Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,425
Asalaam Aleykhum , Ukweli ambao uko wazi ni huu , sisi Watanzania hatuna nchi nyingine zaidi ya hii tuliyomo , tunayoishi , hii ambayo wamezikwa wazazi wetu na ndugu zetu
Nachukua nafasi hii katika hii ijumaa ya kwanza ya mwaka , kuwaomba watukufu Waislam kuiombea nchi hii katika haki na kweli , na hasa kwenye masuala yote yanayohusu uchaguzi , masuala ya Uchaguzi ndio chimbuko kuu la uvunjifu wa amani na mauaji kwenye nchi nyingi Duniani .
Tuombe sana Allah awape uvumilivu viongozi wetu ili waweze kukubali kuwa na uchaguzi ulio huru na haki , Kila siku siyo jana , kwamba unaweza kufanya yaleyale na Wananchi wakanyamaza .
Wabhillah Tawfiq