko sahihi na mawazo ya kweli japo umeyaweka kwenye jamvi la watoto wa Mwakyembe na Mengi...........leo nawashangaa watu wanaoshindwa kuwaza na wala kujiuliza kwa nini mpaka sasa mitambo ya umeme haijaletwa nchini na bado watu hawajui ni kwa nini tuko gizani mpaka sasa.
Rais ameamua tuwashe mitambo ya IPTL kwa gharama ya shilingi billioni 23 kwa mwezi kwa kuwa tuna roho mbaya na chuki dhidi ya mitambio ya dowans na ukijumlisha hofu ya kikwete kwa mwkymb,tunaacha kusave hela zetu kwa kuwasha mitambo ya dowans yenye sifa zifuatazo to compare with iptl
1.tungelipa bilioni 3 kwa mwezi kwa dowans na tutalipa bil 23 kwa mwezi kwa iptl.
2.tunatumia fedha za kigeni kununua mafuta lita elfu 5 kwa siku kwa iptl na tunatumia gas ya asili kwa mitambo ya dowans
3.dowans ni rafiki wa mazingira wakati iptl inachafua mazingira.
4.mitambo yote miwili ina kashfa ya ufisadi na ina kesi mahakamani na inazalisha megawati 100

Fisadi mtoto embu pata kumbukumbu kidogo juu ya richmond and dowans na effect zake..[ame]http://www.youtube.com/watch?v=ZoVSS9qh4kU[/ame]
 
Fisadi mtoto,
Waswahili wanasema Ukikosa ziwa la mama hata la Punda linafaa.. sasa wewe unapokuja pima sababu kwa nini isiwe la nguruwe au mbwa ambaye anapatikana na rahisi kumfuga kuliko Punda unaleta habari nyingine..
Dowans ni Noo! Noo! hili sakata lake linahusiana na Kiongozi wa juu huyu Lowassa anayesifika ambaye tunataka afikishwe yeye mahakamani achana na habari ya Dowans kuwa mahakamani pia.. Hawa wameweka hivyo tu buy time tu na sababu..
IPTL nayo ina matatizo yake lakini ndo tambara la kiraka kuziba pachu la takoni..Binafsi naelewa kwa nini IPTL inasisitizwa kuingia mkataba hatuna sababu nyingine fedha zimeshaliwa kwa mtindo wa EPA..Ni vurugu tupu hatuna la maana zaidi ya kukubali matokeo..
Kwa maneno ya Jk mwenyewe anasema, hii ni mitihani ya Mungu yaani mnajaribishwa imani zenu!

Mkandara mkuu, there is gross mismanagement at government level katika swala hili la umeme.
Nasikitika sana ikiwa mwenyewe JK anasema huu ni mtihani wa Mungu.
Watu wanatanguliza interest zao, matumbo yao,tamaa zao na ufisadi juu kuliko maslahi ya Taifa .
Halafu tunategemea mambo yaende sawa.
Hatutaki kuwachukulia hatua za wazi ili tabia hii ikome, tunabaki kuomba Mungu atupishilie mbali.
Maombi kama haya Mwenyezi Mungu anayaweka pending mpaka sisi wenyewe tuyafanyie kazi.
Kuwasha IPTL is a step in the right direction kuziba pengo la umeme nchini.
Ukiondoa ulafi ,mikataba mibovu na ufisadi sasa hivi kuna enough generating capacity nchini, hatutaki tu kumfunga paka kengele.
 
Yes, I have said it. Ili tuendelee, tunamhitaji Edward Ngoyayi Lowassa!

Ni mchapakazi, mfuatiliaji na mkali asiye na masikhara na walioko chini yake si kuwa wanamheshimu tuu, wanaogopa kushukiwa na zali kutokana na ukali na ufuatiliaji wake.

Kila kazi aliyopewa, kaifanya kwa bidii na kwa ufanisi. Kuna tofauti kubwa sana za kiutendaji kati yake na wenzake walioshika nafasi za uongozi ambazo alizishikilia.

Naamini kwa dhati kuwa ili Tanzania iweze kuamka na kurudi katika mstari ulionyooka wa kujituma, kufanya kazi kwa bidii na maarifa bora na la zaidi kwa nidhamu ili tuendelee vyema na safari yetu ya kujijenga kiuchumi na kijamii ili kuleta maendeleo ya kweli, basi hakuna mwingine zaidi ya Lowassa!

Kama unaye wa kwako, tupe jina na umnadi, wangu miye ni Lowassa!

Mchungaji Kishoka,

Nimesoma hii mistari uliyotiririsha hapa na kuirudia tena na tena. Halafu nikatafakari mambo unayoyaandika hapa siku zote, na hat uliyopata kuyaandika kuhusu huyuhuyu mmasai/mmeru nikakusikitikia sana na zaidi nikaisikitikia nchi yangu Tanganyika.

Naamini sasa kwamba ulipojiita kishoka hukufanya hivyo kwa bahati mbaya, yaani nimewakumbuka vishoka wanaotuunganishia umeme huku mitaani, nikasema kwakuwa jina umejipa mwenyewe sasa umeamua kujidhihirisha sura yako halisi.

Pamoja na yote unayosema, mafisadi mtawatumikia nyie msiokuwa na uzalendo halisi na nchi yenu. Hata ukimpaka mafuta na vikorombwezo vyoote madukani, fisadi lowasa hasafishiki!!!!
 
Kuwa mchapa kazi ni pamoja na kuwa na sifa ya maamuzi ya busara. Hilo ni muhimu pengine kuliko tu kuishia kuchapa kazi. Maana unaweza kuwa unachapaka kati na kupoteza muda katika kazi isiyokuwa na tija katika kubadilisha maisha ya watanzania toka haya mabaya waliyo nayo kwenda aghalau ya kipato cha kati. Lowasa anakosa sifa hiyo muhimu sana katika ngazi yeyote ile ya maisha ya kijamii. Familia lazima iongozwe na kiongozi mwenye maamuzi ya busara siku zote. Baada ya kuwa na maamuzi ya busara basi uchapakazi hufuatia katika kufuatilia hatua kwa hatua utekelezaji wa maamuzi ya busara.

Mfano mzuri na maamuzi yaliyotumika kutoa zabuni ya miradi mbalimbali ya kitaifa hususan ule wa kuzalisha umeme kwa kampuni ya Richmond. Tumepoteza fedha ngapi katika hayo yote? Tumepoteza muda na fedha kiasi gani kwa kuwaruhusu Dowans kurithi Mkataba wa Richmond? Kuwa mchapakazi sharti kuambatane na sifa nyingine ya kuwa na uwezo wa kutoa maamuzi yenye busara ndani yake. Kikipungua hicho basi huyo mtu abaki kuwa mtekelezaji tu na asubiri watu watoe maamuzi ya yeye kutekeleza. Kwa nafasi ya Uwaziri Mkuu bado ni kubwa sana kwa Lowasa. Asimamie utekelezaji wa maamuzi ya Serikali jimboni kwake huko. Hakuna mwanadamu aliye na kila sifa iliyo bora, bali kupitia madhaifu yetu na uwezo wetu kila mtu awekwe sehemu ambapo udhaifu wake hautakuwa pingamizi kufanikisha shughuli iliyolengwa. Ndiyo maana hata kwenye usaili wa ajira watu hulinganisha ili kumpata aliye bora kuliko wote. Hivyo, narudia tena kusema Lowasa kuanzia Uwaziri na kuendea ni nafasi ya juu mno kuliko uwezo wake. Vinginevyo gharama za kutekeleza masuala lengwa huwa za juu mno kuliko kawaida endapo yeye atahusika katika maamuzi.
 
Mkandara,

Ni heri wewe umenisaida kumjibu FMES, maana inaelekea yeye U-Political strategist wake umeanza kuchokachoka na wala haoni na kuelewa ninachozungumza ambacho ni kwa faida yake yeye FMES na wale Wapiganaji wake!

Siasa ni mchezo mchafu, kila mtu anajua. Muulize Malecela, Salim, Msuya hata Lowassa mwenyewe na Kikwete, watakuambia siasa ni mchezo mchafu.

Leo hii kila mtu kakata tamaa ya kuongozwa na Kikwete, lakini hakuna mwenye kuamka na kusema huyu bwana hafai tena! Lakini tunampigia debe na kusema apewe miaka mingine mitano, ili afanye nini?

Kama katika miaka hii mitano ya kwanza kashindwa kuonyesha kuwa ana uwezo wa kuwa Rais, je hiyo mitano iliyobakia atatuthibitishia nini kuwa yeye ana uwezo wa kuongoza nchi?

Hao wanaosema jamani mwacheni Kikwete aendelee kutawala na tatizo si Kikwete bali ni Mafisadi, ni sawa na punguani. Leo tunadiriki kusema eti Mafisadi wana nguvu kuliko dola? Kama ni hivyo basi dola ina maana gani kuendelea kuwepo?

Ikiwa JK na unyenyekevu wake na uadilifu wake anashindwa kuwa na sauti ya kiutawala, yenye nguvu za kirais, si heri basi tumpe huyu Lowassa ambaye anatuhujumu, lakini ana nguvu za kiutendaji na akinena anasikilizwa?

Hatuwezi kuendelea kulaumu Mafisadi kwa kila kitu kinachotokea Tanzania ikiwa Serikali iliyoko madarakani inafanya kazi kama imetekwa nyara! Basi wapeni hao mafisadi hatamu waongoze nchi maana kama wameshikilia nchi nzima kiasi cha Mkuu wa Polisi kudai Polisi haina nguvu kukabiliana na Mafisadi, then pave the way for Mafisadi to rule and govern tujue moja.

Mafisadi hawana tofauti na Mabeberu, lao moja, lakini leo tunakaribisha Ubeberu kwa kupitia mfumo wa kibepari ambao unatuacha tunanyanyasika kwa jina la Uwekezaji.

Then tuwaachie Mabeberu wa ndani watuongoze na wajenge majumba na miji ndani ya nchi yetu na si kupeleka pesa na hazina Toronto exchance kama Barrick wanavyofanya.

Ikiwa Serikali ya CCM inashindwa kutoa hamasa za kuzalisha mali na kuimarisha shughuli za maendeleo, kisa mikono ya mafisadi, ikiwa Serikali ya CCM inashindwa kuleta utiifu na unyoofu wa sheria na kuanuni kisa Mafisadi wana nguvu sana, ikiwa Serikaili ya CCM inakataa hata kuangalia upande wa pili na kubadili mfumo wa katiba ili kuwepo na nguvu mpya ya Uwakilishi na Upinzani ndani ya mfumo wa kisiasa kisa eti Mafisadi hawapendi hilo na si maslahi ya Chama, then kama Chama cha Mapinduzi kimeshikiliwa na Mafisadi, then kila inachokifanya si kwa ajili ya maslahi ya Watanzania au wanaCCM (Chama) bali ni kwa maslahi ya Mafisadi wanaokihodhi chama na kukidhibiti.

Hivyo ama kulikuwa na upeo finyu sana kunielewa au ni hasira za kitoto kukimbilia kudai Mchungaji karukwa akili au kamegewa.

Its all about politics and if they dare to play the dirty game, why should JF and Mchungaji also play dirty game?

But I still stand on my argument, give the job to Lowassa and you will see the turn around, regardless of his filthyness.

As far as I am concerned, there is no one within CCM who is not tainted or will never bow down to preasure from Ufisadi and Mafisadi! They are all the same and to save the party's image they will never dare to reform the party or get rid of Mafisadi led by Lowassa, Rostam, Chenge and others!
 
Fisadi mtoto,
Waswahili wanasema Ukikosa ziwa la mama hata la Punda linafaa.. sasa wewe unapokuja pima sababu kwa nini isiwe la nguruwe au mbwa ambaye anapatikana na rahisi kumfuga kuliko Punda unaleta habari nyingine..
Dowans ni Noo! Noo! hili sakata lake linahusiana na Kiongozi wa juu huyu Lowassa anayesifika ambaye tunataka afikishwe yeye mahakamani achana na habari ya Dowans kuwa mahakamani pia.. Hawa wameweka hivyo tu buy time tu na sababu..
IPTL nayo ina matatizo yake lakini ndo tambara la kiraka kuziba pachu la takoni..Binafsi naelewa kwa nini IPTL inasisitizwa kuingia mkataba hatuna sababu nyingine fedha zimeshaliwa kwa mtindo wa EPA..Ni vurugu tupu hatuna la maana zaidi ya kukubali matokeo..
Kwa maneno ya Jk mwenyewe anasema, hii ni mitihani ya Mungu yaani mnajaribishwa imani zenu!

Mkandara,

Last week, Serikali imetoa tamko kuwa eti haitaingia mkataba na Dowans na haitanunua mitambo kutoka Dowans na hivyo ni marufuku kwa Tanesco na Dowans kufanya biashara.

Lakini, mitambo ya Dowans inaweza kununuliwan mtu yeyote yule na mtu huyo, then anaweza kuifanyai kazi kuzalisha umeme au kuiuza kwa Tanesco bila shida au kuuza umeme kwa Tanesco, ili mradi mitambo hiyo na umeme wake usiseme kuwa ni Dowans!

Sasa nikajiuliza, je ndio ktugani kimefanyika? au ni vipi tunajidanganya? James Carville alisema "it is economic stupid" mimi nasema "it is political stupid"!
 
Mchungaji Kishoka,

Nimesoma hii mistari uliyotiririsha hapa na kuirudia tena na tena. Halafu nikatafakari mambo unayoyaandika hapa siku zote, na hat uliyopata kuyaandika kuhusu huyuhuyu mmasai/mmeru nikakusikitikia sana na zaidi nikaisikitikia nchi yangu Tanganyika.

Naamini sasa kwamba ulipojiita kishoka hukufanya hivyo kwa bahati mbaya, yaani nimewakumbuka vishoka wanaotuunganishia umeme huku mitaani, nikasema kwakuwa jina umejipa mwenyewe sasa umeamua kujidhihirisha sura yako halisi.

Pamoja na yote unayosema, mafisadi mtawatumikia nyie msiokuwa na uzalendo halisi na nchi yenu. Hata ukimpaka mafuta na vikorombwezo vyoote madukani, fisadi lowasa hasafishiki!!!!

Mwita wa Maranya,

Je uliponisoma ulinielewa vizuri? Kama umeshanisoma miaka mingi ya kutosha na kuelewa weledi au siha ya Mchungaji, kimekushinda nini kunielewa na kufikia timilisho kuwa nami ni sawa na vishoka wa Tanesco au Dawasco?

Unajua nakumbuka Kitila Mkumbo aliposema kuwa kina Mwakyembe hawakufuata haki na kanuni kumsulubu Lowassa, watu tulifumbia macho ukweli wa kufuata haki na kanuni na kusema Kitila kapewa chochote na hatukusimamia haki.

Wakati Mwakyembe alipotukanana na Rostam kuhumu umeme wa nguvu za upepo, watu wakadai ah, hakuna kosa kwa Mwakyembe kuwa na kampuni ya umeme alimradi kitendo chake ambaco dhahiri ilikuwa ni kukiukwa miiko na kanuni tukakifanya ni sahihi kwa kuwa yeye ni "mkombozi".

Sasa leo "mkombozi na mpiganaji" akivunja miiko na kukiuka kanuni tunadai Ruksa, lakini tusiyempenda akifanya hilo hilo tunalia apelekwe kwa Pilato asulubbiwe, je haki iko wapi? je lini tunaweza kujenga jamii na Taifa lenye kufuata kanuni, lenye utu na lenye kusimamia haki?

Nimesema tena kwa kujikosoa kuwa hata pamoja na hasira zangu na maudhiko yangu hata chuku dhidi ya Lowassa nilizozisema kwenye Deconstructing Lowassa, bado kuna vitu ambavyo Lowassa alivvyokuwa akifanya kiutendaji kama uchapa kazi, ufuatiliaji na ile uwezo wa kuwa na nguvu za kidola na kufanya watu wachacharike bado anao na ni haiba yake.

Ndio maana nikasema, kuna haja ya kuwa na sacrifice na compromise kutoka kwetu, maana kati kundi na chama alichoko Lowassa, hakuna mwenye nguvu au uwezo wa kuongoza kiutendaji na hata hili la vita vya Ufisadi ni gumu kwao.

Lakini tabia yetu hapa JF ni kutaka tubainishiwe kila kitu, ndio maana umesikia watu wakilialia "aah Mchungaji mbona unatuchanganya, tukueleweje, sasa tufuate lipi unlosema" nami nimewajibu kwa kusema kuwa wao ni watu wazima wenye uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi bila kumtegemea Mchungaji.

Nimewaambia watmie busara zao wanapopewa Kuku na Yai wapigie kura kimoja wapo, lakini wengi humu ndani, wanadai eti wanatakak kujua ni kipi kilitangulia, Kuku au Yai! Ndio maana mko njia panda hamuelewi ninachokisema!
 
Mwita wa Maranya,

Je uliponisoma ulinielewa vizuri? Kama umeshanisoma miaka mingi ya kutosha na kuelewa weledi au siha ya Mchungaji, kimekushinda nini kunielewa na kufikia timilisho kuwa nami ni sawa na vishoka wa Tanesco au Dawasco?

Unajua nakumbuka Kitila Mkumbo aliposema kuwa kina Mwakyembe hawakufuata haki na kanuni kumsulubu Lowassa, watu tulifumbia macho ukweli wa kufuata haki na kanuni na kusema Kitila kapewa chochote na hatukusimamia haki.

Wakati Mwakyembe alipotukanana na Rostam kuhumu umeme wa nguvu za upepo, watu wakadai ah, hakuna kosa kwa Mwakyembe kuwa na kampuni ya umeme alimradi kitendo chake ambaco dhahiri ilikuwa ni kukiukwa miiko na kanuni tukakifanya ni sahihi kwa kuwa yeye ni "mkombozi".

Sasa leo "mkombozi na mpiganaji" akivunja miiko na kukiuka kanuni tunadai Ruksa, lakini tusiyempenda akifanya hilo hilo tunalia apelekwe kwa Pilato asulubbiwe, je haki iko wapi? je lini tunaweza kujenga jamii na Taifa lenye kufuata kanuni, lenye utu na lenye kusimamia haki?

Nimesema tena kwa kujikosoa kuwa hata pamoja na hasira zangu na maudhiko yangu hata chuku dhidi ya Lowassa nilizozisema kwenye Deconstructing Lowassa, bado kuna vitu ambavyo Lowassa alivvyokuwa akifanya kiutendaji kama uchapa kazi, ufuatiliaji na ile uwezo wa kuwa na nguvu za kidola na kufanya watu wachacharike bado anao na ni haiba yake.

Ndio maana nikasema, kuna haja ya kuwa na sacrifice na compromise kutoka kwetu, maana kati kundi na chama alichoko Lowassa, hakuna mwenye nguvu au uwezo wa kuongoza kiutendaji na hata hili la vita vya Ufisadi ni gumu kwao.

Lakini tabia yetu hapa JF ni kutaka tubainishiwe kila kitu, ndio maana umesikia watu wakilialia "aah Mchungaji mbona unatuchanganya, tukueleweje, sasa tufuate lipi unlosema" nami nimewajibu kwa kusema kuwa wao ni watu wazima wenye uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi bila kumtegemea Mchungaji.

Nimewaambia watmie busara zao wanapopewa Kuku na Yai wapigie kura kimoja wapo, lakini wengi humu ndani, wanadai eti wanatakak kujua ni kipi kilitangulia, Kuku au Yai! Ndio maana mko njia panda hamuelewi ninachokisema!

Mchungaji maandiko yako ninayasoma na kuyaelewa sana. Nikizungumzia hapo nilipoweka nyekundu, nataka nikuthibitishie kuwa ni BIG NO. kuna watu wenye uwezo mkubwa kuliko lowasa, tatizo ni kwamba hawajapata nafasi, hawajapewa nafasi. Hebu tuthibitishie pasipo shaka kwamba Tanzania hii imekosa kabisa mtu wa kusimamia kiamilifu maendeleo ya wananchi. Yaani bila lowasa mambo hayaendi? kwani sokoine alitokea wapi?nani alikuwa anamfahamu kabla hajawa waziri wa ulinzi na baadae waziri mkuu? wacha masihara kabisa mchungaji. Nataka nikuhakikishie wewe pamoja na wenzako mnaompigia debe lowasa kwamba, ni afadhali Nape Nnauye apewe huo uPM kuliko fisadi lowasa. Na hii nchi hata siku moja haitajuta wala kusikitika kwa lowasa kutorudi serikalini, zaidi sana itaendelea kusikitika kwa udhalimu alioufanya. Kaulizwa swali dogo tu na mtoto wa kidato cha kwanza pale mwanza kashindwa kujibu halafu unakuja hapa kumtetea hadi povu linakutoka, hapana aisee kwa hili hapana bana.
 
Mchungaji maandiko yako ninayasoma na kuyaelewa sana. Nikizungumzia hapo nilipoweka nyekundu, nataka nikuthibitishie kuwa ni BIG NO. kuna watu wenye uwezo mkubwa kuliko lowasa, tatizo ni kwamba hawajapata nafasi, hawajapewa nafasi. Hebu tuthibitishie pasipo shaka kwamba Tanzania hii imekosa kabisa mtu wa kusimamia kiamilifu maendeleo ya wananchi. Yaani bila lowasa mambo hayaendi? kwani sokoine alitokea wapi?nani alikuwa anamfahamu kabla hajawa waziri wa ulinzi na baadae waziri mkuu? wacha masihara kabisa mchungaji. Nataka nikuhakikishie wewe pamoja na wenzako mnaompigia debe lowasa kwamba, ni afadhali Nape Nnauye apewe huo uPM kuliko fisadi lowasa. Na hii nchi hata siku moja haitajuta wala kusikitika kwa lowasa kutorudi serikalini, zaidi sana itaendelea kusikitika kwa udhalimu alioufanya. Kaulizwa swali dogo tu na mtoto wa kidato cha kwanza pale mwanza kashindwa kujibu halafu unakuja hapa kumtetea hadi povu linakutoka, hapana aisee kwa hili hapana bana.

Mwita,

Tutajie japo watu 10 unaodai wako CCM ambao hawajapewa nafasi!
 
Lowasa ni kiwavi. Tena kiwavi jeshi. Kwa watoto wa wakulima mtakuwa mnakafaham haka kadudu
 
Kusema kweli hata mimi yalipoanza yale mambo ya Richmond nk, nilimwona Lowassa kama fisadi asiyefaa. Lakini baada ya miaka 2 ya kuwa nje ya system ambayo ni sawa na 2 aliyokuwa ndani ya system, nimeona wale waliobaki humo hawajafanya chochote cha kumkaribia kwa ubora wa utendaji.

Baniani mbaya kiatu chake dawa.
Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni.

Lowassa alisema sekondari kila kata. Tunaziona.
Pinda na JK wakasema Kilimo Kwanza. Tunaona na kusikia taarifa za semina, makongamano, warsha nk kwenye mahoteli ya kitalii, lakini mashambani bado ni vumbi na ukame, njaa inashamiri.

Lowassa alisema walimu walipwe mishahara yao ifikapo tarehe 25 kila mwezi. Wanalipwa.
Pinda na JK wakasema malimbikizo ya walimu yatalipwa mwezi ujao, ukaja mwingine, na mwingine,hadi leo ni miaka 2, hadithi tu.

Lowassa aliamuru njia 3 za kutatua msongamano wa magari Dar. Zikafuatwa.
Pinda akasema anapiga marufuku uvaaji wa suti kwenye shughuli za kiserikali. Hadi leo mwenyewe anavaa suti na si yale matenge aliyodai angevaa.

Lowassa aliwafuta kazi on the spot watendaji waliokuwa wanafanya uzembe kwenye kazi zao.
Pinda anaishia kulalamika tu kama mtoto mdogo kuwa ati 'mawaziri wanashindana kununua magari ya bei mbaya'

Pinda na Jk wameitisha kura ya majambazi na wauaji wa albino. A waste of time. Haijasaidia chochote katika kuwakamata, na hata wakifanya hivyo kesi zitafutwa kwa mtindo wa 'nulle prosequi', hakuna ushahidi. Aibu tupu.

Pinda akasema 'Zanzibar si nchi', na eti 'wanaoua albino nao wauawe papo hapo'. Alipobanwa kwa maswali ya wabunge, akabubujikwa na machozi kama shori aliyetishiwa kupigwa chini na buzi lake. Lowassa aliona akilia kama mtoto ataaibisha utu wake na morani wake wapiga kura. Akaona bora kutema kibarua kuliko fedheha. Hata Mtwa Mkwawa tunamsifu hadi leo kwa uamuzi kama huo.

Bora Lowassa tu, he is the lesser devil!
 
Rev.Kishoka,

..wakati Mwakyembe anatoa ripoti yake bungeni alidai kuna mambo wameamua wasiyasema ili kuisitiri serikali isiaibike.

..kwa maneno hayo tayari Mwakyembe amei-discredit ripoti ya kamati yake.

..sasa kwa huyu Lowassa kama anaona ameonewa na Mwakyembe atoke hadharani amtaje mhusika wa mkuu wa Richmond ndani ya serikali ya jamhuri.

..pia atusaidie ktk kuwafichua wote walioshiriki kuingiza pesa chafu ktk kampeni za wanamtandao, na awataje waandishi wa habari wote alikuwa amewanunua na pesa zilikuwa zikitolewa na nani.

..Lowassa akikiri makosa yake na kuwataja washirika wenzake alioshirikiana nao tangu mwaka 1993/94 kuchafua siasa za CCM na Tanzania, na kuahidi kuachana nao, basi tutakuwa tumebakia na Lowassa tunayemhitaji. binafsi nitakuwa tayari kumpigia kura.
 
Yes, I have said it. Ili tuendelee, tunamhitaji Edward Ngoyayi Lowassa!

Ni mchapakazi, mfuatiliaji na mkali asiye na masikhara na walioko chini yake si kuwa wanamheshimu tuu, wanaogopa kushukiwa na zali kutokana na ukali na ufuatiliaji wake.

Kila kazi aliyopewa, kaifanya kwa bidii na kwa ufanisi. Kuna tofauti kubwa sana za kiutendaji kati yake na wenzake walioshika nafasi za uongozi ambazo alizishikilia.

Naamini kwa dhati kuwa ili Tanzania iweze kuamka na kurudi katika mstari ulionyooka wa kujituma, kufanya kazi kwa bidii na maarifa bora na la zaidi kwa nidhamu ili tuendelee vyema na safari yetu ya kujijenga kiuchumi na kijamii ili kuleta maendeleo ya kweli, basi hakuna mwingine zaidi ya Lowassa!

Kama unaye wa kwako, tupe jina na umnadi, wangu miye ni Lowassa!

Mchungaji,

Na-respect baadhi ya mabandiko yako humu jamvini, but kwa hili la EL nasema ni BIG NO. Tutafute wengineo naamini Mwenyezi Mungu ametupa baraka ya kuwa na watu waaminifu, wachamungu, watendaji wazuri sana na wenye hekima na busara zilizotuka; wanaoweza kutongoza vizuri WaTz bila ya shaka yoyote.

Ila kuna mambo kadhaa yanayotukwaza;
1: Tunapenda sana au tumeathiriwa sana na kufuata mkumbo/umaarufu wa watu. (Ushahidi wa hilo; angalia watu woote wanaofadhili au kusaidia jamii kimichezo/sanaa/utamaduni/uchumi n.k, mwisho wao HUGOMBEA CHEO FULANI km vile Ubunge/Udiwani na hata Uraisi. Tuna wasikia kina madega, rage, asha baraka na wengineo wanavyopigana vikumbo; wanajua WAMESHAKUWA MAARUFU MASIKIONI NA MACHONI MWA WATZ, WATACHAGULIWA.

2: Propaganda/ulaghai nao ni sumu kali kwetu; tumezowea kudanganywa na kwa nafsi zetu tunajua tunadanganywa na mwisho wa siku hao wanaotudanganya ndio tunaowarudisha tena ktk uongozi au tunawapigia debe warudi tena ingawa waliharibu au bado wanaharibu.

3: Kutokujiamini kama jamii ambayo inaweza kuleta mabadiliko ya kweli; wengi wetu tunawaona na kuwasikia huku mitaani km "aahh! hata nisipowapigia/nisipompigia kura atachaguliwa tu, bora nimpe yeye huyo huyo" Maneno km haya ni ya mtu aliekata tamaa, na HAFAI KTK JAMII YETU YA SASA.

4: Kuwapenda/Kuwaamini sn watu kupita kiasi; Hili tatizo tunalo WaTz wengi na linatuathiri sn kwa kujua au bila kujua. Mwisho wa siku umpendae akiboronga unashindwa kuamini km kweli yeye aliefanya madudu na unaweza kumtetea hadi tone la mwisho la damu/mate yako. Mifano tunayo humu humu jamvini yaliyotokea kipindi ileeee.......

Mengine mtaongezea..............
 
Back
Top Bottom