Mchambuzi,
Sasa nimegundua jinsi gani Nyerere anabezwa na baadhi ya wenzake CCM,
Nyerere au mwingine yeyote anapokosea ataambiwa kweli, na ukweli sio maana yake kumbeza mtu. Bora anichukie kwa ukweli wangu kuliko kunipenda kwa kumpaka mafuta, hata kama kakosea mie nikenue meno kujichekesha. Unanchekesha!
na nadhani pia wapo viongozi wa CCM vilevile, na sababu zao ni ngumu kuelewa. Ila bila shaka, wengi wao ni wale wasio kuwa na maadili ya uongozi kwahivyo Jina la Nyerere kuwa mwiba mkali kwao. Ni ajabu kwamba hata viongozi wa CCM wapo wanaobeza mafanikioa ya Nyerere;
Hayo ni mawazo yako na siwezi kukupinga kwa mawazo yako. Mimi siongelei mawazo hapa naongelea facts.
Tunampima Nyerere kwa vipimo vya Colgate, TV na Magari? Ina maana kwamba sifa za viongozi wa leo ni upataikanaji wa Colgate, TV na Magari? Nilibahatika kwenda Kiteto na maeneo mengine mengi sana Tanzania huko vijijini na maisha yao kule hayana tofauti na mwaka 1961;
Hivi ulitaka mafanikio ya nchi yapimwe na nini? foleni za sukari ya kilo moja kwa wiki? foleni ya dawa za meno za Maxim? kwa foleni za kwenye UDA kunukishana vikwapa?
Kigezo cha kwenda Kiteto kukuta watu wanaishi kama 1961 si kigezo cha kitaalam hicho, Kiteto na kwingine kwingi Tanzania kuna watu wanaishi kama walivyokuwa wanaishi miaka 200 nyuma ni kwa utamaduni wao na si kwa kuwa wanakosa mahitaji yao. Nnakuhakikishia 1961 Kiteto walikuwa wanaishi vizuri zaidi ya walivyoishi 1967-1985, wakati wa dhiki kila upande, si Kiteto tu, Tanzania nzima. Leo unaniambia Kiteto? ni nini unachokitaka Kiteto cha mahitaji ya kila siku ukakikosa leo hii, wamwagie hizi pumba wengine. Usichanganye "culture" ya Wamasai wa Kiteto kuwabeza kuwa wanaishi kama 1961, nenda leo kaone huko huko Kiteto "ma dish ya satellite" mamtandao ya simu na ma "internet". yaliyokuwepo hayo 1961? Nenda kaone Kiteto leo wanavyolima Mahindi, yalikuwepo hayo 1980? Nnakuhakikishia hata gazeti la Ngurumo na Mzalendo walikuwa hawayajui huko wakati wa Nyerere, nani awapelekee?
Isitoshe, hizo Colgate hazishikiki (huku wengine wakitumia vitu mbadala); TV ndio usiseme kwani sio zaiadi ya 12% ya watanzania wana umeme, leave alone uwezo wa kununua TV sets;
Colgate ipo mpaka ya shillingi mi mbili, kama hutaki kuitumia ni mazowea tu lakini sio kuwa hazipo za bei nafuu. Hiyo argument dhaifu.
Umeme wa Tanesco Tanzania unawafikia zaidi ya 14% ya Watanzania, na hiyo hujaongelea wenye majenereta yao huko ambapo haujafika na haujaongelea wanaojifungia "solar" hujaongelea wanaotumia "vinyesi" kuzalisha umeme wao binafsi. TV wanaziona hata ukipita kwenye vitenbe ndani huko unakuta "madish" wanaona ligi ya Uingereza kama wewe uliopo mjini na bado Serikali inafanya kila njia kuwafikishia umeme, tunayaona kila siku.
Well, Nyerere admits hata mwenyewe kwamba kuna mambo ya maana alifayanya na mengine ya kipumbavu lakini akashangaa awamu za mbele yake zinaacha ya maana na kuchukua ya kipumbavu; we can talk about what made him fail lakini sidhani kama ni mahala pake hapa, kwa sasa tuangalie yafuatayo kwa ufupi tu; ila kwa kifupi ni Nyerere alivyokwisha sema -
yanachukuliwa ya kipumbavu, yanaachwa ya maana.
Nyerere aliipokea hii nchi ikiwa na 95% of Tanzanians as wanavijiji, and 5% as urbanites; Sina haja ya kuziweka takwimu hapa kuonyesha ni jinsi gani mpaka anaondoka social development indicators zilivyokuwa juu kama vile literacy rates at upper 60s percent - one of the highest in Africa; Leo hii, illiteracy in Tanzania is about 30%; and about 24% of Tanzanians hawana elimu of any kind (hawajasoma hata darasa la kwanza); tunazidi kushangilia shule za kata from a quantitative side, and we totally ignore the qualitative side of it; social indicators nyingi sana zinawasuta wale wanaosema leo hii tumepiga hatua kuliko enzi za Mwalimu kijamii tukitazama suala la afya, elimu in qualitative terms hakuna la maana sasa compared to zamani, ila kama hoja zenu ni quantitative, Hurray, mmewapata wajinga.
Ndio maana kwa sasa Serikali hawa "invest" kipumbavu. Hilo ni jibu kwa hayo ya Nyerere hapo juu.
Uchumi wa Mwalimu ulikuwa una trickle down to the 95% of the rural masses, huu wa sasa sio pro poor growth na hatuna haja ya kuweka takwimu hapa kuonyesha hilo kwani zipo wazi kila sehemu; Mpaka mwaka 1985 wakati Mwalimu anaondoka, Tangia Mwalimu kaondoka, hakuna much changes katika composition mfano ya manufacturing on GDP as we can see kwenye figures (see table below);
Hakuna uchumi wa Nyerere " economy wise he was a total failure" kaacha nchi haina "reserve" hata senti moja na BOT imechomwa moto, na akakaa kimya hamna uchunguzi wala kusema ni nini kilichoisibu BOT , au hulijui hilo?
Kilimo - mhango wa kilimo kwenye GDP umepungua na kufikia 28.9%; kwa kawaida hii huwa ni ishara nzuri lakini pale tu kama Kilimo ndicho kinachozalisha then tukipata earnings from there ndio ziende kuamsha na kuendeleza sectors nyingine kama viwanda, mining etc, hivyo ndivyo economic development comes about na ndivyo nchi zote zilianza na kilimo na later kuwa industrialized; hivyo ndivyo green reveolution occurs increase in productivity ya kilimo, then kizalishe na kuleta hela kwa wingi na hela hizo ziwe invested kufungua sekta nyingine za uchumi (sio kutegemea misaada au wawekezaji kufanya hilo); We see in the table below kwamba between independence and now, imepungua from 48% to around 29%; but hizi namba hazina maana yoyote kwani hazina mahusiano yoyote na kilimo kuwa productive na kutupatia uwezo wa kupata fedha ili zijenge viwanda vyetu, zichimbe madini yetu, zifungue taasisi zetu muhimu za umma; the change from 48% to 29% in agricultural composition kwenye GDP hazina association yoyote katika haya; why? Because we dont invest in zaidi ya Mwalimu alivyokuwa anawekez mkazo; tumebaki na porojo tu za Kilimo Kwanza huku matrekta mengi yakienda kwa watu wasio walengwa; Tuangalie mfano in 1961, agricultural machinery, tractors per 100 sq. km of arable land was 31.8; as of 2004 it was down to 23; productivity ya kilimo compared to miaka ya nyuma imepungua sana ebu fikiria in 1961 Cereal production (metric tons) was 1.1 million; by 2009, that figure had only reached to 6.2 million; mind you, in 1961, population yah ii nchi was around 9million, by 2009, 40million plus; hata tukiangalia annual growth in the kilimo sector (see the table below), hatuna cha ajabu cha kujivunia na kumbeza Mwalimu;
Manufacturing hakuna anything impressive tofauti na Mwalimu Nyerere; at most imezidi kuporomoka; manufacturing composition yake on GDP haina tofauti sana na miaka ya nyuma nab ado hatujafikia kiwango cha Mwalimu cha 10.8% (see table below);
Service Sector hakuna ubishi kwamba hii sekta imepanuka zaidi kuliko wakati wa Mwalimu lakini tusisahau kwamba service economy is a new phenomenon, hata nchi zilizoendelea halikuwa jambo la maana zaidi ya industrialization Kwahiyo kwa uwezo wake na bidii yake, a 22% level ya Mwalimu during the 1970 1980 period inastahili pongezi;
| Year | Kilimo as % of GDP | Kilimo annual growth rate | Manufacturing as % of GDP | Manufacturing growth rate | Service Sector % of GDP | Service sector growth rate |
| 1960 1970 (Nyerere) | 43.6% | 3.7% | 8.7% | 10.4% | 15.7% | 7.2% |
| 1970 1980 (Nyerere) | 43.4% | 3.4% | 10.3% | 4.4% | 22% | 15.7% |
| 2006 | 30.4% | 3.8 | 8.5% | 8.4% | 46.7% | 7.1% |
| 2007 | 29.6% | 4.0 | 8.5% | 8.7% | 46.7% | 8.4% |
| 2008 | 29.7% | 4.5 | 8.6% | 9.9% | 47.1% | 7.9% |
| 2009 | 28.7% | 3.2 | 9.5% | 8% | 46.9% | 7.1% |
Source: Various World Development Reports
Napenda kuzidi kusisitiza kwamba kinachofanya watu waone kuna mabadiliko katika pato la taifa (GDP) ni mchango wa sekta ya madini katika GDP, but the question comes this production is for who? Mwalimu aliamua madini yasiguswe kwani yatakuwa abused hivyo yakae tu huko chini kwani hayaozi mpaka watanzania waweze produce wataalum wa kuyafanyia kazi wao wenyewe na kwa faida yao wenyewe; sasa yanaguswa na wawekezaji, na yanakuwa abused, ndio tunashangilia economic growth ya over 6% since mwaka 2000 kama ni mafanikio wakati hii inatokana na mchango wa madini in terms of production peke yake, not income from the sekta? Huu ndio uchumi uchwara.
Its obvious kuna watu wanadanganyika sana na GDP growth bila kuangalia nini kimeipelekea ku behave that way: angalieni hali za wananchi kama zinabadilika, na sio wa mjini, the 70% plus in rual areas! Otherwise hakuna that much of a difference between miaka ya Mwalimu sasa, especially in his first 20 years in terms of Maendeleo na mchango wa kilimo, manfucaturing;
Ni muhimu lakini tukaangalia impact ya kilimo on GDP kushuka from 48% to 29%; again, kwa kawaida haya ni Maendeleo lakini tumeone kwetu sisi hakuna lolote hapo; inatakiwa composition ya GDP ikishuka, kwingine ipande na ajira kwenye hizo sekta nyingine kama viwanda, mining, services zipande; ebu tazama jedwali la hapo chini la hali ya sasa relative to ile ya Mwalimu where about 80% of the labour force was in the agricultural sector, je leo tumepiga hatua kweli?
Table1: Employment in Tanzania According to Sectors (%)
| SECTOR | DAR-ES-SALAAM (%) | OTHER URBAN AREAS (%) | RURAL AREAS (%) | TOTAL(%) |
| Agriculture, Hunting, Forests | 7.1 | 38.0 | 81.8 | 67.9 |
| Fishing | 0.5 | 1.3 | 1.4 | 1.3 |
| Mining | 0.5 | 2.6 | 0.6 | 0.9 |
| Manufacturing | 4.2 | 3.9 | 0.6 | 1.4 |
| Production of electricity, gas and water | 1.0 | 0.9 | 0.5 | 0.6 |
| Construction | 4.6 | 2.8 | 1.0 | 1.6 |
| Trade (retail and wholesale) | 27.9 | 18.6 | 3.6 | 8.3 |
| Hotel and restaurants | 4.5 | 3.3 | 0.6 | 1.4 |
| Transport and communication | 6.7 | 2.9 | 0.4 | 1.4 |
| Financial services | 0.7 | 0.2 | 0.1 | 0.1 |
| Estate leasing | 0.3 | 0.2 | 0.1 | 0.1 |
| Administration, Defence and Public safety | 5.4 | 3.2 | 0.5 | 1.4 |
| Education | 2.3 | 2.6 | 1.1 | 1.4 |
| Health and social welfare | 1.8 | 1.8 | 0.4 | 0.7 |
| Other services | 30.3 | 15.5 | 6.9 | 10.4 |
| Private household employing other persons | 2.1 | 2.1 | 0.4 | 0.9 |
| Diplomatic offices and foreign service organizations | 0.1 | 0.1 | 0.0 | 0.0 |
| Total | 100.0 | 100.0 | 100.0 | 100.0 |
Source: Household Budget Survey + World Bank Data.
The table above proves kwamba GDP composition imeshuka from 48% to 29% sio kwa sababu ajira kwingine zimeongezeka kutokana na mafanikio ya kilimo (agricultural revolution) ambayo yamesaidia kupanua sekta nyingine; instead, ukweli ni kwamba kushuka kwa hii composition ni kwamba watanzania wengi vijijini wamekimbia kilimo kwasababu hakilipi, lakini kama tunavyoona kwenye hizo figures, hawajaenda kwenye viwanda wala service sector wala madini bali kwenye informal sector huko ambapo the so called service sector inawabeba kama wauza vocha, maji ya uhai, magazeti na wabeba zege;
Faizyfoxx, pia on your point kwamba:
It is highly suicidal to economize on expenditures to your economy, to fuel economic growth you have to be extravagant in all aspects. How can you have a growth without spending? simple economy rule; "the more you spend the more you earn the more you earn the more you spend". That is the only way you can measure your growth, you can never ever measure growth by not spending. Be real.
Hata sijui nianzie wapi kukujibu hili, na wengi sana humu tayari wamelielezea sana; cha ajabu ni kwamba, ni wazo hili hili ulilonalo hapa ndilo linalotupelekea sisi kama nchi kufilisika kiuchumi kwani tunakopa kuliko tunavyoweza lipa na tunatumia kuliko tunavyoingiza
Hizo takwimu zako zote pumba tupu, mchele tumekuwekea juu huko kajibu kwanza.