[FONT=Book Antiqua, serif]TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS, IKULU.
[FONT=Book Antiqua, serif]KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Wilboard Slaa, leo, Jumapili, Januari 2, 2011, amekaririwa na Gazeti la Tanzania Daima, linalomikiwa na chama chake hicho, akidai kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya Dowans.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Huu ni uongo wa mchana, ni uzushi wa karne na propaganda ya hatari. Kwa hakika na kwa namna isiyoweza kuelezeka kwa ufasaha, tumeshtushwa sana na kauli hii ya Dkt. Slaa na hatutaki kuamini kabisa wala kukubali kuwa ni kweli kauli hii imetolewa na mtu ambaye majuzi tu alikuwa akiwania kuwa kiongozi wa juu wa taifa letu, yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Na kama kweli Dkt. Slaa ametoa kauli hii na kusema maneno ya namna hii basi sasa Watanzania wanayo kila sababu na haki ya kuamini kuliko wakati mwingine wowote kuwa mzee huyu sasa amechanganyikiwa na ni mtu wa hatari sana kwa utulivu wa nchi hii. Kwa nini?[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Sababu ni rahisi sana. Mheshimiwa Rais Kikwete siyo mmiliki wa Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya Dowans. Hakupata kuwa mmiliki, siyo mmiliki na wala hatakuwa, hata siku moja, mmiliki wa Kampuni hii. [/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Kama Dkt. Slaa anataka kweli kujua wamiliki wa Kampuni ya Dowans, basi atafute ukweli huo na aachae tabia ya kutapatapa na udhabinadhabina yenye lengo la kuwapaka watu watope. Tabia ya kuwasingizia na kusema uongo kuhusu viongozi wa taifa letu ni tabia ya hatari.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Mheshimiwa Rais Kikwete hahusiki na Kampuni ya Dowans wala na kampuni nyingine yoyote ya kibiashara. Yeye ni kiongozi wa juu kabisa wa siasa wa nchi yetu na siyo heshima wala haki kumhusisha na jambo la kutunga na kuzua na lisilokuwa la ukweli wowote.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Kiongozi huyo wa upinzani ametoa shutuma zake dhidi ya Rais Kikwete kufuatia Kampuni ya Dowans kulishitaki Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) na Mahakama hiyo ikaamua kuwa Dowans ilipwe kiasi cha sh bilioni 185.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Dkt. Slaa amezomoko na kumshutumu Rais Kikwete eti kwa sababu Mheshimiwa Rais hakuzungumzia suala hilo katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Ijumaa iliyopita.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Mwaka huu, Dkt Slaa aliwania urais wa Tanzania kupitia CHADEMA na akashindwa vibaya sana. Tokea wakati huo amekuwa mtu wa kutunga na kuzua stori za kila aina ya uongo na umbea kuwachanganya Watanzania kwa sababu ya kinyongo chake cha kushindwa. [/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Tunapenda kuwataka na kuwaomba Watanzania, kama ambavyo wamekuwa wanapuuza uongo na uzushi mwingine wa mara kwa mara wa Dkt. Slaa, waupuuze uzushi na uongo wa sasa kuhusu miliki ya Dowans. Ni sehemu ya tabia iliyoanza kuzoeleka sasa ya Mzee huyo kutapatapa kisiasa.[/FONT]
[FONT=Book Antiqua, serif]Imetolewa na Salva Rweyemamu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais - Ikulu[/FONT][/FONT]
Sikuwahi kutegemea kwamba Salva rweyemamu ni mtu mwenye fitina na hasira namna hii nadhani hasira zake zinajibu hali halisi aliyonayo jakaya kwa wakati huu,kikwete na Slaa wanapishana miaka miwili kwa umri namna nyingine wako umri mmoja kumuita Mzee ni kweli ni mzee lakini salva anataka kutuaminisha kwamba amezeeka hana akili ya kufikiri na kama ni hivyo hofu yetu kwa kikwete kwamba hana akili Salva anaithibitisha
aanaposema kiongozi wa juu sana wa nchi hapaswi kusemwa anataka kutuambia kuwa Kikwete yuko juu ya sheria na ndio maana anafanya kila anachokifanya kufuja rasilimali zanchi kwa sababu anajiona yuko juu ya sheria
jamani salva anasema amezomoka hivi hili ni neno la kiswahili
pia anasema dr Slaa atafute wamiliki wa Dowans kwa nini kurugenzi ya mawasiliano wasituambie wamiliki halisi wa Dowans hivi anadhani sisi wananchi ni mazumbukuku hatujui kuchambua mbichi na mbivu unakataa kusema Raisi Kikwete sio mmliki wa Dowans halafu husemi mmiliki halisi ni nani jibu sisi tunaosoma waraka wake ni kwamba mmiliki ni raisi kikwete bila kificho ila yeye Salva anaendekeza propaganda