Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

Ifakara: Dr. Slaa Hakusalimiana na JK! Kwanini?

View attachment 45696

Hili ni Jukwaa alilokuwa amekaa Dr Slaa na huyo nyuma ni bodyguard wake pia kwenye jukwaa hili walikuwa wamekaa Lema, Josephine na wabunge wengine wa vyama vya upinzani sasa anayesema kuwa alipangiwa kiti cha nyuma aeleze vizuri
Nimekupata mkuu, tumsubiri Pasco, kama alivyosema Gaijin hapo nyuma, Pasco alisema kwamba alimuhoji Dr Slaa na kwamba Dr Slaa alisema kuwa yeye alipangiwa viti vya nyuma na hakuona umuhimu wa kwenda huko mbele kwa ajili ya kupeana mkono na Dr Jk.

Labda mods waligunduwa si kweli ndo maana wakaona ni porojo ya chit chat.
 
Evidence ipo, ila Dr.Slaa hajijui alipopangiwa hata aseme alipangiwa kiti cha nyuma? Au ndio Pasco katudanganya?
Gee labda kama alitafsiri vibaya maana kila mtu aliyekuwepo kwenye mazishi pale makaburini aliona jinsi sitting arrangement ilivyokuwa
 
View attachment 45697

Na huyo ni JK aliyekuwa amekaa Jukwaa kuu kulia kwake alikuwa amekaa Anna Makinda na kushoto kwake alikuwa amekaa mkuu wa mkoa wa Morogoro akifuatiwa na Mbowe halafu Zitto Kabwe, nyuma ya Kikwete kulikuwa kuna hao watu wa Usalama wa Taifa kama unavyoona sasa anayesema Slaa alikaa kitu cha nyuma atueleze vizuri
Ok, tumsubiri Pasco, inaonyesha walipangiwa majukwaa ya tofauti, lakini pia kumbuka kwenye mazishi haya, walikuwa na nafasi za kukutana mara tatu, mara kadhaa pia inasemekana na Dr Kikwete naye hakuhudhuria.

Bottom line, ma guts tells me possibilties za kukutana zilikuwepo, lakini hawakukutana, coincidence?

Anyone can speculate.
 
asiposalimiana nae nongwa, angesalimiana nae ndo ingekuwa nongwa zaidi, kumtafuta kote huko labda walikuwa wamemuandalia polinium 237, wamemkosa sasa wanapayuka kwenye magazeti.
 
Hapana Finest, wewe unasema ulichokiona, na Pasco ameeleza alichojibiwa na Dr.Slaa

Sasa apparently hivyo vitu havi match at all. Alipangiwa kiti cha nyuma na kuamua kukaa jukwaa jengine au alipangiwa jukwaa jengine na kukaa huko lakini akasahau na kusema alipangiwa kiti cha nyuma? Au yote siyo?
Mkuu nini kinachokufanya uamini aliyokuambia Pasco na sio anayokueleza The finest?
 
Hapana Finest, wewe unasema ulichokiona, na Pasco ameeleza alichojibiwa na Dr.Slaa

Sasa apparently hivyo vitu havi match at all. Alipangiwa kiti cha nyuma na kuamua kukaa jukwaa jengine au alipangiwa jukwaa jengine na kukaa huko lakini akasahau na kusema alipangiwa kiti cha nyuma? Au yote siyo?
Hiyo ya kiti cha nyuma nabakia kucheka sana aisee sababu nakumbuka mpaka Dr Slaa alitueleza hadi scenario ya Tabata ilivyokuwa huku mke wake ambaye pia alikuwepo akatueleza ni kwanini Dr Slaa alifika Tabata amechelewa baada ya JK kuondoka, maana Tabata pia wakati JK alikuja ilikuwa the same story
 
Ok, tumsubiri Pasco, inaonyesha walipangiwa majukwaa ya tofauti, lakini pia kumbuka kwenye mazishi haya, walikuwa na nafasi za kukutana mara tatu, mara kadhaa pia inasemekana na Dr Kikwete naye hakuhudhuria.

Bottom line, ma guts tells me possibilties za kukutana zilikuwepo, lakini hawakukutana, coincidence?

Anyone can speculate.


Kwakuwa raisi Kikwete hakutokea nyumbani na uwanja wa viungani ambako kote huko alikuwa ameandaliwa siti, je tuseme naye alimkwepa Dr. Slaa?
 
Ok, tumsubiri Pasco, inaonyesha walipangiwa majukwaa ya tofauti, lakini pia kumbuka kwenye mazishi haya, walikuwa na nafasi za kukutana mara tatu, mara kadhaa pia inasemekana na Dr Kikwete naye hakuhudhuria.

Bottom line, ma guts tells me possibilties za kukutana zilikuwepo, lakini hawakukutana, coincidence?

Anyone can speculate.
Mushi mimi ninachojiuliza ni kwanini watu wanang'ang'ania Slaa ndio amsalimie Kikwete na isiwe Kikwete kumsalimia Slaa kwenye mazishi wameonana sasa nani aanze kushake hands na mwenzake afterall si wameonana macho kwa macho, mimi naona tatizo hapa ni kushikana mikono ili kesho kwenye vichwa vya habari uone habari ifuatayo..."Slaa amtambua Kikwete kama Rais"......."Slaa hatimaye akubali kushikana mikono na Kikwete" yaani hizi ngonjera za waandishi wa habari sijui zitaisha lini anyways unadhani wao watakula na kupata wapi mishahara wasipoleta habari za namna hiyo
 
hiyo pete aliyovaa ina kijisindano kidogo kinachotoa maji, ilitengenezwa maalum kwa ajili ya salam kwa Dr.Slaa, hata hiyo sura ya JK inadhihirisha alivyofedheheka kumkosa Dr.
Teh teh teh!

Is that possible?
 
hiyo pete aliyovaa ina kijisindano kidogo kinachotoa maji, ilitengenezwa maalum kwa ajili ya salam kwa Dr.Slaa, hata hiyo sura ya JK inadhihirisha alivyofedheheka kumkosa Dr.


Umejuaje kwamba hiyo pete ina kijisindano Zumbe wa muheza? Au na wewe ni insider?
 
Mushi mimi ninachojiuliza ni kwanini watu wanang'ang'ania Slaa ndio amsalimie Kikwete na isiwe Kikwete kumsalimia Slaa kwenye mazishi wameonana sasa nani aanze kushake hands na mwenzake afterall si wameonana macho kwa macho, mimi naona tatizo hapa ni kushikana mikono ili kesho kwenye vichwa vya habari uone habari ifuatayo..."Slaa amtambua Kikwete kama Rais"......."Slaa hatimaye akubali kushikana mikono na Kikwete" yaani hizi ngonjera za waandishi wa habari sijui zitaisha lini anyways unadhani wao watakula na kupata wapi mishahara wasipoleta habari za namna hiyo
Nimekupata mkuu, kumbe walikuwa kwenye proximity ya kuweza kupeana mikono?

Ni vigumu kuamini since yeye pia alikuwa mgombea urais.

My guts tells me Dr ana kamgomo baridi, i stand to be corrected.
 
Yaani waandishi wa habari banaa hii yote ni kwa ajili wauze gazeti tu yaani kilichoandikwa hapa na nilichoona Ifakara ni vitu viwili tofauti Dk Slaa alipangwa kukaa jukwaa jingine na Kikwete jukwaa jingine sasa watu walikuwa wanataka kwamba Slaa anyanyuke ndio akamsalimie JK yaani mimi sijaona mantiki yoyote kwenye hili suala zaidi ya watu kulifanya kubwa ili wauze magazeti yaani ukiwa haupo kwenye eneo la tukio waandishi wa habari wanaandika vitu vya ajabu na uwongo tu ili wauze magazeti.

Yaani mtu umepangwa kukaa jukwaa la kushoto kama ilivyokuwa kwa Dr Slaa halafu Kikwete ndio kakaa jukwaa kuu ambapo alikuwa pamoja na Mbowe, Zitto, Makinda, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Job Ndugai na wengineo sasa mtu unataka kuniambia Dr Slaa atoke jukwaa la kushoto ili tu akamsalimie JK jukwaa kuu naona ndio mawazo ya watu yalivyo ikumbukwe pia kiprotokali pia ilikuwa imepangwa hivyo tulipokutana na Slaa, Pasco alimuuliza Dr Slaa kuhusiana na hili na akamjibu vizuri jinsi utaraatibu ulivyokuwa...ila naelewa ni kwa ajili ya kuuza magazeti ndio maana waandishi wa habari lazima waandike hivyo..


hii stori ina utata, swali ni moja tu, Dr Slaa ni mtu mkubwa ndani ya Chadema, iweje yeye wampange jukwaa tofauti na mwenyekiti wake Mbowe, yaani wapangaji wameona wamweke Zitto jukwaa kubwa na Slaa jukwaa dogo la wabunge...probably ni coincidence ila i really doubt that
 
Nimekupata mkuu, kumbe walikuwa kwenye proximity ya kuweza kupeana mikono?

Ni vigumu kuamini since yeye pia alikuwa mgombea urais.

My guts tells me Dr ana kamgomo baridi, i stand to be corrected.
Haya mambo ya siasa Mushi saa zingine najikuta nacheka sana aisee..lol
 
Mkuu nini kinachokufanya uamini aliyokuambia Pasco na sio anayokueleza The finest?


Kwa habari ya chadema na viongozi wake hasa wa kitaifa, na kunapokuwa na suala linalowagusa kwa upande mmoja na upande wa pili serikali, kama chanzo chake ni Pasco siwezi kuiamini moja kwa moja, lazima kwanza kujiridhisha na vyanzo vingine.

Na hii nayo ngoja tumsubiri aje kuthibitisha Dr. Slaa alivyomkwepa raisi Kikwete kwakuwa naye alikuwepo Ifakara atatuwekea picha ya kiti kilichosuswa.
 
Umejuaje kwamba hiyo pete ina kijisindano Zumbe wa muheza? Au na wewe ni insider?

Teh teh teh!

Is that possible?


wakuu najaribu kutafakari tu, nafuta kauli yangu nisije tafutwa mm aisee.
nimeingiwa mashaka na namna wanavyomtafuta Dr. kusalimiana na JK utafikiri Zakayo alivyokuwa anatafuta kumuona Yesu,
 
hii stori ina utata, swali ni moja tu, Dr Slaa ni mtu mkubwa ndani ya Chadema, iweje yeye wampange jukwaa tofauti na mwenyekiti wake Mbowe, yaani wapangaji wameona wamweke Zitto jukwaa kubwa na Slaa jukwaa dogo la wabunge...probably ni coincidence ila i really doubt that
Kwani ni lazima Dr Slaa awe anapangwa Jukwaa kuu?
 
wakuu najaribu kutafakari tu, nafuta kauli yangu nisije tafutwa mm aisee.
nimeingiwa mashaka na namna wanavyomtafuta Dr. kusalimiana na JK utafikiri Zakayo alivyokuwa anatafuta kumuona Yesu,
Hahahahaha!!! Zumbemkuu haya mambo ya siasa wewe yaone hivi hivi tu maana kuna mengine zaidi ya hayo ambayo Slaa alitueleza kule Ifakara nikabakia..:shock::shock:
 
wakuu najaribu kutafakari tu, nafuta kauli yangu nisije tafutwa mm aisee.
nimeingiwa mashaka na namna wanavyomtafuta Dr. kusalimiana na JK utafikiri Zakayo alivyokuwa anatafuta kumuona Yesu,


Ha ha haaa. Mkuu umetishwa mara hii?
Basi futa kauli yako ili yaishe wasije wakakufanyia kitu mbaya!
 
Back
Top Bottom