Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

Pasco alipigwa changa la macho, eti nilipangiwa kiti nyuma, khaa! Katibu Mkuu?
 
hapo inavyoonekana hata JK kamkwepa Dr. wa ukweli.
possible waandishi na makanjanja wa CCM wamejiandaa vilivyo kusubiri Dr. wa ukweli asalimiane na JK ili wapate cha kuandika kukisafisha chama chao, loh! DR. ni mjanja sijapata kuona, hata Nyerere asingekubali kusalimiana na mtu km JK.
 
Ha ha ha! odds za mwana JF's of being struck by lighting in their lifetime is higher than those Dr's kukutana teh teh te!

Yani chances za mwana JF kuwa struck na lighting ni higher zaidi ya Dr Kikwete na Dr Slaa kukutana...?

Really? what are the odds kama kweli ni coincidental?lol
 
On the other note, nakubali Pasco hakutendewa haki.

Ndo ukweli huo.

@Saint Ivuga, i hope you keep your fingers crossed huyo mod awe amelala.lol
 
kwani hawa waandishi walioandika hii habari wanatofauti gani na Pasco? na isitoshe hakuna sehemu waliomhoji dk Slaa hapo

Hivi mnamtegemea

1. Dr Slaa anaweza kukiri mbele ya mwandishi wa habari kuwa anampiga chenga JK hata kama ni kweli?
2. Dr. Slaa kupangiwa kiti cha nyuma kwenye tukio kama lile wakati yeye ni Katibu Mkuu wa Chama?
 
ana haki yakumpiga chenga, wangesalimiana tu, loh! picha zingepigwa nyingi kuliko hata za matukio mengine yote, na leo kwenye hilo hilo gazeti labda walikuwa wameshaandaa heading, Dr. Slaa akubali yaishe kwa JK, sasa amtambua km rais, ................na udaku kibao ungeandikwa kisa kusalimiana tu, hope hata mkuu wa kaya alishauriwa na wasaidizi wake kuwa wakati wakuuza chama ndo huu, hakikisha unapeana mkono na Dr. shubutuuuuuuu.....Dr. kashtuka ujanja wenu.
 
Saint Ivuga, hivi bado tuko siasa, maana thread ikihamishwa unashangaa wakati wa ku scroll down unaona majina ya tofauti, hapo ujuwe upo anga nyingine,ushabebwa juu juu, ngoja nicheki juu kama bado tuko siasa.lol
 
Hilo nakubali, ni heri hata wangeipeleka hoja mchanganyiko bana.

Maybe mods wana sababu nzuri na "madhali wamekabidhiwa rungu, tuombe tu Mungu wawe na akili timamu."

Kuna threads kibao ziko Sisa na ni waay more "chity chaty" than this one

Especially with the fact that Pasco alimuhoji Dr Slaa, mambo mengine mnamwaribia Dr badala ya kumjengea.
Hawa jamaa wanaweza kuwa ma-Salva 2015!
Biased.
 
Hilo nakubali, ni heri hata wangeipeleka hoja mchanganyiko bana.

Maybe mods wana sababu nzuri na "madhali wamekabidhiwa rungu, tuombe tu Mungu wawe na akili timamu."

Kuna threads kibao ziko Sisa na ni waay more "chity chaty" than this one

Especially with the fact that Pasco alimuhoji Dr Slaa, mambo mengine mnamwaribia Dr badala ya kumjengea.

Kama story hii imetoka kwenye magazeti, ni bora maelezo ya Pasco kwa sababu tunaweza kumhoji, na kupata ukweli zaidi kama alivyokuja na updates kuwa alimhoji Dr.Slaa. Tungeweza pia kuhoji kiti kilichokuwa wazi pale mstari wa mbele baada ya Mbowe kilikuwa cha nani, na masuala mengine kama hayo lakini sasa tunalazimika kuchanganya na za kwetu tu na kulichukua gazeti at face value

Huyu Mod aliyeihamishia Chit Chat aliboogie
 
mkuu, nadhani hapo penye bold ndiopenye majibu sahihi................

lakini naomba nikuulize, ....................... ni kwa nini unadhani dr ndiye kasusa na hudhani hata kidogo kuwa (huenda) jk kaambia watu wake kuwa hataki kumshika mkono huyo mtu???...................... nakuomba ujaribu kuwa neutral kidogo ili tupate habari isiyoegemea upande wowote..................

pole na hekaheka za ifakara mkuu....................... RIP regia.......................

slaa anaogopa pollonium ya mwakyembe.
 
nashukuru angalau kamtambua kwamba JK ni rais, kajifunza mengi Ifakara naamini akirudi Ifakara hatakuwa tena yule Dk Slaa tunaemjua, yaani No RESEARCH, NO EVIDANCE

Wewe umejuaje kama hata kuwa yule yule wakati bado hajarudi? Kwanza 'EVIDANCE' ndio nini?
 
What is the big deal Kikwete na Dr Slaa kusalimiana? Itabadili nini? Afu hao waandishi kwanini hawakubalance story? Tena pande zote Kikwete na Dr Slaa? Huu ni mfumo wa habari za udaku?
 
Update.
Nimekuta na Dr. Slaa mahali na kupata fursa ya kumuuliza yale maswali yangu yaliyobakia.

Amenithibitishia kuwa hajawahi kumkacha Jk hata mara moja, bali imekuwa ikitokea by chances tuu hawajakutana!,

Hivyo ile dhana yangu ya muendelezo wa misuso nimeifuta.

Asanteni kwa kunielewa!.

Pasco!.

Asante pia kwa kutafuta na kupata ufafanuzi. Kuna gazeti leo limeripoti haya mambo ya JK na Dr Slaa kukwepana. Sijui ni lini haya magazeti yataitumia Jf kama source ya habari zao kwa uwazi na kuitaja bila kificho.
 
AKWEPA KUKAA JUKWAA KUU,

WENGI WAMZIKA REGIA Juma Mtanda na Shakila Nyerere, Ifakara KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willbrod Slaa, jana alimkwepa tena Rais Jakaya Kikwete safari hii ikiwa katika mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya chama hicho, Regia Mtema yaliyofanyika katika Kijiji cha Lipangalala.

Tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010, ambao Dk Slaa alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 2,271,941 sawa na asilimia 26.34 akiwa nyuma ya Rais Kikwete aliyepata kura 5,276,827 sawa na asilimia 61.17, Dk Slaa hakuwahi kukutana na mkuu huyo wa nchi ana kwa ana. Katika hafla ya kutangazwa matokeo ya urais iliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam, Dk Slaa hakuhudhuria tofauti na ilivyokuwa kwa waliokuwa wagombea wenzake wote.

Jana, Dk Slaa tofauti na viongozi wenzake wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, hakutaka kujiweka katika mazingira ambayo yangemkutanisha na Rais Kikwete katika mazishi hayo. Nyumba kulikofanyika shughuli za awali za mazishi, waandalizi waliandaa majukwaa mawili, moja maalum kwa ajili ya wabunge huku jingine likiwa ni maalumu kwa ajili ya viongozi wakuu ambalo alikaa Mbowe, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe. Mbali ya kukaa viongozi hao, kulikuwa na nafasi ambayo ilikuwa imetengwa maalumu kwa ajili ya Rais.

Mbali ya nafasi hiyo, pia kulikuwa na kiti ambacho ilitegemewa kwamba Dk Slaa angekalia. Hata hivyo, Katibu Mkuu huyo wa Chadema alikikwepa na kwenda kujichanganya katika jukwaa la wabunge na kiti hicho kubaki bila ya kuwa na mtu. Hata hivyo, Rais Kikwete hakuweza kufika nyumbani hadi mwili wa marehemu Regia ulipopelekwa katika Viwanya vya Viungani ambako uliagwa na mamia ya waombolezaji. Uwanjani hapo nako kulikuwa na majukwaa mawili.

Kama ilivyokuwa nyumbani, jukwaa moja lilikuwa la wabunge na jingine la viongozi wa ngazi za juu lakini bado, Dk Slaa alilikwepa jukwaa hilo ambalo Rais alitarajiwa kuwa angefikia. Rais hakuweza kufika Viungani pia. [Rais Jakaya Kikwete akiweka udongo kwenye kaburi la aliyekuwa mbunge wa viti maalum (Chadema) Regia Mtema wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Ipangalala Ifakara mkoani Morogoro jana.

Picha na Juma Mtanda] Rais Jakaya Kikwete akiweka udongo kwenye kaburi la aliyekuwa mbunge wa viti maalum (Chadema) Regia Mtema wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Ipangalala Ifakara mkoani Morogoro jana.

Picha na Juma Mtanda Baadaye wakiwa eneo la mazishi, Rais Kikwete alifika na kushiriki tukio hilo na kisha kusalimiana na wabunge mbalimbali na viongozi waliokuwa wamefika akiwemo Mbowe, Mbunge wa Rombo Joseph Selasini, Zitto na viongozi wengine lakini Dk Slaa hakuonekana.

Ilitegemewa kuwa tukio hilo la msiba lingewaleta wanasiasa hao lakini hadi Rais Kikwete alipoondoka hakuna mahali ambako walisalimiana. Mbali ya tukio hilo, hata katika hafla mbalimbali ambazo viongozi wa Chadema wamekuwa wakialikwa ikiwemo Ikulu, Dk Slaa hakuwahi kuhudhuria.

Novemba mwaka jana viongozi wa Chadema wakiongozwa na Mbowe, walifanya mazungumzo na Rais Kikwete, Ikulu ya Dar es Salaam kujadili suala la Katiba Mpya, lakini Dk Slaa hakuhudhuria.
 
Back
Top Bottom