GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Hivi inakuwaje nchi inakuwa na watu 'wazushi' na 'vizabizabina' na ambao ni hatari kwa 'usalama wa taifa' lakini wakati huo huo hawakamatwi na vyombo vya usalama? Kama Dr. Slaa ni mtu wa namna hiyo kwa nini hawamkamati? Mimi nashindwa kuelewa hapo! Lakini mkuu wa nchi alipata kusema kuwa 'ukiambiwa kitu jaribu kuchanganya na za kwako'!!
Yaani baada ya kushindwa URAIS, kwenye uchaguzi ulio huru na wa haki, Slaa na wapenzi/wanachama wake wamechanganyikiwa kabisa, hawajui wafanyalo wala wafikirialo. Kila siku ni majungu, fitina, uzushi, uzabizabina, unafiki. Kweli CDM si chama cha kuliongoza taifa hili kamwe, Mungu tuepushe nacho, amen !