Ikiwezekana, Bunge lianze na mswada wa dharura kujadili Katiba Mpya; hii Katiba ya sasa kitendo cha Makamu kutambuliwa kuwa mrithi ni hatari

Suala la katiba lipewe kipaumbele sana.

Katiba ni uhai.

Yapo mengi ya hatari sana kwenye katiba hii.

Lakini hili la Mrithi wa rais anayefariki dunia, kuwa ni makamu wa rais (automated) ni hatari sana kwa marais endapo tukipata Makamu asiyemwaminifu.

Pia linachangia sana kumuweka mbali makamu wa rais kuwa karibu na rais kwa hofu ya kutoaminia! (Naturally internal conflict)

Kwa gharama yoyote naomba tuanze na katiba inafaida kwetu sote matajiri na masikini, viongozi na watawaliwa.
Hapana mimi nashauri Bunge lianze kwa kupokea na kujadili Mswada wa Bima ya Afya Kwa Wote (Universal Health Coverage Bill).Hili kwangu na kwa Watanzania wengi ni la muhimu na la haraka sana kuliko la Katiba Mpya, ambalo, kwa kweli ni la viongozi wa CHADEMA tu kwani hata wanachama wao huko Mwanza na Iringa au Mbeya wamewakana na kuwataka viongozi wao waanzie na Katiba yao, ya CHADEMA, kwanza kabla ya hii wanayotaka.
 
Yaani Rais anayechaguliwa kama atamchagua makamu wake mtu ambaye anataka kumuua hakuna wa kulaumu! itakuwa ujinga wa ngazi ya juu
Kwani kuna ajuaye mtu mwingine alichonuia moyoni? Mtu anauawa na mke aliyemchagua mwenyewe tena aliyempenda kwa mapenzi motomoto, sembuse hao waliochaguana kimaslahi tu?
 
Ni bahati nzuri kwamba safari hii aliyeupitia uchochoro huo kapita bila kukusudia, hakupanga iwe hivyo. Lakini natabiri kuwa baada ya watu kuuona uwezekano huo kuna watu wataanza kuufanya uwe mojawapo ya mikakati yao. Hii ni hatari kwa rais aliyeko madarakani. Nashauri utaratibu huu ufutwe haraka kwa maslahi ya taifa.
Makamu wa Rais abaki na nafasi yake hiyohiyo, akitaka urais asubiri muda ufike agombee.
Ikitokea bahati mbaya kama iliyotokea kwa hayati JPM, basi makamu awe kaimu rais kwa muda maalum (kama mwezi tu), chama chake kiteue mtu mwingine kwa utaratibu rasmi, jina lipelekwe bungeni kuthibitishwa awe rais hadi muda wa uchaguzi mkuu kwa mujibu wa kalenda utakapowadia.

Kwani huu uchochoro ni mpya? Hakuna mtu aliyewahi kuwa VP ambaye alikuwa haijui hiyo constitutional line of succession!
 
Kwani huu uchochoro ni mpya? Hakuna mtu aliyewahi kuwa VP ambaye alikuwa haijui hiyo constitutional line of succession!
Hawakuwahi kupata fursa ya kuitumia. Au hawakuwa na tamaa. Hatuwezi kujua yajayo, labda atatokea atakayekusudia kuitumia, of course akiwa na back up ya wanaoamini kuwa watafaidika pamoja naye.
Usipoziba ufa utajenga ukuta.
 
Hawakuwahi kupata fursa ya kuitumia. Au hawakuwa na tamaa. Hatuwezi kujua yajayo, labda atatokea atakayekusudia kuitumia, of course akiwa na back up ya wanaoamini kuwa watafaidika pamoja naye.
Usipoziba ufa utajenga ukuta.

Huu sio ufa. Line of succession kama hii ipo hata kwenye nchi nyingine nyingi. Hakuna ushahidi kwamba imewahi kuwa abused mahali fulani.
 
Hata makamu kutajwa na jambazi mahakamani ni aibu kubwa alipaswa ajiuzulu mana alishiriki ujambazi wa kidola alipokua waziri.
Watanzani tumekubali kuwapa waovu nchi iliyoumbwa na Mungu mwenye sifa zote za haki na utakatifu kuwa mali yao.

Katiba kamwe haitapatikana chini ya CCM ,labda jeshi liwe limeshika nchi kwa muda ili lisimamie hawa wanasiasa wanaoua maslahi ya nchi kwa kulinda vyama vyao huku majeshi yetu wakitumika kama manamba na maslahi duni tofauti na wanasiasa waliojaa ubinafsi na starehe kupitiliza.
Watu wanalesha kwenye mabaa na magesti mwaka mzima halafu tutegemee wapate muda wa kufikiri mustakabali wa nchi.?
Haiwezekani !

Hakuna katiba mpya itakayosimamiwa na wanasiasa hawa wanaowaza kuitafuna nchi.

Katiba ya Warioba imejaa mambo mengi ya msingi lakini wapuuzi na vyama vyao waliona mambo mawili tu :- Serikali mbili,serikali tatu na madaraka ya kuingia ikulu( madaraka).
Hawana muda wa kujadili maslahi ya umma kama makazi bora , ardhi na rasilimali za asili kuwanufaisha wote mana ni mali ya Mungu. Kodi ndio ijenge barabara ila gesi,wanyama ,madini, misitu, mafuta,mlima kilimanjaro n.k. iwe na fungu la kumpa kila mtanzania asiye na ajira wala kumiliki ardhi na nyumba yenye thamani kubwa.

Ujinga wa wanasiasa ulipelekea Dr. Mvungi akauwawa na majambazi ya kisiasa yasiyotaka katiba mpya kwa sababu alikataa kununuliwa . Alisema ni bora abaki jalalani kuliko kusaliti kazi nzuri ya Tume ya Warioba.

Lakini pia suala la Serikali Tatu na mbili ni upuuzi tu mana maendeleo hayawezi kuletwa na Wahuni hata pangekua na serikali mia moja.
Maendeleo yataletwa na watu waaminifu ,wachamungu wa kweli na watenda haki sio magavana wahalifu na wale kama walivyotajwa na Sabaya mhalifu aliyetumia uhalifu kulinda mali za Chama badala ya kwenda mahakamani.
Hata wao hawaiamini mahakama zaidi ya kufanya ujambazi wa kidola kwa wanaowatuhumu kukwepa kodi . Mtu kama amekwepa kodi au ameiba mali za chama alipaswa ashitakiwe mahakamani na sio kupigwa au kutishiwa maisha.

Kuliko kuibadili katiba hii chini ya mivutano ya Chadema na CCM na vyama visivyo na msimamo vinavyokaa katikati kusubiri mshindi waungane naye ni bora tubaki na hii iliyotungwa wakati wa Mwalimu akiwa hai. Kidogo wale waasisi walikua na ubinadam na kujali utaifa.
Hawa CCM madaraka na Chadema wajuaji wa kila kitu hawatatuletea Kamwe katiba mpya labda Mungu aingilie kati itokee serikali ya mpito chini ya majenerali wa Jeshi.
Eti nchi imekaa kimya inawasikiliza familia ya kina Gwajima na wale wasemaji wa vyama sijui kijana gani yule na makatibu wake waajabu ajabu. Kweli tutegemee Katiba mpya. ?
Tumtegemee mtu mmoja kama Mungu ndio ikimpendeza alete katiba mpya?? Duuh,
Bora tumtegemee Mungu asimame mwenyewe mana hatishwi,hahongwi, haogopi, hashindwi, hadhulumu , hasemi uongo na hadanganywi na yeyote.
 
Ni bahati nzuri kwamba safari hii aliyeupitia uchochoro huo kapita bila kukusudia, hakupanga iwe hivyo. Lakini natabiri kuwa baada ya watu kuuona uwezekano huo kuna watu wataanza kuufanya uwe mojawapo ya mikakati yao. Hii ni hatari kwa rais aliyeko madarakani. Nashauri utaratibu huu ufutwe haraka kwa maslahi ya taifa.
Makamu wa Rais abaki na nafasi yake hiyohiyo, akitaka urais asubiri muda ufike agombee.
Ikitokea bahati mbaya kama iliyotokea kwa hayati JPM, basi makamu awe kaimu rais kwa muda maalum (kama mwezi tu), chama chake kiteue mtu mwingine kwa utaratibu rasmi, jina lipelekwe bungeni kuthibitishwa awe rais hadi muda wa uchaguzi mkuu kwa mujibu wa kalenda utakapowadia.
Mataga wanasoma tu
 
Back
Top Bottom