- Bob please mkuu, thank you lakini no thanks mkuu hawa watu niachie hawa wanaotaka wabunge wa Upinzani wasiingie Bungeni maana kuna wabunge mafisadi wa CCM, wanaotaka wananchi wote wa Tanzania wasio mafisadi wahame nchi maana wakiishi humo ndani ya taifa na wabunge mafisadi basi wote wanakuwa mafisadi, wewe huoni kwamba ni hoja mufilisi na mtu mzito kama wewe kuingilia ni kushusha hadhi yako mkuu, hawa wana hoja za kutaka walokole wote wahame hapa duniani kwa sababu hata Mungu anasema ni dunia ya shetani,
Respect.
Field Marsahll Es!
FME,
Mimi naomba nikuulize kitu kimoja tu, ndiyo wewe unazunguka na wapambanaji pia na kuwasaidia kwenye hizo harakati lakini bado hujaweza kujibu hii Mada: Je Wapiganaji walioko CCM wanapi.......... wakiwa humohumo na bado wanaendelea .... humohumo?
Kama umemsoma Rev. Kishoka ameeleza mambo yake mengi....
na juzi juzi ndo wamejiongezea marupurupu manono kwelikweli hao hao, ukichanganya na mfuko wa jimbo n.k. ndo sisi tulioko pembeni tunauliza hivi kweli hawa wako serious kweli au ni usanii?? je hii vita wataiwezaje na wao bado wanaendelea kufaidi keki ya mlalahoi? Tusaidie manake huko karibu nao.