Konny Joseph
Member
- Aug 28, 2016
- 81
- 133
Kumekuwa na dhana inayotengenezwa na serikali ya CCM kwamba kwa kuwa Mwenyekiti wa NEC ni mtu mwenye nyadhifa ya ujaji basi ni wazi kwamba maamuzi yote atakayoyapitisha yatakua ni haki,na hayapaswi kupingwa na mtu yeyote au chombo chochote.
Jamii inapaswa ielewe kwamba heshima ya maamuzi ya jaji inapatikana pale tu Jaji anapokalia kiti cha Mahakama au chombo mfano wa mahakama kama Tume ya Maadili ya Mawakili kupitisha maamuzi.
Maamuzi ya ujaji hayatopatikana ikiwa mtu anatekeleza majukumu mengine nje ya mahakama,kama kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Mwanassheria Mkuu au Mwendesha Mashitaka Mkuu.
Nadharia hii potofu ndio imekuwa inatumiwa na serikali ya CCM kupinga hoja ya maamuzi ya Tume ya Uchaguzi kupingwa Mahakamani kwa kisingizio kwamba maamuzi ya tume yametolewa na mtu mwenye nyadhifa ya ujaji.
Hiki ni kiini macho cha wazi amabacho serikali ya CCM wamekitengeneza ili kulaghai umma kuwa maamuzi yote ya tume yatakuwa halali kwa kutumia kigezo hicho bandia.
Ieleweke kwamba chombo chenye mamlaka ya kutoa haki ni Mahakama peke yakekwa mujibu wa katiba.Tunaposema mahakama ni pale jaji wanapokalia kiti cha mahakama katika kutoa haki.Hii haina maana kwamba mtu mwenye sifa ya jaji anaweza kutoa haki nje ya mipaka ya kimahakama.
Na ndio maana hata kinga ya majaji na mahakaimu inapatikana pale tu wanapokuwa wanatekeleza majukumu ya kimahakama na sio vyenginevo.
Hivyo ni wazi kwamba maamuzi ya Tume ya Uchaguzi yanapaswa kupingwa katika mahakama za kisheria kama zilivo katika nchi nyingi duniani.
Tume kuongozwa na jaji hakuipi tune mamlaka ya kimahakama ya kutoa haki.Hivyo mamamuzi yake hayawezi kuhesabiwa kuwa ni maamuzi ya haki kamwe.
Jamii inapaswa ielewe kwamba heshima ya maamuzi ya jaji inapatikana pale tu Jaji anapokalia kiti cha Mahakama au chombo mfano wa mahakama kama Tume ya Maadili ya Mawakili kupitisha maamuzi.
Maamuzi ya ujaji hayatopatikana ikiwa mtu anatekeleza majukumu mengine nje ya mahakama,kama kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Mwanassheria Mkuu au Mwendesha Mashitaka Mkuu.
Nadharia hii potofu ndio imekuwa inatumiwa na serikali ya CCM kupinga hoja ya maamuzi ya Tume ya Uchaguzi kupingwa Mahakamani kwa kisingizio kwamba maamuzi ya tume yametolewa na mtu mwenye nyadhifa ya ujaji.
Hiki ni kiini macho cha wazi amabacho serikali ya CCM wamekitengeneza ili kulaghai umma kuwa maamuzi yote ya tume yatakuwa halali kwa kutumia kigezo hicho bandia.
Ieleweke kwamba chombo chenye mamlaka ya kutoa haki ni Mahakama peke yakekwa mujibu wa katiba.Tunaposema mahakama ni pale jaji wanapokalia kiti cha mahakama katika kutoa haki.Hii haina maana kwamba mtu mwenye sifa ya jaji anaweza kutoa haki nje ya mipaka ya kimahakama.
Na ndio maana hata kinga ya majaji na mahakaimu inapatikana pale tu wanapokuwa wanatekeleza majukumu ya kimahakama na sio vyenginevo.
Hivyo ni wazi kwamba maamuzi ya Tume ya Uchaguzi yanapaswa kupingwa katika mahakama za kisheria kama zilivo katika nchi nyingi duniani.
Tume kuongozwa na jaji hakuipi tune mamlaka ya kimahakama ya kutoa haki.Hivyo mamamuzi yake hayawezi kuhesabiwa kuwa ni maamuzi ya haki kamwe.