'Wapiganaji' walioko CCM wanapigania nini hasa?

- Bob please mkuu, thank you lakini no thanks mkuu hawa watu niachie hawa wanaotaka wabunge wa Upinzani wasiingie Bungeni maana kuna wabunge mafisadi wa CCM, wanaotaka wananchi wote wa Tanzania wasio mafisadi wahame nchi maana wakiishi humo ndani ya taifa na wabunge mafisadi basi wote wanakuwa mafisadi, wewe huoni kwamba ni hoja mufilisi na mtu mzito kama wewe kuingilia ni kushusha hadhi yako mkuu, hawa wana hoja za kutaka walokole wote wahame hapa duniani kwa sababu hata Mungu anasema ni dunia ya shetani,



Respect.

Field Marsahll Es!

FME,

Mimi naomba nikuulize kitu kimoja tu, ndiyo wewe unazunguka na wapambanaji pia na kuwasaidia kwenye hizo harakati lakini bado hujaweza kujibu hii Mada: Je Wapiganaji walioko CCM wanapi.......... wakiwa humohumo na bado wanaendelea .... humohumo?

Kama umemsoma Rev. Kishoka ameeleza mambo yake mengi....
na juzi juzi ndo wamejiongezea marupurupu manono kwelikweli hao hao, ukichanganya na mfuko wa jimbo n.k. ndo sisi tulioko pembeni tunauliza hivi kweli hawa wako serious kweli au ni usanii?? je hii vita wataiwezaje na wao bado wanaendelea kufaidi keki ya mlalahoi? Tusaidie manake huko karibu nao.
 
Kuna Ulazima wa kubadilisha hali hii!! maaana watu wachache hawawezi kubadilisha mfumo huuu ndani ya Chama chao
 
FMES,

Lowassa hakuondolewa na wapiganaji, alijiondoa mwenyewe kwa upumbavu wake, badala ya kukubali kuwa alifanya makosa na kuzembea kufanya kazi yake.

Mkataba wa Richmond bado uko hai mpaka leo hii, Miezi 18 tangu Lowassa ajiuzulu na mwekezaji hewa analipwa fedha ambazo zingejenga madaraja, barabara, mifereji na kuzipa shule madawati.

Kama Wapiganaji walikuwa na nia ya kweli kuushinda Ufisadi, ilipofika Bunge la June 2008, wasingepitisha Bajeti ya Serikali ilhali mkataba wa Richmond ambaoo umeenda kwa Dowans bado unaendelea na Taifa linaingia gharama kulipia mkataba batili!

Wangekuwa makini, walipokwenda Butiama, wangehakikisha kuwa ndani ya Chama chao, kina Lowassa, Karamagi na Chenge wanapewa karipio kali na kuvuliwa madaraka kama si uanachama wa Chama kwa kukitia aibu chama.

Walichokifanya na ndicho naikiataa, ni kutekenya na kukaa mguu pande.

Huyo Mwakyembe si alikuja Marekani akazunguka majumbani mwa wana JF ambao ndio walimsukuma atafute hiyo ziara ya kuja kuichunguza Richmond?

Kama isingekuwa sisi tangu awali kuweka hadharani ukweli kuwa Kampuni hiyo ni feki, na kila kitu ambacho kiliipa hiyo tume nguvu kufanya kazi yake leo tungekuwa wapi?

Kama leo hii JF isingepata mkataba wa Buzwagi na kuuweka hadharani unafikiri Karamagi angejiuzulu au hata kamati ya Bomani kuundwa na kufanya kazi yake?

Ninachokataa ni kufanya kazi nusunusu na kuanza kujisifu kwa kazi nzuri eti waliofanya.

Mimi na wewe si Wabunge, lakini tunwajibia kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania kulinda mali ya Tanzania. Tunachokifanya hata kwa kujificha iwe ni hiari au kwa hofu ya Usalama kwa kuwa hatutafuni maneno kama wanasiasa ni wajibu wetu ambao pamoja na kuwa Upo kwenye katiba na tunapewa kinga na katiba, bado Serikali na Chama tawala haviheshimu kilichoandikwa kwenye katiba.

Tusiwasifie Wapiganaji kisa eti walifanya kazi nzuri kumshinikiza Lowassa akajiuzulu, huku matatizo ya mfumo wa Nishati na Umeme bado ni makubwa na mapendekezo yao hayajafanyiwa kazi mpaka leo.

Nimehoji mengi kuhusu Wapiganaji ambayo ni kweli hayafanyiki na yanaachiwa yakiendelea Bungeni na ni hili la kulia Ufisadi ndilo tunaliona lililokuu na bora tuwape shangwe?

Walikuwa wapi kukataa kulipwa mishahara mipya kila mwaka huku wafanyakazi wa Tanzania bado hawajaongezewa mishahara? Uchungu gani huo wao waendelee kuneemeka na hata leo hii wamelilia mifuko ya maendeleo ya wilaya, kitu wanachojua si sahihi kwa kuwa tayari kuna bajeti za Wilaya zinazopitishwa na Bunge?

Labda niulize hili jingine, Bunge la Tanzania lina nyumba ya Spika, kwa nini Spika akae kwenye nyumba ya mtu binafsi na si ya Serikali na kulipia hiyo nyumba kwa mwezi kwa gharama za kusomesha Wanafunzi nane pale Chuo Kikuu kwa mwaka?

Siku nikisikia wamekuwa Bangusilo kwa kuipinga Serikali kama kina Njelu Kasaka na hoja ya G55 ambayo ilisababisha Baba yangu mkubwa Mzee Trekta kulazimishwa ajiuzulu kwa kuruhusu Demokrasia itumike na kupoteza Ubunge au kufukuzwa CCM, hiyo ni siku nitakapoamini kweli wana nia ya kulifia Taifa letu na watakachofanyiwa kitawaonyesha Watanzania uozo ulioko ndani ya CCM ambao umekumbatia madaraka na uongozi na kukifanya CCM kionekane ni chama cha Mafisadi.

Nyerere alisema upinzani makini utatoka CCM, kama wao ni wapinzani makini ndani ya CCM basi wasikie kauli yangu niliyohoji kuhusu maslahi ya Mtanzania, Taifa, Ufujaji wa Bajeti, Tabia ya kuombaomba na si kujifanya wao ni vinara wa kumkomboa Mtanzania kwa kupigana na Ufisadi pekee!

Tulianza na vita vya Wahujumu, tukaja mikingamo, fagio la chuma, ripoti ya Warioba, ripoti ya Chifupa na sasa Upapa na Nyangumi, lakini bado Uhujumu, Ufisadi na Rushwa vinaendelea tena nyakati hizi bila woga.

Ningependekeza usome makala ya Mwanakijiji ya kuuelewa Ufisadi na uwape nakala hao Wapiganaji wachache unaofahamiana nao na uwaulize watawezaje kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya mfumo wa Kisiasa, Kisheria na Kiuchumi na si vipodozi vya kumpigia kelele Lowassa na Rostam!
 
FMES,


Mkataba wa Richmond bado uko hai mpaka leo hii, Miezi 18 tangu Lowassa ajiuzulu na mwekezaji hewa analipwa fedha ambazo zingejenga madaraja, barabara, mifereji na kuzipa shule madawati.

Kama Wapiganaji walikuwa na nia ya kweli kuushinda Ufisadi, ilipofika Bunge la June 2008, wasingepitisha Bajeti ya Serikali ilhali mkataba wa Richmond ambaoo umeenda kwa Dowans bado unaendelea na Taifa linaingia gharama kulipia mkataba batili!

Kaka sidhani kama hapa upo sawa. Ngoja nifuatilie zaidi maana nijuavyo huu mkataba ulishavunjwa na fedha ambazo tunawadai ni karibia bilioni 9 zikiwemo Bilioni mbili za faini ya kuchelewa kutekeleza mkataba.

Tusiwasifie Wapiganaji kisa eti walifanya kazi nzuri kumshinikiza Lowassa akajiuzulu, huku matatizo ya mfumo wa Nishati na Umeme bado ni makubwa na mapendekezo yao hayajafanyiwa kazi mpaka leo.
Na ni bora kuwauliza walichangia nini katika kazi hii na mpaka sasa wamefanya nini kuhakikisha serikali inatekeleza jukumu lake kupitisha hili..


Walikuwa wapi kukataa kulipwa mishahara mipya kila mwaka huku wafanyakazi wa Tanzania bado hawajaongezewa mishahara? Uchungu gani huo wao waendelee kuneemeka na hata leo hii wamelilia mifuko ya maendeleo ya wilaya, kitu wanachojua si sahihi kwa kuwa tayari kuna bajeti za Wilaya zinazopitishwa na Bunge?
Sio hivyo tu, na wengine wanaongoza katika kuchukua na hata kushinikiza posho kutoka kwa mashirika ya umma huku wakiwa tayari wamelipwa na bunge na kukiwa na waraka wa katibu kiongozi kukataza hilo.


Nyerere alisema upinzani makini utatoka CCM, kama wao ni wapinzani makini ndani ya CCM basi wasikie kauli yangu niliyohoji kuhusu maslahi ya Mtanzania, Taifa, Ufujaji wa Bajeti, Tabia ya kuombaomba na si kujifanya wao ni vinara wa kumkomboa Mtanzania kwa kupigana na Ufisadi pekee!
Kwa muono wangu Mwalimu Nyerere alikosea hapa.

Yawezekana upinzani wenye nguvu ukatoka CCM lakini sio UPINZANI MAKINI. Mwalimu alitegemea kuwa kutokana na MAFISADI kuanza kubomoa misingi na falsafa za CCM zilizoegemea katika Ujamaa na kuanza kushinikiza UFISADI kwa jina la UBEPARI basi wale waliokuwa wajamaa ama watawafukuza hawa MAKUWADI wa Ubepari ama wao Wajamaa wataondoka humo na kuanzisha upinzani makini wenye kushindana na CCM hovyohovyo yenye kufuata UBEPARI.

Hata hivyo hali inavyoonyesha hilo halitatokea kutokana na kuwa upiganaji wa hawa sio wa tofauti za misingi, falsafa wala itikadi bali ni POWER POLITICS. Yaani kwao wao ni nani ana nguvu na ushawishi mkubwa ndani na nje ya chama na sio tofauti za kiitikadi, misingi, sera, falsafa hata utendaji wa chama...

Katika hali hii ni wazi wakitoka CCM hawa tutakuwa tunatengenezewa bomu la aina ya NARC ambalo litatumia madhila ya UFISADI tunayokumbana nayo kujipigania THEIR TURN TO EAT......MASIHA FEKI hawa na ndio maana mimi sitaki hata kujustify huo mpambano wao ambao ukweli ni kuwa kungekuwa na UPINZANI MAKINI tayari basi watanzania wangefaidika sana na huu unafiki wa so called WAPIGANAJI....

omarilyas
 
Last edited:
Kaka sidhani kama hapa upo sawa. Ngoja nifuatilie zaidi maana nijuavyo huu mkataba ulishavunjwa na fedha ambazo tunawadai ni karibia bilioni 9 zikiwemo Bilioni mbili za faini ya kuchelewa kutekeleza mkataba.


omarilyas

Omar, Nashukuru kwa kuweka sawa jambo hili la mkataba wa Richmond, kwa kuwa utendaji wa Serikali yetu na kujivutavuta na hasa ukizingatia mpaka karibu mwanzoni mwa kota ya pili ya mwaka huu, bado tulikuwa tukizungumzia Richmond Dowans.

Kutoaminika kwa Serikali yetu mara nyingine hutufanya Watanzania tuwe Tomaso na kutaka tukione kikifanyika kwa vitendo na si kauli tuamini kuwa kazi imefanyika.
 
Hata nikirudi katika nafasi zao za Ubunge na mengi ambayo yanafanyika Bungeni, wote hawa, Mwakyembe, Seleli, Kimaro, Sitta, Sendeka, Limbeli, Kilango walikuwa wapi kumtetea Mbunge na mpiganaji mwenzao Zitto alipoleta hija ya kuhoji mkataba wa Buzwagi kama si wao kujiunga pamoja kama Chama Tawala na kumdhalilisha na kumbeza Zitto na si kusimama kidete na kufuata mkondo wa halali na ulio sawa wa kuchangua hoja na kuifanyia uchunguzi?

Hivyo basi siridhiki na sifa tunazowamwagia hapa kuwa wao ni mashujaa, maana tunafurahia yale tunayoyataka kwa nafsi zetu kibinafsi na si kwa manufaa ya Taifa. Walichokifanya na kinachotulewesha ni kile walichokifanya Februari 2008 na kulazimisha Lowassa ajivue Uwaziri Mkuu. Lakini Mkataba wa Richmond bado haujatenguliwa, je mbona bado wako mguu pande huku tunaumia kwa bei kubwa za umeme na mbaya zaidi ukosefu wa umeme kutokana na uzembe uliozaa huo mkataba?

Mchungaji,

Umesema kweli tupu! kwa hakika post yako hii is worth written in goldish ink! kila paragragh inamshinda mwenzie kwa ujumbe mzito uliomo. Umesema yote mie langu dogo tu nalo ni AHSANTE!
 
FME,

Mimi naomba nikuulize kitu kimoja tu, ndiyo wewe unazunguka na wapambanaji pia na kuwasaidia kwenye hizo harakati lakini bado hujaweza kujibu hii Mada: Je Wapiganaji walioko CCM wanapi.......... wakiwa humohumo na bado wanaendelea .... humohumo?

Kama umemsoma Rev. Kishoka ameeleza mambo yake mengi....
na juzi juzi ndo wamejiongezea marupurupu manono kwelikweli hao hao, ukichanganya na mfuko wa jimbo n.k. ndo sisi tulioko pembeni tunauliza hivi kweli hawa wako serious kweli au ni usanii?? je hii vita wataiwezaje na wao bado wanaendelea kufaidi keki ya mlalahoi? Tusaidie manake huko karibu nao.

- Mkuu narudia tena kwamba unahitaji ku-establish JF tunapigania nini na what are our accomplishments, then utawaelewa wapiganaji ingawa wao wanaenda one step zaidi yetu kwa sababu hawajifichi nyuma ya majina ya bandia.

- Serikali inapoongeza marupu rupu yoyote kwa wafanyakazi wake inakuwa ime-research na kutafiti kwa facts, ndio maana ikatoa marupu rupu kwa wabunge, na ndio maana hata Dr. Slaaa hajayakataa hayo marupu rupu wala mbunge yoyote wa Upinzani, ni kwa sababu they deserve it kutokana na uwakilishi wao kwa wananchi most ya hizo hela huwa wanaishia kuwapa wananchi wa majimbo yao, nimeona kwa macho yangu haiwezekani mbunge akaenda jimboni bila kugawa hela kwa wananchi haijawahi kutokea mkuu!

- Eti kama hawa sio wapiganaji una maana Chadema ndio wapiganaji au CUF?

Respect.

FMEs!
 
FMES,

Lowassa hakuondolewa na wapiganaji, alijiondoa mwenyewe kwa upumbavu wake, badala ya kukubali kuwa alifanya makosa na kuzembea kufanya kazi yake.

- Mchungaji ninazo video za siku Lowassa alipoondolewa bungeni, kwanza alishambuliwa sana na wapiganaji ndio akaamua kujitoa, sio kama ulivyoeleza hapo juu hawakwenda bungeni kujadili maji na yeye akaamua kujitoa kwa upumbavu wake, siamini kwamba Lowassa ni mpumbavu kiasi hivho unachosema kwamba wabunge wapiganaji wanaongelea maji yeye anajitoa kwa sababu ya Richimonduli.

Mkataba wa Richmond bado uko hai mpaka leo hii, Miezi 18 tangu Lowassa ajiuzulu na mwekezaji hewa analipwa fedha ambazo zingejenga madaraja, barabara, mifereji na kuzipa shule madawati.

- Si kweli baada ya Lowassa kujiuzulu, Rais alitoa order ya kusimamisha malipo ya Richimonduli baada ya bunge kuamua hivyo.

Kama Wapiganaji walikuwa na nia ya kweli kuushinda Ufisadi, ilipofika Bunge la June 2008, wasingepitisha Bajeti ya Serikali ilhali mkataba wa Richmond ambaoo umeenda kwa Dowans bado unaendelea na Taifa linaingia gharama kulipia mkataba batili!

- Dowans inalipiwa kwa sababu Zitto na wenziwe walihalalalisha huo mkataba, it has nothing to do na wapiganaji.

Wangekuwa makini, walipokwenda Butiama, wangehakikisha kuwa ndani ya Chama chao, kina Lowassa, Karamagi na Chenge wanapewa karipio kali na kuvuliwa madaraka kama si uanachama wa Chama kwa kukitia aibu chama.
Walichokifanya na ndicho naikiataa, ni kutekenya na kukaa mguu pande.

- Wapiganaji 11 hawawezi kuwaondoa mafisadi karibu 5,000 walioko CCM kwa kikao kimoja tu cha Butiama, ni kama vile Zitto alivyoshindwa na wazee wa chama, yaani mtu mmoja tu hawezi kushindana na wazee wengi huko kwenye chama waliomlazimisha kurudisha fomu anahitaji wananchi wengi wa kumuunga mkono kama wapiganaji wanahitaji sana msaaada wetu wananchi, badala ya kuwavunja nguvu kama unavyofanya.

Huyo Mwakyembe si alikuja Marekani akazunguka majumbani mwa wana JF ambao ndio walimsukuma atafute hiyo ziara ya kuja kuichunguza Richmond? kama isingekuwa sisi tangu awali kuweka hadharani ukweli kuwa Kampuni hiyo ni feki, na kila kitu ambacho kiliipa hiyo tume nguvu kufanya kazi yake leo tungekuwa wapi? Kama leo hii JF isingepata mkataba wa Buzwagi na kuuweka hadharani unafikiri Karamagi angejiuzulu au hata kamati ya Bomani kuundwa na kufanya kazi yake? Ninachokataa ni kufanya kazi nusunusu na kuanza kujisifu kwa kazi nzuri eti waliofanya.

- Ndicho exactly ninachosema, wapiganaji wanahitaji msaaada wetu kama tulivyowasaidia kwenye Richimonduli, sisi majina ya bandia tusaidie wwanaojiweka mbele na majina ya kweli, yaani hawa wapiganaji ndio tutafanikiwa kulikomboa taifa, sio kuanza sasa kudai credit wakati taifa linazidi kudidimia.

Mimi na wewe si Wabunge, lakini tunwajibia kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania kulinda mali ya Tanzania. Tunachokifanya hata kwa kujificha iwe ni hiari au kwa hofu ya Usalama kwa kuwa hatutafuni maneno kama wanasiasa ni wajibu wetu ambao pamoja na kuwa Upo kwenye katiba na tunapewa kinga na katiba, bado Serikali na Chama tawala haviheshimu kilichoandikwa kwenye katiba. Tusiwasifie Wapiganaji kisa eti walifanya kazi nzuri kumshinikiza Lowassa akajiuzulu, huku matatizo ya mfumo wa Nishati na Umeme bado ni makubwa na mapendekezo yao hayajafanyiwa kazi mpaka leo. Nimehoji mengi kuhusu Wapiganaji ambayo ni kweli hayafanyiki na yanaachiwa yakiendelea Bungeni na ni hili la kulia Ufisadi ndilo tunaliona lililokuu na bora tuwape shangwe?

Walikuwa wapi kukataa kulipwa mishahara mipya kila mwaka huku wafanyakazi wa Tanzania bado hawajaongezewa mishahara? Uchungu gani huo wao waendelee kuneemeka na hata leo hii wamelilia mifuko ya maendeleo ya wilaya, kitu wanachojua si sahihi kwa kuwa tayari kuna bajeti za Wilaya zinazopitishwa na Bunge?

Labda niulize hili jingine, Bunge la Tanzania lina nyumba ya Spika, kwa nini Spika akae kwenye nyumba ya mtu binafsi na si ya Serikali na kulipia hiyo nyumba kwa mwezi kwa gharama za kusomesha Wanafunzi nane pale Chuo Kikuu kwa mwaka?

Siku nikisikia wamekuwa Bangusilo kwa kuipinga Serikali kama kina Njelu Kasaka na hoja ya G55 ambayo ilisababisha Baba yangu mkubwa Mzee Trekta kulazimishwa ajiuzulu kwa kuruhusu Demokrasia itumike na kupoteza Ubunge au kufukuzwa CCM, hiyo ni siku nitakapoamini kweli wana nia ya kulifia Taifa letu na watakachofanyiwa kitawaonyesha Watanzania uozo ulioko ndani ya CCM ambao umekumbatia madaraka na uongozi na kukifanya CCM kionekane ni chama cha Mafisadi.

Nyerere alisema upinzani makini utatoka CCM, kama wao ni wapinzani makini ndani ya CCM basi wasikie kauli yangu niliyohoji kuhusu maslahi ya Mtanzania, Taifa, Ufujaji wa Bajeti, Tabia ya kuombaomba na si kujifanya wao ni vinara wa kumkomboa Mtanzania kwa kupigana na Ufisadi pekee!

Tulianza na vita vya Wahujumu, tukaja mikingamo, fagio la chuma, ripoti ya Warioba, ripoti ya Chifupa na sasa Upapa na Nyangumi, lakini bado Uhujumu, Ufisadi na Rushwa vinaendelea tena nyakati hizi bila woga.

Ningependekeza usome makala ya Mwanakijiji ya kuuelewa Ufisadi na uwape nakala hao Wapiganaji wachache unaofahamiana nao na uwaulize watawezaje kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya mfumo wa Kisiasa, Kisheria na Kiuchumi na si vipodozi vya kumpigia kelele Lowassa na Rostam

- Mkuu again wapiganaji 11 tu, hawawezi kufanya yote haya uliyoyasema in one year au hata five years, cha muhimu mimi na wewe tujitahidi kuwasaidia na kuwapa support hawa wapiganaji badala ya kuwabeza wakati ukweli ni kwamba wao wako front na sisi tuko nao na majina ya bandia, tuwasaidie na tusaidane nao kulisaidia taifa letu, taifa ni letu sio lao hawa wapiganaji 11 tu, unayoyasema wewe na anayoyasema Mwanakijiji ni maneno tu, yanahitaji hawa wapiganaji 11 kuyafanyia kazi huko bungeni as they always do, ninarudia kwamba mafisadi hawawezi kupoteza millions of money kuhonga wajumbe wa NEC kuwaondoa wapiganaji wasio effective na ambao wala hawawasumbui, haya ni mawazo mufilisi na ni ya kuyaogopa kama ukoma!

Again, please tuwape support hawa wapiganaji wao wanatuhitaji na sisi tunawahitaji.

Respect.

FMEs!
 
Ona unavyorukaruka mkuu, aibu tupu, nimesema nakujua kwa post zako, na si kivingine, umekuja kusema mimi nimenunua nyumba za serikali na meremeta issues. nimekueleza thibitisha , jibu ndio hili!!!, waeleze waungwana mzee umeanza hadithi na unataka niseme ufisadi wako, ufisadi wako ni kupitia post zako! si kivingine, mkuu unaaibika hivi hivi!

Nimesema eleza A-Z yangu, na mimi sitajieleza Mods watataja jina langu, kama mimi fisadi na kelele zote hizi si mnafiki basi? kwa nini usinitaje ? ukishindwa kwangu mimi utaweza kwa akina JK??

Tumekuangalia sana nyendo zako, na hili mkuu unalo, wewe ni fisadi .period! unapita kudanganya hao watu, mpiganaji gani rafiki yako?? njaa tupu!

hujajibu tuhuma, NINGEWAZA kukushtaki kwa mods, kwa kuleta uongo, naona nitapoteza muda, kwanza unawaaibisha mtu kama wewe kutuma post kama hizi, aibu!! kaa kimya ukiona huwezi kuthibitisha madai yako, kaa kimya endapo unajua ulisema uongo, kaa kimya endapo tuhuma hizi ni za kweli kaa kimya, ukikaa kimya unaleta wingu la kuwa inawezekana mimi mwongo! ukijibu kwa staili hii... LOL! watu wanajua kumbe kuna jambo!

YAANI KISAIKOLOJIA NAONA KABISA KUMBE HISIA ZANGU ZILIKUWA KWELI, UTAWATAMBUA KWA POST ZAO TU!

In short, baba yangu mzazi alifariki tangu 1990 nikiwa darasa la nne! nimelelewa na mama yangu nurse hapo agakhan, nimesoma tambaza , tukasambazwa na nikapelekwa moshi, nimesoma huko miaka yangu 5, kabla ya chuo, -UDSM, nimelipiwa na bodi ya mikopo, kipindi hicho full sponsorship, nimemaliza 2006! kozi ya miaka minne. Hii ni katika kukuthibitihsia kuwa wewe ni mwongo!

MODS: madai ya FMES yalikuwa mabaya sana, sijaamua tu kushtaki officially najua ni mzee wa humu, na imetokea mara nyingi anagombana na watu na hafanywi kitu, nimesema athibitishe madai ya kununua nyumba za serikali na eti na kuhusu meremeta ameshindwa! Forum sio nzuri kuwa na watu kama akina FMES mbao wanaweza kuzusha uongo kwa malengo ya kufukuza watu humu au kuwa-weaken. Itafutwe mbinu mbadala ya kudeal naye. This is serious! afute ile post au athibitishe!(simple) thats all! najua itakuwa ngumu kwenu kwani huyu ni mzee wa humu , ila ni vizuri mkatumia busara kumwonya, maana inaonekana ana matatizo au frustration za kuambiwa ukweli.

Sitajibizana naye tena kwenye post nyingine yeyote, unless nikiona issue ni mbaya sana, basi nitadeal naye mimi mwenyewe kwenye post, lakini mnanisamehe maana nitamkimbiza!

FMES nimekuvulia kofia! kumbe elimu za propaganda za akina Kingunge,Hiza na Mrema unaziweka kwenye practise, mimi mhandisi bwana naangalia facts !

SAMAHANI WANA JF kwa kwenda kinyume na maada hii haitajirudia tena.ni katika kumfunda aliyeshindwa hoja na kusema uwongo.

Pole sana Mhandisi, Maumivu yako ya Dhati yameniumiz na Mimi. Endelea kukata Nyanga.
 
Natamani haya maneno niliyowekea green colour kama yangeingia ndani ya mioyo ya watanzania nakugeuka kuwa attitude yetu. Well if we have you few to start with then I believe pole pole hii chachu itachachusha donge zima la watanzania.

Kila mtu akigundua kua ni heri kudanganywa kwa usilolijua kuliko kujidanganya mwenyewe basi kauli za kutaka cheap popularity zingetoeka kati yetu kwani machoni mwa mataifa wote tunawekwa kwenye kundi moja kwamba ni wababaishaji na kwasababu hiyo tunatumiwa kwa maslahi yao (mataifa beberu) huku sisi tukiendelea kujidanganya, kujidharau, kudharauliwa nakufedheheka katika dimbwi la umaskini huku tukikosa confidence ya kufanya chochote chenye manufaa katika dunia hii nakua watu wakuhurumiwa (dhihakiwa) kila wakati.

Inauma tena inauma sana. Ninachojiuliza haya maumivu wengine wanayapata au wachache tu ndo wana feel kuwa embarrassed? What does it profit one to have all the gains of this country while masses are dying every second simply because we are not realistic? wanafiki, waongo, wapenda sifa na wapenda kutukuzwa na kunyenyekewa kama Miungu? God help us until we get the right people and right ideas then we will come back to our senses that we are not that much helpless and poor as few could want us believe.


.

- Dada yangu Felister, ubarikiwe maana maneno yako ni mazito sana, naomba ukipata nafasi uni-beep maana nime-misplace namba yako, ubarikiwe tu dada yangu wa upendo maana maneno yako ni mazito sana!

- Unajua hoja nzito kama hii yako inasimama yenyewe bila matusi wala kejeli, ni mfano wa kuigwa.


Respect.

FMEs!
 
- Mkuu again wapiganaji 11 tu, hawawezi kufanya yote haya uliyoyasema in one year au hata five years, cha muhimu mimi na wewe tujitahidi kuwasaidia na kuwapa support hawa wapiganaji badala ya kuwabeza wakati ukweli ni kwamba wao wako front na sisi tuko nao na majina ya bandia, tuwasaidie na tusaidane nao kulisaidia taifa letu, taifa ni letu sio lao hawa wapiganaji 11 tu, unayoyasema wewe na anayoyasema Mwanakijiji ni maneno tu, yanahitaji hawa wapiganaji 11 kuyafanyia kazi huko bungeni as they always do, ninarudia kwamba mafisadi hawawezi kupoteza millions of money kuhonga wajumbe wa NEC kuwaondoa wapiganaji wasio effective na ambao wala hawawasumbui, haya ni mawazo mufilisi na ni ya kuyaogopa kama ukoma!

Again, please tuwape support hawa wapiganaji wao wanatuhitaji na sisi tunawahitaji.

Respect.

FMEs!

Jemedari FMES,

Mara nyingine huwa unaniacha hoi. Sasa kama uwiano unaousema wa Wapiganaji 11 dhidi ya mafisadi 5000 na bado unadai CCM ni safi, unategemea ni lini hao Wapiganaji wataweza kushika hatamu?

Hiyo kauli yako niliyonukuu hapo juu, mshikaji wako Kitila Mkumbo akiiona, atakupa uanachama wa CHADEMA wa maisha bure... kwi kwi kwi!

Kama kupigana vita dhidi ya Uhujumu vilianza na Sokoine, tukashindwa kubadilisha mfumo wa Kisiasa, Sheria na Kiuchumi ili kupunguza kasi ya Wahujumu, utatuambiaje leo tuikumbatie CCM kwa ajili ya hao 11 ambao wanapigana vita butu?

Je huoni kama Wapiganaji wangewekeza nguvu zao kumpa Mtanzania nguvu za kujitegemea kwa kupeleka maendeleo ya kweli kwa wananchi na hivyo wananchi kuwa na uwezo wa kuwa huru na wenye kujitegemea bila kumtegemea mtu au kuhongeka kirahisi, huoni hii vita dhidi ya ufisadi ingekuwa rahisi?

Leo Mtanzania akijua kuwa ana chakula cha kutosha na cha akiba nzuri, ana ajira yenye kipato kinachokidhi maisha na mahitaji yake, Watoto wake wanakwenda shule na kuelimika na si kutaabika, akiugua anajua akienda hospitali au zahanati yoyote atapata matibabu na hahitaji kupelekwa India, akilima mazao, ana uhakika kuwa ujuzi aliofundishwa, utampa mazao ya kutosha na atapata soko kabambe na si kuhangaika kutafuta mnunuzi, huoni kuwa Mtanzania huyu ni rahisi kwake kupiga kura ya hapana kwa yule ambaye hafai?

Ni mara ngapi humu na hata kule BCS nimesema kuwa kwa Tanzania kupata maendeleo ya kweli na kushinda Ujinga, Umasikini, Maradhi na Ufisadi ni lazima Mtanzania awe huru na mwenye kujitegemea na kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi bila kulazimishwa au kulaghaiwa na kofia, fulana na ubwabwa?

Hitimisho langu ni hili, mtazamo wetu katika wajibu wa hao "wapiganaji" unatofautiana sana na si ajabu kuwa hatuoni wanachokifanya kwa mtazamo mmoja.

Kwangu mimi, mpiganaji wa kutetea haki za Mwananchi na kulinda nchi yake, hachagui vita au adui wa kupigana ili kushinda kinachomdhoofisha. Kwangu mimi vita ya kweli ni ya kupigana na mfumo mzima wa Utawala usio makini, fanisi, uliojaa uzembe, wivu, ufujaji, kutokujali, wenye kauli kibao kama za Ari, Kasi na Nguvu Mpya na hata sasa Kilimo Kwanza lakini hakuna msukumo wa kufanya kauli hizo ziwe vitendo.

Sasa naelewa kuwa mwenzangu mtazamo na matarajio yako kwa Wapiganaji ni kupigana vita moja, ya Ufisadi na zaidi dhidi ya kikundi fulani ambacho hukubaliani nacho kwa sababu fulani.

Hivyo basi, tofauti yetu ni kuwa mimi naangalia kwa upana mstakabali wa Taifa zima kupata maendeleo, kwa kutumia nguzo zile nne za Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora ili kuondokana na Umasikini, Ujinga, Maradhi, Unyonge na Uonevu kwa kutumia Juhudi na Maarifa yanayoambatana na Uwajibikaji, Ufanisi, Unyenyekevu, Busara na Hekima katika kujenga Taifa lenye Umoja wa Kweli, Mshikamano Thabiti na Utulivu wa Roho.

Je weye Rafiki yangu, mtazamo wako ni upi? Je ni ule ule wa kusema ni CCM na CCM pekee, kwa manufaa ya CCM kwanza na ndipo Tanzania tufuate?

Sasa kama tunaimba "Msalaba Mbele, Dunia Nyuma" kanisani na sisi tunaolilia Mabadiliko na vita ya Kweli tunaimba "Tanzania Mbele, Chama Nyuma" weye unaimba "CCM mbele, Tanzania Mwisho"?
 
=Field Marshall ES;579722][


- Mchungaji ninazo video za siku Lowassa alipoondolewa bungeni, kwanza alishambuliwa sana na wapiganaji ndio akaamua kujitoa, sio kama ulivyoeleza hapo juu hawakwenda bungeni kujadili maji na yeye akaamua kujitoa kwa upumbavu wake, siamini kwamba Lowassa ni mpumbavu kiasi hivho unachosema kwamba wabunge wapiganaji wanaongelea maji yeye anajitoa kwa sababu ya Richimonduli.

Je Lowassa aliambiwa ni lazima ajiuzulu? Hata kama walimshambulia kuna aliyemwambia ni lazima ajiuzulu? Kama walimwambia anapaswa kuwajibika, angeweza kuwajibikia kwa kukubali alikosea hatua za kiutendaji na kufanya uamuzi mbaya. Sasa kama baada ya yeye Kiungwana kukubali alikosea na Wabunge wakashurtisha kura ya kutokuwa na Imani, hapo tungeelewana kuwa alilazimika kujiuzulu. Lakini hilo halikutokea. Narudia kwa Upumbavu wake aliamua kujiuzulu, kama Mzee Mwanakijiji anavyosema, aliamua kuzira, sawa na mtoto mdogo anavyoamua kuzira kutokana na upumbavu na ukosefu wa Busara na Hekima. Silika ya kukataa kujirudi ni kitu cha kawaida kwa Lowassa na ni mtu mwenye kiburi sana kukubali anapokosea!

- Si kweli baada ya Lowassa kujiuzulu, Rais alitoa order ya kusimamisha malipo ya Richimonduli baada ya bunge kuamua hivyo.
- Dowans inalipiwa kwa sababu Zitto na wenziwe walihalalalisha huo mkataba, it has nothing to do na wapiganaji.


Sijasema mahali popote kuwa mkataba ulisitishwa au Raisi alitoa amri mkataba ufutwe au kusimamishwa. Sijauliza ni nani alihalalisha mkataba hivyo kusema ni kina Zitto ni kusingizia. Nimeuliza, kwa nini baada ya mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe kutolewa Februari 2008 wakati wa kikao cha Bajeti Juni 2008 hakuna aliyeukuta kuhoji kwa nini mkataba haujavunjwa? Kwa nini waliruhusu Bajeti ikapita huku mkataba ambao uliingia kwa hujuma na Batili ulikuwa bado ni halali na hata kwa mrithi wa Mkataba huo Dowans? Kama walitishwa Bungeni au kuwekwa kigoda kama KIkao cha Chama (kama Zitto alivyowekwa kati na Wazee wa CHADEMA), kwa nini walipotoka kwenye kikao hicho hawakuukana UCCM ambao tayari wameshaona kuwa hauna manufaa na haujali maslahi ya Tanzania?

Umemtaja Zitto, kwani Zitto alipiga kura pekee yake? ni Wabunge wangapi wa Upinzani walioko katika kamati ya Bunge ya Nishati au kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma? Hao wengine waliopiga kura kuiidhinisha mkataba wa Dowans ni kina nani na ni wa Chama gani?

- Wapiganaji 11 hawawezi kuwaondoa mafisadi karibu 5,000 walioko CCM kwa kikao kimoja tu cha Butiama, ni kama vile Zitto alivyoshindwa na wazee wa chama, yaani mtu mmoja tu hawezi kushindana na wazee wengi huko kwenye chama waliomlazimisha kurudisha fomu anahitaji wananchi wengi wa kumuunga mkono kama wapiganaji wanahitaji sana msaaada wetu wananchi, badala ya kuwavunja nguvu kama unavyofanya.

Kumwambia mtu ukweli kuwa anachokifanya hakileti matunda wala hakina mwelekeo wa kuleta manufaa ni kuvunja nguvu? Common Bother, hebu nikuulize wewe na Wapiganaji wanaolia kuwa nawavunja nguvu, kuwahoji kwa nini walikubali mishahara minono huku kima cha chini hakimsaidi mtu wa kawaida hata kulipia pango bila mtu huyu kutafuta fedha za ziada? Hivi wanaelewa kuwa mfumo wa Kifisadi umeshikilia nchi na kuota mizizi kutokana na Wananchi kukosa kipato cha kukidhi mahitaji? Je nilikosea kuwaambia kuwa wamefanya makosa kuidhinisha Rushwa na Takrima inayotolewa na mafisadi kwa Wananchi wa majimbo yao ili wachague mafisaidi kwa kudai hiyo ni mali yao waile na badala ya kuwapeleka Wanaotoa hongo mikononi mwa vyombo vya sheria?

- Ndicho exactly ninachosema, wapiganaji wanahitaji msaaada wetu kama tulivyowasaidia kwenye Richimonduli, sisi majina ya bandia tusaidie wwanaojiweka mbele na majina ya kweli, yaani hawa wapiganaji ndio tutafanikiwa kulikomboa taifa, sio kuanza sasa kudai credit wakati taifa linazidi kudidimia.

Unapowapelekea Dataz "Wapiganaji" kuna hata siku moja tumekudai malipo zaidi ya kudai wafanyie kazi tunachokisema? Kama Taifa linadidimia na wao Wapiganaji, wameegemea kulalamikia Ufisadi tuu na kuruhusu mengine yaendelee, unatarajiaje kuwa watashinda vita?


- Mkuu again wapiganaji 11 tu, hawawezi kufanya yote haya uliyoyasema in one year au hata five years, cha muhimu mimi na wewe tujitahidi kuwasaidia na kuwapa support hawa wapiganaji badala ya kuwabeza wakati ukweli ni kwamba wao wako front na sisi tuko nao na majina ya bandia, tuwasaidie na tusaidane nao kulisaidia taifa letu, taifa ni letu sio lao hawa wapiganaji 11 tu, unayoyasema wewe na anayoyasema Mwanakijiji ni maneno tu, yanahitaji hawa wapiganaji 11 kuyafanyia kazi huko bungeni as they always do, ninarudia kwamba mafisadi hawawezi kupoteza millions of money kuhonga wajumbe wa NEC kuwaondoa wapiganaji wasio effective na ambao wala hawawasumbui, haya ni mawazo mufilisi na ni ya kuyaogopa kama ukoma!

Again, please tuwape support hawa wapiganaji wao wanatuhitaji na sisi tunawahitaji.

Mimi natoa maoni yangu na uchambuzi wangu bila kumdai mtu ujira wala malipo. Nayasema ninayoyasema kutokana na mapenzi yangu kwa nchi yangu. Ni wajibu wangu kikatiba na nadharia yangu inanituma kusemahayo. Ndiyo ni maneno, lakini nimetafakari, nimefanyia vipimo na ndipo huzungumza. Hata Zitto na Slaa, siwaoniei aibu, wakikosea nawaambia.

Kwani Mkoloni si tulimngoa kwa kuanza na maneno, kisha Wananchi wakaamka na kufanya vitendo?

Labda nikuulize, je ulishawahi kuwapa "Wapiganaji" ule Waraka wa Mchungaji? Je waliposoma walikuambia nini? Je waliona nini ambacho ni muhimu ambacho walipaswa wakichukulie kwa dhati kuwa Waraka ule ni kilio cha Mtanzania na si MwanaCCM pekee? Kama waliupuuzia, je walikwambia ni kwa sababu gani?

Azimio la Arusha lilikuwa ni maneno, ambayo tuliyageuza kwa kiasi kikubwa kuwa vitendo, Azimio la Musoma, Azimio la Iringa, Mwongozo wa Chama 1981, Vita vya Uhujumu, vyote hivi vilianza kama maneno na tulipo hapa leo hii, tunachambua kile kilichofanya kazi na kile kilichoshidnikana na kumka rasmi kuwa kuna yanayopasa kurekebishwa.

Ninachowapigia kelele Wapiganaji na ndio kisa cha Mzee Mwanakijiji kuhoji Wanapigania nini ni mtazamo wetu kuwa vita hivi vinapiganwa na Wapiganaji kwa makosa na kuna mianaya mingi ya wao kuleta mabadiliko ambayo wala haihitaji kupigiana kelele au kuzidiana maarifa na mafisadi kama vile kuhakikisha kuwa Mtanzania anakuwa na furaha na fahari kuishi katika nchi yake akiwa amejitosheleza na hana wasiwasi kuwa atapata wapi chakula au kupoteza ardhi yake!


Mzee Mwanakijiji kauliza Wanapigania nini, mimi nawauliza Wanampigania nani vita hivi? Nani kawatuma kupigana?
 
Mwanakijiji! Hao ni makamanda wapiganaji wanaopigania mali yao ya UFISADI isitoke ndani ya chama. 40 years ya CCM hakuna mabadiliko sasa ni nini hii kama si uozo? Watu ni walewale kila siku tena na kutuongezea vizazi vyao ndani ya Chama na uongozi. Ndoa, ushemeji, ukwe, uwifi, ubibi na ubabu ndivyo vinavyotawala bungeni then wanatuambia kuna makamanda humo? Juzi nilijitahidi kumsikiliza raisi japo alikuwa akinibembeleza na usingizi nikagundua zile zilikuwa mbwembwe tu za kampeni ambazo ameshazianza kitambo, tunahitaji kusikia mabadiliko na haki zetu anatuelezea jinsi ya anavyotumia kipaji chake cha kwenda kututangazia umaskini kwa kuomba omba nchi jirani angali tu matajiri wa mali ziliwazo na MAFISADI WAKE. Kelele za makamanda hawa ni sawa na Chura ampigiapo Tembo, CCM NI SERIKALI NA SERIKALI NI CCC PAMOJA NA UFISADI UKIWA MALI YAO.
 
Jemedari FMES,

Ngoja niwasaidie Wapiganaji kwa namna ingine, labda mnaweza kuona busara na upenyo katika vita mnayoifanya.

Kwanza, kuna Wapiganaji wangapi kutoka Zanzibar? Je wanapigania nini? Ama kuna Wapiganaji wangapi kutoka vyama vya Upinzani ambao mmeshikamana? Je ndani ya Chama Chenu CCM, mna wafuasi wangapi katika Bunge, Mkutano Mkuu, NEC na CC?

Sasa nitawapa somo lahistoria na mjiulize kama mmechukua na kufikiria mambo jinsi ninavyoeleza.

Kwenye vita kuu ya pili ya Dunia, Uingereza, Ufaransa na Urusi, zilibidi zishikamane na hata kumkaribisha Marekani na kwa umoja pamoja na kila mmoja wao kuwa na malengo yake binafsi, wakaweza kumwangusha Hitler.

Marekani walipoamua kwenda kumbomoa Sadaam, walitafuta washiriki ili kujenga umoja na wakaingia vita na kisha kumuangusha Sadaam.

Swali kwangu, kuna wajumbe wangapi NEC ambao wanatoka Zanzibar? je CC na ni Wabunge wangapi wa CCM wanatoka Zanzibar? Je kilio chao ni nini na wao wanapigania nini?

Kama kikao cha Butiama kilitawaliwa na masuala ya Zanzibar na kama sikosei taratibu za CCM ni kura za makundi au mkusanyiko, je mliwafuata wenzenu wa Zanzibar kujadili vita vyao nanyi mkawaambia yanayowakabili katika vita vyenu, huku adui wenu nyote ni mmoja?

Je mkiungana na hao Wapiganaji wa Zanzibar ambao wao wanataka Serikali tatu, mafuta na Mahakama ya Kadhi, nanyi mkajumuisha Vita vya Ufisadi, kufutwa mikataba ya madini na kulazimisha uwajibikaji, hawaoni kuwa wakiungana pamoja na kuwa wana vitu tofauti, wanaweza kupata sauti moja kubwa ya Upinzani na kuwashinda Mafisadi wanaokitawala CCM na kuishikilia nchi?

Kama kuna Wabunge takriban 40 wa Upinzani, mkajiunga na nyinyi Wapiganaji wa Bara 11, mkawachukua na wale Wapiganaji wa CCM Zanzibar, ni rahisi kwenu kupata theluthi moja ya kura Bungeni.

Sasa kwa kuwa Zakumi anapenda mahesabu na takwimu, atakuambia theluthi moja ina nguvu na inaweza kuleta mabadiliko na kuweza kuvutia sehemu kubwa ya wale ambao bado hawajakata shauri.

Waswahili husema, kidole kimoja hakiui chawa, waambie wapiganaji watafute wapiganaji wengine waungane kumshinda Adui!
 
Nadhani wanavyofanya hao makamamnda wa ufisadi ni sahihi kabisa hasa ukizingatia kuwa kumkosoa mwenzio lazima kuanzie kwako lazima ujisahihishe kwanza wewe, wanavyofanya makamanda wa ufisadi ni sahihi kabisa, mimi kama mtoto wa mlala hoi nadhani wanafanya sawa ni juhudi hizo hizo zinazofanywa na vyama vya upinzani na watu kama kina slaa na zitto na wengine, na kama ikiwezekana nasi wananchi tujiunge na vyama vichafu kama ccm kwa lengo la kukisafisha na kuweka mifumo ya uwazi ya uzibaji wa mianya ya rushwa.
 
Mimi nina mtazamo tofauti kuhusu hawa Wapiganaji wa Ufisadi ndani ya CCM. Kutokana na hali ya siasa ya nchi yetu ya kutokuwa na Upinzani husioeleweka ndio maana tunahitaji kuwa na watu wa aina hii ndani ya chama kinachotawala. Ni kweli kuwa wote wako kwenye "tenga moja". Lakini pia napata picha ya kwenye kilicho kwenye imani zetu kuwa kama kuna mmoja ameamua kuokoka basi hasikimbie na kuwaacha wasioamini ila apambane nao uko uko ndani na kuwaambia ukweli kuwa ili kufika Mbinguni ni lazima "uokoke" hakuna njia ya mkato.
Kwa maana nyingine ni kwamba tunawahitaji haoa "wanaoitwa" na "kujiita" wapiganaji CCM kuendelea kukifanya wanachokifanya pasipo kuogopa wenzao ambao sio "waamini" wenzao
Nimalizie kwa kuwapongeza
 
MAPAMBANO YA UFISADI + MAKAMANDA WA UFISADI = PROPAGANDA KWAMBA KUNA MATUMAINI NDANI YA CCM

WAPIGANAJI Vs WAPAMBANAJI (MTANDAO) = YALEYALE

Badala ya mapambano dhidi ya ufisadi wao wapo katika mapambano ya ufisadi.....

omarilyas
 
Najiuliza maswali haya....

  1. Hivi kuna watu wa CCM wanapigana dhidi ya ufisadi?
  2. Wanatumia nyenzo gani?
  3. Wanapigania wapi?
  4. Nyenzo watumiazo wanapata wapi?
  5. Nini/Lini mategemeo yao?
Ukiacha kupata taarifa za vyombo vya habari sijui hii vita inaendaje.
 
Jemedari FMES,

Ngoja niwasaidie Wapiganaji kwa namna ingine, labda mnaweza kuona busara na upenyo katika vita mnayoifanya.

Kwanza, kuna Wapiganaji wangapi kutoka Zanzibar? Je wanapigania nini? Ama kuna Wapiganaji wangapi kutoka vyama vya Upinzani ambao mmeshikamana? Je ndani ya Chama Chenu CCM, mna wafuasi wangapi katika Bunge, Mkutano Mkuu, NEC na CC?

Sasa nitawapa somo lahistoria na mjiulize kama mmechukua na kufikiria mambo jinsi ninavyoeleza.

Kwenye vita kuu ya pili ya Dunia, Uingereza, Ufaransa na Urusi, zilibidi zishikamane na hata kumkaribisha Marekani na kwa umoja pamoja na kila mmoja wao kuwa na malengo yake binafsi, wakaweza kumwangusha Hitler.

Marekani walipoamua kwenda kumbomoa Sadaam, walitafuta washiriki ili kujenga umoja na wakaingia vita na kisha kumuangusha Sadaam.

Swali kwangu, kuna wajumbe wangapi NEC ambao wanatoka Zanzibar? je CC na ni Wabunge wangapi wa CCM wanatoka Zanzibar? Je kilio chao ni nini na wao wanapigania nini?

Kama kikao cha Butiama kilitawaliwa na masuala ya Zanzibar na kama sikosei taratibu za CCM ni kura za makundi au mkusanyiko, je mliwafuata wenzenu wa Zanzibar kujadili vita vyao nanyi mkawaambia yanayowakabili katika vita vyenu, huku adui wenu nyote ni mmoja?

Je mkiungana na hao Wapiganaji wa Zanzibar ambao wao wanataka Serikali tatu, mafuta na Mahakama ya Kadhi, nanyi mkajumuisha Vita vya Ufisadi, kufutwa mikataba ya madini na kulazimisha uwajibikaji, hawaoni kuwa wakiungana pamoja na kuwa wana vitu tofauti, wanaweza kupata sauti moja kubwa ya Upinzani na kuwashinda Mafisadi wanaokitawala CCM na kuishikilia nchi?

Kama kuna Wabunge takriban 40 wa Upinzani, mkajiunga na nyinyi Wapiganaji wa Bara 11, mkawachukua na wale Wapiganaji wa CCM Zanzibar, ni rahisi kwenu kupata theluthi moja ya kura Bungeni.

Sasa kwa kuwa Zakumi anapenda mahesabu na takwimu, atakuambia theluthi moja ina nguvu na inaweza kuleta mabadiliko na kuweza kuvutia sehemu kubwa ya wale ambao bado hawajakata shauri.

Waswahili husema, kidole kimoja hakiui chawa, waambie wapiganaji watafute wapiganaji wengine waungane kumshinda Adui!

Rev Ushauri mzuri.

Lakini sometimes is easy said than done kama uwanja wa mpira kwenye mashindano ambayo timu uipendayo inacheza na wewe uko bench unavyoweza kukosoa mchezaji wakutegemewa alivyojifunga goli.

Tatizo kubwa linalotusumbua ni life after the action you decide to take. Kwa nchi kama za kwetu unaweza kujikuta wewe kwa mob psychology ukaishia kuwa Bangusilo maana kati ya hao kumi na moja walio ji identify huenda wawili tu ndo wanamaanisha na wengine sitaki na taka. Ukiangalia wewe ndo tegemeo la ukoo mzima na family iliinvest kwa wewe kufika hapo what do you do?

Vita kama hiyo rahisi kwa watu ambao calculated risk is more than 50% sasa who knows may be thats what they are doing sasa si ndiyo na wewe ukawa mpiganaji wa wanyuma (comanding unit) msituni na wao wako front line? Kama hata waliweza kuwa consult at certain point huoni hata hapo wali dare?
 
Mkuu nashukuru kwa mawazo yako. Ukweli uko wazi kuwa hawa wanaopigana sasa ni kweli wanasema mambo yaliyowazi lakini walikuwa wapi? Kwanini waanze sasa tena baada ya watu fulani kuweka wazi orodha ya mafisadi (japo tunashukuru kwa kupata japo kidogo)? Maana kama kweli walikuwa wanapambana na ufisadi walikuwa ndani hivyo walikuwa na data mbona hawakuzitoa mpaka watu fulani walipoanza?

Mimi nadhani hapa kuna vitu chini ya kapeti. Kwenye uchaguzi uliopita wa 2005 kulikuwa na wanaCCM waliofaidika na ufisadi (waliokuwa karibu na mafisadi) hivyo mambo yalikuwa raisi kwao kwani resources walikuwa nazo za kumwaga (za wizi na udanganyifu). Kuna wale waliokuwa wanasupport watu wao na watu wao wakatolewa kwa mizengwe mfano Dr. Salim mpaka leo wana hasira kwa kutokutendewa haki. Hivyo hawa wapambanaji wako wa aina nyingi chini ya mwanvuri mmoja. Kuwatenganisha ndiyo ngumu kuwa yupi ni mkweli na yupi muongo.

Kama kweli ni wapambanaji walitakiwa wapambanie system ibadilishwe siyo kupiga kelele za mafisadi, mara leo walitaka kuniua, mara wanatuma watu jimboni kunichongea etc. Hapa kwanza wanapigania MAJIMBO YAO then ndiyo hakina SISI HOEHAE.

KAMA KWELI NI WAPAMBANAJI WAPIGANIE MABADILIKO YA MFUMO KWANI HATA WAKIWAELEZA WANANCHI WATAWAELEWA VINGINEVYO YATAKUWA YALEYALE YA MATUMBO KWANZA THEN WANANCHI.
 
Back
Top Bottom